Hapa cha kuangalia ni kwanini pesa hizo zilipitia mkombozi? Kulikuwa kuna lengo gani? Mfano Labda
Anna Tibaijuka anaweza kusema sababu za pesa za mchango wa Babro Johnson zilipitia mkombozi bank na sio account ya shule moja kwa moja! Pengine ni nani kati yao alipendekeza pesa zipitie huko na kwa sababu gani?
Inawezekana kweli mpokea pesa alipokea pesa bila kujua ni haramu au lah lakini kuna maswali anapaswa kuyajibu!
Mimi Jana nilitetea pengine hana kosa lolote na hajui lakini nimeanza kujiuliza why mkombozi account na sio Mama ana au Babro johnson bank account?
Halafu swala la kusema BOT waifungie Mkombozi kisa imepokea pesa hilo si sawa,Mkombozi wanafanya biashara na hawawezi bagua wateja na katika hili sijaona kosa lao kabisa labda ikithibitika wamehusika!
Hosea kusema atawashitaki walio pokea pesa hili nalo linaweza lisiwe sawa maana kupokea pesa linaweza lisiwe kosa kabisa labda kama ithibitike watuhumiwa walikuwa wanajua ni pesa haramu na walikuwa kwenye deal!
Kwangu Mimi naona
Anna Tibaijuka ana maswali machache ya kujibu kwenye hili sakata na kujinasua!
Cc
nyumba kubwa