Huo Ni utani kwakweli
Nina jamaa zangu wamejiunga huko
Wanalalamika kuhusu huo utaratibu na mbaya zaidi wanalipishwa Ada nyingine ikiwa washamaliza kulipa Ada kamili ya mwaka husika
Hao jamaa wako vijijini huko hakuna network na wengine hata hio zoom hawaijui
Hiko chuo kinaleta utani
Kama wanataka face to face session wawaite kwenye vituo vyao wawafanyie hio ishu
Na kutaka walipe hizo session Tena ikiwa wamemaliza kulipa Ada Ni utapeli wa wazi wazi
Sent using
Jamii Forums mobile app
Kiongozi, hutaki kukubali mabadiliko, hao jamaa zako walio kijijini mmewasiliana kwa kutumia nini?
Kulipa Ada mara mbili? nawe pia umekubaliana na hili?? mwanafunzi akubali kulipa ada mara mbili!? nae amekubali??
Nakuwa na maswali sababu nimeona hii post yako ni kama umeandika kwa ushabiki na sio uhalisia! hao wanafunzi waliolipishwa ada mara mbili wamechukua hatua gani? je , hawana nyaraka za malipo ya ada ya awali??
Pia kiongozi, OUT imekuwa ikitoa distance learning! hivyo unavyozungumza swala la Corona nashindwa kupata logic yako hasa ni nini!
OREX imeanzishwa ili kukidhi mahitaji muhimu ya kupima uwezo wa wanafunzi juu ya yale aliyojifunza kwa njia ya mazungumzo, nashangaa mwanafunzi anachoogopa ni nini hasa! mpaka sasa ivi sijui nini drawback ya hii njia, kwa sabab ni assessment kwa njia ya mazungumzo,
Juu ya matumizi ya application ya zoom, mkuu umesema hana mtandao kijijini, then hapo hapo hawezi kutumia zoom!! tuelewe kipi kati ya hayo mawili?
Nadhani mshauri huyo rafiki yako ajifunze kutumia zoom kama alivyojifunza kutumia whatsapp.
Nimeandika ivo kwakuwa, sababu alizotoa hazina uzito ukilinganisha na faida zinazopatikana katika matumizi ya mtandao husika.
Huyo rafiki yako (zako) ni muoga wa kuongea Kiingereza, anabaki kutoa lawama!
Nashangaa sana, kwa wewe unaelalamika juu ya elimu masafa inayotolewa na OUT lakini unasahau kuwa wanazuoni wengi hapa tanzania wamesoma kwa elimu masafa toka vyuo vya nje! nina ushahidi mkubwa sana katika taasisi zitoazo Elimu ya juu!
Mkuu, badilika, usichukue maneno ya mtu mmoja ukaja na hitimisho bila kautafiti kadogo, OUT, inahitaji ujipange hasa, na unasisitizwa kuwa flexible ili kuendana na aina ya elimu itolewayo hapo.
Vitu muhimu ni kuwa na
1. Muda
2. Simu janja (smartphone) computer, etc.
3. Flexible
4. Focused
5. Curious kujua matumizi ya apps za mawasiliano eg. youtube, moodle, zoom, whatsup etc etc
Hongera kwa Menejiment ya OUT kwakuendana na technologia ya kisasa