Daah Ajira ngumu aisee!

Daah Ajira ngumu aisee!

Asante kwa ushauri mzuri.
 
Halafu ndo mnasema turudi bongo usawa wenyewe wa kusaga lami hivi? Wengine hatuna ma connection bora tujisogezee siku tu huku.

Nilitaka kujua mdau ana profession gani ili kama haiko marketable tushauri kitu relevant, lakini mdau kasomea uhasibu, ambao unatakiwa kila sehemu.

Halafu anakwambia kujiajiri hana hata pa kuanzia. Let's face it, hata hicho kilimo kinahitaji kujipanga.
 
Wanasema toa pesa upate kazi. Wengine wanakwambia uwape kuanzia laki 7.....ukiwambia wakupe kazi then watachukua kwenye mshahara wanakataa. Wanasema mkono kwa mkono. Ukijichek..hizo laki saba huna. Na jamaa anayekwambia ukimwangalia..kakaa kitapelitapeli tu. Mpaka usawa huu nilishalizwa 300,000.
 
Hihihihi...Henge bana. Sa matusi ya nini dadaangu¦¦¦¦....hutupendi machadema sio??...anyways..Nisamehe bure dada Henge.
 
Kaka pole sana, jitolee tu mwisho wa siku utapata kazi nzuri, kuna dada mmoja alikuwa anajitolea NSSF miaka 3 sasa kapata kazi hapo hapo hivi karibuni. Usikate tamaa ipo siku yako.

Mkuu natumai kb52 ni mwanaume. Usimkompee na mwanamke plse.
 
Last edited by a moderator:
Hihihihi...Henge bana. Sa matusi ya nini dadaangu¦¦¦¦....hutupendi machadema sio??...anyways..Nisamehe bure dada Henge.

Pole sana kamanda.
Mi kuna siku niliomba kazi sehemu, jamaa walinijibu kwa ku-recycle barua ya application yangu kua hakuna kazi, watanijulisha zikipatikana. Mpaka leo kimya.
 
Asante kwa kutambua hilo
 
Ivi ccm bado ipo bro?..
 
Halafu ndo mnasema turudi bongo usawa wenyewe wa kusaga lami hivi? Wengine hatuna ma connection bora tujisogezee siku tu huku.

Nilitaka kujua mdau ana profession gani ili kama haiko marketable tushauri kitu relevant, lakini mdau kasomea uhasibu, ambao unatakiwa kila sehemu.

Halafu anakwambia kujiajiri hana hata pa kuanzia. Let's face it, hata hicho kilimo kinahitaji kujipanga.

Kilimo bila pesa ni kazi bure, kila kitu kinahitaji pesa kwenye kilimo
 
NiPM nikupe tacts za kutafuta kazi. Mimi nimepita huko ila baada ya kujua nifanyeje naogelea ziwani, madimbwi swimming pool, hadi kwenye ndoo ukiniwekea maji nachapa mwende.

Kikubwa zaidi ni kuwa na subra, Mungu anatoa kwa muda wake. Ki binadamu unaona kama ni mazingaombwe, usikate tamaa we endelea kuomba, acha kuhesabia cv ulizowahi tuma, JIPE MOYO.
 
NiPM nikupe tacts za kutafuta kazi. Mimi nimepita huko ila baada ya kujua nifanyeje naogelea ziwani, madimbwi swimming pool, hadi kwenye ndoo ukiniwekea maji nachapa mwende.

Kikubwa zaidi ni kuwa na subra, Mungu anatoa kwa muda wake. Ki binadamu unaona kama ni mazingaombwe, usikate tamaa we endelea kuomba, acha kuhesabia cv ulizowahi tuma, JIPE MOYO.

Na mi naomba hyo maujanja plse.
 
Asante Da Caro. Nshaku PM tayari.
 
Fanya mitian ya nbaa ..ukipass omba kweny audit firms utapata ...accounting is a tough but rewarding profession ..pia Muombe sana Mungu na usiache kwenda kanisani /mskitini ...serikalin ni ngumu sana kupata kama huna referee these days
 
Wazo zuri kaka. Nashukuru Mungu nilipata hela ya kujisajiri tu kwenye bodi hiyo ya NBAA. Sasa ni kama mwanachama tu na Nilitegemea ningepata ajira ningekua nafanya kazi huku nasoma...sasa sina hata pesa ya kulipia mitihani hiyo na hata pesa za maandalizi ingawa nnaouwezo kabisa wa kufaulu bila kurudi nyuma. Na kiujumla mitihani hiyo haihitaji ujiandae huku ukiwa na stress kama time hii nilivyo. Natamani sana lakin ndio ivo bro. Kwani hakuna kitu napenda kama kusoma.....Hua nahisi ni kusoma ni kama hoby kwangu.
 
Nimeandika thread hii nikiwa na lengo la..."Nipe Nyavu na mie nivue Usinipe Samaki"


Wenye nyavu watusaidie sie tunaoishi kama ndege tutoke tunduni. Tafadhali!!
 
Back
Top Bottom