Daah Ajira ngumu aisee!

Daah Ajira ngumu aisee!

PESA YA PHOTOCOPY,BAHASHA,STAMPS NA MUDA NI MTAJI TOSHA kwako.
Ok mi nikupe ushaur huu: pls achana kbs na mawazo ya kuajiriwa maana ajira zimekuwa magumashi sana cku hzi..,mi nilipomaliza digrii yangu ya uhasibu moja kwa moja nilirudi kijijin nikiwa na laki tatu na sitini elfu(360000) nkaanza mradi wa ufugaji wa kuku wa kienyeji kwa kufuata ushaur na maelezo yalipo humu humu jf.,amini usiamin saiz siwaz kutafuta ajira ila nina vijana watatu nimewapa ajira tunasaidiana kulea kuku hao ambao wananiingia NET PROFIT ya 9M kwa mwaka,najenga sasa,nakausafir kangu,mtoto anasoma english medium na sasa nashauriana na wife aache kazi yake ya ualim tupige mzigo huu. Yan hyo pesa ya photocopy,stamp,bahasha na muda huo ulikuwa mtaji tosha.
hongera mkuu!!
 
Daah kaka naona ushauri huo tosha alafu sasa ivi kazi ngumu broo tuna jiajili aiku izi
 
Story yako imenisikitisha sana ingawa ndani inafurahisha/kuchekesha...pale unaposema unajuana na boss kumbe sio...anyway mi nafikiria siku moja niweke story yangu hapa nahisi unaweza kumwaga machozi...soko la ajira kwa bongo ni gumu sana..ingawa sasahivi na-perform nzuri kwenye ajira yangu bt the story real pains a lot!!

Anyway mwombe Mungu 1day utatoka tu kamanda
 
NiPM nikupe tacts za kutafuta kazi. Mimi nimepita huko ila baada ya kujua nifanyeje naogelea ziwani, madimbwi swimming pool, hadi kwenye ndoo ukiniwekea maji nachapa mwende.

Kikubwa zaidi ni kuwa na subra, Mungu anatoa kwa muda wake. Ki binadamu unaona kama ni mazingaombwe, usikate tamaa we endelea kuomba, acha kuhesabia cv ulizowahi tuma, JIPE MOYO.

Naomba maujanja na mimi job seeker
 
Hongera kwa juhudi zako lakini pia usikate tamaa. Kama kuna mabosi serikalini walikuahidi kazi sidhani kama wataweza kukuajiri maana siku hizi ajira serikalini zinatangazwa na utumishi wa umma. Labda kwenye sekta binafsi, vuta subira sehemu zingine mpaka nafasi iachwe wazi kama kuna mtu kwa sasa. kuhusu kujitolea hapo inabidi uwe multi professional. Kazi nyingi za kujitolea ni za kijamii hivyo uanzie kwenye vikundi vidogo ujifunze wanavyofanya kazi kisha endelea kwenye vikundi vikubwa. usijali kuhusu mshahara jitolee na hakikisha unafanya kazi kwa kutumia akili na juhudi usioneshe uzembe ukikosea mahali usiwe mbishi omba radhi na jambo kama hulielewi waulize wahusika hata kama unaona elimu yao ndogo kumbuka wanakuzidi uzoefu wa kazi. Mwisho utajikuta uko mahiri na itakuwa rahisi hata mashirika makubwa kukuajiri maana pamoja na elimu pia wanaangalia uwezo wa kufanya kazi.
Pia, jaribu kutafuta kazi mikoani hasa kwenye miji ambayo haijakua sana huko jamii ndo inahitaji msaada. Kwa mji kama Dsm nafasi kama hizo nichache sana na watu ni wengi. Mikoani vikundi na mashirika ya kusaidia jamii yapo mengi.
Hapo baadaye hata wewe unaweza kujiajiri kwa kutumia taaluma yako ya uhasibu au ukapata kazi za uhasibu za kuajiriwa, baada ya kupata pa kuanzia.
 
Pole sn ht mie nimesota 4 2ys ila kw sasa namshukuru Mwenyez Mungu angalau kdgo uckate tamaa tym wl tel.
 
Duh pole mwana. Tatizo inawezekana nafasi zipo ila kwa picha ya waajiri walio wengi mtu ukiwa na accouting tu nayo ni shida. Ndiyo maana Accounting and finance inakuwa na maana zaidi kwenye soko la ajira. Suala lingine, kutuma CV kama uyoga kwenda kwa kila mtu nayo inaweza kuwa usumbufu kwa hao mabosi. Nadhani labda ungejribu kuiweka CV yako more professional, pia tafuta sehemu ya japo ujitolee bure. Ila Pole sana.
"Pia tafuta sehemu ya japo ujitolee bure". Mkuu akijitolea bure atakula nini?
 
Mkuu nimepata wazo jingine sio kwamba nadiss au vipi ila kwasababu umesomea accounting..me nadhani wewe una uwanja mpana sana wa ajira jaribu kuomba hata nje ya field yako maana sehemu nyingi sana(matangazo ya kazi) ukiwa na knowledge ya mambo ya accounting or finance unakua kwenye nafasi nzuri tu ni kutwist tu cover letter na kuandika experience ya kizushi..bila kusahau kubwa kuliko yote kumuomba Mungu
 
Mjuni umenikumbusha, dah nimeshauza vyombo kwa jampuni pale Morocco(by far 2000) nliuza wiki 2 nkakimbia. Kweli maisha safari ndefu jamani, ninaimani ipo siku utafanikiwa bwa mdogo, tumepita wote ktk hizo challenge but saiv aagh shwari tu

Mimi naamini kuwa pa1 na kuwa na background mbaya ya familia bado ukitulia unaeza fanikiwa.

Daaah mimi kipindi nimemaliza form six enzi hizo miliona tangazo kwenye gazeti wanahitaji wasambazaji wa bidhaa kwa wateja wao nikajua fresh nini unawapelekea watu order zao daah ile kufika aisee interview nini kila kitu fresh si ndo wakanigeia mavyombo kwenye fuko kubwa africa nzima daah ilibidi niishie njiani jamaa niliekabidhiwa anielekeze nikamwambia ebana mimi sikujua kama kazi yenyewe ni hii ka vipi wacha niende home nikaconfirm daah sijatia mguu mpaka kesho ofisi ilikua maduka mawili jina limenitoka
 
Serikali bana,sasa mnawakamata watu kisa wamechelewa kumaliza mkutano wao??hai make sense why CCM mnaangaika sana na Chadema??

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Wadau nimeitwa kwenye interview tra. Niombeeni niipate hiyo nafasi amina. Nashukuru kwa mchango wa mawazo yenu. Mungu atubariki sote
 
Wadau nimeitwa kwenye interview tra. Niombeeni niipate hiyo nafasi amina. Nashukuru kwa mchango wa mawazo yenu. Mungu atubariki sote
halafu unajisahau na ID nyingi nyingi..
 
tupia cv kwenye recriuting agencies pia kama erolink, rada, shughurika, elite carrier na nyinginezo!!! nami pia nilipitia maisha hayo, nikafunga nikasali nikatoa zaka then nikamwambia Mungu mwaka 2012 ukiisha sijapata kazi narudisha vyeti kijijini kwa mama then naanza umachinga hata wa kumwaga viatu ubungo ambao mtaji wake sio zaidi ya laki. muujiza ukatendeka mwazi wa 11 mwaka jana.
 
Asante kwa mawazo. But leo nimeitwa interview TRA...na Arusha kampuni ya wazungu.
 
Asante kwa mawazo. But leo nimeitwa interview TRA...na Arusha kampuni ya wazungu.

kwa experience niliyonayo interview sio kupata kazi tho ina add confo!!! yote ya kheri kaka
 
Pole mkuu,but i don't mean to insult you!...ungesomea mambo ya engineering kama sie,msoto ungeupata but not that much!
 
Back
Top Bottom