Cosa nostra

Naleo boss of all bosses 'Don Riina' amefariki dunia akiwabado anatumikia kifungo.... shukrani mkuu kwabandiko maridhawa.!
 
COSA NOSTRA: SEHEMU YA I



Kwa miaka mingi sasa kumekuwepo na hadithi nyingi sana kuhusu Kundi maarufu la uhalifu la Mafia.

Hadithi hizi zimewafanya wengi kutamani kufahamu umahiri, mbinu na usiri unaotawala katika ulimwengu wa kundi hili maarufu la uhalifu la Mafia au 'Cosa Nostra' kama wenyewe wanavyojiita.

Tofauti na watu wengi wanavyodhani kuwa Mafia ni kikundi Fulani cha uhalifu, hii sio sahihi.
Mafia sio 'kikundi' cha uhalifu bali ni mkusanyiko wa vikundi vingi vya uhalifu vinavyo julikana kiitaliano kama "cosca". Vikundi ambavyo kiuhalisia ni koo (familia) kila kimoja kinakuwa na eneo lake la kufanyia shughuli zake ambalo wenyewe wanaliita "Borgata".

Vikundi hivi vyote kwa pamoja vinakuwa chini ya Mwamvuli mmoja ambao wenyewe wanauita "Cosa Nostra" kwa kiitaliano ambayo inamaanisha "Kitu Chetu" (Our thing).


Neno lenyewe Mafia lina maana ya "Ujasiri na Uzuri" (boldness, bravado).




KUANZISHWA KWA MAFIA.

Kwa karne nyingi katika jimbo la Sicily nchini Italia, kiasi kikubwa cha ardhi kilimilikiwa na watu wachache ambao walikuwa ni wakulima wakubwa.

Mwaka 1860 Sicily ikatengwa kutoka Italia na kuwa jimbo linalojitegemea.
Hii ikapelekea mamlaka za jimbo la Sicily kuchukua kutoka wakulima wote wenye ardhi kubwa na kuigawa kwa wananchi.

Lakini mamlaka za mji wa Sicily ikaamuru kuwa kila mwananchi ambaye atapewa ardhi atatakiwa kulipa "kipande" kidogo kwa mmliki wa ardhi ambaye ardhi yake ilichukuliwa na serikali na kugaiwa kwake. Kipande hiki kilitakiwa kulipwa kila mwaka kutoka kwa mkulima mdogo kwenda kwa mkulima mkubwa aliyepokonywa ardhi na serikali.

Hatua hii ilikuwa na faida pamoja na changamoto. Faida yake ilikuwa ni kwamba wakulima wengi sasa walikuwa na ardhi ya kulima.
Lakini hasara yake ilikuwa ni kwamba ilianza kupandikiza hisia kwa wananchi kuwa wakulima wakubwa wanawanyonya na kuwaonea.

Wakulima wengi wakaanza kukaidi agizo la kuwalipa kipande cha kila mwaka wakulima wakubwa na baadhi yao wakaanza kuvamia makazi ya wakulima wakubwa na kuiba.

Katika kipindi hiki jimbo la Sicily lilikuwa na changamoyo kubwa ya kutokuwa na Polisi wa kutosha.
Jimbo zima lilikuwa na askari 350 pekee.

Hii ilifanya kazi ya kuzuia vitendo vya kihalifu kuwa ngumu na hii ikasababisha uhalifu kuongezeka kila siku.

Ndipo hapa wakajitokeza wahalifu ambao walijiunga katika vikundi na kutoa huduma ya kuwalinda kwa malipo ya fedha matajiri na kufuatilia madeni yao kwa wakulima wadogo.

Vikundi hivi viliundwa na wahalifu wenye weledi ambao wao walitoa huduma kwa matajiri kuwatafuta watu waliwaio waibia mali zao na hata wale ambao hawataki kulipa vipande kwa ajili ya ardhi waliyopewa.

Kutokana na ufanisi wa vikundi hivi, mamlaka za kisheria pia zikaanza kuvutiwa na huduma zao.

Kama nilivyosema awali kuwa katika kipindi hiki mji wa Sicily ulikuwa na upungufu mkubwa wa polisi. Lakini si hivyo yu bali pia ufanisi wa vikundi hivi ulikuwa ni mkubwa kuliko polisi kutokana na uwezo wao wa kuwakamata wahalifu au kurejesha vitu vilivyoibiwa.

Baada ya vikundi hivo kuanza kutengeneza faida kubwa, baada ya kugunduliwa kwa malighafi ya Sulphur katika mji wa Sicily, wahalifu wakubwa wakaanza kutengeneza vikundi ndani ya faimilia/koo zao.

Hii ilikuwa ni miaka ya 1900.


Kugunduliwa kwa malighafi ya Sulphur katika jimbo la Sicily kulimaanisha kuwa vipato vya watu viliongezeka kutokana na shughuli za uchimbajo malighafi hii, hii ilimaanisha kuwa pia uhitaji wa kujilinda na kulinda mali uliongezeka pia. Hii maana yake kuwa huduma za ulinzi wa Mali na mtu zinazotolewa na familia hizi za kihalifu uhitaji wake ukaongezeka maradufu.

Baada ya shughuli za familia hizi za kihalifu kuongezeka maradufu, ukaonekana umuhimu wa kufanya kikao cha pamoja ili familia hizo zote zikubaliane namna ya utendaji kazi wake na maeneo ya utendaji kazi ili kuepusha kujikuta wanaingia kwenye malumbano au vita ya kugombea maeneo ya kufanyia shughuli.

Ni katika kikao ambapo wakakubaliana kuweka mfumo wa ufanyaji kazi unaofanana kwa familia zote, na wakaweka Sheria ambazo wenyewe waliziita "umirta".
Sheria hizi zilihusu usiri (kutunza siri za shughuli zao), kujitenga/kutoshirikiana na polisi, alama (signal) za siri za kutambuana na kujitenga na jamii ya kawaida (kutochangamana).

Ni katika kikao hiki ambapo viongozi wa kila familia wakaanza kuitwa "Don" (Sir). Na ni katika kikao hiki ambapo umoja wao huu wa familia zao ukaanza kuitwa "Mafiosi" (Mafia) wenyewe wakiwa na maana ya "Men of honour" (Watu wa Heshima).

Baada ya kutengeneza mtandao huu, na kugawana maeneo ya kufanyia kazi ndani ya jimbo la Sicily, ndipo hapa ambapo shughuli za Mafia zikaanza kubadilika kutoka katika kuzuia uhalifu na badala yao wao wenyewe wakageuka wahalifu, tena wahalifu wa daraja la kwanza.

Wakaanza shughuli za utekaji na kudai kulipwa ili kumuachia mateka (kidnapping for ransom), wakaanza na shighuli za usafirishaji wa binadamu na madawa ya kulevya. Lakini pia hawakuitelekeza shughuli yao ya miaka yote. Kuwalinda vidosi (protection), tofauti tu ni kwamba sasa walikuwa wanawalinda watu wenye utajiri mkubwa mkubwa sio vijisenti.

Hadi kufikia katikati ya miaka ya 1910 ushawishi wa Mtandao wa Mafia katika mji wa Socily ulikuwa ni mkubwa kupindukia.
Ndipo hapa ambapo wakachukua hatua nyingine ya ziada kuhakikisha wanakuwa imara zaidi.

Wakahakikisha kwamba Gavana wa mji huo wa Sicily anatoka katika mtandao wao katika kila uchaguzi uliokuwa unaitishwa.
Hili walifanikisha kwa kutisha wapiga kura na kuwalazimisha kuchagua mtu wao. Lakini pia waliwatishia maisha wagombea wengine na kuwalazimisha kujitoa kwenye kinyang'anyiro hivyo wagombea wao walipita bila kupingwa kwenye chaguzi nyingi.

Ushawishi wa Mafia katika mji wa Sicily ukaongezeka na kufikia kilele cha juu kabisa na ikawa kana kwamba wanaumiliki mji wa Sicily.


Mafia vs Benito Mussolini.

Mwanzoni mwa miaka ya 1920 Jimbo la Sicily lilirudishwa katika utawala wa nchi ya Italia. Katika kipindi hiki kiongozi mkuu wa nchi alikuwa ni Waziri Mkuu Benito Mussolini, kiongozi katili, na dikteta aliyeogopwa kila kona.

Mwaka 1924 Mussolini alifanya ziara ya kiserikali katika jimbo la Sicily.

Katika ziara yake alikaribishwa na Gavana wa mji wa Sicily aliyeitwa Fransesco Cuccia. Huyu licha ya kuwa Gavana wa jimbo la Sicily pia alikuwa ni moja ya mabosi wa ngazi za juu wa Mafia.

Katika mapokezi yake inasemekana alishangaa kuona Mussolini ameongozana na maafisa wengi wa Ulinzi kutoka Roma.

Ndipo hapa inaelezwa akamnongoneza Mussolini na kumwambia "Mtukufu Waziri Mkuu huitaji ulinzi wote huu ukiwa na mimi". Akimaanisha kuwa kwa kuwa yeye (wao mafia) wanaumiliki mji wa Sicily hivyo hakuna mtu yeyote anayeweza kuthubutu kumdhuru mgeni wa ngazi za juu aliyekuja kuonana na Gavana (Bosi wa Mafia).

Inasemekana Mussolini alikasirishwa vikali na kauli hii na akamkemea vikali Gavana Fransesco Cuccia na kumueleza kuwa haitaji Ulinzi wake.

Kitendo hiki cha kukemewa kilimuudhi sana Gavana, na akawaeleza vijana wake watoe maagizo kwa wananchi kuwa wasihudhurie mkutano wa Mussolini uliopangwa kufanyika kesho yake.

Ni kweli kesho yake Mussolini alipokwenda katika mkutano wa kuhutubia wananchi wa Sicily akajikuta yuko peke yake na walinzi wake. Hata Gavana hakuwepo.

Mussolini akauliza ni nini kimetokea? Ndipo akaambiwa kuwa Gavana huyo ni moja ya mabosi wa Mafia na alichukizwa na jinsi alivyo mkemea jana hivyo aliamuru wananchi wasijitokeze kwenye mkutano wa Mussolini.

Mussolini akachukia kweli kweli, hii ilikuwa ni dharau kubwa kwa mtu wa aina yake. Akarejea Roma na kuahidi kumfundisha somo Gavana Francesco Cuccia na watu wa dizaini yake.

Aliporejea Roma akateua kikosi maalumu cha kijeshi kilichoitwa Carabineti na kukiagiza kwenda jimbo la Sicily kuwakamata na kuwafunga wanachama wote wa Mafia na wanaowashabikia.

Kikosi hiki cha kijeshi kilikuwa ni moja wapo ya vikosi vya weledi (special forces) vya jeshi la Italia na kijulikana kwa ukatili wake na ufanisi.

Kikosi kikaingia ndani ya Italia na kuanza msako wa wanachama wa Mafia Jimbo zima, kitongoji kwa kitongoji, mtaa kwa mtaa na nyumba kwa nyumba.

Oparesheni yao ilikuwa na mafanikio makubwa kwani walifanikiwa kuwatia gerezani zaidi ya wanachama 11,000 wa Mafia na kuwaua wengine.

Kwa miaka kadhaa Mafia ikafutika kabisa kwenye jimbo la Sicily na nchi ya Italia kwa ujumla.

Lakini mabosi wa juu wa Mafia (Dons) wengi wao walifanikiwa kutoroka na kukimbia nchi kwenda kuishi uhamishoni. Hii ndio ilikuwa mojawapo ya sababu kuu ya Mafia kuenea nje ya nchi ya Italia.

Mfano Don Carlo Gambino na Joseph Bonanno walikimbilia nchini marekani mji wa New York na kwenda kuanzisha upya shughuli za mafia huko na kuwa moja ya Mafia waliofanikiwa zaidi katika historia ya mtandao huu wa kihalifu.



MAFIA WANAANZA KUJIJENGA TENA UPYA.

'Habari njema' kwa mafia ilikuwa ni pale ilivyoanza vita kuu ya pili ya dunia.

Baada ya vita kukolea, majeshi ya umoja wa magharibi yakiongozwa na marekani (Allied Forces) mwaka 1943 yakavamia Italia na zaidi ya wanajeshi nusu milioni.

Mojawapo ya miji ya kwanza kabisa kuvamiwa na Majeshi ya Marekani na washirika wake ilikuwa ni jimbo la Sicily.

Baada ya kuvamiwa na vuruga za vita kukolea magereza mengi yaliharibika na wafungwa wote wakiwemo mafia kutoroka.

Baada ya majeshi ya kifashisti yakiongozwa na Mussolini kushindwa, na Mussolini mwenyewe kuuwawa, majeshi ya magharibi yakaanza kuchagua uongozi wa muda kwenye miji mbali mbali nchini Italian.

Wanasiasa wengi wanao fungamana na Mafia walichangamkia fursa hii na kuteuliwa kuwa viongozi katika jimbo la Sicily.

Jambo kubwa lililowasaidia ilikuwa ni vile toka awali (kabla ya vita) walikuwa hawaungi mkono sera za kifashisti na ukomunisti ulioanzishwa na Benito Mussolini.

Baada ya Mafia waliofungwa kutoka magerezani na viongozi wao kuchukua tena madaraka, taratibu mitandao yao ya kihalifu na shughuli zao zikaanza kurudi tena katika jimbo la Sicily na Italia kwa ujumla.









SEHEMU YA II




VITA KUU YA KWANZA YA WENYEWE KWA WENYEWE.

Baada ya vita kuisha na Italia na Dunia yote kurudi katika halia ya kawaida, shughuli za kihalifu za Mafia ziliendelea.

Mwaka 1962 Moja ya mabosi wa mafia aliyeitwa Don Cesare Manzella aliandaa mpango wa kusafirisha mzigo mkubwa wa madawa ya kulevya kutoka Italia ili kuuingiza mchini marekani.

Mzigo huu ulisafirishwa kwa meli.

Kama ilivyo ada kwenye shughuli za mafia mtu akiwa na "dili" alipaswa pia kuhusisha familia nyingine za Mafia katika kulitekeleza, hivyo basi Don Manzella akawapa jukumu familia ya Grecos na La Barberas kusimamia usafilishaji wa mzigo huo.

Wakiufikisha marekani walitakiwa kuuwasilisha mzigo kwa Bosi mwingine aliyeitwa Don Calcedonio Di Pisa.

Mzigo ulipofika marekani na kupokelewa na Don Di Pisa na kisha kuupeleka kwa wanunizi wa jumla, akalipwa hela ndogo na kuwaambia waliouleta (familia ya Grecos na La Bearbaras) kuwa wanunuzi wamemtapeli wakidai mzigo ni Mdogo.

Familia ya La Berbaras hawakuamuamini wakamshutumu kwa ameiba sehemu ya mzigo na kuuficha kabla ya kupeleka kwa wanunuzi wa jumla.

Suala hili ikabidi lipelekwe kwenye tume ya Mafia (nitaeleza baadae kuhusu Tume za mafia).
Kwa mshangao mkubwa Tume ikafikia hukumu kuwa ni kweli wanunuzi wa jumla wamemtapeli Don Di Pisa na kumpa hela ndogo..

Suala hili likawatia hasira familia ya La Berbaras na kuamua kuwawimnda na kuwauwa kuanzia aliyewatuma kupeleka mzigo marekani (Don Manzella) na waliyemkabidhi mzigo Don Di Pisa.

Kitendo cha kuuwawa kwa mabosi hawa kikaanzisha mtafaruku mkubwa baina ya familia tofauti tofauti ndani ya Mafia huku kila familia ikiegemea upande fulani.

Mtafaruku ukawa mkubwa kiasi kwamba ukatengeneza uhasimu wa familia tofauti ndani ya mafia na punde tu wakaanza kuwindana na kuuwana mchana kweupe.

Jambo baya zaidi hawakuishia kuuwana wenyewe kwa wenyewe tu bali pia hata wasiohusika walikumbwa na madhira haya.

Kwa mfano polisi waliokuwa wanahisiwa kuunga mkono familia fulani waliwindwa na kuuwawa na familia nyingine.

Pia marafiki wa familia hii waliwindwa na kuuwawa na familia nyingine.

Ndani ya miezi 6 ( May 1962 hadi January 1963) kulikuwa na vifo zaidi ya 700 vilivyosababishwa na ugomvi wa familia za Mafia.

Ndipo hapa serikali ikabidi kuingilia kati na kuanza kuusambaratisha mtandao wa Mafia.

Zikaendeshwa oparesheni maalumu za kijeshi kuwatambua na kuwakamata wanachama wa familia za mtandao wa Mafia.

Ndani ya miezi miwili pekee wanachama 177 wa familia za mafia walikamatwa.

Hii ikasababisha wanachama wengine wa familia zote kusitisha shughuli zao na kujificha.

Zaidi ya miaka mitano (1963 - 1968) hakukuwa na shughuli zozote za kihalifu za mtandao wa Mafia.





VITA KUU YA PILI YA FAMILIA ZA MAFIA


Kwa miaka mitano hakukuwa na shughuli za mtandao wa Mafia, lakini ilipofika mwishoni mwa mwaka 1969 taratibu sana mtandao wa mafia ukaanza kurejea tena katika shughuli zake.

Ilipofika mwaka 1970 nchini ufaransa serikali iliendesha oparesheni kali ya kufunga maabara za kihalifu zilizokuwa vinatengeneza madawa ya kulevya aina ya Heroin.

Pia walipiga marufuku uvutaji na uingizaji wa sigara nchini Ufaransa.

Hivyo basi uhitaji wa madawa aina ya heroin na sigara ukakua kwa kasi kubwa nchini ufaransa.

Mabosi wa mtandao wa Mafia wakaona fursa adhimu ya kibiashara. Hivyo basi wakaitisha mkutano na kusuluhisha migogoro yote iliyotokea huko nyuma.
Wakaweka lengo moja tu kuwa, mtandao wa Mafia uteke soko heroin na sigara nchini ufaransa na marekani.

Wakafungua maabara za kutengeneza heroin na kutengeneza mitandao ya kihalifu ya usambazaji mizigo.

Baada ya mwaka mmoja wakawa wameteka soko la heroin nchini Ufaransa.
Baada ya hapo wakaingia marekani hasa majimbo ya kaskazini na kuanza kutengeneza mitandao ya uuzaji na usambazaji wa heroin.

Hili walilifanikisha kwa ustadi mkubwa kwani, migahawa mingi ya kuuza Pizza (Pizzaria) nchini marekani ilimilikiwa na waitaliano.

Kwahiyo waliingia makubaliano na wenye migahawa ambapo mzigo wa heroin ulifikishwa kwao na wao walitumia kivuli cha kuuza pizza kuwapa wauzaji wa mtaani (street dealers).

Ndani ya miaka miwili tu Mafia wakawa wanamiliki 80% ya soko la heroin kwa majimbo ya kaskazini mwa Mareni.

Ndipo hapa wanasema "palipo ridhiki hapakosi fitna".

Mwaka 1975 kipindi ambacho mapato yatokanayo na shughuli za Mafia yako juu sana, kiongozi wa familia ya Carleone aliyeitwa Don Luciano Leggio ambaye pia alikuwa ni mjumbe wa tume ya Mafia (Mafia Commission) akaanzisha kampeni ya siri ya kuunganisha familia za Mtandao wa Mafia na akaziita Corleonesi yeye mwenyewe akiwa kama kiongozi Mkuu.

Lengo kuu lilikuwa ni kutawala kuatawala biashara na shughuli za Mafia huku wakiwatenga familia nyingine ambazo zilikataa kujiunga katika umoja huo wa Carleonesi.

Katikati ya mwaka 1975 Don Leggio akapata Bahati mbaya kukamatwa na serikali akishutumiwa kwa kosa la uuaji na akatupwa gerezani.

Hii ilimlazimu kumuachia madaraka msaidizi wake aliyeitwa Don Salvatore Riina.

Baada ya Don Riina kuchukua madaraka akaanzisha mipango ya kuwaondoa katika Tume Mabosi wa familia ambazo walikataa kujiunga na umoja wao wa Carleonesi.

Nieleze kwa ufupi kuhusu Tume ya Mafia (Mafia Commision)

Hiki ni kakao maalumu au baraza ambalo linaundwa na mabosi wa familia zote za Mafia.
Kazi kubwa ya Tume hii ni kusuluhisha migogoro, kugawa maeneo ya biashara na kuweka mikakati ya kibiashara.

Kwa hiyo Don Riina akatamani Tume hii itawaliwe na mabosi wanaounga mkono umoja wao wa Carleonesi pekee.

Hivyo akaanza kuzusha tuhuma za uongo dhidi ya mabosi wenzake ambapo tuhuma hizo zilisababisha mabosi hao kukosa sifa ya kuendelea kuwa wajumbe wa Tume ya Mafia.

Don Riina alienda mbali zaidi mpaka kufikia hatua ya kupanga mauaji ya mabosi wa familia zilizokuwa zimekataa kujiunga na umoja wa Carleonesi.

Hapa ndipo vita kuu ya pili ilipoanzia.

Wanachama wa familia nyingine nao wakaanzisha oparesheni za kulipa kisasi kwa kuuwa wanachama wa familia zilizojiunga katika umoja wa Carleonesi.

Lakini Don Riina alikuwa na mbinu adhimu za kihalifu. Alichokifanya ilikuwa ni kuwahonga baadhi ya wanachama wa familia pinzani ili kuwaua wenzao wanaoendeleza vita dhidi ya umoja wa Carleonesi.

Hadi kufikia mwaka 1978, Don Riina alifanikiwa kuiweka kiganjani Tume ya Mafia kwa kuingiza mabosi wa familia za umoja wa Carleonesi pekee na yeye mwenyewe akijipa cheo cha uongozi wa Tume ya Mafia.
Ndipo hapa alipopachikwa jina la "Boss of Bosses".

Baada ya mafanikio haya Don Riina akavimba kichwa zaidi.

Don Riina akaanzisha vita na waandishi wa habari walioiandika Mafia vibaya, akaanzisha vita na mauaji ya Polisi ambao waliendesha oparesheni zilizokuwa kinyume na mafia.

Don Riina akaenda mbali zaidi akaaendesha utekaji na mauaji ya viongozi wa serikali ambao walikuwa wanaipinga Mafia.

Mauaji haya yalikuwa ni mengi katika miaka ya 1980 kiasi kwamba ikaamsha hasira za wananchi.

Kwa miaka yote wananchi walikuwa wamejiweka kando (neutral) katika ugomvi wa serikali na Mafia.
Lakini kutokana na mauaji yaliyokuwa yanaendelea ikawafanya wananchi waanze kuipinga Mafia wazi wazi na kuanzisha harakati za kuishinikiza serikali kuitokomeza Mafia nchini Italia.

Mwaka 1988 serikali ikaanzisha rasmi oparesheni ya kuwasaka mabosi wa familia za Mafia.

Mwaka 1993 wakafanikiwa kumkamata Don Riina na kumtupa gerezanj.

Kitendo hiki kilikuwa kama kimewawehusha wanachama wa Mafia kwani wakaanza kutekeleza matukio ya kigaidi kitu ambacho hakikuwahi kushudiwa kikifanywa na Mafia hapo kabla.

Wanachama wa mafia wakaanzisha matukio ya kulipua majengo ya serikali, vituo vya mabasi, mahoteli na sehemu za utalii. Lengo lao kubwa lilikuwa ni kuishinikiza serikali kumuachia Don Riina.

Serikali ikasimama imara na kukataa kata kata kumuachia Don Riina.
Ndipo hapo ilipobidi Don Leoluca Bagarella arithishwe uongozi mwaka huo 1993.

Lakini Don Bagarella akafanya makosa ya kuendeleza staili ile ile ya uongozi ya Don Riina. Kuiandama serikali, waandishi wa habari na kuuwa wanachama wa familia nyingine ambazo hazipo kwenye umoja wa Carlonesi.

Hii ikisababisha Don Bagarella kutodumu sana kwenye uongozi kwani miaka miwili baadae yaani 1995 alikamatwa na serikali ya Italia na kutupwa gerezani.

Hii ikatoa fursa kwa uongozi mpya kushika hatamu, ambapo Don Bernardo Provenzano akachukua madaraka ya uongozi wa familia za Mafia.

Mara baada ya Don Provenzano kuchukua madaraka akajiapiza kuirudisha Mafia katika misingi yake ya weledi, ufanisi na kuheshimiana wenyewe kwa wenyewe (Loyalty).



KUREJEA TENA KWA MAFIA KATIKA "UTUKUFU" WAKE.

Don Provenzeno kwanza kabisa akapiga marufuku kwa wanachama wa Mafia kufanya mauaji ya viongozi wa serikali, waandishi wa habari na polisi.

Pia akapiga marufuku wanachama wa Mafia kuuwa mashahadi wa kesi za serikali dhidi ya Mafia na kama mbadala alianzisha utaratibu wa kuwahonga mashahidi na kuwatorosha wakaanze maisha sehemu nyingine.

Pia akamaliza kwa kusuluhisha vita zote za kifamilia katika mtandao wa Mafia na kuwasisitiza wao wote wako kwenye timu moja, kwamba ni wote ni ndugu chini ya mtandao wa Mafia.

Baada ya miaka kadhaa Mafia ikatulia na kurudi katika weledi na ufanisi wake.

Kuna tuhuma ambazo hazijathibitishwa zinazoeleza kwamba Don Provenzena aliwasiliana na Bw. Silvio Berlasconi ambaye alikuwa katika harakati za kuanzisha chama chake cha Ferzo Italia ili aweze kugombea Uwaziri Mkuu wa Italia.

Inasemekana kwamba Don Provenzeni alimpa ofa Berlasconi kuwa watamsaidia ashinde katika jimbo la Sicily na maeneo mengine ya nchi ambayo wanaushawishi.
Ombi lao kwao ni kwamba akiingia madarakani alegeze sheria zinazopinga Mtandao wa Mafia (anti-Mafia law) hasa hasa kipengele maarufu kinachojulikana kama "article 41-bis".

Shutuma hizi zimepingwa vikali na Silvio Berlosconi mwenyewe na chama chake lakini baadae Berlosconi alishinda uwaziri Mkuu akipita kwa kishindo katika jimbo la Sicily.
Pia mwaka 2002 kifungu cha sheria cha "article 41-bis" kiliacha kutumiaka, kitendo ambacho kilizua maswali mengi.

Don Provenzeno hakuishia hapo tu kudhihirisha kuwa japokuwa watangulizi wake walipenda utengano yeye anapendelea zaidi ushirikiano.

Ndipo hapa ambapo aliwasiliana na nguli wa mihadarati kutoka Mexico Bw. Joaquin Guzman au maarufu kama "El Chapo" na wakaanzisha ushirikiano wa kibiashara kati ya mtandao wa Mafia na genge la Sinaloa Cartel linalomilikiwa na El Chapo.

Pia Don alianzisha utaratibu maalumu wa kuwafanya wahalifu wa Mafia wawe wa kipekee.
Utaratibu huu aliuita "Pax Mafiosa" (Mafia Quietness (ukimya wa Mafia)).

Chini ya utaratibu huu aliamuru kwanza wanachama wote wa Mafia kuacha kujigamba na kujitanabaisha katika jamii. Aliamuru wanachama wa Mafia kuishi kama mashushushu bila watu kuwafahamu na shughuli zao ziendeshwe kimya kimya na kwa usiri mkubwa.

Chini ya Don Provenzena Mafia ikarudi katika "ubora" wake.

Ingawa Don Provenzena alikamatwa na kutupwa gerezani mwaka 2006, lakini bado alama yake ya kiuongozi (legacy) inaendelea kuiongoza Mafia mpaka leo hii chini ya Don Messina Denaro ambaye ndiye kiongozi wa sasa.

Mwisho.

The Bold.
Mkuu The bold siku moja ikikupendeza nitag katika nyuzi hizi mkuu unanitenga!!!!!
 
Back
Top Bottom