BabaDesi
JF-Expert Member
- Jun 30, 2007
- 6,032
- 3,944
B
Kuna uwezekano mkubwa sana huyo unaemuita kaka hana mtoto hata mmoja kiuhalisia. Hata huyo anaefikiria ni wake kwa mkewe sio wake.
Wote Jingaz ..!Katika mazingira fulani kaka na dada (mama zao mtu na mdogowe) wakajikuta wameanza mahusiano hatimaye kupata mtoto.
Dada alipoulizwa na wazazi wake kuhusu mimba akamsingizia mtu hewa, mtoto akazaliwa maisha yakaendelea, na huduma zinatolewa kwa usiri mkubwa sana mpaka sasa.
Wakati hayo yanafanyika Kaka mtu alikuwa tayari ana mke na mtoto mmoja mchanga.
Miaka 10 Sasa jamaa hajabahatika kupata mtoto mwingine kwa mkewe, pia kajaribu kutafuta nje ya ndoa imeshindikana kabisa, dada alishaolewa na amejaaliwa watoto wawili wengine.
Sasa Kaka anataka amchukue mwanaye aliyezaa na dada yake amlee kama mwanaye na awe sehemu ya urithi wake, lakini dada hataki kwasababu watu wanasema mtoto anafanana na Mjombaake (baba) Kwahiyo akimchukua siri itavuja,Kaka naye anatishia kutotoa msaada wowote endapo hatapewa mwanawe.
Kwenu wanaJF mnawaambia nini hawa wazazi mtu na dada yake.