Covid-19: Ugonjwa wa Corona ushauri wa bure kwako Rais Magufuli

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,846
35,851
Moja kwa moja kwako kwenye mada.

Hatimaye ninakundikia wewe ushauri huu wa bure nikifahamu fika kuwa hujapungukiwa na washauri, na kuwa uko nao washauri walio mahiri kabisa, wenye kulipwa vilivyo kutokana na kazi hiyo.

Hata hivyo kumbuka mheshimiwa, Goliath lilikuwa jitu la kutisha (lenye silaha hatari) ambalo kwa uweza wake mola lilisimamishwa ni kijana mdogo aliyekuwa na kombeo na jiwe tu, zana duni kabisa.

Kwa taarifa zilizopo hadi sasa katika Afrika peke yake watu wapatao 109 tayari wamesha kufa kwa covid-19 na hii inaendelea kuongezeka kwa kasi kubwa zaidi:

COVID-19: Coronavirus hits 46 countries in Africa, kills 109 people

Italy pana wahanga zaidi ya 10,000 waliokwisha kufa hadi sasa. New York peke yake ni wahanga zaidi ya 1,000. China wao wametangaza rasmi kufanikiwa kuutokomeza ugonjwa huu.

WHO wanaonya kuwa katika wiki tatu zijazo tokea sasa tunaweza kuiona Afrika ikiwa katika hali mbaya sana. Labda hata kuwa ni mbaya zaidi kuhusiana na ugonjwa huu kuliko hata ilivyo ulaya na marekani kwa sasa. Hii ni kama hatua thabiti kabisa hazitachukuliwa pasipo na kuchelewa zaidi.. WHO wanazo sababu za kutosha kabisa kuendelea kutoa maonyo haya.

WHO wanasisitiza umuhimu wa 'social distancing' yaani kuwatenga watu walio wazima na walio waathirika ili hatua zichukuliwe. Hii ikiwa ndiyo njia pekee iliyozaa ushindi na kuonekana kisayansi kuwa sahihi zaidi.

Hii ni vita kubwa wala si ndogo na wewe ndiye jemedari wetu.

Walioambukizwa Uingereza ni pamoja na Malkia Elizabeth, Prince Charles, waziri mkuu Boris Johnson (watu wazito kabisa) na wengi wengine mashuhuri na hohehahe, wakubwa kwa wadogo duniani kote.

Ugonjwa huu unaweza kumpata mtu yeyote na wakati wowote.

Ugonjwa huu unatishia kwa dhahiri kabisa uwepo wetu kama taifa. Muda wa kuchukua hatua ni sasa kabla hatujachelewa mno.

Wapo wenzetu tunao fanana nao katika mazingira kama yetu kuweza kujipanga hata kuamua ya nini cha kufanya katika namna inavyofahamika zaidi kuliko kusubiria zahama hili linalokuja litufikie tukiwa tumemwachia Mungu. Kumwachia Mungu hakuna maana ya kutochukua hatua.

Kwa hali inavyokwenda mkuu, ilikuwa vyema ukarejea Dar es salaam au Dodoma (yaliko makazi yako rasmi) kwa ajili ya kuongoza mapambano haya sasa wewe mwenyewe.

Mikusanyiko yote kila mmoja kwa jina lake ni muda wa kuisitisha sasa. Hivi vijiwe vyote, viwe vya kahawa au tangawizi ni muda wa kuvifunga maana vinachangia mikusanyiko ambayo ndiyo njia kuu ya maambukizi.

Mkuu, penye nia pana njia. Tutie nia pamoja sote kama taifa tutashinda.
 
Sioni implementation ya maana ya kuzuia mikusanyiko, juzi na jana nimeona huku kwetu watu wamejazana kwenye mnada wanarushiana nguo kutoka kwenye magari, kuna baadhi ya makanisa ya walokole bado wanaendelea na mikusanyiko ya ibada, watu bado wanaenda kwenye mishe zao na daladala zinajaza kama kawaida, hapa ni Mungu tu atuepushe na madhara makubwa..
 
Acha kwanza kitu kinoge kwanza mzee. Africa hatujazoea kuchukua hatua vitu vikiwa na impact ndogo, acha kwanza kitu inonge, karata ni hiyo tu.

Hata tufanyeje hatuna rasimali za kusimamia ipasavyo

Mimi napendekeza raisi atangaze wanaotaka lockdown mikono juu na wanaotaka shuguli ziendelee kwa tahadhari mikono juu, wengi wape!

Hapo ataepuka lawama.
 
Sioni implementation ya maana ya kuzuia mikusanyiko, juzi na jana nimeona huku kwetu watu wamejazana kwenye mnada wanarushiana nguo kutoka kwenye magari, kuna baadhi ya makanisa ya walokole bado wanaendelea na mikusanyiko ya ibada, watu bado wanaenda kwenye mishe zao na daladala zinajaza kama kawaida, hapa ni Mungu tu atuepushe na madhara makubwa..

Hii Vita mheshimiwa rais inabidi akaisimamie na kuiondosha mwenyewe.

Mikusanyiko ni lazima ikome.

Haya ya ficha ficha kwenye huu ugonjwa ni wakati wa kuyaweka sawa.
 
Acha kwanza kitu kinoge kwanza mzee. Africa hatujazoea kuchukua hatua vitu vikiwa na impact ndogo, acha kwanza kitu inonge, karata ni hiyo tu.

Hata tufanyeje hatuna rasimali za kusimamia ipasavyo

Mimi napendekeza raisi atangaze wanaotaka lockdown mikono juu na wanaotaka shuguli ziendelee kwa tahadhari mikono juu, wengi wape!

Hapo ataepuka lawama.
Hahahaha
Sasa itasaidia nn
Lockdown watakuwa wachache
Na bahati mbaya hakuna pakukimbilia
Kikinuka Ni humu humu
 
Tuna wajuaji wengi sana, alafu acha kumhusisha Mungu kwenye hofu zako.
Nakuomba,
Kama UNATAKA lockdown si uanze kwani umekatazwa?

Iyo misongamano ya watu uliionaje Kaka sio wewe unayeongeza misongamano mtaani.

Watu tuache KULALAMIKA, haturidhiki,

Unataka lockdown anza kujifungia leo kwani utakamatwa? Tatzo uzi wako umeuandika kikejeli sana.

Kwaiyo unataka kutuambia nchi za ulaya ambazo wako watu wanapukutika daily serikali zao zilifanya uzembe?

Njooo hapa New York uone watu walivo lockdown lakn maambukizi Ni mbele kwa mbele.

Watu Kama nyie ndo wale mliambiwa na Gidion kurudi nyuma wakati akienda kupigana vita, (heri kwenda na watu wachache wenye ushujaa kuliko kwenda na maelfu wenye hofu)

Kwaiyo mwisho wa siku unataka useme jitihada za serikali ndo zimeisaidia kuiondoa Corona? Tanzania ina rasilimali gani za kupambana na Corona? Juzi unajua USA imesaidi Dolla biliobi ngapi za kupambana na ugonjwa lakn Bado?

Jana ulishuhudia wanachi wa Rwanda walioko lockdown wakigombania unga wa msaada?

Ushauri wangu kwako;: Tuache KULALAMIKA juu ya maamuzi ya serikali kwani ndio ukomavu wa imani pia serikali inaepuka kufanya maamuzi bila kuangalia side effects!

Lockdown inaanza na wwe mwenyewe.
 
Hili gonjwa kwa hali inayoendelea sasa nchini kwetu kila mtu ashinde mechi zake, ukiona inafaa kujilockdown fanya hivyo, ukiona haifai fanya vinginevyo, nadhani ni vyema kila mtu kuanza action na nafsi yake na watu wanaomzunguka (familia).
 
Tumia limao, chumvi na maji ya moto mara 3 kwa siku au zaidi, corona itakwisha yenyewe, fanya hivyo mara uonapo dalili kisha wahi hospitali.
 
  • Thanks
Reactions: UCD
Acha kwanza kitu kinoge kwanza mzee. Africa hatujazoea kuchukua hatua vitu vikiwa na impact ndogo, acha kwanza kitu inonge, karata ni hiyo tu.

Hata tufanyeje hatuna rasimali za kusimamia ipasavyo

Mimi napendekeza raisi atangaze wanaotaka lockdown mikono juu na wanaotaka shuguli ziendelee kwa tahadhari mikono juu, wengi wape!

Hapo ataepuka lawama.

Mkuu, hata hivyo tatizlo la kura ni kuwa 1+1 = 2 bila kujali wasiojua wangapi wanasema 1+1 = 4.
 
me naona tuachane na lockdown sijui knockdown maana hata waliofanya lockdown haijawasadia sisi tuendelee kuchapa kazi atakayeambukizwa aambukizwe watakaobahatika kubaki wataendeleza kizazi
after all hatuiishi milele
 
Hahahaha
Sasa itasaidia nn
Lockdown watakuwa wachache
Na bahati mbaya hakuna pakukimbilia
Kikinuka Ni humu humu

Yeah hivyo hivyo Raisi akitoa hivyo ataepuka lawama kuliko sasa, maana wananchi watakuwa wamechagua wenyewe
 
Hili gonjwa kwa hali inayoendelea sasa nchini kwetu kila mtu ashinde mechi zake, ukiona inafaa kujilockdown fanya hivyo, ukiona haifai fanya vinginevyo, nadhani ni vyema kila mtu kuanza action na nafsi yake na watu wanaomzunguka (familia).
Unaji lockdown vipi mkuu wakati unatakiwa uwepo kazini, na unajua maofisi yetu yalivyojaa majungu. utasikia hataki kuja kazini kwa makusudi, anajiona kibosile..
 
Hamna baya litakalo tukuta mungu anatulinda pia kuhusu kuchukua tahadhar. Tumesha chukua ndiomana tunanawa kila muda pili Sio sababu who wamesema ndio sisi tufate mbona kwenye Ebola waliongea mengi ya kutisha kushinda haya wanayo ongea sasaiv sis nch tumesha mkabidh mungu pia hao WHO wanatumiwa na shetan kuzivunja Iman zetu ambazo ndio Kinga zetu ili tu shetan atutawale
 
Angalia hapo
20200330-110114~2.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe unataka wafunge vijiwe vya kahawa ili waje kula kwako? Cha muhimu ni kufuata masharti ya usafi kama kunawa mikono wakati wote na yule anayegundulika natengwa sehemu iliyotengwa. Huoni US wenyewe wameona ni muhimu wananchi wao kurudi makazini!!?

Tulia acha wasiwasi kama umepangiwa kufa kwa corona utakufa tu. Mbona hushangai malaria tunaambukizana kila siku na tunakufa kila siku nenda kwenye hospitali zetu uone wagonjwa wa malaria wanavyojaa kuliko hata hao wa corona.

Problem imeletwa na wazungu kwa kuwa hawakuzoea communicable disease huko kwao ndiyo maana wanahaha sana. Si mara ya kwanza kwao kuwa na social distancing hata 1918 kulikuwa na mafua makali wakakimbizwa mitaani.

Mkuu ukitaka uishi vizuri ishi maisha ya kiafrika huu ugonjwa wa corona hautakusumbua utaingia na utatoka pia acha wasiwasi. Kwa taarifa yako WASIWASI HUUA!.
 
Back
Top Bottom