Dar: Halima Mdee afikishwa Mahakamani Kisutu, apewa dhamana

Dar: Halima Mdee afikishwa Mahakamani Kisutu, apewa dhamana

Unajifanya hujui aliropoka nini? Arudie tena aone moto

utoto unakusumbua, kwani kumkandamiza mtu kwa kutumia madaraka kwako unaona sifa? yamkuta mjombo wako siku moja kule kijijini kwenu au wewe mwenyewe ndipo utajutia kushabikia ujinga unaofanywa
 
Tanzania bado saaana, kuja kupata viongozi wenye nia na dhamira ya kweli ya kuiletea hii nchi maendeleo, labda siyo karne hii.
 
Halima Mdee aliyekaa akisalimiana na Esther Bulaya

Mbunge wa Kawe Halima Mdee, hatimaye amefikishwa Mahakamani Kisutu Dar es Salaam.

Bado sijajua atashitakiwa kwa makosa yapi kwani ndo yupo Kisutu.

Hapo awali Mdee aliwekwa Korokoroni Oysterbay Polisi kwa amri ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Hapi. Hata baada ya Masaa 48 kuisha, hakuachiliwa huru kwani aliendelea kushikiliwa.

Halima Mdee(Mb, CHADEMA) akamatwa na Polisi. Apelekwa Oysterbay...

Stay tuned..

UPDATES:

"Mdee alitoa lugha ya matusi na maudhi kwa kiongozi wa nchi, tulimuhoji na baada ya mahojiano tumemfikisha Mahakamani."- Kamanda Mkondya

"Mhe. Halima mdee tulimkamata maeneo ya Ubungo kwa sababu alikua na kikao na waandishi wa habari akipinga maamuzi ya Rais"- Kamanda Mkondya
---------------

UPDATE: 10, JULAI, 2017

Mbunge Halima Mdee ameachiwa kwa dhamana ya Milioni 10 na wadhamini wawili. Ushahidi haujakamilika na kesi imeahirishwa hadi August 7, 2017.

Ni kifungu gani cha sheria za Tanzania kinachosema kupinga maamuzi ya raisi ni jinai? Tupeane habari.

Maamuzi gani aliyoyapinga? Naomba tujuzane.

Aliyapinga kwa kufanya nini?

Waandishi wa habari aliokuwa nao, nao walikamatwa?

Ahsante.
 
I love this picture.

19905046_727918110748335_1860843072704581655_n-jpg.539023

me too
 
Sawa.
Kwa manufaa ya wengi naomba majibu kwa anayeelewa.

Nimesoma sehemu hapa kwamba alikamatwa baada ya kkuta Ubungo akiwa na mkutano na waandishi wa habari kupinga maamuzi ya raisi. Je hili ni la kweli?

Sheria gani ya nchi inayompa raisi mamlaka ya kutoa maamuzi na yasipingwe wala kuhojiwa na kwamba anayehoji ama kupinga anafanya kosa la jinai? Naomba kufahamishwa.

Alimpinga raisi juu ya maamuzi yapi?

Alifanya nini kinachoonekana kwamba amepinga?

Hao watu aliokuwa nao, maana yake alikuwa anafanya conspiracy kuvunja sheria za nchi. Nao walikamatwa?

figganigga, njoo hapa utoe ufafanuzi kwa kuwa wewe ndiye uliyesema "Alikuwa anafanya mkutano na waandishi wa habari kupinga maamuzi ya raisi.
 
Next time asirudie kumtukana tena Rais wetu mpendwa..

Sent from my SM-N9005 using JamiiForums mobile app
Mkuu , habari za Geita , baada ya salamu naomba kujulishwa Matusi ya Mdee kwa Mtukufu wetu .
 
Dhamana Milion 10? Mbona watu wanatupa pess jamani? Au ndo kukomoana? Kwa kesi ya dhamana Milioni 10?
 
Back
Top Bottom