CoW yazidi kusambaratika

CoW yazidi kusambaratika

Konda wa bodaboda Asante kwa kuniita huku japo naona kama ni mipasho tu na hamna chochote humu mnachojadili kinachohitaji matumizi ya akili. Kuna mambo kadhaa nafaa kuyaweka bayana hapa.
- Mgogoro baina ya Kenya na Uganda kuhusu hilo eneo la Migingo haujaanza jana, ni jambo ambalo huwa linaendelea kutatuliwa, uhusiano wetu na Uganda upo thabiti haswa kibiashara.

- Hilo la bomba, Waganda wana haki ya kuchagua eneo ambalo halitawapa wasiwasi kwenye gharama na usalama. Hivyo tunahitaji kuwahakikishia hayo au waende kwingine. Hii ni biashara na kama nisemavyo kila siku humu, hamna cha undugu kwenye biashara ila maslahi. Ujio wa Waganda huko Tanzania ni kwa sababu ya mahesabu yao na ikitokea sisi Wakenya tumeshindwa kuwadhihirishia matakwa yao, basi wapo radhi kuchagua wanakotaka.
Kuna kikao kitafanyika ndani ya siku kumi baina ya Waganda na Wakenya kujaribu kuona kama tunaweza afikiana kwenye hili, sasa hivi tayari tuna bomba kuanzia Eldoret hadi Mombasa, hivyo tunaweza waambia Waganda kwamba tutengeneze bomba la kuunga hili ambalo lipo tayari, kimsingi tutajaribu kuwahakikishia na kurekebisha kilicho wafanya watelekeze mkataba wa hapo awali baina yetu. Lakini ikishindikana basi tunaachia bila majungu, nothing personal, hii ni biashara tu.

- Muungano wa CoW upo kwa ajili ya maslahi, hamna cha undugu wala nini, dunia ya sasa haitaki maisha ya kusuasua na uwoga uwoga, maamuzi lazima ufanye kwa haraka maana hamna muda tena. Miaka ya hapo awali ilikua rahisi kuwa wavivu na kulalia maskio, lakini huo muda haupo tena.

Na ndio unaona hata rais wenu Magufuli hilo ameshalijua na hazubai tena, uchaguzi uliofanyika huko kwenu uliwadhihirishia viongozi wa CCM kwamba wananchi wamechoka na maisha ya umaskini wakati wana raslimali za kila aina. Kila siku wimbo ni ule ule, Tanzania ina ardhi nyingi zaidi ya mataifa yote EAC, ina madini, ina vivutio bora, ina bandari kubwa, maziwa na bahari n.k lakini bado inatajwa kwenye orodha ya nchi maskini wa kutupwa, huku ikihangaika kushindana na nchi ndogo ndogo kama Kenya.

CCM waliponea kwenye tundu la sindano maana walitumia nguvu nyingi sana kurejea kwenye madaraka. Hata kule Zanzibar bado wanayumba tu, wamelazimika kuwajaza wanajeshi kila kona.

Cha msingi, ifahamike muungano wa CoW upo kwa ajili ya kuharakisha yale tunayoyaweza na kuachia yale magumu hadi baadaye. Na sio lazima kila tutakachoanzisha kifaulu kwa mpigo mmoja tu, patakua na changamoto kadhaa mwanzoni, lakini taratibu tutazirekebisha tu. Hivi sasa DRC na Ethiopia tayari wameanza mikakati ya kujiunga na huu muungano, maana kila yeyote amekaribishwa na kujiunga na chochote humo atakacho ona kinamfaa, sio lazima uratibishe kila kitu, tunakuachia ujiunge na kitakachokufaidi, humu hatuna mambo ya undugu, hata Magufuli mwenyewe alishasema yupo tayari kuihusisha nchi yake kwenye hii miradi ya CoW.

Sasa hivi tupo mbioni kumfikishia Kagame reli ya SGR itakayowezesha mizigo kufika Kigali ndani ya masaa 24. ujenzi tayari unafanywa kwa spidi ya kufa mtu. Hiyo reli hatimaye itaunga hadi kule Burundi na DRC, na pia itakua ya msaada sana kwa wajasiria wa Tanzania Kaskazini. Hatuna muda wa kupoteza.
Unazungumziaje kuhusu suala la ardhi kwenye shirikisho ukizingatia kwamba ni Tanzania na Kenya pekee ndizo nchi zenye ardhi kubwa kuliko zote ndani ya shirikisho. Mkuu Ngongo amesema kwamba kuna baadhi ya nchi zinataka raia wao wawe na haki sawa ya kumiliki ardhi sawa na raia wa nchi yenye ardhi kubwa, nini maoni yako?
 
Unazungumziaje kuhusu suala la ardhi kwenye shirikisho ukizingatia kwamba ni Tanzania na Kenya pekee ndizo nchi zenye ardhi kubwa kuliko zote ndani ya shirikisho. Mkuu Ngongo amesema kwamba kuna baadhi ya nchi zinataka raia wao wawe na haki sawa ya kumiliki ardhi sawa na raia wa nchi yenye ardhi kubwa, nini maoni yako?

Mambo yapo mengi ya kuungana na sio lazima tuungane kwenye ardhi, fahamu kwenye CoW kila mshirika ana uhuru wa kuchagua asichotaka kuhusishwa nacho, na kuunga kwenye kinachomfaidi. Huwezi kununa kwa kila kitu kisa ardhi, kila ukiombwa na kuagizwa tuungane kwenye mengine kama elimu, miundo mbinu, biashara n.k. unanuna eti ardhi ardhi.

Cha msingi na muhimu ni kuwa na sera nzuri za ardhi, hata usipoungana na wenzio lakini uwe na sera mbovu, bado hiyo ardhi yako italiwa na kutafunwa tu. Hapo Tanzania nimeona jinsi wageni kutoka mbali wanavyomega ardhi, ilmradi wana hela za kumwaga. Wawekezaji wageni kutoka mbali wamenunua ardhi nyingi sana halafu badala ya kuwekeza, wanatumia kupata mikopo, huo ni mfano mmoja tu, ila kuna mengi yanafanyika.

Hivyo, ukigoma kuungana na wenzio kisa unataka kuwabana kwenye masuala ya ardhi halafu mwenyewe una sera mbovu na ufisadi kiasi kwamba Mwarabu na Muhindi anatua na mkoba wake na kufanya yake, utakua hujafanya chochote.
 
Mambo yapo mengi ya kuungana na sio lazima tuungane kwenye ardhi, fahamu kwenye CoW kila mshirika ana uhuru wa kuchagua asichotaka kuhusishwa nacho, na kuunga kwenye kinachomfaidi. Huwezi kununa kwa kila kitu kisa ardhi, kila ukiombwa na kuagizwa tuungane kwenye mengine kama elimu, miundo mbinu, biashara n.k. unanuna eti ardhi ardhi.

Cha msingi na muhimu ni kuwa na sera nzuri za ardhi, hata usipoungana na wenzio lakini uwe na sera mbovu, bado hiyo ardhi yako italiwa na kutafunwa tu. Hapo Tanzania nimeona jinsi wageni kutoka mbali wanavyomega ardhi, ilmradi wana hela za kumwaga. Wawekezaji wageni kutoka mbali wamenunua ardhi nyingi sana halafu badala ya kuwekeza, wanatumia kupata mikopo, huo ni mfano mmoja tu, ila kuna mengi yanafanyika.

Hivyo, ukigoma kuungana na wenzio kisa unataka kuwabana kwenye masuala ya ardhi halafu mwenyewe una sera mbovu na ufisadi kiasi kwamba Mwarabu na Muhindi anatua na mkoba wake na kufanya yake, utakua hujafanya chochote.
Vipi Kenya mkuu, nasikia kuna matajiri wakubwa wanamiliki ardhi kubwa huku wananchi wakikosa ardhi ya kilimo na shughuli za makazi
 
Vipi Kenya mkuu, nasikia kuna matajiri wakubwa wanamiliki ardhi kubwa huku wananchi wakikosa ardhi ya kilimo na shughuli za makazi

Kenya tulishakubali tuna matatizo ya kihistoria ya ardhi na tumeboresha sera haswa kwenye katiba mpya.
Mambo mengi yamefanyika na tunaendelea kuboresha. Serikali inanunua ardhi na kuwagawia raia. Mfano ni ile ardhi ya Waitiki.
 
Kenya tulishakubali tuna matatizo ya kihistoria ya ardhi na tumeboresha sera haswa kwenye katiba mpya.
Mambo mengi yamefanyika na tunaendelea kuboresha. Serikali inanunua ardhi na kuwagawia raia. Mfano ni ile ardhi ya Waitiki.

Kachukueni ardhi kwa Kenyatta.
 
Kachukueni ardhi kwa Kenyatta.

Kama wewe mfuatiliaji wa taarifa za Kenya utaona kwamba tayari na hiyo pia tunaimega japo taratibu. Kadiri muda unavyoenda na changamoto zinavyozidi kuongezeka, familia ya Kenyatta watajikuta wameachia pia. Rais Uhuru alishasema mwenyewe hana usemi kuhusu hiyo ardhi maana ni ya familia na yeye kama mmojawapo wa wana wa hiyo familia hawezi fanya maamuzi binafsi bila kuwaomba wengine.

Kwa mfano leo hii haiwezekani mwana mmoja wa aliyekua rais Mkapa au Mwinyi akafanya maamuzi juu ya mali ya familia yote ya Mkapa. Hapa kwetu Uhuru anabanwa na sheria na mfumo, lakini taratibu hiyo ardhi itatwaliwa tu, vijana wanazaliwa kila siku wasiokua na subira na ambao hawajui wala kufahamu michango ya hayati marehemu Kenyatta, hivyo hawataendelea kuvumilia umaskini wakati wanaona kuna familia zenye ardhi kubwa kubwa.

Cha msingi ni kwamba, imetuchukua muda mrefu kuboresha sera za mambo ya ardhi. Tumeweka nguzo zote muhimu na kuhakikisha jamii itanufaika pakubwa na mifumo yetu ya ardhi. Na kama nilivyotaja, serikali tayari inanunua ardhi kubwa kubwa na kuwagawia raia maskini.
 
Kama wewe mfuatiliaji wa taarifa za Kenya utaona kwamba tayari na hiyo pia tunaimega japo taratibu. Kadiri muda unavyoenda na changamoto zinavyozidi kuongezeka, familia ya Kenyatta watajikuta wameachia pia. Rais Uhuru alishasema mwenyewe hana usemi kuhusu hiyo ardhi maana ni ya familia na yeye kama mmojawapo wa wana wa hiyo familia hawezi fanya maamuzi binafsi bila kuwaomba wengine.

Kwa mfano leo hii haiwezekani mwana mmoja wa aliyekua rais Mkapa au Mwinyi akafanya maamuzi juu ya mali ya familia yote ya Mkapa. Hapa kwetu Uhuru anabanwa na sheria na mfumo, lakini taratibu hiyo ardhi itatwaliwa tu, vijana wanazaliwa kila siku wasiokua na subira na ambao hawajui wala kufahamu michango ya hayati marehemu Kenyatta, hivyo hawataendelea kuvumilia umaskini wakati wanaona kuna familia zenye ardhi kubwa kubwa.

Cha msingi ni kwamba, imetuchukua muda mrefu kuboresha sera za mambo ya ardhi. Tumeweka nguzo zote muhimu na kuhakikisha jamii itanufaika pakubwa na mifumo yetu ya ardhi. Na kama nilivyotaja, serikali tayari inanunua ardhi kubwa kubwa na kuwagawia raia maskini.

Kenya bado sana. Serikali haina sauti kwenye ardhi za watu binafsi.
 
Ifahamike rasmi Burundi ni mshirika mtiifu kwa Tanzania yanapokuja maswala ya EAC.Hivyo Katibu Mkuu raia wa Burundi ni pigo kubwa sana kwa muungano wa CoW

Mkuu Ngongo kuna wakati nilifikiria Burundi ikiungana na Tanzania lingekuwa jambo jema sana, actually Burundi na Tanzania gotta lot in common, tuungane kama ilivyo Zanzibar wao wawe na Serikali yao na kujihamlia mambo yao. Hayo ni maoni yangu.
 
Mkuu Ngongo kuna wakati nilifikiria Burundi ikiungana na Tanzania lingekuwa jambo jema sana, actually Burundi na Tanzania gotta lot in common, tuungane kama ilivyo Zanzibar wao wawe na Serikali yao na kujihamlia mambo yao. Hayo ni maoni yangu.

Mkuu Bukyanagandi muungano na Tanzania unaweza kumaliza matatizo yao ya kikabila.Zanzibar bila Tanganyika hali ingekuwa mbaya kuliko Burundi ya leo.
 
Walikuwa Na Muunga no wa kinafiki
Tanzania nimtakuja tu
Na kujibaragqzua koote lakini watatulia
MK254
 
Mkuu asigwa unajua M7 ana ndoto za urais wa EAC kila akipiga hesabu zake Tanzania imekuwa kikwazo kwake haitaki mambo ya haraka haraka hii ndio sababu kuu ya Uganda kupendelea CoW yenye malengo ya kupeleka mambo haraka haraka kabla M7 ajatwaliwa na Mungu hasa tukizingatia umri wake umekwenda kilometa nyingi sana.

Kenyatta na Kenya wanataka kutawala biashara ya bidhaa za viwandani kwakuwa wana viwanda vingi ukilinganisha na nchi nyingine za EA hawajali nani atakuwa kiongozi mradi mambo yao yanakwenda vizuri

Rwanda inataka ardhi na usalama katika jumuiya.Mambo hayo yanakinzwa na katazo la Tanzania kukatalia ardhi yake huku Rwanda ikilemewa na wingi wa watu na uhaba mkubwa wa ardhi.Kitendo cha Tanzania kupeleka majeshi yake Congo DRC kulikata mirija yake ya wizi wa rasilimali za Congo mambo yote haya yalichangia Kagame kuichukia Tanzania na hasa Kikwete.
MK254
 
Mkuu kwanini ni Rwanda tu iwe na ardhi ndogo na sio Burundi na Uganda kwa pamoja? Je wanakabiliana vipi na hali hiyo ya ukosefu wa ardhi, au ndio kuwahamisha raia wao kuja kwetu Tanzania kwa mwamvuli wa wakimbizi?
Wanataka kujitanua kama Israel
Kitu ambacho hakiwezekani
 
Mkuu Uganda sidhani kama ina matatizo ya ardhi, kinachoikabili Uganda ni uchumi mbovu na waasi kaskazini mwa nchi.

Burundi tatizo la ardhi analo lakini ameshajiridhikia na matatizo yake na Rais wao ni Mlokole mzuri tu, kifupi keshajijua yeye ni mnyonge na amekubali unyonge wake.

Rwanda yeye ni kichwa ngumu, tatizo la ardhi analo kubwa mno na anatafuta njia mbadala wa ardhi, mkakati ulikua ni kuimega Congo na ukabuma, Tanzania ni pamoto sana huu mkakati wa kuimega hauwezekani.
Tena asije kurogwa kujaribu upuzi huo
Naamini itakuwa kiama kwake
 
Mkuu Ngongo kuna wakati nilifikiria Burundi ikiungana na Tanzania lingekuwa jambo jema sana, actually Burundi na Tanzania gotta lot in common, tuungane kama ilivyo Zanzibar wao wawe na Serikali yao na kujihamlia mambo yao. Hayo ni maoni yangu.
Mkuu huo muungano unadhani ungekuwa na makubaliano gani kwa sababu tayari umesema watakuwa na serikali yao?
 
mada tamu sana napenda sana wakuu mnavyotingishana kwa hoja
 
Mkuu huo muungano unadhani ungekuwa na makubaliano gani kwa sababu tayari umesema watakuwa na serikali yao?

Mkuu kwani muungano wa sisi na Zanzibar huko je, mbano wana Serikali yao? Burundi wanaweza kufuata mkondo huo huo, muugano utawapa bonasi ya ziada in terms of usalama, ulinzi, kupunguza msuguano wa kikabila unao chochewa na majirani zao etc.
 
Mkuu kwani muungano wa sisi na Zanzibar huko je, mbano wana Serikali yao? Burundi wanaweza kufuata mkondo huo huo, muugano utawapa bonasi ya ziada in terms of usalama, ulinzi, kupunguza msuguano wa kikabila unao chochewa na majirani zao etc.
Hilo linawezekana mkuu, lakini kumbuka population ya Zanzibar ni 1.5Millions wakati warundi ni almost 12Millions ambao ni kama robo ya Watanzania wote millioni 48.
Tukiwabeba warundi kuwaingiza huku kwetu tunakua tumebebamzigo mkubwa sana wa watu ambao sidhani kama ardhi yetu inaweza kuwa accomodate.

Kumbuka hawa jamaa ni wafugaji kama walivyo wamasai, sasa kama wamasai wasiofika millioni 2 tu wanatupa headache kwa migogoro ya wakulima na wafugaji kila siku Morogoro huko, tukibeba load ya 12Millions inkuwaje??
Maana yake ni kuwa tutakuwa tumekuza migogoro ya wakulima na wafugaji kama mara 6 hivi
 
Hilo linawezekana mkuu, lakini kumbuka population ya Zanzibar ni 1.5Millions wakati warundi ni almost 12Millions ambao ni kama robo ya Watanzania wote millioni 48.
Tukiwabeba warundi kuwaingiza huku kwetu tunakua tumebebamzigo mkubwa sana wa watu ambao sidhani kama ardhi yetu inaweza kuwa accomodate.

Kumbuka hawa jamaa ni wafugaji kama walivyo wamasai, sasa kama wamasai wasiofika millioni 2 tu wanatupa headache kwa migogoro ya wakulima na wafugaji kila siku Morogoro huko, tukibeba load ya 12Millions inkuwaje??
Maana yake ni kuwa tutakuwa tumekuza migogoro ya wakulima na wafugaji kama mara 6 hivi

Mkuu asigwa ni kweli tukiungana na Burundi zipo athari zake lakini pia zipo faida zake.Yafaa wataalam wa uchumi,jamii na siasa wakafanya uchambuzi wa kina kupima hizo faida na hasara lakini kubwa zaidi ni utayari wa warundi na wataganyika wenyewe kuungana na si kulazimisha kama ilivyo Zanzibar.Mwaka 2011 tulitoa uraia kwa wakimbizi 8000 wa Rwanda na Burundi,Mwaka juzi tulitoa uraia 1,500 wakimbizi wa kisomali wapo kule Handeni Tanga mwaka jana tulitoa uraia kwa warundi 162 na bado zipo dalili ya kuendelea na zoezi la kugawa uraia kila mwaka hasa nchi zenye matatizo ya usalama kama Burundi na Congo DRC.
 
Back
Top Bottom