Daladala za Arusha zagoma

Nimeshagombana na polisi hapa Clock tower sasa hivi eti anasema " kama huna akili huna akili tu" akimaanisha kuwatukana hawa jamaa wa daladala waliogoma nami nikamjibu" Kwa mtu asiye na akili ndiye tu atakeyeona hawa waliogoma hawana akili" basi akaondoka na bunduki yake akibwatabwata akaelekea kujificha maeneo ya TANESCO. Hapa kwa mkuu wa Mkoa kulikuwa na maadhimisho ya sikukuu ya Mashujaa na hawa madereva walipoonekana wanaelekea kwa mkuu wa mkoa ndo mabomu yakapigwa hapa clock tower na sasa wameelekea Meru Post na wamesema watakuwa mtaa wa Sabena kumsubiria mkuu wa wilaya.
 
mi nipo maeneo ya sakina,Arusha.jamaani wa huko mjini shwari,ni kweli wanapiga mabomu?
 
inakuwaje wapambane police na madereva? inamaana police wanawalazimisha madereva kuendesha magari au?
 
Inaelekea hawa wakazi wa Arusha wana ujasiri sana sijui,ni kama wa Mara,kila mara haya matukio yanatokea huko.Sasa wanadai nini?nauli ziongezwe?
 
Sasa hivi niko hapa makao mapya , mabomu yanalindima nyuma ya offisi yangu , hii leo noma.
 
Aa wapi wewe?
We si najua ukionaga hali hiyo unahamia kwa Mama pale City centre!!:dance:...Ndo uzuri wa kudeka kwa wazazi huu!

Unajua kuisha aga ni noma kuridi tena... Nita endelea na zoezi langu lakutembea kutoka Nduruma mpaka mjini...
 
Sasa hivi polisi wanapambana na madereva wa daladala waliogoma.....ni vurugu tupu.... si unajua tena hawa Polisi wetu wamefundishwa kupiga risasi za kichwa.......


ndio ilikua sehemu ya kujifunzia kulenga shabaha...........uliza utaambiwa.
 
ni bora maana na huo unene wako.......labda leo utakuwa umeondoa kilo 2 umebakiwa na 86.....kazana hata zibakie 70

Wakigoma wiki hivi naweza ni pendeza na labda kuwa kiportable... Lakini kuna watu wananipenda na unene wangu hivi hivi...
 
Si umeona eeh?
Kwa ufupi hali ni mbaya sana barabarani.
Abiria wanapata shida isiyo kifani, maana ni route-march iliyoenda shule!
Sababu:
Madereva na makondakta wa vifodi wanalalamikia suala la wao kukamatwa kila wakati na kuswekwa ndani kwa makosa yasiyo na maelezo ya kuridhisha!
Mfano, dereva akishusha abiria mahali, anakamatwa na kupigwa faini au kutupwa selo, wakati barabara za Arusha nyingi hazina vituo official!

Kuna madereva wasiopungua 5 wapo Kisongo Gereza la mkoa, na hivyo madereva wote wameamua kuwa hawatatoa huduma ya usafiri hadi hao wenzao watakapoachiliwa huru bila masharti yoyote!

Duuuuh Hapo sasa ndipo penyewe ulichokisema kweli mkuu nami ndivyo nilivyo ambiwa.

Kuna tatizo mmoja katika Hizi sector zetu za serikali Management zao ndio chanzo ya yote haya na hili liko mikoani kote Maaaan Wananchi hawajui utawala gani huu wa sheria unafuatwa nai holela holela tu bali liendende na hili linachangia sana kwa viongozi wengi wa sector hizi zina maslahi ndani humo, Haya kwamfanoArusha ndio maana twashidwa jua ni JIJI au sio JIJI maana kimpangilio wa Majiji haistahili kuitwa JIJI mfano mdogo tu ati barabara nyingi hazina Official vituo na hili liko karibu nchi nzima kuzorota kwa Maskali wetu na kwa uzembe wao kuto linda na kufuatasheria au kujua je sheria inafwatwa na raia hakufanyiki na mpaka sasa imekuwa ni mazoea.

Nachokisema hapa viongozi wetu ndio chanzo chz matatizo haya na ndio mwanzo wa Migomo utakapo anzia kesho tu mtasikia wananchi wameingia mtaaani hawamtaki Mayor na wala Rais maana kama ni hawa vijana wamegoma tuu kwa hilo la Police kutokuwa na utawala bora wa sheria sasa mwategemea nini.

Huo Mkoa sasaumejaa na wanamapinduzi wengi sio chadema peke yake hata wana CCM ,TLP CUF wamechoshwa na porojo za serikali hiii nandiko mambo ya migomo na maaandamano yatakapo anzia leo Rais uko zako mtwala huku wenzio wamegoma sherehe ya mashujaaaa ndio watu watakapo ichukulia ushujaaa.

My Take: Viongozi kuweni makini na maamuzi makini sio kuamka na kuchukuwa sheria bila kuichunguza kwanza wewe kama wewe kiongozi jitizame je hiyo sheria unayo ichukuwa ni haki sawa au Pili Biashara nyingi za Viford arusha zina milikiwa na Police mfn Gari za USA Mjini kwa Jina NDESAMBURO ziko zaidi ya 50 mwategemea huo mgomo huko arusha huja anzia ndani na hao hao maaskari si wana miliki Daladala?? Vyombo vyetu vya sheria vinaburuzwa na hawa hawa viongozi tulio wapa dhamana ya kutuongoza
 
Si umeona eeh?
Kwa ufupi hali ni mbaya sana barabarani.
Abiria wanapata shida isiyo kifani, maana ni route-march iliyoenda shule!
Sababu:
Madereva na makondakta wa vifodi wanalalamikia suala la wao kukamatwa kila wakati na kuswekwa ndani kwa makosa yasiyo na maelezo ya kuridhisha!
Mfano, dereva akishusha abiria mahali, anakamatwa na kupigwa faini au kutupwa selo, wakati barabara za Arusha nyingi hazina vituo official!

Kuna madereva wasiopungua 5 wapo Kisongo Gereza la mkoa, na hivyo madereva wote wameamua kuwa hawatatoa huduma ya usafiri hadi hao wenzao watakapoachiliwa huru bila masharti yoyote!
kwa taarifa nilizonazo ni 34 na wengi wao ni wa barabara ya Mjini - Engosheraton na Mjini -Uswahilini ambao huwa wana-park pale karibu na CRDB
 
inakuwaje wapambane police na madereva? inamaana police wanawalazimisha madereva kuendesha magari au?

Madereva wamechoshwa na kunyanyaswa na Police so leo wameamua kuacha magari nyumbani...hakuna hiece barabarani leo so nafikiri polisi wetu wanataka kutumia ubabe ili magari yarudi barabarani.....
 
Naenda kuongeza nguvu maana siyo mambo ya daladala tu bali maisha hayaeleweki kwa ujumla kupitia serikali hii
 
Nimepita barabara ya Idara ya maji na uhuru nikajichanganya na vijana yaani wanachopanga ni kuvamia maduka yaliyoko uhuru road hasa ya simu maana wanadai kama ajira zao wanazo zitegemea ni udereva na ukondakta na sasa magari yana kamatwa basi itabidi wagawane umasikini na matajiri wa Arusha..mmoja nimemsikia akisema nasubiri kinuke siongopi mabomu na risasi nitazama kwenye duka la mdosi nichukua phone kama 5 za ukweli basi...
 
Back
Top Bottom