Hili la Unyonyaji wa Clouds media huwezi kuliona kwa juu juu kama unavyochukulia mkuu.
Pata picha ni msanii gani amefikia mafanikio anayostahili chini ya media hii hususani kutokea pale kwenye jumba lao la THT?
Sikatai kwamba kuna wasanii wamejizika wenyewe lakini pia wapo wengi wanaliwa indirect bila wao kujua.
Unasema kwamba kwa nini wasanii wasiende radio nyingine!? Tatizo sio radio nyingine bali utambue Ruge na Kusaga ni zaidi ya clouds wanapokosana na msanii wanaziba mirija mingi na hyo ndio hofu kuu ya wasanii wetu wengi walioko chini ya hii media na ni haki yetu kuwasemea mana tunaishi nao huku mitaani tunajua jinsi gani wanalalamika lakini hofu inawatawala.
Wasanii wengi wanaogundua hili wanaongea kwa uchungu but hawana jinsi kwa sababu wameshika makali. Waliojaribu ni hao akina Jide, Wagosi, Sugu na vingega wengine lakini hawatoshi na hawana impact kubwa kwa maana waliobaki bado wanaiabudu clouds.!!
Hebu waonee huruma hawa wasanii wetu wanaolipwa kiduchu kwa kazi kubwa. Kazi anayofanya Barnaba sio wakua hapo alipo sasa stuka kaka...
Sasa hivi kuna chekeche cheke tour ya Kiba Tz nzima mtizame jasho analotoa halafu subiri akirudi kariakoo umuulize ameingiza sh ngapi kwa tour hiyo then utagundua ni kwa nini tunasema wananyonya.
Kama ni mmoja wa hapo mawingu I'm very sorry brother.
Umewataja waliothubutu... je, miongoni mwao nani yupo kwenye game zaidi ya Jide? Vinega gani unaowasema wewe manake ninaowafahamu ni kwamba walisharudi kujisalimisha kwa Clouds kwamba walikuwa wameingizwa chaka na Sugu... au kuna vinega wengine! Unawataja Wagosi... are serious man? Ulitarajia ile staili ya muziki wa Wagosi bado wangeendelea kutoboa wakati muziki umebadilika sana na wao hawataki kubadilika? Nani hivi sasa anaweza kukaa kusikiliza au ku-download wimbo unaozungumzia habari cjui za manesi, mwenyekiti wa mtaa cjui kafanya nini, matrafiki na mambo mengine kama hayo? Najua hata hao watatafuta mchawi kumbe mchawi ni wao wenyewe wasiotaka kubadilika kutokana na game lilivyo! Na hili la kutotaka kubadilika linawaathiri hata wanamuziki wa nje... sio Tanzania! Leo ukiangalia wanamuziki wa America wa miaka 10 iliyopita, majority hawapo kwenye game na hivi sasa kuna new faces na wale ambao bado wapo kwenye game ni kwavile wanajua soko linataka nini! Sasa ikiwa kote huko wengine wanaingia wengine wanapotea, what's so special kwa hawa wa Tanzania ambao mtu akipotea tu basi lazima atafute mchawi?? Q-Chifu alipopotea alimsingia Diamond kwamba kamroga... hao ndio Watanzania, hawakubali kwamba wana matatizo wao binafsi lakini kila linalotokea, lazima watatfuta mchawi!!!
Hip hop ambayo ameifanya mtu kama Sugu ni tofauti na hii ya sasa... so, usitarajie anakuja tena na mambo ya "Sugu moto chini, ooooo, Sugu moo chini, haaaaaa....!" halafu utarajie watu watakusikiliza na wakiacha kukusikiliza utafute mchawi! Mitoto ya zamani ilikuwa kama mazuzu, ukiiimbia kuku kapanda baiskeli, yenyewe inafurahia tu... hawa watoto wa dijitali nani umweleze habari za bata kavaa laizoni halafu ukipotezewa usingizie Clouds??
Tatizo lingine la hawa wakongwe ni kutotaka kukubali kwamba madogo wanaokuja kwenye game siku hizi wapo tight huku wao wakijivunia ukongwe! Huku mtaani unakutana na madogo wanaimba au wanadondosha ma-punch line hadi unawaogopa!
Umetaja THT... be honest! Hivi kweli unaweza kuwalinganisha wasanii wa THT na wasanii wengine ukiondoa wale ambao tayari wana majina makubwa? Au mafanikio unayosema wewe ni yapi?
Kwamba Clouds wanakata mirija yote!! Yaani unataka kuniambia Clouds wana ubavu wa kwenda kumwangia msanii kwenye radio mshindani wake? Au umesikiliza maneno ya Jay Dee? Hivi kweli unataka kuniambia yule Jay Dee wa Understand ft TID, Machoz, Malaika, n.k ndie huyu wa Joto Hasira na Yahya? Kuwa mkweli kisha ongea na nafsi yako ujitajie nyimbo tatu za JD unazozikubali kama hujakuta zote ni za miaka 5 iliyopita!!!
Yule mshikaji wake Mkoloni (jina limenitoka)! Katoa wimbo wala haeleweki ikiwa ni mdumange, mduara au ngoma za kwao Tanga! Watu wakikupotezea uwalaumu Clouds??
Tatizo wengi wenu mnasikiliza maneno ya watu ambao wameshindwa tayari na ukichunguza karibu wote ambao wanakuwa wanapiga kelele wanakuwa hawana jipya vinginevyo nitajie msanii mmoja ambae amelalamika wakati bado akiwa hot! Ngoma ikiwa hot haizuiliki hususani dunia ya leo yenye radio kila kona, social networks n.k coz' hivi sasa wanaosikiliza nyimbo kupitia radio ni wachache zaidi ukilinganisha na wale wanaosikiliza kupitia other medias!