CUF waishambulia CHADEMA

Nickname, that's called politics, mara nyingine lazima usimamie unachokiamini hata kama utachukiwa na wengi kama matokeo ya imani yako. Lakini ni wangapi kweli wanaoichukia CHADEMA? Mimi na watu wengine wengi sana tunaipenda CHADEMA! Mimba ya CUF itatoa "Si riziki". Subiri uone!
 
kama yepi ?

kukubali vyama viwili kuunda umoja na kuviona vyengine kwa kua na uwakilishi mdogo si wapinzani ?


chadema mtulie muache makeke


ngoma yataka matao
Kama matao yenyewe ni CUF basi hakuna haja ya kucheza hiyo ngoma.
 
Huyu hamad rashid hajui maana ya kumachua kwani amejengwa kwa misingi ya mawazo mgando. Leo hii watu wapo serious na mageuzi yeye analeta siasa za znz (siasa legevu) za mguu sawa mguu legeza. Kwanza ngoma ya upinzani jamani mnavyoiona kina tundu, wa kuongozwa na mtu mzembe mzembe kama huyu hamad? naomba mtutake radhi sisi tuliochagua chadema.
Pili- hamad anataka chadema wasuluhishwe na mbatia(kibaraka) wa cc.hem mtu ambaye amefungua kesi dhidi ya matokeo ya mdee,haamini wadada tena wadogo wamemtoa jasho la maana mpaka wazee wamemuonea soni na kumpa moyo.
Sasa mtu anayekufungulia kesi utaungana naye vipi? huu ndo unafoki ccm waliouzoea na cuf wanataka kuambukiza vyama vyote
 
Inasikitisha tunapoongelea mambo ya msingi watu wanakimbilia udini udini utafikiri kama ni waumini wa kweli!
Tukumbuke pia tulishaambiwa sio wote wanaokuja kwa gia ya upinzani ni wapinzani wa kweli,nafikiri mmeliona hilo wenyewe mara kibao.
Pia hii ndoa ya CUF kuolewa na CCM inabadilisha mwelekeo wa upinzani kwa upande wa CUF,hapo iko wazi na inatakiwa kama wapinzani wanashirikiana na CUF wawe makini na mienendo yao kwani wakicheza vibaya chama chao kinaweza kufa au kikatumiwa na ccm kuua upinzani.Kingine inaonyesha wazi CUF hawakupendezwa wao kupigwa kikumbo na chadema,sasa tukiangalia hayo na mengine mengi utaona wazi kwamba bora Chadema waendelee kivyao vyao,itakuwa uwendawazimu eti kumshirikisha Mrema kwenye kambi ukategemea mambo yaende sawa na ndio maana utasikia Chadema hawakutaka vyama vingine zaid ya CUF inaeleweka walimaanisha nini haikuwa lazima kutaja majina ya mbunge gani hawamuhitaji.
 

Kwa kutumia mfano wako wa Mwanamke Malaya CUF, Huoni kwamba CHADEMA ikiwa na uhusiano na huyu mwanamke malaya (CUF), Unajiweka katika mazingira hatarishi ya kuambukizwa maradhi ya Ukimwi(UFISADI) alionao Mume wa CUF ambae ni CCM? Sote tunajua CCM inaugua huu ugonjwa wa UFISADI ambao hauna kinga wata Tiba, Sasa iweje ushauri Chadema kuwa na uhusiano na Mwanamke Malaya(CUF) ambae ana uhusiano na Mgonjwa CCM?

Huoni kwamba hii itakua ni tiketi ya kujitakia ya kuambukizwa haka ka-ugonjwa?

Hii ni akili kweli?:nono:
 
Hakika nawaambia.
CUF hawajui lolote juu ya ndoa yao na CCM bali CCM wanajua fika wanachokitaka ktk ndoa hii.
Hamad naye kama zuzu anachekelea tu na ku'dance tune ya CCM.
Hamad akajifunze kutoka Kenya.
Akina Odinga wameunda serikali ya kitaifa lakini dhamila ya mapinduzi ipo pale pale hawadanganyiki na vijivyeo.
Niliwategemea sana CUF kule Zanzibar labda wangetuonyesha mfano kwa kuleta mapinduzi halisi kumbe zilikuwa njaa tu zile.
Nisije nikatukana, ngoja niishie hapa.
 
Nyie mlishaungana nao sisi hatuwataki hao.
 
Haya nakupa jibu kwa lugha hiyo hiyo:-

Sasa ulimtongoza wa nini kama unaogopa Ukimwi hali ukijua fika anatembea na CCM. Je, nia yako ilikuwa kulala naye tena?..
Kisha nachokisema mimi, sio lazima utembee naye kimwili ni urafiki na mahusiano ya mazungumzo pengine utamsaidia yeye na maradhi yake na pia kujua baadhi ya matatizo yake ikiwa ni pamoja na kukutonya wote walioambukizwa ukimwi na huyo CCM usije wavaa wewe kimapenzi..
 
Yaani Lipumba alishindwa hata kwao Tabora? Sasa atatwambia nini?:rip:cuf
 
Dua la kuku hilo wewe mwana CCM
 
Kwani mwanamke (CUF) anaruhusiwa kuwa kwenye ndoa mbili kwa wakati mmoja?
 

who the hell is cuf?? huyo rashid ni mnafiki sana katika chaguzi zote huko nyuma walikuwa hawamtambui salmin amour (1995) na karume (2000 & 2005) leo wameolewa na sisiemu ndo wanawageuka chadema, wanafiki wakubwa, warusi kwa zenji hatuwahitaji huku bara kwanza ndo wamejaa udini mtupu!
 
Mkandara huwa ninakuelewa na kukubaliana nawe kwa mambo mengi. Lakini samahani kwa hili sintakubaliana nalo na nasikitika kwamba unambebesha lawama Mbowe bila sababu kwa sababu na mimi ningekuwa mbowe ningechukua msimamo huo huo. Nina mashaka kwamba katika mkakati huu una agenda mbaya na Chadema na si bure.
Nimesema na narudia si vema kwa namna yoyote ile Chadema kuungana na CUF tena kwa hizi mbwembwe za CUF kila mmoja apambane kivyake. Nadhani hata ungeita msimamo huo wa Chadema kuwa ni wa Kishenzi bado nasisitiza si sawa chadema kuungana na CUF tena. Nadhani CUF ndio washenzi lakini Chadema ni wastaarabu.
 
CHADEMA wembe huo huo hakuna kuungana na mamluki CUF, tena sitaki kusikia habari ya mazungumzo ha hao waio na mbele wala nyuma achaneni nao kabisa. Ndumila kuwili hao watendeni mbali kabisa. CHADEMA inaweza bila msaada wa hao wala UROJO.:nono:
 
Kikwete na sera ya udini
Hivi leo nimesikia kikwete anasema kuna udini mkubwa sana hapa Tanzania na akaongea kwa msisitizo kabisa,guys is it true?
Ianzishie thread kwani nadhani this is not a right place to discuss these issues.

Hapa tuko kwenye issue za Rashid na muunganiko wa cuf na chadema
 
Jamani kumbe CHADEMA wana maadui wengi ,CUF wanakeraa sana ,toka waunde serikali (waolewe) na CCM wana nyodo sana.Sijui mimba inawasumbua?? Khaa!!!!!!!!:


I like this
 
Mkuu wangu nadhani bado kabisa hujanipata na wala hutaweza kunielewa ikiwa umeshindwa kunielewa hapo juu. Katika mfano wetu hapo juu nachosema mimi kwamba yale mahusiano baina ya Chadema na CUF yasipotee tu kwa sababu CUF ni mwanamke anayetafuta chake.

Chadema hawana sababu wala haja ya kuungana au kurudia mahusiano yake na CUF kama ilivyokuwa zamani, sipendi wala sipendekezi lakini kama wataweza kumweka hasira na wivu CCM Kisiasa basi ni pale Chadema watakapo onyesha wapo bado karibu na vyama vingine vya Upinzani na hasa CUF hata kama..

Kutokana na wivu wa mtandao hasa tunavyomjua jamaa yetu asiyependa kuona mazoea ya namna hii watalazimika kujiuliza mengi sana.

Kumbuka ikiwa Zitto leo mnamwekea mashaka sana kwa sababu yupo karibu na JK au kaunga mkono baadhi ya maswala ya JK,iweje kuwa vigumu kwenu pia kutumia mbinu hiyo hiyo ya CCM kuwaweka ktk mashaka?..Sikupenda kuandika mengi kuhusiana na hili isipokuwa kama mimi ningekuwa Mbowe na tumeweza kufika hapa tulipo na CUF, bado ningeelea kuwatumia ktk baadhi ya maswala tunayokubaliana nao na ningehakikisha zaidi nafahamu kila hatua ya mapatano yao na CCM zaidi ya wao kuyajua ya Chadema.

Labda nikutonye tu kwamba tazama baraza la mawaziri litakalo tangazwa, utashangazwa na mengi..
 
hamad rashid mnafiki mkubwa, hana lolote, mbona Znz yeye alikuwa wa Kwanza kutomtambua Karume kwa kutokushinda Urais, hadi Serikali ya umoja wa kitaifa ilipoundwa na kuua upinzani Znz ndio wakamtambua na CHADEMA wanafanya hivyo hivyo na hatutaki serikali ya kuunganisha CHADEMA na CCM, tulishinda kihalali, Hamad alitaka achaguliwe awe tena kiongozi wa upinzani bungeni kakosa, CHADEMA waliona huyu si mpinzani ni mkinzani, safiiiii, he is a scraper
 
Mkuu wangu uloyasema sii kweli, Chama kilichoshika nafasi ya pili ndicho chenye jukumu la kumchagua kiongozi wao wa Upinzani..walichokitaka CUF ni kushirikishwa vyama vyote vya Upinzani na sioni baya ikiwa ni kushirikishwa tu kuunda kambi..Elewa moja hawa wote wanataka Ulaji katika hayo mabaraza yatakayo undwa...Njaa babu njaa! bado hamjui tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…