Mzito Kabwela
Platinum Member
- Nov 28, 2009
- 18,908
- 7,751
Mimi nimemuomba jana contacts zake ili awe upande wa pili wa mahojiano..
Nasikiliza kipindi cha Jahazi hapa cha Clouds FM, Ephraim Kibonde na Gadna wametumia zaidi ya dakika 5 za kipindi chao wakiponda na kulalamika kuwa JF inajadili mambo binafsi ya watu badala ya kuzungumzia hoja.
WanaJF mnachukuliaje mtazamo huu?
Je, ni kweli kuwa hakuna mambo ya msingi tunayojadiliana hapa jamvini au mwenzetu ni kipofu hatembelei JF zaidi ya kusimuliwa yanayojiri humu??
Nlifikiria mletaji wa post hii angelituwekea hicho walichosema hasa. Mimi nahisi kuna ukweli wa waliyoyaongea kwa kiasi hicho hicho mleta post hii alichotujuvya.
Na majibu yaliyofuata baada ya post hii, mengi yao yameakisi kule kule kwanye madai ya walalamikiwa ie Kibonde na Gadna, watu badala ya kujadili uhalali wa madai yao, wamekwenda kwenye vitu visivyonamsingi wowote kwenye hoja yao au malalamiko yao, masuala ya elimu, nani kawatafutia kazi za utangazaji, itikadi zao za siasa hazihusu kitu kwenye mada hii au madai waliyoyatoa zaidi ya kuthibitisha kile wanachokilalamikia humu jamvini. Hayo ndiyo yale mambo binafsi wanayolalamika kuwa jamvini humu yanashikiwa bango kuliko hoja za maana.
Sote tunakumbuka majadala wa kipuuzi uliowahi kuletwa humu jamvini kuhusu "ukabila" wa mwanamziki nguli, Lady jaydee. Mjadala ule ni wazi kuwa uligusa maisha yake binafsi zaidi kuliko mambo mengi ya maana ambayo unaweza kumuongelea mtu kama Jay dee, ukabila wa mtu ni mambo yanayomhusu mwenyewe unless otherwise, ameyaweka mwenyewe katika mjadala wazi unaoleweka na siyo mtu akurupuke tu kuja na mada ihusuyo mambo ya mtu kujisifia tu kwa raha zake.
Nionavyo, watu humu wabadilike, waache kujifanya kujuwa kwingi na kudhihirisha kuelimika kwao kudogo, ambako wao wanakuona kukubwa, kwa kuacha kujadili "issues" na kujadili watu, hayo ni mambo ya walioishiwa na hoja kama vile mwanamme mpumbavu anaposhindana na mwanamke kwa maneno, mwishowe akishindwa anaamua kurusha ngumi. Tubadilikeni jamani! na si kila anayesema ukweli zidi yetu aonekane adui au haipendi JF, sisi si malaika kama kila kitu tupo sawa, tunakosea na tunawakosea watu, kama waungwana na wasomi kweli, tunavyojidai, basi tukubali kujisahihisha tunapoikosea, siyo kupayukwa payukwa pale ukweli unapotugusa.
Angalia hicho ulichokiandika hapo juu kinafanana na huo u-"great thinker" unaojinasibu nao? mm siuiti upuuzi kwasababu tu naheshimu maoni yako hata kama tunatofautiana kwa namna fulani. Ulitakiwa kama hujafahamu uulize na kuuliza haitokufanya uonekane mjinga hata kama ww ni Profesa au "great thinker No.1", mimi sikuongelea kuhusu thread yenyewe kumuhusu jaydee au yeyote yule, nilichokimaanisha hapo ni mjadala uliofuatia mada ile, watu wameongelea vitu private mno vya jaydee havihusiani hata na huo u-celebrity wake, uandishi ambao mm sijauona popote pale, hata hivyo vyombo vya habari vya majuu vinavyoandika kuhusu ma-celebs, vinaandika vitu relevants vya ma-celeb hao...si porojo tu.Sorry kwenye highlights umeandika upuuzi mtupu na umeonyesha uelewa mdogo,pengine wewe na wote wanaokusapoti kwenye upuuzi huo uelewa wenu pia una mashaka,either mmeguswa kutokana na ukweli kwamba ndiyo nyie kina Kibonde ama mna mahusiano ya karibu....Nasema ni upuuzi kwasababu hamjatumia muda kufikiri a little bit more.
JF ina majukwaa mengi,na kama wewe ni great thinker basi unajua nini maana ya celebrity,issue ambayo ina jukwaa lake.....Sasa ukienda kwenye jukwaa la celebrity ni kipi kinacojadiliwa humo ambacho si personal?
Kwa celebreities everything is a fair game,kama mjadala ulipekwa jukwaa la tofauti,hiyo si shida,eventually mods huamishia kunakohusika....Nendeni mkadig more deep utaona kwamba given their status,hata yaliyosemwa kuhusu wao si mabaya kabisaa!
Najua wengi wetu tunafikiri,lakini ni tofauti sana "Kufikiri zaidi kidogo" jambo ambalo wengi wetu hatufanyi humu!
Nasapoti pia wenye kuulizia elimu zao....Hatuwezi kuwa na watu bogus kwenye idara nyeti kama za kuwahabarisha wananchi kwa kisingizio cha ucelebrity,na kama hawaja qualify inavyotakiwa kwenye fani ni vyema pia tukajua,its time tukabadilika na ku run things professionaly na si kwa kujuana juana nk.