Saint Ivuga
JF-Expert Member
- Aug 21, 2008
- 54,363
- 58,386
haw chadema wanachochoe vurugu soon watahamia kwa watoto wa kindergaten wagome.. Au sio magamba?
Aa wapi wewe?Ni poa tu nimepata kisingizio cha kufanya mazoezi leo asubuhi nahisi wakiendelea wiki hivi nitakua fiti mbaya...
Ni poa tu nimepata kisingizio cha kufanya mazoezi leo asubuhi nahisi wakiendelea wiki hivi nitakua fiti mbaya...
yah hata mimi nasikia mabomu maeneo ya meru posta...nasikia milio ya mabomu! kunani?
Kwa nini hao mateja wasiwafanyie hivyo hao police?Nikiwa kwenye usafiri binafsi ASUBUHI YA leo, maeneo ya JR nimeshuhudia gari, COASTER ikipopolewa mawe na kuvunjwa vunjwa vioo, na kuna baadhi ya abiria wameumizwa kwa mawe, kisa amepakia abiria!Kwa ufupi ni kwamba kila eneo la kituo kumewekwa MATEJA wanaohakiki utekelezaji wa azma yao, na vijana hao hawaelewi kitu, walishaajikatia tamaa ya maisha kiasi wanaona kuangusha tofali kwenye windscreen ni kazi ndogo!
Mabomu ya machozi yameanza kurindima maeneo ya posta kuelekea kilombero. Hali sio shwari kabisa, watoto wa shule wanarandaranda tu mitaani na watu wanakimbiakimbia hovyo. Tuombee tu utulivu upatikane na uzima kwa watu!
Wadau, huku barabarani naona mkusanyiko mkubwa wa watu na pikipiki za kutosha. Nilisikia kutakuwa na mgomo, je ndio huu? shida ni nini?