#COVID19 COVID-19 is historical in Tanzania: Why don't USA, UK, EU and others copy from Tanzania how to fight against the Corona Virus?

Pole ndugu yangu Nguruvi3, mimi nimeinua mikono. How does one argue with this...

View attachment 1707920

Fikiria mtu mzima na akili yake timamu anaanzisha mada jukwaa la GT lenye kichwa cha habari...

COVID-19 is historical in Tanzania: Why don't USA, UK, EU and others copy from TZ how to fight against Coronavirus?​


How does one respond? Where does one start? What does one say? Oh, I rest my case!
Aisee! Unajua, Wakuu wangu mnanistaajabisha sana sana!

Nimejifunza mengi kutoka kwenu, na sijachoka. Pia ni ninyi mlionifundisha namna bora ya kujadiliana na mkisisitiza ili niwe mshiriki mzuri na bora wa mijadala lazima nijikite kwenye hoja na si haiba, huluka, maringo, mbwembwe( kwa kifupi personality) za mtoa hoja.

Najiuliza, hivi maelekezo yenu yale ya kushiriki mjadala vizuri bila kushambulia utu wa mtoa hoja yalikuwa ya kunidhiaki ama sasa hivi mnajidhiaki wenyewe!?
====
Kwenye hoja yako ya historia.

Tulianza na covid19(2019), mwaka jana mwishoni tuna covid mpya ya Uingereza/Afrika Kusini (2020), juzi Ijumaa (2021) tumeambiwa kuna covid mpya na imegudulika huko Norway.

Kilichotokea mwaka jana nchini mwetu Tanzania unakijiua mbali na vitisho kutoka kwa ndugu yetu ( anajijua) wa humu jamvini kuwa watanzania tutapukutika na miili yetu kuzagaa mitaani! Mungu alitusimamia vitisho vikashindwa vibaya sana kama H.R. Clintoni na kura za urais wa US 2016! Ni historia hii, unataka hivyo hivyo hutaki hivyo hivyo!

Binafsi, mnazidisha sana wasi wasi wangu juu ya ninyi wakuu kughadhabishwa na wale wanao hoji ubora na ufanisi wa mbinu zinazotumika kukabiliana na CORONA hasa kwa ndugu zetu wa nchi za Ulaya magharibi na Amerika.

Poleni kwa msukosuko wa hali ya hewa huko Texas!
 
If the disease hadn't reappeared, our bet would have been a stroke of the genius. As a matter of fact, it was a brilliant idea for few months until the second wave spoiled the party.
Now you are talking. Stroke of genius and a brilliant idea, it was, you say? And who are we to disagree with you! :)
 
...
Hivi unataka kuwafanya Watanzania wapumbavu sana hawana masikio, hawana macho wala hawaelewi!
....
Najua Watanzania siyo wapumbavu, najua wana masikio na macho wanayo; ni ndio maana nawaandikia ;) Najua wanaelewa vema nia yenu ovu kwa vile mnatuonea gere hatujapigwa lockdown wala baba yake lockdown kama ninyi. Hakuna mask mandate wala nini. Tuko as free as molecule! You can only wish!

The more hysterical you become, the more assured we should become that we are over the target. A few more weeks and we should be home and dry!

Misery loves company, we know :D , but we refuse to accompany you to misery ya kujitakia!
 
Aisee! Unajua, Wakuu wangu mnanistaajabisha sana sana!

Nimejifunza mengi kutoka kwenu, na sijachoka. Pia ni ninyi mlionifundisha namna bora ya kujadiliana na mkisisitiza ili niwe mshiriki mzuri na bora wa mijadala lazima nijikite kwenye hoja na si haiba, huluka, maringo, mbwembwe( kwa kifupi personality) za mtoa hoja.

Najiuliza, hivi maelekezo yenu yale ya kushiriki mjadala vizuri bila kushambulia utu wa mtoa hoja yalikuwa ya kunidhiaki ama sasa hivi mnajidhiaki wenyewe!?
..

Ukiona a whole host of logical fallacies kwenye hoja zao, sio kwamba hawawezi kujadili bila hivyo --- wako carried away na emotions kwa nini sisi hatufungiwi? Kwa nini hakuna campaigns za kuleta hofu na taharuki kwa wananchi? Why should we have what they crave kule waliko dunia ya kwanza?

Crab-in-a-basket syndrome.
 
A sovereign country which can't meet its on obligation without international handouts.
Zakumi, those are old stories, we have moved away from donor dependency syndrome. As you know elections in Africa including Tanzania were funded by Western countries for a very long time, hence those countries using their money to determine what should be done etc.

Can you tell me which obligations Tanzania has failed to fulfil and waiting for donor countries?
 
Aisee! Unajua, Wakuu wangu mnanistaajabisha sana sana!

Nimejifunza mengi kutoka kwenu, na sijachoka. Pia ni ninyi mlionifundisha namna bora ya kujadiliana na mkisisitiza ili niwe mshiriki mzuri na bora wa mijadala lazima nijikite kwenye hoja na si haiba, huluka, maringo, mbwembwe( kwa kifupi personality) za mtoa hoja.
Ndugu yangu TUJITEGEMEE, je nawe unaamini kuwa Donald Trump ataapishwa kuwa Rais wa Marekani tarehe 4 Machi 2021? Wako wanaoamini kuwa Joe Biden hakuapishwa tarehe 6 Januari 2021 na kwamba kilichofanyika ni kiini macho tu kwani Donald Trump hangeweza kuruhusu kitokee. Pia wana imani kuwa hata Mungu angeingilia kati kuzuia kuapishwa kwa Joe Biden!

TUJITEGEMEE, ukikutana na mtu anayeamini hivyo na tayari anapanga kwenda Washington DC kuhudhuria kutawazwa kwa Donald Trump kama Rais wa Marekani je nawe utaamini? Wako wengi wanaoamini hivyo ndani ya Marekani kwenyewe na wanazo websites zinazowahamasisha wanaoingia humo. Jizuie kuokoteza vitu mtandaoni na kuvileta hapa jamvini. Kwa sasa naachia hapo...



 
Huyu jamaa yuko Marekani. Atakuwaje hajui? :oops:
Kwahiyo akikuambia ule kinyesi utakula!
Huko Marekani kuna watu wasiojua kama sehemu nyingine duniani.
QAnon unaokopi wanajua kuna majuha tu na wanafanya hivyo wakijua yapo US na duniani kwingine.
Pengine kwa kutokujua ndio maana unakopi na kupesti kila kitu bila kuchuja.

Muhimu hapa ni kuwa nimebomoa hoja za uongo za huyo jamaa na wewe huna hata mstari mmoja unaoujua.

Waeleze Watanzania kuhusu nyungu na inafanyaje kazi! ha ha ha
 
Najua Watanzania siyo wapumbavu, najua wana masikio na macho wanayo; ni ndio maana nawaandikia ;) Najua wanaelewa vema nia yenu ovu kwa vile mnatuonea gere hatujapigwa lockdown wala baba yake lockdown kama ninyi. Hakuna mask mandate wala nini. Tuko as free as molecule! You can only wish!
Yeah right! Watanzania wamezika na wanazika. Uliza viongozi wa dini watakueleza misa za maiti na sala za Jeneza ni ngapi na wanaona nini!

Watu wanapoteza familia ya watu 3 , 4 etc katika wiki au mwezi halafu wewe una 'dance on the grave' kwamba wapo free as molecule.
 
Kwahiyo akikuambia ule kinyesi utakula!
Huko Marekani kuna watu wasiojua kama sehemu nyingine duniani.
QAnon unaokopi wanajua kuna majuha tu na wanafanya hivyo wakijua yapo US na duniani kwingine.
Pengine kwa kutokujua ndio maana unakopi na kupesti kila kitu bila kuchuja.
Huyo Mlenge, nimeamua hata kum-ignore, nasoma tu post zake kupitia nukuu kama hiyo ya kwako. Hivi sasa wako watu humu kazi kubwa wanaoifanya ni kuokoteza tu wanayokutana navyo mtandaoni bila utafiti wowote, udadisi wowote na wala kuhoji msimamo na imani ya wanahusika. Halafu kwa sababu ya cookies, ukikosea ukaingia tu kwenye hizo websites ujue umetekwa.

Hata kuhusu COVID-19 na chanjo yake ni hivyo hivyo, wapinzani wakubwa wanaopotosha jamii wako huko huko Marekani ila uzuri wa huko ni kwamba mwisho wa siku ukweli husimama. Nguruvi3, unakumbuka tulivyopingwa humu kuhusu uchaguzi wa Marekani na misimamo ya watu kama TUJITEGEMEE na Mlenge? Walikuwa wakiitazama Marekani kwa jicho la Kitanzania!
 
Waeleze Watanzania kuhusu nyungu na inafanyaje kazi!
Ukweli unanisikitisha kwa namna unavyodharau kazi za matabibu wetu wa jadi! Kwa hili naona dalili za wengi wenu kuwa waoga kuwa kujitegemea katika kila nyanja za kuimarisha nchi.
 
Ukweli unanisikitisha kwa namna unavyodharau kazi za matabibu wetu wa jadi! Kwa hili naona dalili za wengi wenu kuwa waoga kuwa kujitegemea katika kila nyanja za kuimarisha nchi.
Eleza nyungu inafanyaje kazi? Nyungu inatengenezwa na nini? kwanini nyungu ya Singida ni tofauti na ya Tanga?

Dawa za asili zipo tena zimeanishwa kisayansi na wataalam wanaendelea kuziangalia.

Kama unaweza kushambulia usalama wa vaccine ili isiletwe, basi tupe uhalali usalama wa nyungu!

Mlenge teh
 

The link below is the successful story of vaccine from Israel (Taifa teule). Now the nation of Karl Peters have your say.​

Israel eases restrictions following vaccine success Israel eases restrictions following vaccine success

Wadachi na Wafelmishi ni watani. Mdachi mmoja alitusimulia kuhusu Waflemishi.

Siku moja Mdachi alimkuta Mflemishi ananyunyizia majivu kwenye shamba lake huko Ubelgiji.

Mdachi akauliza, "Ni ya kazi gani hayo majivu?"

Mflemishi akajibu, "Ni ya kufukuza tembo wasije kuharibu mazao shambani."

Mdachi akasangaa, "Lakini hakuna tembo Ubelgiji!"

Mflemishi akajibu, "Bwashee, unaona kumbe majivu yanafanya kazi yake iliyokusudiwa!"

Thus endeth the today's lesson.
 
Huyo Mlenge, nimeamua hata kum-ignore, nasoma tu post zake kupitia nukuu kama hiyo ya kwako.
Mkuu upotoshaji ulizidi tukaona kuukalia kimya hatutaitendea jamii haki. Ni ngumu sana kwasababu tuna deal na vitu vingi, moja ignorance na pili moral decay na tatu selfishness.
Watu wanavyopukutika halafu mizaha ya ....too shall pass au tumeshinda n.k. inaudhi inakera na inasikitisha sana.
Hivi sasa wako watu humu kazi kubwa wanaoifanya ni kuokoteza tu wanayokutana navyo mtandaoni bila utafiti wowote, udadisi wowote na wala kuhoji msimamo na imani ya wanahusika. Halafu kwa sababu ya cookies, ukikosea ukaingia tu kwenye hizo websites ujue umetekwa.
Tena wanaokoteza uchafu unao fit narrative zao. Kwa mfano, Mlenge hawezi kutetea hoja hata moja ya video aliyookota. Lengo lake lilikuwa kuwapotosha wananchi
Hata kuhusu COVID-19 na chanjo yake ni hivyo hivyo, wapinzani wakubwa wanaopotosha jamii wako huko huko Marekani ila uzuri wa huko ni kwamba mwisho wa siku ukweli husimama.
Watu hawaijui Marekani. Juzi wamepeleka kifaa Mars na kinaleta picha nzuri kuliko ya iphone au samsung anayomiliki Mlenge. Hiyo ni Maili milioni 300 na imechukua miezi 7 kufika katika speed ya 12,000km/hr .
Huko Marekani ndiko kwenye watu wenye akili za kila aina na ndio wanaongoza dunia hii.

Huko Marekani kuna wajinga sana ambao wanatumwa kwenda kuvamia congress. Huko Marekani kuna watu wanoamini Trump atarudi madarakani March na wanamchangia pesa.
Huko Marekani kuna QAnon wanaoamini Hillary Clinton anakula nyama za watoto n.k.

Kwa wanaoijua Marekani , ni taifa kubwa lenye kila kitu. Diversity ndio nguvu yao na walioangalia NASA mission utaona diversity inavyosaidia maendeleo ya Taifa hilo tajiri kwa akili na mali duniani.

Juzi Biden katangaza Bilion 4 $ kusaidia chanjo kwa nchi masikini. Kwamba, kwa nchi masikini chanjo iwe bure.

Huyo mpuuzi anayeishi Marekani bandiko #143 anasema ameugua Covid akapona, asichowaeleza watu ni kuwa alikuwa katika ventilator. Hivi tuna ventilaor nchini?

Nguruvi3, unakumbuka tulivyopingwa humu kuhusu uchaguzi wa Marekani na misimamo ya watu kama TUJITEGEMEE na Mlenge? Walikuwa wakiitazama Marekani kwa jicho la Kitanzania!
Bwana wee , tukaambiwa Trump haondoki, zikiandikwa 'mtrix'' mwisho wa siku aliondoka bila kuambiwa na mtu
Marekani ni taifa jingine, wakitaka wanaweza, period

Mkuu Mag3 , unahitaji Microphone na Amplifier ili kufikisha ujumbe. Unajua kazi ya amplifier
 
...
Watu wanavyopukutika ...

Kwa hiyo unaona waliokufa hawatoshi, mpaka unafosi kingi wafe wengine kwa chanjo ambazo hazijathibitishwa?

Tukinukuu:

1. What to Know About Post-Vaccine Deaths and Allergies

Norwegian officials were the first to report people dying after being inoculated, saying in mid-January that 33 people age 75 and older had died a short time after receiving the Covid vaccine from Pfizer Inc. and BioNTech SE.
...
The U.K.’s Medicines and Healthcare Products Regulatory Agency reported that as of Jan. 24, there were 143 deaths shortly after injections with the Pfizer-BioNTech vaccine and another from AstraZeneca Plc

in the U.S., the Centers for Disease Control and Prevention said that as of Feb. 7, there were 1,170 reported deaths among people who received either the Pfizer-BioNTech vaccine or another from Moderna Inc.

Wataalam wa Afya walioko Marekani kwenyewe nao wanakataa chanjo. Nukuu:
2. Alarming number of US health care workers are refusing COVID-19 vaccine

US health care workers are first in line to receive the COVID-19 vaccine — but an alarming number across the country are refusing to do so.

Earlier this week, Ohio Gov. Mike DeWine disclosed that about 60 percent of the nursing home workers in his state have so far chosen not to get vaccinated.

More than half of New York City’s EMS workers have shown skepticism, The Post reported last month.

And now California and Texas are experiencing a high rate of health care worker refusals, according to reports.

3. DeWine says 60% of nursing home workers not electing to get vaccine

Tunajua mnalazimisha Tanzania iweke lockdown, kwa vile huko mlikojilipua kuna lockdown. Acheni wivu.
 
Ikiwa unajiunga na uzi huu, usibabaishwe na jitihada za kuutoa kwenye reli: Uzi ni wa Septemba 2020, ukielezea mafanikio ya Tanzania dhidi ya wimbi la kwanza la ugonjwa wa korona.

Unaowaona sasa hivi wanatoka out of woodwork kubeza jitihada zilizoko kupambana, watakimbia tena kujificha wakisubiri likitokea wimbi lingine.
 
Now you are talking. Stroke of genius and a brilliant idea, it was, you say? And who are we to disagree with you! :)

Well the government took a bet and at some point the bet seemed to work. However, corona took a different turn and we couldn't ride our luck for a long period of time. Now we look like cave people.
 
Yeah right! Watanzania wamezika na wanazika. Uliza viongozi wa dini watakueleza misa za maiti na sala za Jeneza ni ngapi na wanaona nini!

Watu wanapoteza familia ya watu 3 , 4 etc katika wiki au mwezi halafu wewe una 'dance on the grave' kwamba wapo free as molecule.
Wamekufa kwa sababu zipi? Inaweza kutokea kabisa familia kupoteza watu zaidi ya wawili katika siku saba hata watatu. Je, sababu ni nini? Je vipi watoto wanapozaliwa hakuna maswali ni shangwe na vigelegele bali wanapokufa baada ya maisha yao ndio nongwa.
 
Zakumi, those are old stories, we have moved away from donor dependency syndrome. As you know elections in Africa including Tanzania were funded by Western countries for a very long time, hence those countries using their money to determine what should be done etc.

Can you tell me which obligations Tanzania has failed to fulfil and waiting for donor countries?

We still depend on foreign aid. The level of aid is below what used to be. But, we aren't out of the wood yet.
 
Back
Top Bottom