Daah Ajira ngumu aisee!

Daah Ajira ngumu aisee!

Nimekufurahisha nini??..kuhangaika kwangu ama?..sijakuelewa
 
tatizo lenu vijana siku hizi mmekariri tu kuwa mkimaliza chuo tu basi ofisi inakusubiri wapewa funguo tu....jamani vijana amkeni tufikirie na mpango mwingine (plan B) kama kujiajiri au kuunda vikundi na kutafuta kitu cha kufanya na kwa njia ya vikundi mikopo inakuwa inapatikana...katika maisha kaka ni lazima ukiwa na ishu yako unataka kuifanya jaribu kuwa na alternatives ili hii ikikwama basi unaswitch kwa nyingine...ni marufuku kukariri!!!!!!!!!!!!!!! pia ujue kuwa hizo kazi ulizokosa hazikuwa rizki yako na kwamba rizki yako ipo njiani na utakuja kufanikiwa...haya yanayokukuta kwa hivi sasa ni kwamba unatengeneza history ya maisha yako na wakati umefanikiwa utakuwa unakumbuka tu kama history....kumbuka pia 'likuepukalo lina kheri na wewe'...kwa hiyo usife moyo endelea kuhangaika huku ukiwa na alternatives zako pia...kila la kheri ndugu yangu, mambo yatakuwa mazuri tu kwa wakati wa Mwenyezi Mungu...inshaallah!!
Wajamen wana JF...nimetumia kila mbinu kupata kazi sijafanikiwa. Nakumbuka nilikua nikitoa copies za vyeti na CV nyingi sana...kama zaidi ya 200....nikaanza kua nazitembeza na kibegi changu cha kisomi huku nikiwa nimevalia nguo safi nadhifu za kiofisi. Nilikua nikiandika barua nyingi sizizokua na address ya ofisi..but kila nilivyoona bango la ofisi...nilikua nikikopi address yake na kwenda pemben na kupaste kwenye barua mojawapo kati ya nilizokua nikiziandaa.

Kasheshe ilikua jinsi ya kuingia pale ofisi husika. Mlangoni getin mara nyingi nilimkuta mlinzi..."unashida gani?..unaenda kumuona nani?..sign daftari hili" hayo ni baadhi ya maswali niliyokua nikiulizwa. Nikifanikiwa kumpita japo wengine walikua wakinizuia katukatu...nakumbana na mtihani wa mwisho wa pale kwa sekretari wa boss..ofisini hapo. Hawa walikua wakiniuliza.."unashida gani?..ya binafsi au ofisi?"..ukisema ya kiofisi imekula kwako...watakuuliza "una appointment letter??"..ukisema huna basi ndio hutaweza kumuona boss. Kwani mimi nia yangu kubwa ilikua ni kumeet na mwenye mbwa tu. Mwanzon ilikua ngumu sana kumet nao sana kwani swali la kusema nna appointment na boss lilinishinda sana..nikawa nafel na kujikuta sipati fursa ya kumuona. Nikabuni mbinu ingine.



Safari hii...nilivyokua nikuulizwa na sekrtar kama ni shida ya binafsi au kiofisi...nilisema shida ya binafsi.....nikawanaulizwa tena. Unafahamiana na boss?..nikawa nawajibu kwa konfidens..ndio. Ananiliza jina langu kisha boss anapigiwa simu...ngriiiii...halo boss Hamidu anataka kukuona...anasema wewe mnafahamiana..ni ndugu yako....boss nikawa namsikia anasita kidogo...Hamidu???..anyways mruhusu aingie.



Kimbembe ni kwa boss....it was funny...maboss wengi walifurahi sana...nikawa nawachana..nawaambia nyie ni wagumu sana kuwapata...na sometimes CV zetu hazifiki kwenu..ma PS au walinzi wanazichana. Niliongea yangu...wengine walikaribisha chai au chakula na wengine walinipa pesa ya nauli. But mwishoni niliwaomba Busness card zao. Hapa nilipo nina zaidi ya 120 ya kadi. Wengi walinipa matumaini kua "kama wakitangaza watanikonsider"..wengine waliniambia nisubiri baada ya miezi kadhaa...etc etc blah blah kibao.


Nilikua nikiwasiliana nao kwenye namba zao za simu kuwakumbushia. Nikawa napigwa danadana tu..longolongo kibao. Wengine wakanichenjia niwape cash kidogo...na bahati mbaya sikua na chochote.



Nilikua nikitembea sana...maofisi mbali mbali ya posta..vingunguti na kote dar es salaam. Nilikua nikituma pia kwa njia ya posta barua zingine.


Nilifanya hivyo kwa njia ya analogia na digitali.Nimetuma mails nyingi sana za kazi. Hapa sasa ivi nilikua naangalia. .toka 2009 hadi sasa nimeshatuma mails 1999+ za maombi ya kazi bila mafanikio.


Nikajiunga na linkedin website...hapa nikameet na proffessionals wengi sana....maboss kibao...nikawanawatumia CV zangu direct. I mean..nikisikia nafasi imetangazwa...naingia linkedin..nawasiliana na mtu ambae anafanyakazi sehemu hiyo. So nakua like natuma maombi mara 3...kwa huyo jamaa...kwa mails ya ofisi na sanduku la ofisi.


Kuna mtandao pia nikifakiwa kuuona..unaitwa CEOs roundtable...hapa nilimeet na ma CEOs na kuwatumia resumes zangu bila mafaniko.



Kuna tovuti za kutafutia kazi kama zoomtanzania...proffessionalapproach. ...kazibongo...vijanatz...pataajira..kokorikoo...britermonday...mwananchi etc etc..nimekua nikizitembelea kila mara mpaka tovuti za nchi za uarabu.




Ilifikia kipindi niliamua kwenda kutafuta kazi mining...kwenda kusotea kazi. Kukaa pale getini na CV zako na kusubiria mzungu wa kampuni flani apite uchonge nae unampa CV lakin hola. Nakumbuka nilipata kazi Barrick Buzwagi kama Security Officer..siku ya kwenda kuripoti nikaambiwa jina halionekani. Daah




Kiukweli nimetumia mbinu mbali mbali sana. Hata kubeba matofali pale kona ya msamvu niliwahi kubeba pia. Niliumia mikono sana na mwili kukosa nguvu. Tofali moja kubeba ni sh. 25.



Sasa waweza kujiuliza elimu yangu ipo vipi?..kiukweli nna elimu ya kawaida tu. Nilisoma seminary na kupata alama nzuri tu za fom 4 na six vilevile....chuo nikasoma mara mbili....advanced diploma ya accounts na postgraduate diploma ya accounts.



Nasikia tu watu wanasema vijana rudini vijijini kwenu mkalime....wengine...vijana mjiajili.....hapa ndo nachanganikiwa kabisa. Naanzajeanzaje sasa kwa mfano...ebu tuambiane wadau....wayeyote aliyepitia situatiation kama yangu aseme katokaje. Kwani hapa nipo nipo tu kama lipicha la michelini au lisanamu la bunduki la pale posta. Nimeganda....
 
Wajamen wana JF...nimetumia kila mbinu kupata kazi sijafanikiwa. Nakumbuka nilikua nikitoa copies za vyeti na CV nyingi sana...kama zaidi ya 200....nikaanza kua nazitembeza na kibegi changu cha kisomi huku nikiwa nimevalia nguo safi nadhifu za kiofisi. Nilikua nikiandika barua nyingi sizizokua na address ya ofisi..but kila nilivyoona bango la ofisi...nilikua nikikopi address yake na kwenda pemben na kupaste kwenye barua mojawapo kati ya nilizokua nikiziandaa.

Kasheshe ilikua jinsi ya kuingia pale ofisi husika. Mlangoni getin mara nyingi nilimkuta mlinzi..."unashida gani?..unaenda kumuona nani?..sign daftari hili" hayo ni baadhi ya maswali niliyokua nikiulizwa. Nikifanikiwa kumpita japo wengine walikua wakinizuia katukatu...nakumbana na mtihani wa mwisho wa pale kwa sekretari wa boss..ofisini hapo. Hawa walikua wakiniuliza.."unashida gani?..ya binafsi au ofisi?"..ukisema ya kiofisi imekula kwako...watakuuliza "una appointment letter??"..ukisema huna basi ndio hutaweza kumuona boss. Kwani mimi nia yangu kubwa ilikua ni kumeet na mwenye mbwa tu. Mwanzon ilikua ngumu sana kumet nao sana kwani swali la kusema nna appointment na boss lilinishinda sana..nikawa nafel na kujikuta sipati fursa ya kumuona. Nikabuni mbinu ingine.



Safari hii...nilivyokua nikuulizwa na sekrtar kama ni shida ya binafsi au kiofisi...nilisema shida ya binafsi.....nikawanaulizwa tena. Unafahamiana na boss?..nikawa nawajibu kwa konfidens..ndio. Ananiliza jina langu kisha boss anapigiwa simu...ngriiiii...halo boss Hamidu anataka kukuona...anasema wewe mnafahamiana..ni ndugu yako....boss nikawa namsikia anasita kidogo...Hamidu???..anyways mruhusu aingie.



Kimbembe ni kwa boss....it was funny...maboss wengi walifurahi sana...nikawa nawachana..nawaambia nyie ni wagumu sana kuwapata...na sometimes CV zetu hazifiki kwenu..ma PS au walinzi wanazichana. Niliongea yangu...wengine walikaribisha chai au chakula na wengine walinipa pesa ya nauli. But mwishoni niliwaomba Busness card zao. Hapa nilipo nina zaidi ya 120 ya kadi. Wengi walinipa matumaini kua "kama wakitangaza watanikonsider"..wengine waliniambia nisubiri baada ya miezi kadhaa...etc etc blah blah kibao.


Nilikua nikiwasiliana nao kwenye namba zao za simu kuwakumbushia. Nikawa napigwa danadana tu..longolongo kibao. Wengine wakanichenjia niwape cash kidogo...na bahati mbaya sikua na chochote.



Nilikua nikitembea sana...maofisi mbali mbali ya posta..vingunguti na kote dar es salaam. Nilikua nikituma pia kwa njia ya posta barua zingine.


Nilifanya hivyo kwa njia ya analogia na digitali.Nimetuma mails nyingi sana za kazi. Hapa sasa ivi nilikua naangalia. .toka 2009 hadi sasa nimeshatuma mails 1999+ za maombi ya kazi bila mafanikio.


Nikajiunga na linkedin website...hapa nikameet na proffessionals wengi sana....maboss kibao...nikawanawatumia CV zangu direct. I mean..nikisikia nafasi imetangazwa...naingia linkedin..nawasiliana na mtu ambae anafanyakazi sehemu hiyo. So nakua like natuma maombi mara 3...kwa huyo jamaa...kwa mails ya ofisi na sanduku la ofisi.


Kuna mtandao pia nikifakiwa kuuona..unaitwa CEOs roundtable...hapa nilimeet na ma CEOs na kuwatumia resumes zangu bila mafaniko.



Kuna tovuti za kutafutia kazi kama zoomtanzania...proffessionalapproach. ...kazibongo...vijanatz...pataajira..kokorikoo...britermonday...mwananchi etc etc..nimekua nikizitembelea kila mara mpaka tovuti za nchi za uarabu.




Ilifikia kipindi niliamua kwenda kutafuta kazi mining...kwenda kusotea kazi. Kukaa pale getini na CV zako na kusubiria mzungu wa kampuni flani apite uchonge nae unampa CV lakin hola. Nakumbuka nilipata kazi Barrick Buzwagi kama Security Officer..siku ya kwenda kuripoti nikaambiwa jina halionekani. Daah




Kiukweli nimetumia mbinu mbali mbali sana. Hata kubeba matofali pale kona ya msamvu niliwahi kubeba pia. Niliumia mikono sana na mwili kukosa nguvu. Tofali moja kubeba ni sh. 25.



Sasa waweza kujiuliza elimu yangu ipo vipi?..kiukweli nna elimu ya kawaida tu. Nilisoma seminary na kupata alama nzuri tu za fom 4 na six vilevile....chuo nikasoma mara mbili....advanced diploma ya accounts na postgraduate diploma ya accounts.



Nasikia tu watu wanasema vijana rudini vijijini kwenu mkalime....wengine...vijana mjiajili.....hapa ndo nachanganikiwa kabisa. Naanzajeanzaje sasa kwa mfano...ebu tuambiane wadau....wayeyote aliyepitia situatiation kama yangu aseme katokaje. Kwani hapa nipo nipo tu kama lipicha la michelini au lisanamu la bunduki la pale posta. Nimeganda....

Pole sana Mkuu!!Usikate tamaa kwa jitihada zako soon utapata kazi......la msingi Omba Sana Mungu uku ukijibidiisha kutafuta kuna mahali anakupeleka,we all don't knw whr?I am sure next tym utaleta ushuhuda humu JF wa kazi uliyoipata.
 
Mimi nilipomaliza chuo nilikaa mwaka mmoja bila shughuli yeyote,
Baadaye nikaenda kwenye kakampuni nikawa natembeza vyombo, unauza bei ya juu, unakata pesa ndiyo mshahara wako, usipouza na wewehela huna, nilivumilia ili tu kukicha niwe na pa kwenda. Nilijifunza five steps to sell, Sijui eight steps to success lakini baada ya mwaka mmoja sikuona gain yeyote, nilikuwa napata hela ya kula tu halafu kazi ngumu kwrlikweli, unatembea mitaani hadi sole za viatu vinaisha, hujauza

Baada ya mwka mmoja niliacha, nikaenda kufundisha shule za kata, imagine, graduate unafundisha form one na form two physics na hesabu,mshahara elfu 70, nikawa nafundisha vishule viwilikwa wakati mmoja, Nikawa napata pesa ya nauli kwenye interviews mbalimbali,

Baadaye nikapa sehemu nzuri kutokana na elimu yangu, sasa hivi mambo safi.

Kwa hiyo unaweza kuona kuwa nilikaa almost miaka mitatu ndipo nikapata sehemu ya maana.

Kwa hiyo na wewe kama umesota kwa mmiaka miwili au mitatu usiogope, ndivyo ilivyo.

Mjuni umenikumbusha, dah nimeshauza vyombo kwa jampuni pale Morocco(by far 2000) nliuza wiki 2 nkakimbia. Kweli maisha safari ndefu jamani, ninaimani ipo siku utafanikiwa bwa mdogo, tumepita wote ktk hizo challenge but saiv aagh shwari tu

Mimi naamini kuwa pa1 na kuwa na background mbaya ya familia bado ukitulia unaeza fanikiwa.
 
pole mkuu.nimesikitika pale ulipo pata kazi ya ualinzi,kuripoti wanadai jina halionekani.
Imewahi kunitokea inayofanana na wewe baada ya kufanya interview sita za mchujo na kupita na kupigiwa simu ya hongera na kwamba nikachukue mkataba ofisini kwao ili niende nao kwenye kituo chao cha kazi,bahati nilikuwa sikai mbali na kituo.Ile kufika pale nakutana na wengine walioambiwa wachukue mikataba yao ya kazi,nikiwa nafuraha huku naomba nipewe mkataba wangu, muhusika anadai jina langu halipo wala mkataba wangu,nikawaambia mbona mmenipigia simu kama saa 1 imepita ,yule mdada akanijibu kimkato ,haoni jina langu, kwa hiyo sikuipata hiyo kazi.
Sijapata kazi mpaka sasa na wala sitafuti, ila mambo yangu yataenda kupitia ajira binafsi(mikakati imeanza), Kila mtu ana njia yake Mungu aliyomuandikia ya kupata kipato.
pole,ila usivunjike moyo mkuu endelea na aina nyingine ya jitihada

Mmh so sad, dah naomba isinitokee maana mchana ntakuwa na usaili
 
Nashukuru kwa kunipa moyo jombaa. Much love
 
Tuanzie kwenye basics

1. Asilimia ngapi ya mombi yako unaitwa?(<5%)- jaribu kufanyia kazi cv yako, cover letter na viambatanishi....makosa madogo madogo kama spelling error, fonts kachumbari, alignment, pengine na GPA labda ni Dwarf inatosha kum-turn off mtu kukuita....Google how to write a CV and cover letter....Match your CV to the particular JD +organisation...hakuna kitu kama 'one size fits all'. Umesema unaandika barua nyingi unapaste address tu?? Really...

2. Unaomba kazi sehemu gani au kazi zipi?? kwa sifa zako compee ni kubwa sana hasa za watu ambao hata wamekuzidi sifa kwa hivyo sitegemei unaomba kazi za 'accounts tu' maana UDSM+UDOM+IFM+TUMAINI+MUCOBBS+TIA+IAA+MYSORE+BANGALORE+CARDIFFF+ ETC...zinatoa watu wa kutosha kila mwaka wenye sifa na wamejipanga kwa hiyo....expand your grazing field to maximise your niche.......

3. Unaitwa kwenye usaili na kisha unakosa kazi kwa asilimia zipi? je tatizo ni kuwa huna vipawa vya usaili....fanyia kazi confidence, kujieleza vizuri, social skills, body language, research kazi unayoomba na kampuni husika vizuri, onyesha enthusiasm za kutosha hata kama fake, drop a bomb yaani, unawaacha watu dah huyu jamaa katu-impress lazima tumchukue......ongea lugha moja na anayekusaili....tell them what they want to hear......ingia google jipige msasa haswa....invest muda kiasi na resources kama internet+vitabu au hata usaili usio wamalengo kama rehersal ya kazi zenyewe....

4. Unaitwa kazini unagomea maslahi madogo? hapa inabidi ujiangalie kuwa huna hata uzoefu wa kazi, watu hawafahamu utendaji wako kwa hiyo unaweza kuanza mdogo mdogo baada ya mwaka unahamia pengine au utaongezewa kima cha masurufu....

5. Unatafuataje kazi? usilenge tu advertised job.....update profile kule recruitment agency watu wakuone wakuite kwenye intial assessment ushindwe mwenyewe....career tab kwenye 'company portal' etc...

6....

7...

Naomba nisaidie hizo recruitment agency za Tanzania mkuu, walau 3 tu nina shida nazo
 
Unazikumbuka zile, Introduction,short story, presentation,close na reharsh?
Au ulikimbia kabla ya kujua five steps to sell?
Mjuni umenikumbusha, dah nimeshauza vyombo kwa jampuni pale Morocco(by far 2000) nliuza wiki 2 nkakimbia. Kweli maisha safari ndefu jamani, ninaimani ipo siku utafanikiwa bwa mdogo, tumepita wote ktk hizo challenge but saiv aagh shwari tu

Mimi naamini kuwa pa1 na kuwa na background mbaya ya familia bado ukitulia unaeza fanikiwa.
 
PESA YA PHOTOCOPY,BAHASHA,STAMPS NA MUDA NI MTAJI TOSHA kwako.
Ok mi nikupe ushaur huu: pls achana kbs na mawazo ya kuajiriwa maana ajira zimekuwa magumashi sana cku hzi..,mi nilipomaliza digrii yangu ya uhasibu moja kwa moja nilirudi kijijin nikiwa na laki tatu na sitini elfu(360000) nkaanza mradi wa ufugaji wa kuku wa kienyeji kwa kufuata ushaur na maelezo yalipo humu humu jf.,amini usiamin saiz siwaz kutafuta ajira ila nina vijana watatu nimewapa ajira tunasaidiana kulea kuku hao ambao wananiingia NET PROFIT ya 9M kwa mwaka,najenga sasa,nakausafir kangu,mtoto anasoma english medium na sasa nashauriana na wife aache kazi yake ya ualim tupige mzigo huu. Yan hyo pesa ya photocopy,stamp,bahasha na muda huo ulikuwa mtaji tosha.
 
Asante kwa link hiho mkuu.
 
Usihangaike piga 0719836781 au 0765666390 mwambie matatizo yako atakusafishia nyota nakuambia hutachuku mwezi unakitengo.serious mkuu
 
Back
Top Bottom