Civil Engineers weka neno hapa.

Mjomba Fujo

JF-Expert Member
Oct 27, 2012
2,322
5,946
1710273328124.png

Angalizo;
Hii picha ya mtandaoni, kwa hiyo msitumie muda mwingi kuwasimanga waliojenga bali weka majibu ya kitaaluma.
 
Hii inaitwa flat slab (slab ambayo inaungwa moja kwa moja na nguzo bila uwepo wa mkanda). Kwa hapo, span ya jengo ni kubwa sana, angalau kidogo kungekuwa na nguzo zingine kati kati ili kugawa hiyo span. Hapo slab imeshindwa kujibeba yenyewe (self weight) ikaundergo deflection kabla hata mzigo mwingine kuwepo juu yake

Hiyo ni moja, lakini failure nyingine ya flat slab huwa inatokea kwenye perimeter ya column. Mfano wa flat slab ni sawa na mtu achukue sindano azisimamishe then juu aweke kitambaa cha nguo, muda wowote mzigo ukizidi kiasi kilichopigiwa hesabu, slab inatoboka kwenye nguzo na kushuka chini ndio maana wengine huwa wanaweka drop panel na column capital kwenye nguzo ili angalau kupunguza hiyo risk ya slab kutoboka
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom