CWT yapinga walimu kusafiri bure

CWT yapinga walimu kusafiri bure

Ila kama nitakuwa sijakosea kwa kauli aliyoitoa Makonda alisema pande zote waliafikiana(wamiliki wa daladala na waaalimu). So it means huyu jamaa ameudanganya umma wa watanzania???
Kama angefanya mkutano na makondakta na madereva ingekuwa bora zaidi!!
 
Misifa.Afu kibaya zaidi katoa tangazo la kimkoa bila kumshirikisha hata mkuu wa mkoa.

kama ulisikiliza habari amesema ana baraka za mkuu wa mkoa ,,,, usikurupuke mkuu
 
Hiyo lift na allowance ni kwa walimu tu au na watumishi wote wa serikali??

Kama ni kwa walimu tu, why?? Kwani watumishi Wengine km manesi, wahudumu wa ofisi, makatibu muhutasi, watunza kumbukumbu, walinzi, watendaji wa vijiji na mitaa etc, etc wao hawastahili hiyo allowance na lift?
Hapa tunazungumzia project ya Makonda. Yeye watumishi wa umma alioona wana mazingira magumu ni waalim tuu, sijui kachukua vigezo gani.
Haya sasa wenyewe hawataki
 
Mkuu askali halikuwa tangazo, na kwa nature ya kazi yao, ilikuwa rahisi kwao kutekeleza hlo, wala si udhalilishaji, ila kwa waalim asee hapana napinga kwa nguvu zote....
Toa sababu, kwanini kwa askari sio udhalilishaji lakini kwa walimu ni udondoshaji!!
 
Yeye Mkoba hajui shida za walimu badala ya kushukuru yeye anaanza kulaumu ,nia apate ujiko kuwa alishiriki kufanikisha hilo jambo,huo ni wivu wa kike,jeyeye na chama chake ni kipi wamefanya kusaidia waalimu kuondokana adha ya maisha duni na tabuwanazopata kila siku

matatizo ya walimu yanasababishwa na mslahi dini na serikali haiwezi kukwepa majukumu ya kuongeza mishahara ya walimu kwa kuongea na wamiliki wa mabasi ili wasafiri bure kwanza ni udhalilishaji we unawajua makonda ,wasumbufu balaa mwisho wa siku wawa ambie waalimu kua wasimame hawaruhusiwi kukaa hapa dawa ni kuwanunulia costa maarum au walipe allowance ya nauli kila mwez
 
M nauliza maamuz ya Huyo jamaa,alikurupuka kumchapa vibao mzee yule wa katiba,sishangai akikulupuka kwenye hili,walimu kupitia mwenyekiti wenu tuko pakoja,maana m ni kwalimu nafundisha kino naish tmk cjui hapo inakuwaje na napanda magar mawil
 
konda : cheke cheke! abilia nauli

abiria: mi mwalimi

konda: onyesha kitambulisho

mwalimu: (anashika mfukoni) hiki hapa

konda (anakichukua kile kitambulisho na kukikodolea macho pande zote mbili)....

konda: (anarudisha kitambulisho) sasa mbona umekalia siti

mwalimu : kwan kuna tatizo?

konda: hebu wapishe waliolipa nauli wakae

mwalimu: (kwa hasira) hebu acha kunizaliliasha kijana

konda: (akimuangalia mwalimu usoni) hivi we unaona ni haki kukaa wakati alielipa nauli amesimama?

mwalimu (kimya)

konda: kwanza nyie walimu nina hasira na nyie sana

mwalimu (kwa ghadhabu) hasira?

konda: eeh kwanza mlinichapa sana bado nifeli.... na leo unapanda gari yangu huna nauli..

abiria wengine: hahahahahaha

konda: dah yani sipendi kupakia hizi chenga kubwa

mwalimu: nani chenga?

konda : yan wewe ni chenga kuliko huyo mwanafunzi unaemfundisha

mwalimu: (kwa tabasamu la aibu) kivipi?

konda : we umekalia siti hujalipa hata mia lakin dogo kasimama na amelipa 200..

konda (kwa kejeli) sasa sema wewe na dogo nan chenga?

mwalimu (kwa hasira anafungua pochi na kutoa sh 5000 ) kata mia nne yako mbwa wewe.


MAKONDA WAZO LAKO NI GUMU KUTEKELEZEKA LABDA MWALIMU AWE NA ROHO YA JIWE
 
Hii nchi bana yaani hata kama kitu kinafaida kama hujashirikishwa unapinga
 
Sijui nikutukane? Mtu kakesha nje we umelala kwa raha zako na mumeo then aanze tu kutoa nauli... Yaani afanye kazi mbili alipe huku akiendelea kukulinda...!!!!!
!!
!
!
Kupanga ni kuchagua. Kwani anakesha bure? Nani kamchagulia hiyo kazi/shughuli? Hakuna aliyemlazimisha mtu kwenda kuwa katika kada hizo na wasijifanye wazalendo they were just running out of options.
 
!
!
Sasa kuchangia hapa as if labda walilazimishwa, noo. Hawa watu ni ama walipenda au hawakuwa na machaguo mengine wakakimbilia huko. Na kwa kufanya hivyo wanalipwa hawafanyi bure. Kwa nini wapande daladala bure sasa?
 
Walimu wapande daladala bure kwa msingi upi?! Wawai shuleni kufundisha watoto wetu?! Labda hili lina mantiki, lakini je, kwanini manesi na madaktari wasipande daladala bure ili kuwai kuokoa maisha ya ndugu zetu watanzania wenzetu?
Na kwanini wanajeshi na polisi nao wasisafiri bure ili wawahi vituo vyao vya kazi ili kutulinda sisi wananchi?!
Na kwanini wafanyakazi wa serikali wasipande daladala bure ili wawahi kwenye ofisi za umma kuhudumia wananchi??!
Na kama walimu wanapanda bure na angali wanalipwa mishahara kwann wanafunzi ambao hawalipwi mshahara nao wasipande bure hizo daladala??!

Binafsi sioni logic ya mwanafunzi kulipia afu mwalimu asilipie, this is crayz!!

Huyu Makonda need to be checked! He is not okay, kama ni kutafuta political kick this is not right.
 
Hapa tunazungumzia project ya Makonda. Yeye watumishi wa umma alioona wana mazingira magumu ni waalim tuu, sijui kachukua vigezo gani.
Haya sasa wenyewe hawataki
Kwa hiyo makonda ndo alipe walimu hiyo allowance?
 
!!
!
!
Kupanga ni kuchagua. Kwani anakesha bure? Nani kamchagulia hiyo kazi/shughuli? Hakuna aliyemlazimisha mtu kwenda kuwa katika kada hizo na wasijifanye wazalendo they were just running out of options.
Lkn kaa ukijua kazi zingine ni risk kuliko zingine, na haiwezekani tu kwa kuwa ni option basi watu waende kada zingine...hata asipochagua huyu atachagua mwingine mwisho wa siku walinzi lazima wawepo na ni lazima kuwapa vipaumbele kwa aina ya kazi wanayofanya na risk iliyopo...for instance police akiwa ndani ya sare ujue yupo kazini...so haiingii akilini anayekulinda tena akulipe...
 
hapa ni kukurupuka tu kuanzia chini hadi juu !
mabasi ya mwendo kasi vipi ?
tuliambiwa january 16 au bado haijafika?
 
Mwenyekiti wa chama cha walimu Tanzania G. Mkoba amesema haoni kama ni sahihi kwa mkuu wa wilaya ya Kinondoni kuingia kwenye makubaliano na wenye mabasi ya daladala ya kuwasafirisha walimu bure bila kuwashirikisha walimu wenyewe, hivyo ameshauri kuwa ni vizuri mambo yanayowahusu waalimu yakawa yanawashirikisha walimu.

Chanzo: Clouds tv

Sasa Walimu watajua adui yao ni nani.
 
Kitambulisho lazima kisainiwe na DC makonda.....
Umaarufu usio na tija. Makondakita ni raia wa Kenya.
 
Mzigo wa serikali kutaka kuhamishia kwa wafanyabiashara punguza au toa kodi agiza bus yabebe walimu bure na si kufanya mambo yasioeleweka...kodi ya mapato inaongezeka harafu watumishi wa Umma woote unataka wapande bure Mafuta hushushi bei kodi coaster 20milion gari la 1998 bado sumatra hapo na fine za bara barani unataka bilion 2 kwa mwezi zitoke kwetu na watumishi wa Umma wengi wapande bure ?
 
Lkn kaa ukijua kazi zingine ni risk kuliko zingine, na haiwezekani tu kwa kuwa ni option basi watu waende kada zingine...hata asipochagua huyu atachagua mwingine mwisho wa siku walinzi lazima wawepo na ni lazima kuwapa vipaumbele kwa aina ya kazi wanayofanya na risk iliyopo...for instance police akiwa ndani ya sare ujue yupo kazini...so haiingii akilini anayekulinda tena akulipe...

!
!
Vipi kuhusu manesi?
 
Back
Top Bottom