Dar: Maandamano makubwa katikati ya Jiji

Dar: Maandamano makubwa katikati ya Jiji

Status
Not open for further replies.
Mkuu unataka siasa zifanywe na watu wasiokuwa na dini?Maalim seif ,Prof Lipumba,Jussa Ladhu Jussa kwenye CUF hawana dini?Jk Kikwete wa CCM hana dini?
Hivi saif Sharif,Lipumba,JK na jussa ni mashehe wa msikiti gani? Kumbuka CUF pia ilianguka kutokana na kuegemea upande mmoja.
 
Kuna sheria gani ambayo inasema usipojiandikishwa sensa ni kosa? Vipi kupiga kutokupiga kura nalo ni kosa au sensa tu?

sheria ya takwimu namba 1 ya mwaka 2002..na adhabu yake ni kifungo cha miezi 6 na faini ya laki 6.
 
Kama serikali yetu ni sikivu hata kutekeleza mara moja Madai ya waislamu jana hiyohiyo, Mbona serikali hiyo haitekelezi madai ya wananchi juu ya kuchukuliwa hatua wauaji wa mwabepande, arusha, tarime, morogoro, shinyanga, zanzibar na iringa???
 
Mkuu adolay,
Wewe ni Mkiristo mie ni Muislam siku zote tujadiliana kwa nidhamu bila kejeli za kidini wala dharau mpaka mmoja atapochoka na munakasha anaondoka zake kwa amani.

Mkuu lakini leo naona umeshindwa kuwa fair kwa kwa kejeli na matusi ya Chadema wenzako na lawama umewatupia CCM.

Mkuu sidhani kama kuna chama cha siasa ambacho kinaweza kufanikiwa kuchukuwa nchi kikitegemea wafuasi wa dini moja, tujenge heshima kwenye imani zetu hakuna mmbora zaidi ya mwingine, takuambia kitu kimoja wananchi wakiungana kwa pamoja ndio wanaweza kuibana serikali, lakini jamaa zako wanashindwa kuelewa kejeli na dharau dhidi ya Waislam wazidi kumualibia Dr Slaa na Chadema mbele ya jamii ya Kiislam.

Kama tutaendelea hivi tusahau kuitoa CCM madarakani.


Mkuu Ritz

Napenda tu usipoteze imani yako kwangu, mambo ya dini tumekuwa siku zote tukiyajadili nakweli msimamo wangu siku zote ukivuta kumbukumbu vema huwa nawatupia lawama kikwete na ccm mwisho huwa namalizia na kauli mbiu tanzania yetu sote watanzania waaminio na wasionaimani.


Nachukia sana kejeri, dharau, mafumbo na matusi kutoka mtu yeyote wa imani yoyote kwenda kwa mwingine mwenye imani tofauti. Kuabudu ni haki ya kikatiba ya mtu yeyote kwa tanzania yetu ilimradi havunji sheria.


Mkuu Rtiz sina hakika waliotoa kejeli, mafumbo na matusi katika maada hii na zinginezo kama ni chadema, lakini kama baadhi yao ni cdm wanapaswa kulaaniwa vikali na mungu awashukie kwa kauli zao zisizonaubinadamu wala chembe ya kumcha mungu, na tabia hii ikome mara moja.


Tanzania ni yetu sote kwanini tutukanane? tunapata faida gani? Inaumiza sana na hakika moderators should act on this soon so that we stay in peace as Tanzanians not as Christians or Muslims we are all sister and brothers why behaving in this way.

Mkuu wakati mwingine ni akili za watu na vichwa vyao lakini hiki kitendo kimeniuma sana na kukilaani kwa nguvu zangu zote.
 
Ni vizuri pia huyu MBUFYA akajua ya kuwa tafsiri ya neno "Uislam,Islam,As'salaam"..ni amani. Hivyo usishangae Waislam kufanya maandamano bila kusababisha vurugu. Ni kitu kigumu kwa Chadema lakini kwa waislam sio tatizo hata kidogo. Maandamano makubwa kama yale yangefanywa na Chadema wangemwaga tu damu na kuua angalau mtu mmoja kwa makusudi ili wapate cha kusema majukwaani.

Nafikiri unachanganya mambo hapa katika hili, hivi ni maandamano yapi ya chadema ambapo walimwaga damu au kuua mtu, ebu taja angalau moja tu. Acha kuruhusu akili yako kutumiwa kwa propaganda za kitoto, jaribu kujiridhisha na kile unachokisikia au kuambiwa, hata kama unaweza kuwa unamchukia mtu au chama fulani, si busara kusema UONGO unadhalilisha utu wako mwenyewe kama kweli wewe ni mwisilam muumin. Pili unaposema maandamano makubwa kama hayo kwanza unajionyesha utupu wako bila sababu, sijawahi kuwaona CDM wamefanya maadamano ya kidini popote pale kwa hiyo haukuwa na haja ya kuyalinganisha maadamano ya jana na CDM, lakini pia kama uko sawa naomba unisaidie kukumbuka maadamano ya CDM ambayo hata nusu yake unaweza kuilinganisha na mkusanyiko huu wa jana. Nashawishika kuamini kuwa wewe haujawahi hata siku moja kuyaona maadamano ya CDM vinginevyo una tatizo fulani la msingi..
 
Ukitaka kujua Chadema ni chama cha kina nani soma michango yao katika hii thread mpaka raha.

Si hata wewe unaona RAHA eeh! Jee nao wangedai hadi waandamane ili kwenye sensa kiwekwe kipengele cha CDM hapo naona ungeona UTAMU! au?
 
Kila member wa CDM hukejeli na kudharau Waislam. Lakini ikumbukwe kuwa kadiri usiku unapokuwa mzito basi kunakaribia kupambazuka. Na ishara zimeonekana jana. Hiyo ndio ppls power bana!
Endeleeni Kubezana kutukana!!
 
Hamna kitu sipendi kama udini,watu wanachukiana hapa kwa ajili ya dini za weupe...kama izi dini zinashindwa kuwaunganisha na kupendana basi hazina maana yoyote kwenu..imefikia hatua mtu anaomchukia mwenzake kisa anaitwa Juma au John.
 
Mkuu Ritz

Napenda tu usipoteze imani yako kwangu, mambo ya dini tumekuwa siku zote tukiyajadili nakweli msimamo wangu siku zote ukivuta kumbukumbu vema huwa nawatupia lawama kikwete na ccm mwisho huwa namalizia na kauli mbiu tanzania yetu sote watanzania waaminio na wasionaimani.


Nachukia sana kejeri, dharau, mafumbo na matusi kutoka mtu yeyote wa imani yoyote kwenda kwa mwingine mwenye imani tofauti. Kuabudu ni haki ya kikatiba ya mtu yeyote kwa tanzania yetu ilimradi havunji sheria.


Mkuu Rtiz sina hakika waliotoa kejeli, mafumbo na matusi katika maada hii na zinginezo kama ni chadema, lakini kama baadhi yao ni cdm wanapaswa kulaaniwa vikali na mungu awashukie kwa kauli zao zisizonaubinadamu wala chembe ya kumcha mungu, na tabia hii ikome mara moja.


Tanzania ni yetu sote kwanini tutukanane? tunapata faida gani? Inaumiza sana na hakika moderators should act on this soon so that we stay in peace as Tanzanians not as Christians or Muslims we are all sister and brothers why behaving in this way.

Mkuu wakati mwingine ni akili za watu na vichwa vyao lakini hiki kitendo kimeniuma sana na kukilaani kwa nguvu zangu zote.

Mkuu adolay,
Nashukuru sana kwa majibu yako murua na ya kutia matumaini Tanzania ni yetu sote wala hakuna kikundi chenye mamlaka na haki dhidi ya wengine, hii migogoro ya kidini ndio baina yetu ndio mtaji mkubwa wa CCM.

Wakati mwingine watu wanaweza kudhani Waislam wote ni CCM hapana watu wanakeleka na dharau na kejeli wanafanyiwa na baadhi ya Pro-Chadema JF Mkuu wangu bahati nzuri humu JF tunajuana kwa michango yetu na misimamo yetu kuna Chadema Great thinkers, kuna Chadema-Kata.

Wakati mwingine sidhani kama Dr Slaa anapendezwa na michango ya wafuasi wake humu JF hata akija kujibu hoja watu wanalipiza kisasi kwa kumjibu hovyo Dr Slaa ndio maana siku hizi umuoni JF yupo zake FB.

Mkuu jaribu kuwa unakemea maovu kutoka kwa wale wote wanaochafua jukwaa na kuvunja umoja wetu.
 
Last edited by a moderator:
Nimejibu hoja ya mtoa hoja kuwa "Chadema itisheni maandamano kuwapongeza waislam", tatizo langu lipi?

Hata hivyo tumeshuhudia maandamano na mikutano ya Chadema sehemu nyingi..huwa yanaambatana na mauaji kama kule Arusha, Igunga, Morogoro, iringa n.k. Unataka nikupe ushahidi wa kimahakama kuthibitisha hayo?
 
Ritz hata nawashangaa hawa jamaa waislam wajinga,wapuuzi,hawajaenda shule,wamesoma madrasa tu,sasa mnatoka povu la nini na watu kama hao? Nyinyi wasomi mnaojua kuvaa suti kwanini msihamasishane wenyewe mkawaacha waislam na ujinga wao? Au mnakhofia kura hazitatosha?

Aaaaaaaah ujakosea wanaogopa Kura hazitatosha ..ivi wasomi wao hawatatosha kweli kufanya waingie ikulu?
 
Mkuu adolay,
Nashukuru sana kwa majibu yako murua na ya kutia matumaini Tanzania ni yetu sote wala hakuna kikundi chenye mamlaka na haki dhidi ya wengine, hii migogoro ya kidini ndio baina yetu ndio mtaji mkubwa wa CCM.

Wakati mwingine watu wanaweza kudhani Waislam wote ni CCM hapana watu wanakeleka na dharau na kejeli wanafanyiwa na baadhi ya Pro-Chadema JF Mkuu wangu bahati nzuri humu JF tunajuana kwa michango yetu na misimamo yetu kuna Chadema Great thinkers, kuna Chadema-Kata.

Wakati mwingine sidhani kama Dr Slaa anapendezwa na michango ya wafuasi wake humu JF hata akija kujibu hoja watu wanalipiza kisasi kwa kumjibu hovyo Dr Slaa ndio maana siku hizi umuoni JF yupo zake FB.

Mkuu jaribu kuwa unakemea maovu kutoka kwa wale wote wanaochafua jukwaa na kuvunja umoja wetu.



Bila shaka mkuu Ritz, tanzania ni yetu sote bila kuthaminiana na kuheshimiaka ni kuukaribisha uadui baina yetu- tuko pamoja na tuhimizane na kuutukuza utanzania wetu.
 
laiti kama kelele hizi zinazopigwa sasa juu ya mauaji ya kikatili yanayofanywa na jeshi letu tusingeweka double standards tungefanikiwa kupambana na ukatili huu pia na kuiondoa ccm madarakani kirahisi.Nakumbuka mauaji ya Zanzibar baada ya maandamano yalikuwa makubwa sana,idadi ya wafu ilkuwa kubwa na mali nyingi ziliangamia lakini watanzania wakashawishiwa wayaone yale ni tatizo la kichama cha cuf na udini wa wazanzibar ikapita, yakaja ya morogoro watu wakaamka wakaanza piga mayowe yakapita, yakaja ya Iringa duuh ni hatari.HIVI TUNGEANZA MAKELELE HAYA TANGU MWANZO TUNGEKUWA TUMEFANIKIWA MAPEMA KABISA.Tatizo ni ubaguzi wa watanzania ndio unaotumaliza! Na ngoja tuone uchaguzi ukikaribia utasikia tu hili ni chaguo la mungu,hili lina maslahi ni dini yetu,hili linatufaa na kadhalika!!
 
Ni vizuri pia huyu MBUFYA akajua ya kuwa tafsiri ya neno "Uislam,Islam,As'salaam"..ni amani. Hivyo usishangae Waislam kufanya maandamano bila kusababisha vurugu. Ni kitu kigumu kwa Chadema lakini kwa waislam sio tatizo hata kidogo. Maandamano makubwa kama yale yangefanywa na Chadema wangemwaga tu damu na kuua angalau mtu mmoja kwa makusudi ili wapate cha kusema majukwaani.

Kama hayo unayoyasema ni kweli basi Middle East kungekuwa ni kisima cha amani!!! Labda hakukumwagika damu kwa vile................................ police wanawaogopa!!
 
Nimejibu hoja ya mtoa hoja kuwa "Chadema itisheni maandamano kuwapongeza waislam", tatizo langu lipi?

Hata hivyo tumeshuhudia maandamano na mikutano ya Chadema sehemu nyingi..huwa yanaambatana na mauaji kama kule Arusha, Igunga, Morogoro, iringa n.k. Unataka nikupe ushahidi wa kimahakama kuthibitisha hayo?

Mimi nimeshangazwa kuona unaburuzwa kwenye upuuzi wa comments kama hii iliyotoka kwa unayemdhania kuwa mfuasi au mpenzi wa CDM bila kuchambua na kuona kama ina maana yoyote, yaana ni sawa na unitembelee nyumbani kwangu mwanangu akukojolee halafu wewe unikasirikie mimi na kuamua kuacha kabisa kuja nyumbani kwangu tena......!!

Je umewahi kujiuliza nani alisababisha mauaji hayo, ni nani aliua watu katika sehemu zote hizo...?? Naamini unamfahamu na ndio maana hakuna hata kesi moja CDM wameshitakiwa kwa mauaji katika matukio yote hayo kwa sababu mshitaki anajijua fika ndiye aliye ua. Hebu nikufungue kidogo kifikra, chadema walifanya maadamano arusha wakapigwa mabomu na polisi na kuua watu watatu. Baadae CDM walifanya tena maadamano makubwa zaidi hapo hapo arusha tena yakafunga mitaa kadhaa na tena wakiwa wameumizwa siku chache kazaa lakini hakukuwa hata aliyejikwaa kusema mtu fulani alizimia, hata pale ambapo wananchi waliwataka CDM kuamuru walipize ni viongozi wa CDM waliotumia busara na kuwatuliza...hilo ni moja naweza kukupa mifano mingi tu. Anyway, ninachotaka kusema au kukushauri kama wngine ambavyo wamesema ebu tuache kuchanganywa na baadhi ya watu wanaingiza itikadi za kidini miongoni mwetu na sisi bila kutafakari na kuchambua tukameza kila kitu ili hali tunajua ukweli ni upi. Ebu tuwa makini katika mambo haya, wote ni wamoja kama watanzania (wakkristo, waislamu, wabudha, wa dini za asili na wasiokuwa na dini). Tukumbuke historia za siasa za nchi yetu jinsi ambavyo CCM imefanikiwa kututawala kwa propaganda za kidini kuanzia NCCR, CUF na sasa hawataki kuacha wamezigeuzia CDM na sisi tunakubali kuwa vipofu hata ambapo tunashuhudia mambo yakifanyika kwa macho yetu bado tunakubali kuwa bendela yao kwa kufuata wanachosema wao katika propaganda zilizojaa ujinga fulani. Ebu tukue kama watanzania na tutumie utashi na akili zetu kujiamlia na kufuata ukweli halisi.
 
laiti kama kelele hizi zinazopigwa sasa juu ya mauaji ya kikatili yanayofanywa na jeshi letu tusingeweka double standards tungefanikiwa kupambana na ukatili huu pia na kuiondoa ccm madarakani kirahisi.Nakumbuka mauaji ya Zanzibar baada ya maandamano yalikuwa makubwa sana,idadi ya wafu ilkuwa kubwa na mali nyingi ziliangamia lakini watanzania wakashawishiwa wayaone yale ni tatizo la kichama cha cuf na udini wa wazanzibar ikapita, yakaja ya morogoro watu wakaamka wakaanza piga mayowe yakapita, yakaja ya Iringa duuh ni hatari.HIVI TUNGEANZA MAKELELE HAYA TANGU MWANZO TUNGEKUWA TUMEFANIKIWA MAPEMA KABISA.Tatizo ni ubaguzi wa watanzania ndio unaotumaliza! Na ngoja tuone uchaguzi ukikaribia utasikia tu hili ni chaguo la mungu,hili lina maslahi ni dini yetu,hili linatufaa na kadhalika!!


Haijulikani unalalamika, unakemea, unashauri au na wewe unaendeleza ubaguzi. Mimi kelele nimezisikia siku nyingi tangu mauaji ya zanzibar, ila lazima utambue kitu kinachoitwa MWAMKO sio kitu cha siku moja, na tabia za watu huwa zinakuwa na vichochezi vya aina nyingi. Wewe unawaza hivyo unavyowaza kutokana na influence ama za dini, kabila, elimu, watu wanaokuzunguka, habari unazosikiliza na vitu vingi ambavyo kwa ujumla wake vinaitwa socialization.

Watanzania wa miaka ile, walikuwa vile kwa sababu walipaswa kuwa vile na sio lazima wawe hivyo milele
 
wajinawako, mabadiliko yanaanza na mtu mmoja mfano ni tunisia.
anza sasa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom