Cv za wake za watu!

Marital status some times ina chanagia kupata ama kutopata kazi (kwa baadhi ya sehemu lkn),binafsi nilishawahi kukosa kazi kwa sabababu tu sijaoa na ilikuwa ni International Orgaznization (ilikuwa ni ya Switzerland)
 
Sasa kama hujui hata barua ya kuomba kazi inafananaje, ukiwa kama mwajiri uatakuwa unaajiri wafanyakazi kivipi?

Au wajarisimali hawaajiri in 200 years to come?

Naajiri mtu kwa ajili ya kufanya kazi hiyo kaka, mi najua kusoma cheque tu.
 
Hasa waajiriwa wa fesibuku, wote ni kompliketed

Wengine wanaweka - Marital status: Complicated.

Ukisoma CV nyingi za Watanzania utaishia kuziweka kwenye bin zote.
 
Reactions: EMT
so proud, so married!! hivi kuna watu wanaficha eeeeeeeeee?? lord have mercy!
 

Mkuu yepi yamekukuta Kamanda na kujikuta una Jump into that Conclusion ???
 
Well said
 
Nyani unaandika kama vile hizo standards uliziweka wewe. Sasa ujinga mkubwa sana wa kuweka hiyo hali ya kindoa ni nini?? Kaka si kila unalodhani ni sahihi kwako lazima liwe sahihi kwa wengine.

Marital status inahusikaje na uwezo wako wa kufanya kazi? Na unaajiriwa kwa sababu ya marital status au uwezo wa kufanya kazi?

Wekeni basi na vyama vyenu vya kisiasa bila kusahau makabila, dini, hobbies, magonjwa ya zinaa mlowahi kuyapata, na kadhalika.
 
Kwangu mimi akiandika single anachezea taraka sita na likizo ya miaka mitatu ili ale msoto na fedhea kitaa.
 
Hasa waajiriwa wa fesibuku, wote ni kompliketed

Unakuta kwenye CV yake kaandika yuko single, lakini ukienda kwenye fesibuku yake kaandika married.

Kwenye twita yake kaandika happily married with two very cute kids.

Hivi vyuo vyetu siku hizi vina career departments ambapo wanafunzi wanaelekezwa jinsi ya kuandika CV, nk?

Kuna waajiri wengine wakikutana na CV inayozidi kurasa mbili za A4 inaenda moja kwa moja kwenye bin la taka.

Kuna waajiri wengine wamechoshwa na CVs ambazo mara nyingi zinakuwa na irrelevant information na kuamua ku-design application forms ambazo zinataka tuu information ambazo mwajiri husika anazitaka.

Hizo form hazina sehemu ya kujaza marital status na blah blah nyingine zinazotetewa hapa. Tena zina-limit idadi ya meneno ya kujieleza kwenye kila swali ili kuondoa hizo blah blah.

Nilishasema ili hii nchi ijikomboe inabidi ijikomboe kwa kila kitu na si kwenye sihasa tuu. Ukisoma baadhi ya michango ya watu kwenye hii thread unaweza kupata hint ni kwa nini baadhi ya waajiri wanapendelea kuajiri foreigners.

Maana kama hayo ndiyo mambo wanayoweka kwenye CV zao, basi nyingi zitakuwa zinaishia kwenye bin la taka.
 
Sidhani kama kuna mahali mtu anafundishwa kuandika CV, labda huko kwenye communication au development studies.

Kuna mtu CV yake ni kama research report, kurasa nyingi, kila ukifika mwosho unasahau hata jina lake ni nani. Mie nikikutana na ya hivi kitu cha kwanza kinachonijia kichwani ni magumashi, anataka anichanganye nisijue hata qualifications zake zikoje.

Kwa kweli bado tuna safari ndefu sana, tunaandika vingi visivyohitajika wakati mwingine.

 
Reactions: EMT
Hivi vyuo vyetu siku hizi vina career departments ambapo wanafunzi wanaelekezwa jinsi ya kuandika CV, nk?

Hilo la career services dept. hata mimi nimeuliza sana watu lakini hakuna hata mmoja aliyesema zipo vyuoni. Sasa naelewa ni kwa nini watu wanaweka hayo madudu ambayo hata hayahusiki kabisa. Unaweka marital status, dini yako, na kabila lako.....like srlsly? Kaazi kweli kweli.

Kuna waajiri wengine wakikutana na CV inayozidi kurasa mbili za A4 inaenda moja kwa moja kwenye bin la taka.

Yaani uweke personal info kama hizo tena juu kwenye resume...hahahaa....kama mimi ndo hiring manager wala sitasumbuka na kuendelea kuisoma. Naidumbukiza kwenye shredder tu.

Nilishasema ili hii nchi ijikomboe inabidi ijikomboe kwa kila kitu na si kwenye sihasa tuu. Ukisoma baadhi ya michango ya watu kwenye hii thread unaweza kupata hint ni kwa nini baadhi ya waajiri wanapendelea kuajiri foreigners.

Sisi umakini ni sufuri kabisa aisee. Jambo tunaloliweza ni ubabaishaji tu. Na ndo maana unaona bado hatuna hata huduma za maji na umeme zenye uhakika ilhali nchi zingine huduma kama hizo siyo tatizo kabisa yaani.
 
Reactions: EMT
Sidhani kama kuna mahali mtu anafundishwa kuandika CV, labda huko kwenye communication au development studies.

Kwenye shule za wenzetu mnafundishwa jinsi ya kuandika hizo resumes, cover letter, na namna ya kufanya usaili kwa kutumia mock interviews.

Yaani ukimaliza shule kweli unakuwa umepikika na kama hujapikika basi tatizo ni lako mwenyewe na si kwamba hukufundishwa au huduma na rasilimali za kukusaidia hazikuwepo.

Professional resume unaweka marital status....utadhani unaweka profile kwenye dating site...good grief.
 
Vingine hata kama hukufundishwa inabidi ujifunze mwenyewe, na kwa msaada wa internet mambo yamerahisishwa sana mbona?

Kamamtu hajui, si basi angalau afanye hata homework ya kutafuta samples za CV kwa wengine? Hata kuperuzi tu kujua do's and don'ts mtandaoni. Kuna watu wanakwenda kwenye interview bila hata kutafuta taarifa za kampuni/kazi wanayoenda kufanyiwa usaili, hadi unabaki unashangaa mtu huyu alikuwa anafikiria nini.

 
Ngoja nikaangalie Cv yamama watoto wangu haraka!!Jana tu katoka kuipeleka ubalozi Fulani!!Naalivyo mrembo mpaka sijiaminiamini vile!!Mmenitisha nyie acha tu!!:A S confused::A S confused::A S confused::A S-frusty:
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…