MK254
JF-Expert Member
- May 11, 2013
- 33,569
- 53,583
Huwezi kuweka hoja bila kusema mambo ya ujamaa?
Subiri mjamaa Magufuli atakavyowaonesha.
Bavaria samahani lakini ninapojadili na Mtanzania, haswa wazee wazee wale hawajatoka nje ya Tz huwa inabidi niwaelewe kwa wao kushirikisha kila kitu kwa mtazamo wa ujamaa. Utakuta mnapojadili biashara za kimataifa na mahesabu yake, anahusisha mambo ya undugu na fadhila humo.
Dunia ya sasa haipo huko tena, mambo yanaendeshwa kiubepari na unyang'au, na ndio naona rais wenu Magufuli amefaulu kuiga kabisa mfumo wa ubepari. Haswa jinsi anavyowafuta watu huko bila kujali undugu wala nini, yeye anatumbua tu. Pia naona amefaulu kutupiga mieleka ya kiunyang'au kwenye hili la bomba, hakupoteza muda alipokutana na Museveni, ni kama alimpiga ambush hivi. Huo ndio tunaita unyang'au, dunia ya sasa inataka kuendeshwa hivyo.
Kwa kweli huyo rais wenu anaridhisha kwa jinsi anavyotenda kazi, japo naona kidogo amepiga breki kwa issue ya juzi ya January Makamba. Nilitaka nione hatua atakayochukua pale ngoma imemfikia kwa mtu wake wa karibu. Huyo dogo Makamba naona anataka kumuaibisha mzee Yusuf Makamba ambaye niliishi sana kwenye hoteli yake Morogoro, na alitupokea binafsi kwa heshima na alituchekesha sana kila siku. Sasa dogo anakua waziri wa kwanza kutajwa kwenye kasha ndani ya hii awamu ya tano.