Chonde chonde chama changu CHADEMA

Chonde chonde chama changu CHADEMA

Kwa magamba kupokelewa kutoka stesheni ya reli ni sawa. Cdm, mara intelijensia, mara foleni, mara barabara nyembamba...
tungekuwa na malengo kama wenzetu CCM tungekubaliwa
 
mkuu mtu mwenye akili timamu hata siku moja hawezi shabikia mambo yanayoweza hatarisha amani ya nchi

Aliyekwambia Tanzania tuna amani ni nani?

WATANZANIA TUNA UWOGA , SIO AMANI TUNADANGANYWA, sacrifice for your son and daughter AMKA KIFIKRA.
 
kaka ben huwezi fananisha ujerumani na tanzania kumbuka kule kulikuwa na utawala dhalimu,,,, mandela alipambana na wakoloni sasa sisi tuko huru tunajitawala wenyewe unajua kuruhusu maandamano hovyo inaweza kutokea ya misri nchi yetu ni changa sana kubeba madhila hayo ni bora tuone mbali bora ungefanyika mkutano bila maandamano

Bora kuwa maskin wa mali kulko wa akili,hv wew unajitawala au unatawaliwa?Yanayotendka Tz n haki?Wewe umetumwa na CCM.
 
mkuu haki ipi unajua tanzaniaa siku zote ina bahati ya kupata viongozi wapole na wasikivu hv tunaonewa na nini sisi?? mamlaka hii hata mbowe ameikubali na hata ikulu walienda kumwangukia rais sasa napata shida na kauli zako
Mimi sipati shida na kauli zako. Na kama hujui Haki zipi nazungumzia, hata mimi sijui Amani ipi unayoizungimzia!!

MUNGU IBARIKI TANZANIA!!!!
MUNGU IBARIKI CHADEMA!!!!
 
Bora kuwa maskin wa mali kulko wa akili,hv wew unajitawala au unatawaliwa?Yanayotendka Tz n haki?Wewe umetumwa na CCM.
vipi matokeo yako ya form four umepata ngapi???
 
Mimi sipati shida na kauli zako. Na kama hujui Haki zipi nazungumzia, hata mimi sijui Amani ipi unayoizungimzia!!

MUNGU IBARIKI TANZANIA!!!!
MUNGU IBARIKI CHADEMA!!!!
mkuu acha kumkufuru mungu huna amani?? nenda kongo,,rwanda na mali ukajionee tusishabikie ujinga
 
Aliyekwambia Tanzania tuna amani ni nani?

WATANZANIA TUNA UWOGA , SIO AMANI TUNADANGANYWA, sacrifice for your son and daughter AMKA KIFIKRA.
akianza mwenyekiti wangu kuji sacrifice na mimi ntafuata
 
Wandugu nawaomba viongozi na wanachama wote wa CHADEMA kuachana na suala la maandamano ya DSM nawashauri watii mamlaka zilizopo hata biblia inatuagiza.

Tutaumiza wanachama wetu bure chonde chonde jamani AMANI NI KITU CHA THAMANI KUBWA HAIPATIKANI KWA BEI RAHISI

Mwungwana

Hebu kwa uungwana wako kabisa, unaweza kutuambia wananchi wenzako na Watanzania wenzako tunaoomba nchi hii itamalaki amani inayotokana na kuonekana kutendeka kwa haki na matumaini ya wananchi kwa viongozi wao, mapokezi yapi yaliwahi kuuwa watu au kuumiza watu?

Unajua maana ya neno mamlaka ambalo moja ya vitabu vitakatifu, kama ulivyokinukuu, kimelizungumzia? Je unajua kuwa mamlaka huendana na uhalali kutoka kwa watu?

Nikuulize pia, CHADEMA wakiachwa wakawapokea wabunge wao kisha wakaelekea kwenye eneo la mkutano, nani ataumia?

Hivi pale Morogoro, Jeshi la Polisi walipoamua kuvuruga mapokezi ya wana CHADEMA waliokuwa wanakwenda kuwapokea viongozi wao kutoka Dar es Salaam, yaliyoua ni mapokezi au ni polisi, waliokubali kutekeleza maagizo ya CCM na baadhi ya watendaji serikalini?

Ujumbe wako kamanda ulifaa kweli kweli kwenda kwa akina Kova na nwenzake akina Kenyela, ambao hawana sababu yoyote ya kutumika kudhihirisha hofu ya CCM mbele ya Watanzania?
 
mwungwana

hebu kwa uungwana wako kabisa, unaweza kutuambia wananchi wenzako na watanzania wenzako tunaoomba nchi hii itamalaki amani inayotokana na kuonekana kutendeka kwa haki na matumaini ya wananchi kwa viongozi wao, mapokezi yapi yaliwahi kuuwa watu au kuumiza watu?

Unajua maana ya neno mamlaka ambalo moja ya vitabu vitakatifu, kama ulivyokinukuu, kimelizungumzia? Je unajua kuwa mamlaka huendana na uhalali kutoka kwa watu?

Nikuulize pia, chadema wakiachwa wakawapokea wabunge wao kisha wakaelekea kwenye eneo la mkutano, nani ataumia?

Hivi pale morogoro, jeshi la polisi walipoamua kuvuruga mapokezi ya wana chadema waliokuwa wanakwenda kuwapokea viongozi wao kutoka dar es salaam, yaliyoua ni mapokezi au ni polisi, waliokubali kutekeleza maagizo ya ccm na baadhi ya watendaji serikalini?

Ujumbe wako kamanda ulifaa kweli kweli kwenda kwa akina kova na nwenzake akina kenyela, ambao hawana sababu yoyote ya kutumika kudhihirisha hofu ya ccm mbele ya watanzania?
narudia tena naumia sana na nafsi zinazojeruhika mantiki yangu ni kwamba kama polisi wamekataa haina haja ya kushindana
 
Wandugu nawaomba viongozi na wanachama wote wa CHADEMA kuachana na suala la maandamano ya DSM nawashauri watii mamlaka zilizopo hata biblia inatuagiza.

Tutaumiza wanachama wetu bure chonde chonde jamani AMANI NI KITU CHA THAMANI KUBWA HAIPATIKANI KWA BEI RAHISI
Ni haki yao kikatiba,polisi wanatakiwa wawepo ili kulinda amani tu na si vinginevyo,watakao umiza watu ni polisi sio CDM,au umesahau kuwa sasa hivi polisi ni adui ya wananchi kwa matukio mbalimbali ya uuwaji wa raia wasio na hatia kwa kisingizio cha kuuwawa na "kitu chenye ncha kali''kwa taarifa yako nchi nyingi zilipita kwenye hii hali unayosema ya AMANI lakini wanaoharibu AMANI sio raia ila ni watawala kwa kubinya demokrasia hadi inafika mahali wananchi wanasema liwalo na liwe,umesikia ya mtwara????vyama tisa vimesema vinaandaa maandano makubwa kuhusu ule mtanange wa gesi baada ya kugundua kuwa Waziri mkuu aliwadanganya alipotembelea mtwara wakati serikali inajua kabisa kuwa mpango wa ujenzi wa bomba la gesi uko palepale na vimesema havitaomba kibali polisi kwani hiyo ni haki yao ya msingi sasa wewe hapo unasemaje???.Kutoweka kwa amani TZ ni suala la muda tu wala usijifariji kuwa una amani ya kudumu hapa kama watawala wenyewe ni hawa.
 
ni haki yao kikatiba,polisi wanatakiwa wawepo ili kulinda amani tu na si vinginevyo,watakao umiza watu ni polisi sio cdm,au umesahau kuwa sasa hivi polisi ni adui ya wananchi kwa matukio mbalimbali ya uuwaji wa raia wasio na hatia kwa kisingizio cha kuuwawa na "kitu chenye ncha kali''kwa taarifa yako nchi nyingi zilipita kwenye hii hali unayosema ya amani lakini wanaoharibu amani sio raia ila ni watawala kwa kubinya demokrasia hadi inafika mahali wananchi wanasema liwalo na liwe,umesikia ya mtwara????vyama tisa vimesema vinaandaa maandano makubwa kuhusu ule mtanange wa gesi baada ya kugundua kuwa waziri mkuu aliwadanganya alipotembelea mtwara wakati serikali inajua kabisa kuwa mpango wa ujenzi wa bomba la gesi uko palepale na vimesema havitaomba kibali polisi kwani hiyo ni haki yao ya msingi sasa wewe hapo unasemaje???.kutoweka kwa amani tz ni suala la muda tu wala usijifariji kuwa una amani ya kudumu hapa kama watawala wenyewe ni hawa.
amani ni tunda la gharama ni vyema kuilinda kuliko mboni la jicho lako
 
kaka ben huwezi fananisha ujerumani na tanzania kumbuka kule kulikuwa na utawala dhalimu,,,, mandela alipambana na wakoloni sasa sisi tuko huru tunajitawala wenyewe unajua kuruhusu maandamano hovyo inaweza kutokea ya misri nchi yetu ni changa sana kubeba madhila hayo ni bora tuone mbali bora ungefanyika mkutano bila maandamano

Mwungwana

Unataka CCM na serikali yao wafanye yapi ndiyo utambue kuwa wameshafika level ya Hitler au makaburu wa Afrika Kusini, ambao wewe unawaita wakoloni. Kumbuka ukaburu si rangi...

Wanaua watu kwa risasi, (refer. mauaji ya Daudi Mwangosi, Ally Zona, Mbwana Masoud, Msafiri Mbwambo, n.k), bila hatia kama ambavyo walifanya akina Hitler, Botha na wenzake na wengine wote wa namna hiyo, kwa sababu tu wanapingana nao kimawazo na kupinga ufisadi na ubadhirifu wanaofanya dhidi ya nchi.

Wanafunga uhuru wa fikra na mawazo mbadala, (kufungiwa kwa Mwanahalisi), wanateka, kutesa na kuua, refer Dkt. Ulimboka, vitisho kwa viongozi wa kisiasa kama Dkt. Slaa, Mnyika na Lema na viongozi wa makundi mbalimbali katika jamii wanaopigania haki na stahili za Watanzania.

Sasa wanafikia mahali wanaanza hata kuwabana wawakilishi wa wananchi ndani ya bunge, ambapo kiuhalisia ni kwamba wanazuia wananchi wasiiwajibishe serikali, bado unaona CCM na serikali yake wanastahili kuangaliwa tu!

Nimekutajia baadhi ya matendo ya Ki-Hitler na Kikaburu kwa uchache sana.

Nakuuliza tena, kwa uungwana wako mwungwana, tuambie basi mapokezi ambayo yaliwahi kuua watu, kuumiza watu au kuvuruga amani kwa namna yoyote ile..
 
Mwungwana

Unataka CCM na serikali yao wafanye yapi ndiyo utambue kuwa wameshafika level ya Hitler au makaburu wa Afrika Kusini, ambao wewe unawaita wakoloni. Kumbuka ukaburu si rangi...

Wanaua watu kwa risasi, (refer. mauaji ya Daudi Mwangosi, Ally Zona, Mbwana Masoud, Msafiri Mbwambo, n.k), bila hatia kama ambavyo walifanya akina Hitler, Botha na wenzake na wengine wote wa namna hiyo, kwa sababu tu wanapingana nao kimawazo na kupinga ufisadi na ubadhirifu wanaofanya dhidi ya nchi.

Wanafunga uhuru wa fikra na mawazo mbadala, (kufungiwa kwa Mwanahalisi), wanateka, kutesa na kuua, refer Dkt. Ulimboka, vitisho kwa viongozi wa kisiasa kama Dkt. Slaa, Mnyika na Lema na viongozi wa makundi mbalimbali katika jamii wanaopigania haki na stahili za Watanzania.

Sasa wanafikia mahali wanaanza hata kuwabana wawakilishi wa wananchi ndani ya bunge, ambapo kiuhalisia ni kwamba wanazuia wananchi wasiiwajibishe serikali, bado unaona CCM na serikali yake wanastahili kuangaliwa tu!

Nimekutajia baadhi ya matendo ya Ki-Hitler na Kikaburu kwa uchache sana.

Nakuuliza tena, kwa uungwana wako mwungwana, tuambie basi mapokezi ambayo yaliwahi kuua watu, kuumiza watu au kuvuruga amani kwa namna yoyote ile..
huo ni UCHOCHEZI tu
 
akianza mwenyekiti wangu kuji sacrifice na mimi ntafuata

Aliwahi kusema alipokuwa Marekani akiongea na waatanzania wanaoishi huko kwamba
,

"Katika vita hii ya kutafuta ukombozi wa taifa hili, mkiniona mimi MBOWE nimepigwa risasi nimeanguka chini, MSILIE! chukueni mwili wangu muusogeze pembeni na msonge mbele mpaka ukombozi upatikane."
 

Aliwahi kusema alipokuwa Marekani akiongea na waatanzania wanaoishi huko kwamba
,

"Katika vita hii ya kutafuta ukombozi wa taifa hili, mkiniona mimi MBOWE nimepigwa risasi nimeanguka chini, MSILIE! chukueni mwili wangu muusogeze pembeni na msonge mbele mpaka ukombozi upatikane."
haha does it makes real sense?
 
Back
Top Bottom