SEHEMU YA II
VITA KUU YA KWANZA YA WENYEWE KWA WENYEWE.
Baada ya vita kuisha na Italia na Dunia yote kurudi katika halia ya kawaida, shughuli za kihalifu za Mafia ziliendelea.
Mwaka 1962 Moja ya mabosi wa mafia aliyeitwa Don Cesare Manzella aliandaa mpango wa kusafirisha mzigo mkubwa wa madawa ya kulevya kutoka Italia ili kuuingiza mchini marekani.
Mzigo huu ulisafirishwa kwa meli.
Kama ilivyo ada kwenye shughuli za mafia mtu akiwa na "dili" alipaswa pia kuhusisha familia nyingine za Mafia katika kulitekeleza, hivyo basi Don Manzella akawapa jukumu familia ya Grecos na La Barberas kusimamia usafilishaji wa mzigo huo.
Wakiufikisha marekani walitakiwa kuuwasilisha mzigo kwa Bosi mwingine aliyeitwa Don Calcedonio Di Pisa.
Mzigo ulipofika marekani na kupokelewa na Don Di Pisa na kisha kuupeleka kwa wanunizi wa jumla, akalipwa hela ndogo na kuwaambia waliouleta (familia ya Grecos na La Bearbaras) kuwa wanunuzi wamemtapeli wakidai mzigo ni Mdogo.
Familia ya La Berbaras hawakuamuamini wakamshutumu kwa ameiba sehemu ya mzigo na kuuficha kabla ya kupeleka kwa wanunuzi wa jumla.
Suala hili ikabidi lipelekwe kwenye tume ya Mafia (nitaeleza baadae kuhusu Tume za mafia).
Kwa mshangao mkubwa Tume ikafikia hukumu kuwa ni kweli wanunuzi wa jumla wamemtapeli Don Di Pisa na kumpa hela ndogo..
Suala hili likawatia hasira familia ya La Berbaras na kuamua kuwawimnda na kuwauwa kuanzia aliyewatuma kupeleka mzigo marekani (Don Manzella) na waliyemkabidhi mzigo Don Di Pisa.
Kitendo cha kuuwawa kwa mabosi hawa kikaanzisha mtafaruku mkubwa baina ya familia tofauti tofauti ndani ya Mafia huku kila familia ikiegemea upande fulani.
Mtafaruku ukawa mkubwa kiasi kwamba ukatengeneza uhasimu wa familia tofauti ndani ya mafia na punde tu wakaanza kuwindana na kuuwana mchana kweupe.
Jambo baya zaidi hawakuishia kuuwana wenyewe kwa wenyewe tu bali pia hata wasiohusika walikumbwa na madhira haya.
Kwa mfano polisi waliokuwa wanahisiwa kuunga mkono familia fulani waliwindwa na kuuwawa na familia nyingine.
Pia marafiki wa familia hii waliwindwa na kuuwawa na familia nyingine.
Ndani ya miezi 6 ( May 1962 hadi January 1963) kulikuwa na vifo zaidi ya 700 vilivyosababishwa na ugomvi wa familia za Mafia.
Ndipo hapa serikali ikabidi kuingilia kati na kuanza kuusambaratisha mtandao wa Mafia.
Zikaendeshwa oparesheni maalumu za kijeshi kuwatambua na kuwakamata wanachama wa familia za mtandao wa Mafia.
Ndani ya miezi miwili pekee wanachama 177 wa familia za mafia walikamatwa.
Hii ikasababisha wanachama wengine wa familia zote kusitisha shughuli zao na kujificha.
Zaidi ya miaka mitano (1963 - 1968) hakukuwa na shughuli zozote za kihalifu za mtandao wa Mafia.
VITA KUU YA PILI YA FAMILIA ZA MAFIA
Kwa miaka mitano hakukuwa na shughuli za mtandao wa Mafia, lakini ilipofika mwishoni mwa mwaka 1969 taratibu sana mtandao wa mafia ukaanza kurejea tena katika shughuli zake.
Ilipofika mwaka 1970 nchini ufaransa serikali iliendesha oparesheni kali ya kufunga maabara za kihalifu zilizokuwa vinatengeneza madawa ya kulevya aina ya Heroin.
Pia walipiga marufuku uvutaji na uingizaji wa sigara nchini Ufaransa.
Hivyo basi uhitaji wa madawa aina ya heroin na sigara ukakua kwa kasi kubwa nchini ufaransa.
Mabosi wa mtandao wa Mafia wakaona fursa adhimu ya kibiashara. Hivyo basi wakaitisha mkutano na kusuluhisha migogoro yote iliyotokea huko nyuma.
Wakaweka lengo moja tu kuwa, mtandao wa Mafia uteke soko heroin na sigara nchini ufaransa na marekani.
Wakafungua maabara za kutengeneza heroin na kutengeneza mitandao ya kihalifu ya usambazaji mizigo.
Baada ya mwaka mmoja wakawa wameteka soko la heroin nchini Ufaransa.
Baada ya hapo wakaingia marekani hasa majimbo ya kaskazini na kuanza kutengeneza mitandao ya uuzaji na usambazaji wa heroin.
Hili walilifanikisha kwa ustadi mkubwa kwani, migahawa mingi ya kuuza Pizza (Pizzaria) nchini marekani ilimilikiwa na waitaliano.
Kwahiyo waliingia makubaliano na wenye migahawa ambapo mzigo wa heroin ulifikishwa kwao na wao walitumia kivuli cha kuuza pizza kuwapa wauzaji wa mtaani (street dealers).
Ndani ya miaka miwili tu Mafia wakawa wanamiliki 80% ya soko la heroin kwa majimbo ya kaskazini mwa Mareni.
Ndipo hapa wanasema "palipo ridhiki hapakosi fitna".
Mwaka 1975 kipindi ambacho mapato yatokanayo na shughuli za Mafia yako juu sana, kiongozi wa familia ya Carleone aliyeitwa Don Luciano Leggio ambaye pia alikuwa ni mjumbe wa tume ya Mafia (Mafia Commission) akaanzisha kampeni ya siri ya kuunganisha familia za Mtandao wa Mafia na akaziita Corleonesi yeye mwenyewe akiwa kama kiongozi Mkuu.
Lengo kuu lilikuwa ni kutawala kuatawala biashara na shughuli za Mafia huku wakiwatenga familia nyingine ambazo zilikataa kujiunga katika umoja huo wa Carleonesi.
Katikati ya mwaka 1975 Don Leggio akapata Bahati mbaya kukamatwa na serikali akishutumiwa kwa kosa la uuaji na akatupwa gerezani.
Hii ilimlazimu kumuachia madaraka msaidizi wake aliyeitwa Don Salvatore Riina.
Baada ya Don Riina kuchukua madaraka akaanzisha mipango ya kuwaondoa katika Tume Mabosi wa familia ambazo walikataa kujiunga na umoja wao wa Carleonesi.
Nieleze kwa ufupi kuhusu Tume ya Mafia (Mafia Commision)
Hiki ni kakao maalumu au baraza ambalo linaundwa na mabosi wa familia zote za Mafia.
Kazi kubwa ya Tume hii ni kusuluhisha migogoro, kugawa maeneo ya biashara na kuweka mikakati ya kibiashara.
Kwa hiyo Don Riina akatamani Tume hii itawaliwe na mabosi wanaounga mkono umoja wao wa Carleonesi pekee.
Hivyo akaanza kuzusha tuhuma za uongo dhidi ya mabosi wenzake ambapo tuhuma hizo zilisababisha mabosi hao kukosa sifa ya kuendelea kuwa wajumbe wa Tume ya Mafia.
Don Riina alienda mbali zaidi mpaka kufikia hatua ya kupanga mauaji ya mabosi wa familia zilizokuwa zimekataa kujiunga na umoja wa Carleonesi.
Hapa ndipo vita kuu ya pili ilipoanzia.
Wanachama wa familia nyingine nao wakaanzisha oparesheni za kulipa kisasi kwa kuuwa wanachama wa familia zilizojiunga katika umoja wa Carleonesi.
Lakini Don Riina alikuwa na mbinu adhimu za kihalifu. Alichokifanya ilikuwa ni kuwahonga baadhi ya wanachama wa familia pinzani ili kuwaua wenzao wanaoendeleza vita dhidi ya umoja wa Carleonesi.
Hadi kufikia mwaka 1978, Don Riina alifanikiwa kuiweka kiganjani Tume ya Mafia kwa kuingiza mabosi wa familia za umoja wa Carleonesi pekee na yeye mwenyewe akijipa cheo cha uongozi wa Tume ya Mafia.
Ndipo hapa alipopachikwa jina la "Boss of Bosses".
Baada ya mafanikio haya Don Riina akavimba kichwa zaidi.
Don Riina akaanzisha vita na waandishi wa habari walioiandika Mafia vibaya, akaanzisha vita na mauaji ya Polisi ambao waliendesha oparesheni zilizokuwa kinyume na mafia.
Don Riina akaenda mbali zaidi akaaendesha utekaji na mauaji ya viongozi wa serikali ambao walikuwa wanaipinga Mafia.
Mauaji haya yalikuwa ni mengi katika miaka ya 1980 kiasi kwamba ikaamsha hasira za wananchi.
Kwa miaka yote wananchi walikuwa wamejiweka kando (neutral) katika ugomvi wa serikali na Mafia.
Lakini kutokana na mauaji yaliyokuwa yanaendelea ikawafanya wananchi waanze kuipinga Mafia wazi wazi na kuanzisha harakati za kuishinikiza serikali kuitokomeza Mafia nchini Italia.
Mwaka 1988 serikali ikaanzisha rasmi oparesheni ya kuwasaka mabosi wa familia za Mafia.
Mwaka 1993 wakafanikiwa kumkamata Don Riina na kumtupa gerezanj.
Kitendo hiki kilikuwa kama kimewawehusha wanachama wa Mafia kwani wakaanza kutekeleza matukio ya kigaidi kitu ambacho hakikuwahi kushudiwa kikifanywa na Mafia hapo kabla.
Wanachama wa mafia wakaanzisha matukio ya kulipua majengo ya serikali, vituo vya mabasi, mahoteli na sehemu za utalii. Lengo lao kubwa lilikuwa ni kuishinikiza serikali kumuachia Don Riina.
Serikali ikasimama imara na kukataa kata kata kumuachia Don Riina.
Ndipo hapo ilipobidi Don Leoluca Bagarella arithishwe uongozi mwaka huo 1993.
Lakini Don Bagarella akafanya makosa ya kuendeleza staili ile ile ya uongozi ya Don Riina. Kuiandama serikali, waandishi wa habari na kuuwa wanachama wa familia nyingine ambazo hazipo kwenye umoja wa Carlonesi.
Hii ikisababisha Don Bagarella kutodumu sana kwenye uongozi kwani miaka miwili baadae yaani 1995 alikamatwa na serikali ya Italia na kutupwa gerezani.
Hii ikatoa fursa kwa uongozi mpya kushika hatamu, ambapo Don Bernardo Provenzano akachukua madaraka ya uongozi wa familia za Mafia.
Mara baada ya Don Provenzano kuchukua madaraka akajiapiza kuirudisha Mafia katika misingi yake ya weledi, ufanisi na kuheshimiana wenyewe kwa wenyewe (Loyalty).
KUREJEA TENA KWA MAFIA KATIKA "UTUKUFU" WAKE.
Don Provenzeno kwanza kabisa akapiga marufuku kwa wanachama wa Mafia kufanya mauaji ya viongozi wa serikali, waandishi wa habari na polisi.
Pia akapiga marufuku wanachama wa Mafia kuuwa mashahadi wa kesi za serikali dhidi ya Mafia na kama mbadala alianzisha utaratibu wa kuwahonga mashahidi na kuwatorosha wakaanze maisha sehemu nyingine.
Pia akamaliza kwa kusuluhisha vita zote za kifamilia katika mtandao wa Mafia na kuwasisitiza wao wote wako kwenye timu moja, kwamba ni wote ni ndugu chini ya mtandao wa Mafia.
Baada ya miaka kadhaa Mafia ikatulia na kurudi katika weledi na ufanisi wake.
Kuna tuhuma ambazo hazijathibitishwa zinazoeleza kwamba Don Provenzena aliwasiliana na Bw. Silvio Berlasconi ambaye alikuwa katika harakati za kuanzisha chama chake cha Ferzo Italia ili aweze kugombea Uwaziri Mkuu wa Italia.
Inasemekana kwamba Don Provenzeni alimpa ofa Berlasconi kuwa watamsaidia ashinde katika jimbo la Sicily na maeneo mengine ya nchi ambayo wanaushawishi.
Ombi lao kwao ni kwamba akiingia madarakani alegeze sheria zinazopinga Mtandao wa Mafia (anti-Mafia law) hasa hasa kipengele maarufu kinachojulikana kama "article 41-bis".
Shutuma hizi zimepingwa vikali na Silvio Berlosconi mwenyewe na chama chake lakini baadae Berlosconi alishinda uwaziri Mkuu akipita kwa kishindo katika jimbo la Sicily.
Pia mwaka 2002 kifungu cha sheria cha "article 41-bis" kiliacha kutumiaka, kitendo ambacho kilizua maswali mengi.
Don Provenzeno hakuishia hapo tu kudhihirisha kuwa japokuwa watangulizi wake walipenda utengano yeye anapendelea zaidi ushirikiano.
Ndipo hapa ambapo aliwasiliana na nguli wa mihadarati kutoka Mexico Bw. Joaquin Guzman au maarufu kama "El Chapo" na wakaanzisha ushirikiano wa kibiashara kati ya mtandao wa Mafia na genge la Sinaloa Cartel linalomilikiwa na El Chapo.
Pia Don alianzisha utaratibu maalumu wa kuwafanya wahalifu wa Mafia wawe wa kipekee.
Utaratibu huu aliuita "Pax Mafiosa" (Mafia Quietness (ukimya wa Mafia)).
Chini ya utaratibu huu aliamuru kwanza wanachama wote wa Mafia kuacha kujigamba na kujitanabaisha katika jamii. Aliamuru wanachama wa Mafia kuishi kama mashushushu bila watu kuwafahamu na shughuli zao ziendeshwe kimya kimya na kwa usiri mkubwa.
Chini ya Don Provenzena Mafia ikarudi katika "ubora" wake.
Ingawa Don Provenzena alikamatwa na kutupwa gerezani mwaka 2006, lakini bado alama yake ya kiuongozi (legacy) inaendelea kuiongoza Mafia mpaka leo hii chini ya Don Messina Denaro ambaye ndiye kiongozi wa sasa.
Mwisho.
Join my exclusive whatsapp group kusoma makala na simulizi kila siku - 0718 096 811 (kuna "subscription fee")
The Bold.