Mkuu mbona hauelewi? Mie sizungumzia beef lao,sipo hapa kama mshabiki wa Jay dee na wala sina chuki na clouds. Hata hivyo ni utoto kwamba uichukie clouds kwa sababu unampenda Jay dee au umchukie Jay dee kwa sababu unapenda clouds,hilo ni beef lao.
Kwahiyo naomba kwanza utambue kuwa sipo hapa kumshabikia Jay dee na wala sina chuki na clouds.
Hebu chukua mfano kama ile nyimbo ya Nay na Diamond halafu labda clouds wana beef na Diamond kama ilivyo kwa Jay dee. Au ile nyimbo ya Ali kiba na Jay dee single boy.
Hivi hizo nyimbo ukitoa sauti ya Diamond ktk nyimbo ya Nay, au utoe sauti ya Jaydee ktk nyimbo ya Ali kiba unafikiri kutakuwa na maana gani ya kupiga hizo nyimbo? Na muathirika hapo atakuwa ni nani ktk utoto wa aina hiyo?
Unajua huwezi kuzungumzia suala hili bila kugusia bifu la Clouds na Jide kwa kuwa ndio chanzo cha haya yote unless kama mtu atataka kuonesha upande mmoja wa tatizo... kwamba Clouds wanafanya wafanyayo bila sababu!
Tukirudi mfano wa wimbo wa Diamond vs Nay wa Mitego na ule Kiba vs Jay Dee, hii mifano haisadifu wimbo wa Alikufa kwa Ngoma hususani wimbo wa Diamond vs Nay Wa Mitego ambao sauti zao wameingiza kwa overlapping... ni kama majibizano fulani sasa katika mazingira kama hayo huwezi ku-mute coz' mashairi yameingiliana! So, ktk mazingira kama hayo, Diamond akipiga marufuku nyimbo au sauti yake isichezwe kwenye kituo chochote kile... NARUDIA ... KWENYE KITUO CHOCHOTE KILE manake haya mambo yapo kwenye stations zote! Ikitokea hali kama hiyo, Muziki Gani haitapigwa moja kwa moja kwa kuwa mashairi yameingiliana mno na hakuna option nyingine!
Ukija kwenye case ya Single Boy, Kiba vs Jide, huu wimbo hauna overlapping ya mashairi kwahiyo watakacho-opt ni kupiga verse ya kwanza na biashara itaishia hapo kv Jide amefanya verse ya pili exclusively! Na hili suala la wimbo kupigwa verse moja tu na kuhamia verse nyingine ni la kawaida sana studio hata pasipo na migogoro kama hii... kama wewe ni mtu wa disco, naamini umeona mara kadhaa hilo likifanyika pia kwahiyo hakutakuwa na jipya!!!!
Kutokana na ukweli huo, ndio maana hata hao Clouds wanashindwa kuipiga Hawajui ya Mwana FA featuring Lady Jay Dee kwavile kwenye huu wimbo sauti/mashairi yameingiliana sana sawa na wimbo wa Muziki Gani wa Nay vs Diamond na katika mazingira kama hayo kunakuwa hakuna option nyingine zaidi ya kuacha kuupiga moja kwa moja!!!
Tofauti na hayo, Amekufa kwa Ngoma, mashairi hayajaingiliana hata kidogo... sauti ya Jide inasikika kwenye chorus peke yake! Wimbo una zaidi ya dakika 4 wakati chorus zote ukichanganya, haifiki hata dakika moja! Kwahiyo huwezi kuacha kupiga 80% ya wimbo kwa ajili ya 20% iliyopo kwenye chorus pekee! Aidha, wimbo kupigwa bila chrous hata pasipo na migogoro nalo ni jambo la kawaida sana na kila wakati linafanyika na radio zote!!!
Suluhisho la haya ni moja tu... kumaliza mgogoro ingawaje wakati mgogoro unaanza, Ruge mara kadhaa alinukuliwa kama kuna tatizo wakutane waingalie tatizo lipo wapi hasa kisha wayamalize... unfortunately, Jide akakataa! Narudia, ukitaka kuwa fair, huwezi kukwepa kuelezea bifu lao!