""Kuna uwezekano mkubwa kabisa kwamba hao wauaji walikuwa ni wafungwa wa makosa makubwa kama ya mauaji na walitumiwa kwa kazi hiyo ambayo iliratibiwa na hao niliowataja hapo juu, ingawa hakuna ushahidi.
Hivyo wafungwa hao inawezekana wanasubiri kunyongwa kabisa kumaliza kazi na maisha yataendelea.""
Mkuu kuna kitu nimekuelewa hapo...kwenye hiyo comm'nt yako.. na ndio maana unakuta mission imefeli kabisa kutokana na kukosa uweledi.. lakini hata hivyo mpango si uliratibiwa na "inner cycles" wa MBS ...(kwa mujibu wa cia)..imekuwaje mpango upangwe kizembe namna ile ..??..
Khashoggi alikuwa anawindwa na lilikuwa ni suala la muda tu.
Kilichotokea yaani mission kufeli ni kwamba wale watu walikuwa wanatekeleza ile "extradition process" kwamba wamchukue na kumpeleka Riyadh.
Lakini alipokataa ndipo wakaanza kupigana humo ndani na masumbwi kutupwa lakini Khashoggi alikuwa pake yake dhidi ya watu zaidi ya 20, hivyo akashindwa vita hiyo na kudungwa sindano ya sumu au yenye dawa kali ya usingizi.
Dawa hiyo ilikuwa ni kali na ikamfanya apoteze fahamu na mwishoe kupoteza uhai na hayo ni maelezo ya majasusi wa Uturuki.
Khashoggi alifanya kazi ndani ya balozi za Saudia mjini London na Washington, hivyo alikuwa ni mmoja wa watu wa ndani kabisa yaani "jikoni".
Ukiwa mtu wa namna hii kwa nchi hizi kama Saudi Arabia, unatakiwa ama ukae kimya ule maisha au ujifiche kabisa, lakini sio kuonekana unatoa siri za wale waajiri wako wa zamani.
Kuna uwezekano mkubwa kabisa mauaji ya Khashoggi yangeweza kuepushwa maana iinaelezwa kwamba CIA na MI6 walifahamu juu ya mpango wa kumteka Khashoggi na kumuua wiki tatu kabla!
Ila tayari Inasemwa kwamba Mohammed bin Salman hakufahamu mpango huo kabisa, ingawa kuna mashaka juu ya hilo.
Hawa watu 15 walipelekwa Instabul kwa ajili ya kazi hiyo ya mauaji lakini Salman hakuwa anafahamu jambo hilo, hiyo ndo hitimisho.
Pia pale ubalozini kuna wafanyakazi wapatao 45 hivi na wote wanafanyiwa uchunguzi kubaini ni wepi walikuwa na mazungumzo na Khashoggi.