Lord OSAGYEFO
JF-Expert Member
- Feb 19, 2021
- 3,086
- 4,881
Ukweli utawala wa awamu ya 5 kuruhusu wamachinga na mama lishe.
Kufanya biashara popote watakapo na wasibughudhiwe ulikuwa na ushamba wa aina yake. Zamani maeneo ya Posta yalikuwa ni maeneo ya kuvutia sana sio kwa wageni bali hata kwa wenyeji.
Yalikuwa masafi yasiyo na misongamano ya hovyo kama Manzese, Kariakoo, Mwenge, Buguruni na Mbagala. Leo Posta ni kama hayo maeneo.
Wamachinga wamepanga bidhaa zao mpaka barabara, mama lishe na majiko yao wanapika supu chai na chapati bado kidogo kuna mtu ataweka jiko la kuchoma mahindi na viazi kwenye Mnara wa Askari.
Tunaiomba manispaa ya jiji iwaondoe kabisa wamachinga na mama lishe eneo hilo na maeneo ya ofisi za umma ili kulifanya liwe safi na kuvutia.
Kufanya biashara popote watakapo na wasibughudhiwe ulikuwa na ushamba wa aina yake. Zamani maeneo ya Posta yalikuwa ni maeneo ya kuvutia sana sio kwa wageni bali hata kwa wenyeji.
Yalikuwa masafi yasiyo na misongamano ya hovyo kama Manzese, Kariakoo, Mwenge, Buguruni na Mbagala. Leo Posta ni kama hayo maeneo.
Wamachinga wamepanga bidhaa zao mpaka barabara, mama lishe na majiko yao wanapika supu chai na chapati bado kidogo kuna mtu ataweka jiko la kuchoma mahindi na viazi kwenye Mnara wa Askari.
Tunaiomba manispaa ya jiji iwaondoe kabisa wamachinga na mama lishe eneo hilo na maeneo ya ofisi za umma ili kulifanya liwe safi na kuvutia.