Lord OSAGYEFO
JF-Expert Member
- Feb 19, 2021
- 3,086
- 4,881
Hakika jiji la Dar es Salaam limevamia na wafanyabiashara wajasiamali maarufu machinga, mama lishe, wauza chips wauza mitumba kila kona. Wametanda pembezoni mwa barabara mbalimbali za jiji wakifanya biashara.
Posta ndio usiseme kila sehemu ni vibanda vya mitumba, mama lishe wakipika vyakula mbalimbali, vibanda vya wauza chips vimeshamiri mpaka imekuwa kero.
Hatukatai machinga kufanya biashara lakini watengewe maeneo rasmi sio barabarani au mbele za maofisi na maduka. Ukifika chuo cha IFM wauza mitumba, wachoma chips wamejaa eneo la chuo mpaka shule ya msingi bunge.
Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
Posta ndio usiseme kila sehemu ni vibanda vya mitumba, mama lishe wakipika vyakula mbalimbali, vibanda vya wauza chips vimeshamiri mpaka imekuwa kero.
Hatukatai machinga kufanya biashara lakini watengewe maeneo rasmi sio barabarani au mbele za maofisi na maduka. Ukifika chuo cha IFM wauza mitumba, wachoma chips wamejaa eneo la chuo mpaka shule ya msingi bunge.
Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app