CUF waishambulia CHADEMA

Ukitafakari kura za wagombea uwakilishi SADC kwa upande wa upinzani utagundua kuwa Wabunge wote wa CCM, NCCR, TLP, CUF etc walimpigia mgombea kupitia CUF. Hii inathibitisha kuwa CCM na CUF ni kitu kimoja na ndio sababu mgombea wa CUF alijitoa kugombea unaibu spika ili apate support ya CCM kwenye uwakilishi SADC:nono:
 
Mimi naona kwa hili kuwa kama Zanzibar vyama viwili ndio vimeungana serikari ya Kitaifa kwa nini wasihusishe na vyama vingine huko zenji?

Mundo, you have nailed it all mkuu; kama kweli Hamad Rashid anaiponda CHADEMA kwa kutotaka kushirikisha vyama vingine vya upinzani zaidi ya CUF wao CUF na CCM wangeshirikisha vyama vingine pia kuunda serikali huko Zanzibra, kitu ambacho CUF hawakukifanya huko Zanzibar kwa nini wanalazimisha kifanywe na CHADEMA huku Bara? UNAFIKI!

Hapa ninachoona, na kipo wazi ni kuwa CUF kipo kwa manufaa ya Wazanzibari zaidi na si Watanzania, wao wamepata huko Zanzibar ambapo ndipo walipopapigania hadi kumwaga damu basi hawana haja na ukombozi wa Watanganyika!
 
Hivi tatizo la CUF ni nini?
Hivi hawa CHADEMA SI NDIYO WALISEMA WAKIPEWA RIDHAA NA WANANCHI WATAUNDA
SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA?
Sawa ridhaa ya kambi ya upinzani wameipata kwanini wameshindwa kuunda kambi ya upinzani yenye sura ya kitaifa angalau kuonyesha kwamba walichokua wakikihubiri kwenye majukwaa ndiyo hicho wangekifanya?Kwani huu Muafaka wa CUF NA CCM UMEANZA LEO?Kwahiyo sioni sababu ya kuwaita CUF ni CCM B kwavile wametekeleza kile walichokubaliana na CCM ktk vikao walivyofanya na wala haikuwa siri.Afadhali huyo Hamadi ametoka hadharani na kueleza tatizo ambalo lina ukweli ndani yake kwasababu hakuna kiongozi mwenye dhamana kutoka chadema amelikanusha.kwanini chadema badala ya kujenga umoja wao wanaona ni bora wao peke yao kwa vile wanamajority ni haki yao lkn inadhoofisha kambi ya upinzani kwani sasa badala ya wao kupambana na adui yao CCM wameongeza maadui ndani ya bunge,Unajua ni rahisi tu kusema vyama vingine ni maamluki kwa kiujumla au kusema vyama vingine ni wabinafsi lkn wewe usiwe mbinafsi umefanya nini kuonyesha kwa vitendo kwamba si mbinafsi?Kama mambo yataendelea hivi kuna hatari huko mbeleni, watanzania wanafuatilia kwa makini kile walichowapa kama mwanzo wa uaminifu wao kwenu CHADEMA.Hivi kama haya anayoyasema Hamadi kuviunganisha vyama vingine ktk ushirikiano kuna ubaya gani?Au ndiyo lile bifu la ni wadogo ni sawa na sisimizi bado linaendelea.wapinzani futeni bifu zenu na onyesheni kujali umoja kwani umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu.
 
Hivi na CHADEMA Walipokuwa wanakampeni kama wakipewa ridhaa kuongoza wataunda serikali ya umoja au sura ya kitaifa walikuwa wanamaanisha nini?Na je hiyo serikali wangeiunda na watu kutoka vyama gani?
 
Masikini cuf wazee wa ngangari..poor thee!
 
Hivi karibuni kumekuwa na kasi ya wanasiasa wa Tanzania kupenda sifa za usomi hata kama hawakwenda shule, Mwanasiasa akiwa na SETIFICATI tu anajitutumua kama ana Shahada ya Uzamili. Sasa ukikuta ana shahada ya kwanza , basi atajiita DR.fulani wa fulani wakati anajua kabisa , hastahimili level hiyo ya usomi . Hii yote ni kutaka sifa za kipumbavu wakati watu wenyewe hawana tija, kazi kuiba kodi za walalahoi tu.

Nikupe mfano wa viongozi 2 ambao sijawahi kusikia wanaitwa kwa sifa zao ingawa ni akina Mama waliokwenda shule:-

1. Bi Condoleeza Rice ( PhD Holder)
2. Angela Merkel(PhD Holder)
Hawa wote hutajwa kwa kuanzia na neno Bi......... lakini Tanzania mwisho kero mtu hata hawezi kuandika Project Proposal anajiita Dr.
 
 
Muafaka ni wa CUF na CCM. Masharti ya muafaka wao imekuwa siri kati ya vyama hivyo viwili na hawakutaka kuvishirikisha vyama vingine hata kama walijua wasingeshiriki kwenye serikali ya Zanzibar kwani ni ukweli kuwa chama kisicho na wawakilishi isingekuwa rahisi kushirikishwa kwenye serikali. Haiwezekani CUF wajifanye wapinzani katika bunge la JMT, vinginevyo ni kujidanganya tu. Siamini kama Chadema wapo tayari kujidanganya.

TLP pia ni kujidanganya. Wote tunajua kipindi chote cha zaidi ya miaka miwili mwenyekiti wao ambaye bahati mbaya ndio mbunge mwenyewe alivyokuwa akifanya. Hatuhitaji kufafanua zaidi kuhusu huyu mzee wa kiraracha.

Checyo wa UDP..huyo huyo Mh. Hamad alimfukunza kwenye baraza lake kivuri kwa sababu ya unafiki wake, au anajifanya amesahau, basi tutamkumbusha.
NCCR...Mwenyekiti wao muda wote ameifanya Chadema kama ndio wapinzani wake wakuu hata kipindi ambacho chama chake hakikuwa na mbunge. Siku zote amekuwa akiponda hoja ya mafisadi, sasa utawashirikisha vipi watu wanaopingana nanyi katika mtizamo????

Ni kweli wengi watasema umoja ni nguvu, lakini siamini kama kwa umoja wa kinafiki utaweza kuleta nguvu.

Maoni yangu ni kuwa hata ikibidi CHADEMA wamtambue Kikwete lakini suala la kushirikiana na wapinzani mchwara halitakuwa jema kwa CHADEMA na kwa wapenda mageuzi kwa ujumla wake.
 
Jamani vyama vya upinzani,mwazo mzuri tumeuanza tupendane, tushirikiane tutawaondoa CCM madarakani, CCM wameungana wanabebana na sisi kambi ya upinzani tusibebane ila tulitete taifa letu
 
Mimi naona mambo matatu, kwanza kuwa ile mbegu ya udini aliyopanda Kikwete sasa inaanza kustawi, pili makombo toka kwenye meza y CCM sasa yameishibisha CUF mpaka imevimbiwa, tatu ile ndoa ya CCM na CUF sasa imejibu mimba changa ndiyo inawapa tabu CUF mpaka wanaweweseka.
 
cuf waweke mambo yao sawa kwanza kwa kuwa cuf zina mapande manne 1cuf mageuzi 2cuf upemba 3cuf udini 4cuf uccm tushirikiane na cuf ipi ili cuf ipi isichonge?maana kila cuf ina malengo yake....


ww mgonjwa

nani kakwambia kua cuf wanataka kushirikiana na chadema ?

chadema ndio walioomba kushirikiana na cuf lkn wengine watoswe cuf kachomoa
 
Katika siasa hakuna adui wala rafiki wa kudumu.
 
Cuf na chadema wote wamekosea.....................pia napenda kusahihisha jaama aliyesema chadema walisema wataunda umoja wa kitaifa.....! Hiyo ni kweli....ila hata wao kafu walisema hivyo......lakini angalia zanzibar ......umoja wa kitaifania cuf na ccm tu???????????????????????? '''tafakari chukua hatua''''
 
Jamani kumbe CHADEMA wana maadui wengi ,CUF wanakeraa sana ,toka waunde serikali(waolewe) na CCM wana nyodo sana.Sijui mimba inawasumbua?? Khaa!!!!!!!!:angry:

Ho tayari wameisha bebeshwa mimba na ukimwi juuu, kazi kwao kusuka au kunyoa tena watapigwa changa la macho baya sana 2015
 
Napata Wakati mgumu sana ni wapi democrasia ya kweli tunaipeleka CUF Ni chama kilichokubalina na CCMkuendesha Serikali ya pamoja Zanzibar leo tena kije kuungana na CHADEMA ilikufanya kazi pamoja YA UPINZANI BUNGENI.CUF inasimamia wapi kukosoa Kazi zake inayotekeleza kikiwa madarakani ama kusaidia kutekeleza Ilani ya CCM kama walivyokubali Zanzibarkwa ni sitashangaa kusikia JK akimteua Waziri toka CUF kwani ni wamoja hao.MKINISAIDIA HAPO BASI NITAJUA CHADEMA wanatakiwa kusimama upande wa CUF ama peke yao?
 
Loud and clear... CUF wameamua kuwa wanafiki... lakini cha maana ni chadema kurudi kambini na kupanga upya mambo yao

Thanks for the post

Mkuu walirudi kambini, ipi hiyo. Kwa jinsi mambo yalivyojiri CUF hawako kambi moja na Chadema na Chadema wakisisitiza kufanya nao kazi pamoja hakika watadhoofu kuelekea 2015. Fikiria " ".
 
Juzi wakati Mhe. Mohamed Habi Mnyaa alipokuwa anatangaza nia yake ya kujiondoa katika kinyanganyiro cha unaibu Spika alitamka wazi wazi kwamba anajiondoa kufuatia maridhiano kati ya CUF na CCM (Zanzibar) na anaweka jina lake kwenye kinyanganyiro cha Ubunge wa SADC. Kama ilivyotegemewa wabunge wote wa CCM walimpigia Mnyaa kura na amepita. Hivi sasa CUF na CCM lao ni moja. CUF wana bifu na CHADEMA kwa vile chama chao "is on the decaying trend" huku Tanzania Bara kiasi cha kupitwa na NCCR-Mageuzi katika viti vya ubunge. Prof. Lipumba amekosa kupta hata kura Milioni moja katika uchaguzi hata katika maeneo yanayowaunga mkono CUF! The writting is on the wall. CUF kitabaki chama cha visiwani.
 
Kwani na CUF bado ni wapinzani au? Si nimemwona yule kiongozi wao,SEIF akikaa kama serikali ktk hafla ya Pinda leo? Au kuna serikali nusu inajipinga na nusu ndo serikali ? Mbona upuuzi unazidi? Hamad rashidi wewe si mpinzani tena,kaa ujielewe! Hii ni sawa na kusali kanisani alaf unajiita ustadhi!!!
 
JUma Duni Haji Waziri wa....... ndani Serikali ipi!!!

CUF = CCM
 

Kazi nzuri hii, CUF=TLP=CCM hawa wanataka kuivuraga chadema na wanatumiwa makusudi kabisa Wana JF nazani lazima tutumie uwezo wetu kuwaeleza ndugu zetu huu uovu wa CUF kutaka kushirikiana na CCM kuliangamiza taifa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…