Chombo cha NASA chafanikiwa kutua Sayari ya Mirihi (Mars), kitakusanya na kurudisha sampuli za mawe duniani

Sam Gidori

Senior Member
Sep 7, 2020
165
414
Shirika la Marekani la Utafiti wa Anga (NASA) limesema ndege yake ya utafiti imefanikiwa kutua katika Sayari ya Mirihi (Mars) imefanikiwa kutua salama na kushusha kifaa cha utafiti kilichopewa jina Perseverance katika sayari hiyo nyekundu.

1613684476490.png


Hii ni hatua mpya katika utafiti wa anga za juu, ambapo kifaa hicho chenye ukubwa unaolingana na gari dogo kitakusanya sampuli za mawe kutoka katika sayari hiyo na kuyaleta duniani kwa mara ya kwanza katika historia ya mwanadamu.

Lengo la kutuma kifaa hicho cha utafiti ni kuangalia uwezekano wa kuwapo uhai katika sayari hiyo ya nne katika Sayari za Mfumo wa Jua, na kitapeleleza kwa muda wa miaka miwili.

Kwa sasa, wahandisi na wafanyakazi wa NASA wanashusha pumzi ya ahueni baada ya chombo hicho kufanikiwa kutua, kwani ni takriban nusu tu ya vyombo vya anga vilivyowahi kutumwa katika Sayari Nyekundu vimefanikiwa kutua salama!

Matokeo ya utafiti utakaofanywa na chombo Perseverance utamsogeza mwanadamu karibu zaidi na lengo la siku moja kuishi katika Sayari ya Mirihi. Licha ya kutumia gharama kubwa ya zaidi ya dola bilioni 3 (Sawa na zaidi ya Tsh. trilioni 6 na bilioni 900), NASA ina matumaini ya kupata matokeo yenye kulingana au zaidi ya thamani hiyo ya fedha kutokana na utafiti huo.

Chombo hicho kimetua karibu na eneo lililopewa jina Kreta ya Jezero, bonde lenye upana wa kilomita 12 lililopo karibu na Ikweta ya sayari hiyo. Eneo hilo linaaminika kuwahi kuwa na mto uliotengeneza delta zaidi ya miaka bilioni 3.6 iliyopita, hivyo kufanya uwezekano wa kuwapo viumbe hai au masalia ya viumbe hai kuwa mkubwa.

1613684449422.png

Marekani inapewa changamoto na mataifa ya China na Umoja wa Falme za Kiarabu ambao pia wametuma vyombo vyao vya anga katika Sayari hiyo Nyekundu kupeleleza uwezekano wa uwepo wa uhai. Wingi wa shughuli za anga katika sayari hiyo kunaifanya kuwa kitovu cha utafiti wa anga za juu kwa takriban kipindi cha karne ijayo.
 
Wazungu wanawekeza nguvu nyingi kwenye maswala ya anga za mbali ambako hata wakisema wakaishi huko maisha yatakuwa ya gharama kubwa kuliko hapa duniani ambako bado hawajapamaliza.

Sijui kuna nini kwenye hizi mission zao
Sababu dunia haitaendelea kuwepo milele na wala haitoweza kuwa inhabitable milele.

Wako wapi Dinosaurs?

Wanachofanya ni kugeuza human specie kuwa multi planetary.

Hivyo kama siku kukitokea threat ambapo itapelekea dunia kuwa uninhabitable. Means itabidi binadamu wafanye fast evacuation to another planet ili human specie kutobecome extinct kama dinosaurs.

Wao wanajaribu na kujitahidi kuona future kwa ajili ya future humans na sio kuwa selfish.
 
Well done NASA.
Jurjani umeona lakini?
Wewe hapo umeona nini ? Mpaka unaniuliza kama nimeona?

Kwani hapo bibie kitu kimekufanya mpaka ukasidikisha hiyo habari? Je, hukuona haja ya kuhoji au hupaswi kuhoji?

Mimi mpaka hapo nina maswali zaidi ya matatu ya kuhoji juu ya habari hiyo. Huku ushahidi wa picha nikiudhohofisha sababu hata mimi naweza kubuni picha kama hiyo.

Tukirudi katika swali lako, hapo nimeona picha tu sijaona kipya. Ili niweze kuwaamini tu ni kuwa watuambie kwanini walituambia kuna mtu alienda mwezini na kwanini hawaendi tena?
 
Wenzako wanajifungia ndani wanafanya tafiti za mabilion ya pesa wewe from no where.. i mean not from no where like no where yani kwenye sofa la shemeji yako hapo unaita "UONGO".
Unao ushahidi wa haya unayo yaandika au huwa unayasoma kama habari tu za kwa kwenye magazeti.
 
Naanza kuunganisha doti kuwa huwenda Ilipokuwa iikisemwa kuwa toka nchi uipendayo na uende nchi nyingine huwemda watu enzi hizo waliweza kitoka sayari moja kwenda nyingine.

Ama inaposemwa kuwa akatoka na kwenda mbali na uso wa bwana huwenda ilikua kutoka sayari moja kwenda nyingine.

Au kwa ujumla space yoote au mjumuiko wa sayari zote ndio dunia na yayari mojamoja ndio nchi ama miji. Who knows hapo mars ndio miji ya sodoma na gomorah?
 
Back
Top Bottom