Chombezo: Chachandu za Beka wa Tanga

Chombezo: Chachandu za Beka wa Tanga

Hatareeeee!!Mtam kama Mcharo!!

Lakini hii sasa sifa kila siku Beka!
Tunaumizana Dushe jamani!
 
Kila ninapomaliza kusoma hii hadithi vyombo vinaamka balaa
 
Mpenzi msomaji, wiki iliyopita niliishia pale
Beka ambaye ameanza kuwashughulikia
viumbe alipokivamia kifua cha Rey na
kukiletea fujo za kutosha kwa kuzipekecha
embe bolibo zake , sijui kazing ’ ataje hadi
mtoto wa watu akawa hoi. Je, kilifuatia nini?
Songa mbele na chombezo hili lisiloisha
utamu.
Baada ya kuona Rey kaishiwa nguvu na
kabaki kamtumbulia macho , Beka aliyekuwa
kalishika jambia lake kali aliliweka ndani ya
ala ya Rey aliyewahi kulicheza segere la
wakubwa mara mbili tangu akue, mtoto wa
kike akatoa ushikiriano mzuri .
Kutokana na ushirikiano wa uhakika aliotoa
Rey wa kwenda kulia Beka alipokwenda
upande huo na kwenda kushoto Beka
alipomtaka kufanya hivyo na kubinjukia juu
Beka alipomuinulia pande hizo ,wote wawili
walivunja madafu kwa pamoja .
Jambo ambalo ni nadra sana kutokea kwa
wanaume wengi , licha ya Beka kuvunja dafu
na kumnywesha Rey aliyelipokea kwa
mhemko wa hali ya juu, bado damu
ilimwenda kasi , si akaendelea kucheza
pekechapekecha.
Kutokana na jinsi Rey alivyokuwa
akihamasisha kufuatia kila kiungo chake
kuwa softi kama siyo laini , kijana huyo
ambaye kuanzia leo namwita kijana wa kazi,
akapasua tena dafu la pili ambalo lilikuwa
tamu sana na kumnywesha mtoto wa watu ,
Rey akawa hoi.
Wakati Beka akifanya yake , mzee Kibandiko
naye kule chimbo alikuwa akimpelekesha
puta mama Havijawa aliyetoa ushikirikiano
kwa kuzungusha nyonga kama Wamachinga
wanapocheza ngoma yao ya Sindimba.
Mzee Kibandiko ambaye hakuna kitu
asichokipenda kwenye ulimwengu wa
malovee kama kumuacha mwenzake
akihangaika juu ya mnazi.
Alipoona anakaribia kupasua dafu alimsubiri
mama huyo, mama Havijawa aliposogea
karibu kabisa akalipasua dafu kwa ufundi na
kunyweshana maji yake kwa pamoja .
“ Sikutegemea kabisa kama unayaweza
mambo!” mama Havijawa alimwambia mzee
Kibandiko akiwa kajilaza hoi .
“ Kwa nini unasema hivyo ?” mzee Kibandiko
aliyekuwa anajua kilichomfanya mama huyo
kutoa kauli hiyo alimuuliza.
“ Wewe ni noma tena balaa wa malavidave ,
yangekuwa yanafundishwa ningesema una
Phd, ” mama Havijawa alifunguka ,
wakacheka .
Mama huyo alimwambia mzee Kibandiko
kwamba alimkumbusha enzi za usichana
wake wakati akitoka na kijana aliyemuingiza
kwenye ulimwengu wa mapenzi .
“ Alikuwa anakufanyia nini?” mzee Kibandiko
alimwuliza .
“ Si kama ulivyonifanyia wewe !” mama huyo
alimwambia.
“ Mimi nimekufanyia nini?” mzee Kibandiko
alimwuliza .
“ Umeniandaa vizuri sana halafu hujaniacha
hewani, yaani kuanzia leo nitakula sahani
moja na mkeo na ikibidi kuwa nyumba ndogo
yako ya kudumu na iwe hivyo ,” mama
Havijawa alimwambia mzee Kibandiko
aliyeishia kucheka.
“ Hata wewe umenikumbusha enzi za ujana
wangu ulivyokuwa unanifanyia, hakika
wanawake wa Tanga mmejaaliwa kuijua
sanaa ya mapenzi , ” mzee Kibandiko
alimwambia mama huyo.
Wawili hao walisifiana na kutaniana na
mwisho walikubaliana kukutana tena
Jumamosi iliyofuata ili wapeane mahabati ya
kutosha .
Kwa kuwa siku hiyo mzee Kibandiko alikuwa
na fedha za kutosha alimpatia mama huyo
shilingi 20, 000 kisha wakaoga pamoja ,
wakapigana mabusu ndipo mzee huyo
akatangulia kutoka na kushika njia kwenda
kwake.
Mama Havijawa ambaye hakutegemea
kupata mshiko ule na jinsi mzee Kibandiko
alivyoijua sanaa ya mapenzi , akaishia
kutabasamu na kuahidi kutomuacha .
Mama huyo alitoka pale gesti akiwa na aibu
flani hivi , si unajua tena alitoka kuchepuka
na mume wa mtu na isitoshe bado ilikuwa ni
mapema!
Kule nyumbani kwa mzee Kibandiko, tayari
Beka alishamsindikiza Rey akawa amelala
chumbani kwake kwa uchovu wa kazi nzito
aliyoifanya, kwani ndani ya muda mfupi
alikuwa ameshawacharaza mtu na mdogo
wake bakora nne.
“ Hivi sasa nimefungulia mbwa, msichana
yeyote atakayejipendekeza simuachi ng ’ o!”
Beka aliwaza .
Kijana huyo hakuishia hapo , alipanga kwenda
kuwatambia rafiki zake ambao walikuwa
wakimcheka na kumwambia alikuwa mtoto
wa mama kwa vile alikuwa akipenda kukaa
nyumbani .
Wakati Beka akiwaza hivyo , nyumbani kwa
akina Rhoda hakukuwa shwari kwani
msichana huyo alimbana Rey amweleze
kilichomfanya achelewe .
“ Dada Rhoda jamani , nilipotoka kwa Beka
nilipitia kwa akina Raheli nimepiga naye stori
kidogo nikaondoka ,” Rey ambaye kwa mtu
makini angemtambua kwamba alitoka kula
tenda muda mfupi uliopita alimwambia dada
yake .
Hata hivyo , utetezi wake haukusaidia kwani
Rhoda alihisi kuna kitu cha ziada walikifanya
na Beka , akaamua kumfuata Raheli kupata
ukweli.
Wakati Rhoda akielekea huko, huku nyuma
Rey alikosa raha sana kwani alijua uongo
wake ungebainika na ambacho kingefuatia ni
mtifuano tu !
“ Hata akijua nimetoka na Beka poa tu , kwani
nami nampenda sana, ” Rey alijisemea
moyoni.
Rhoda hakutumia muda mrefu alirejea na
kumwambia Rey kwamba alikuwa na bahati
sana kwani Raheli alimhakikishia kwamba
alipitia kwao .
“ Una bahati sana Raheli kaniambia ulipitia
kwao , leo hapa nyumbani ungepaona
pachungu,” Rhoda alimwambia Rey .
“ Tatizo dada Rhoda huwa hupendi kuniamini,
sasa wewe ulifikiria naweza kukusaliti kwa
mpenzi wako ?” Rey alimuuliza dada yake
huku akimshukuru sana Raheli kumwambia
alipitia kwao .
Beka akiwa amelala hajiwezi kwa uchovu
alimsikia baba yake aliyekuwa karejea
akimwita, alipoitika mzazi wake huyo
akamuuliza alikuwa akifanya nini,
akamwambia alilala .
Alipopewa jibu hilo alihisi Beka ambaye
alikuwa kaanza utundu wa mademu alikuwa
na msichana ndani, si akazama chumbani
kwake.
Mzee huyo ambaye kichwani alikuwa ziro
kama siyo sifuri , alipoingia chumbani na
kuona kitanda kipo vuluvulu aliishia
kutabasamu.
“ Baba mbona unatabasamu , nini
kimekufurahisha?” Beka aliyejishtukia
alimuuliza mzazi wake .
“ Yaani nimefurahi kwa jinsi
unavyonifurahisha siku hizi halafu watu
wengine wanakusema vibaya , kweli kuishi
uswahilini ni tabu tupu!” mzee huyo
alimwambia Beka .
“ Akina nani wanaonisema vibaya ?” Beka
akamwuliza .
“ Wapo watu wanasema eti kwa vile unafanya
vizuri shuleni unaringa sana, ” mzee huyo
alimdanganya mwanaye .
“ Baba achana na watu hao kwani duniani
kila kitu kibaya kwa watu , kwa mfano
ningekuwa mwizi au mtu wa kufuatilia
mambo ya wasichana pia wangesema , ” Beka
alimwambia baba yake .
Baada ya kutoa kauli hiyo , mzee Kibandiko
alicheka, akamwambia naye alikuwa
amechoka ngoja akapumzike chumbani
kwake.
“ Baba huendi Maramba kumjulia hali
shangazi anayeumwa ?” Beka aliyekuwa
anahitaji sana uhuru wa kubaki peke yake
pale nyumbani ili azidi kuwaumiza watoto wa
watu alimwuliza baba yake .
“ Nitaenda ila ngoja kwanza nipumzike kwani
nahisi uchovu sana ,” mzee huyo aliyetoka
kumbingirisha mtu alimwambia mwanaye .
Baada ya kuambiwa hivyo , Beka akawa
mpole ndipo baba yake akaenda chumbani
kwake.
“ Najua akiondoka kurudi hapa itakuwa
keshokutwa, lazima nimwambie Rhoda aje,
tena siku atakayokuja nitamwambia apike na
kufanya usafi wa chumba changu , ” Beka
aliyeanza kuwa mhuni aliwaza .
Je, kilifuatia nini? Usikose uhondo huu wiki
ijayo .
 
style ya hadithi za jf zinavyoisha! duh ndo maana willy gamba namkubali akileta mzigo unakuwa taslimu but wacha tuwe na subra inawezekana pana mkwamo kwa mleta uzi.
 
Mpenzi msomaji , wiki iliyopita niliishia pale
baba Beka alipokuwa akitafakari vimbwanga
vya mama Havijawa aliyempagawisha si
kidogo walipokuwa wakipeana malovee .
Je, kiliendelea nini ? Tuwe pamoja …
MZEE Kibandiko aliwaza jinsi mama huyo
alivyokuwa akitoa mihemko flani hivi ambayo
hakuwahi kuisikia kwa mwanamke yeyote
aliyewahi kutoka naye.
Hakuishia hapo , aliwaza pia kuhusu mama
huyo alivyokuwa na nyonga teketeke na jinsi
alivyokuwa akiwajibika kwa kuizungusha
pande zote za dunia kwa kasi .
Mwisho alijikuta akicheka peke yake
alipokumbuka jinsi mama huyo alivyojikunja
na kujikunjua na kuvitupa viungo vyake huku
na huko walipopasuliana madafu na
kunyweshana maji yake .
“ Yaani pale nilijua mtu anakata roho, kweli
mama Havijawa ana vionjo vya aina yake ,
nami naahidi sitamuacha kama alivyoahidi
kutoniacha, ” mzee huyo aliwaza.
Kama ilivyokuwa kwa mzee Kibandiko, mama
Havijawa naye alipofika kwake alifikia
kujibwaga kitandani kwani mambo
aliyofanyiwa na mzee Kibandiko hayakuwa
ya kawaida .
“ Yaani sikutegemea kama angekuwa mahiri
wa mapenzi , hata alipokuwa akinisomesha
nilijua anataka kunipaka shombo kama
ilivyowahi kutokea kwa mzee Maneno,”
mama huyo alijisemea moyoni .
Mama huyo aliyekuwa akiishi peke yake huko
nyuma alikuwa akisumbuliwa sana na mzee
Maneno lakini siku aliyoamua kumpa tende
zake tamu , mzee Maneno ambaye ana
maneno mengi kama jina lake lilivyo
alishindwa kazi .
“ Muziki wa baba Beka siyo wa kitoto, yaani
naamini hata hawa vijana wa siku hizi
wanaokula chipsi na mayai ya kisasa
hawawezi kumfikia, kwa kweli kajua kunipa
raha,” mama huyo aliwaza .
Kwa jinsi alivyofikishwa pale alipopataka
alimuonea wivu mama Beka kwa jinsi
alivyokuwa akiridhishwa na mumewe ,
akaahidi kula naye sahani moja .
Kufuatia uchovu wa makasheshe aliyopewa
na mzee Kibandiko, hakuchukua muda mrefu
alipitiwa na usingizi kama ilivyokuwa kwa
mzee Kibandiko na mwanaye Beka .
Ilipofika saa tisa alasiri ndipo baba Beka
alishtuka usingizini akaamka na kwenda
kuoga, wakati anaoga Beka naye aliamka.
“ Kumbe na wewe ulikuwa bado umelala ?”
mzee huyo alimwuliza mwanaye.
“ Yaani leo nahisi kuchokachoka, ” Beka
alimwambia baba yake bila kujua mzee huyo
alikuwa anaelewa kilichosababisha awe
katika hali ile .
“ Sasa ni hivi , mimi nakwenda Maramba
kumjulia hali shangazi yako , ofisini nimepewa
ruhusa ya siku mbili , kuwa makini hapa
nyumbani , sawa ?” mzee huyo alimwambia
mwanaye.
Beka alimweleza hakuna shida, kabla baba
yake hajaondoka alimpitia shilingi 20, 000 za
matumizi wakaagana na mzee huyo
akaelekea stendi tayari kwa safari ya
Maramba .
Kitendo cha baba yake kuondoka
kilimfurahisha sana Beka ambaye alipanga
kuzitumia siku hizo mbili vizuri kustarehe na
Rhoda pamoja na mdogo wake Rey .
“ Leo ngoja nipumzike ila kesho asubuhi na
mapema lazima nimfuate mmoja wao , yaani
watanikomaje !” Beka alijisemea moyoni.
Siku hiyo jioni Beka aliamua kwenda
kuwatambia rafiki zake akina Frank,
alipokutana nao bila hata ya kuulizwa alianza
kuwasimulia jinsi alivyomlamba Rhoda na
mdogo wake .
“ Acha kutudanganya , wewe mtoto wa mama
unaweza kumpata Rhoda kirahisi namna
hiyo ?” Frank alimwuliza .
Licha ya Beka kuwahakikishia kwamba tayari
alimfyekelea mbali Rhoda na mdogo wake ,
hawakuweza kuamini kitendo kilichomfanya
Beka awe mpole .
Alipoona wenzake hawakuamini maneno
yake , aliwaaga na kuwaambia siku moja
wataamini , akashika njia kurudi kwao .
“ Beka bwana , anataka kutupiga changa la
macho kirahisi anafikiri sisi ni vijana wa
kijijini, ” Said aliwaambia wenzake
wakacheka .
“ Mimi nimefurahi sana ulivyomchana mpaka
akawa mpole , hiyo ndiyo dawa ya watu
waongo, eti kamlamba Rhoda na mdogo
wake , hivi anafikiri kuwapata mademu wazuri
ni kazi rahisi ee ?” James alidakia ,
wakacheka .
Je, kilifuatia nini ? Usikose uhondo huu wiki
ijayo.
 
style ya hadithi za jf zinavyoisha! duh ndo maana willy gamba namkubali akileta mzigo unakuwa taslimu but wacha tuwe na subra inawezekana pana mkwamo kwa mleta uzi.

Naam.. nilikwama kidogo harakati za maisha zinakaba koo mkuu... samahani kwa usumbufu wowote uliojitokeza.. naahidi tutakua pamoja hadi mwisho wa hadithi...tuvumiliane mkuu

mbna haiendeleiii

inaendelea nilikwama kidogo maisha yanakwenda resi sana

Week hii hakuna mwendelezo

Hahahaha...

Mmh imeisha auu

Hapana mkuu, inaendelea

Haiendelei tu????

Inaendelea mkuu
 
Van shukran sana na tupo pamoja life ipo resi kikweli kweli na subra ndio ngao yetu.
 
Back
Top Bottom