Filosofia ya Rorya
JF-Expert Member
- Sep 20, 2021
- 3,214
- 3,587
Huduma ya UALIMU wa Neno la MUNGU kwa miaka ya karibuni imedhihiri kuwa na mlipuko wa kuenea kwa kasi ya ajabu kuliko huduma zingine kama Uchungaji, Uinjilisti na Ushuhudiaji.
Kabla ya majira ya mlipuko huo, huduma ya Ualimu wa Neno la MUNGU haikuwa na nafasi kubwa ndani ya Kanisa.
Makanisa mengi yalizuia huduma hii kama ambavyo Huduma (Ministries) zinazoendeshwa na Mitume na Manabii zinavyozuia pia huduma ya Ualimu wa Neno la MUNGU.
Hata hivyo, huduma hii imevamiwa na baadhi ya Watumishi wa kujipachika wasio na vigezo, ambao hata hivyo hawadumu na huduma hii bali wanalenga kutengeneza majina makubwa na baadaye kutamani huduma zingine za Utume na Unabii wanakoweza kumiliki Madhabahu, wafuasi na mapato. Mitume na Manabii wengi wamepatikana kwa njia hii.
Hii ndiyo hali iliyofanya wilaya ya Mbozi kuongoza dunia kwa uwiano wa Makanisa na watu (Church Per Capita).
Mwalimu mmoja wa Neno la MUNGU nilimhoji kuhusiana na madai haya, akajitetea kwamba Kanisa libebe lawama kwa sababu vyuo vya Kanisa havina mtaala wa mafunzo ya huduma ya Ualimu wa Neno la MUNGU.
Hali hii inatoa mwito kwa Makanisa kuja na mpango maalum wa kuwachagua, kuwapima, kuwachuja na kuwapa vibali/leseni Walimu wa Neno la MUNGU wanaojizukia na kutamalaki Madhabahu.
Soli Deo Gloria.
Kabla ya majira ya mlipuko huo, huduma ya Ualimu wa Neno la MUNGU haikuwa na nafasi kubwa ndani ya Kanisa.
Makanisa mengi yalizuia huduma hii kama ambavyo Huduma (Ministries) zinazoendeshwa na Mitume na Manabii zinavyozuia pia huduma ya Ualimu wa Neno la MUNGU.
Hata hivyo, huduma hii imevamiwa na baadhi ya Watumishi wa kujipachika wasio na vigezo, ambao hata hivyo hawadumu na huduma hii bali wanalenga kutengeneza majina makubwa na baadaye kutamani huduma zingine za Utume na Unabii wanakoweza kumiliki Madhabahu, wafuasi na mapato. Mitume na Manabii wengi wamepatikana kwa njia hii.
Hii ndiyo hali iliyofanya wilaya ya Mbozi kuongoza dunia kwa uwiano wa Makanisa na watu (Church Per Capita).
Mwalimu mmoja wa Neno la MUNGU nilimhoji kuhusiana na madai haya, akajitetea kwamba Kanisa libebe lawama kwa sababu vyuo vya Kanisa havina mtaala wa mafunzo ya huduma ya Ualimu wa Neno la MUNGU.
Hali hii inatoa mwito kwa Makanisa kuja na mpango maalum wa kuwachagua, kuwapima, kuwachuja na kuwapa vibali/leseni Walimu wa Neno la MUNGU wanaojizukia na kutamalaki Madhabahu.
Soli Deo Gloria.