Ahsanteni wote mlio.comment kwenye huu uzi. Napenda kusema yafuatayo.
1. Wale mnaosema kuwa hii ni habari ni ya kutunga, napenda kuwaambia kuwa hata mimi natamani sana iwe its just a story, but kwangu mimi huo ndio uhalisia wangu, kwenu nyie it might be just a story, ila kwangu mimi ndio uhalisia. Nimekuwa nikiingia JF as a guest user kwa zaidi ya miaka miwili sasa, na nilipokuwa nafikiria sehemu ambayo naweza nikashusha yaliyo moyoni mwangu nikaona JF ni sehemu sahihi. Kwa hiyo ugeni wangu si hoja ya kufanya mtilie mashaka niliyoandika.
2. Nimeona watu wengi humu hasa wanaume wamenitukana na kunikejeli sana, lakini inbox yangu hadi sasa imejaa PM kama 25 ambapo 22 kati ya hizo zote ni za kunitongoza.
3. Nawashukuru sana walionipa moyo na kunishauri, wengine hadi wameni PM na kunipa ushauri zaidi inbox. Mwenyezi Mungu awabariki sana. Nilishaanza kupiga hatua katika safari yangu ya kubadilika na hadi sasa ninaendelea vizuri sana, nitatilia maanani sana ushauri wenu. This is what i needed.
4. Naamini my past is the past na kama nilivyosema naamini na ninafahamu kuwa naweza kuwa mke bora kabisa na nikawa mama bora pia,uamuzi uko juu yangu na nimeshaamua tayari na kama nilivyosema, nimeshaanza kupiga hatua.