Mpenzi msomaji, wiki iliyopita niliishia pale Beka alipompagawisha kinoma Manka mpaka binti wa watu akatoa kilio cha raha. Je, kilifuatia nini? Songa mbele na utamu huuâ¦
Beka hakuishia hapo alizidisha manjonjo yaliyomuacha hoi Manka aliyeamua kujibu mashambulizi na mwishowe wote walijikuta wakiwa kama walivyokuja katika dunia hii iliyojaa kila aina ya fujo.
Wakiwa katika hali hiyo, Beka hakuona sababu ya kuremba wakati alikwishaamua kuwashughulikia viumbe hao, sijui alimpinduaje Manka pale sofani, mtoto akaanza kulia kwa raha.
Kilio cha Manka kiliongeza morali ya Beka kuwajibika juu ya âjukwaaâ lake ambapo alimchezesha segere mpaka wote walipofika Kigoma mwisho wa reli kwa pamoja.
âIla wewe Beka wewe!â Manka alimwambia Beka.
âIla mimi nini dada mzuri?â Beka alimwuliza.
âRudia tena hiyo sentensi yako,â Manka alimwambia.
Bila kujua Manka alitaka kusema nini, Beka akamwambia; âNimesema hivi, ila mimi nini dada mzuri?â
âYaani Beka haya uliyonifanyia unaweza kumfanyia dada yako?â Manka alimwuliza.
Kufuatia kuulizwa hivyo, Beka aligundua alikosea kumwita Manka dada, akamuomba msamaha kwa kusema; ânisamehe mpenzi wangu.â
âHapo sawa, ila sikutegemea Beka kama umjuvi wa mapenzi, siyo siri unayaweza,â Manka alimfagilia Beka.
âSiyo sana, najifunza tu mpenzi wangu,â Beka alimwambia Manka utafikiri walikuwa wapenzi wa muda mrefu.
âEti unajifunza tu, yaani wewe ni noma kwa kweli!â Manka alimwambia Beka aliyeishia kucheka.
Kwa jinsi alivyokuwa amepagawisha vya kutosha, Manka alijikuta akimfungukia Beka kwamba tangu alipohamia Tanga kutoka mkoani Mbeya, hakuwa na mpenzi.
âTafadhali Beka naomba niwe mtu wako wa kudumu, nakuahidi nitakupenda kwa dhati,â Manka alimwambia Beka.
Beka alifurahi kusikia hivyo na kumkaribisha, kwa furaha waliyokuwanayo walipigana mabusu na kuanza kuleteana fujo tena, si Beka ambaye damu ilikuwa ikimwenda mbio akapata moto, akamlamba bakora ya pili ya uhakika.
Kufutia bakora hiyo iliyokwenda shule, Manka aliishiwa nguvu kabisa na kujilaza pale sofani, akapitiwa na usingizi, Beka alipotazama sakafuni na kuziona nguo zao zilivyokuwa zimetawanyika kama hazikuhitajika tena kuvaliwa akaanza kucheka.
âKudadeki, mtoto kachokaje! Chezea Beka wewe!â Beka alijisemea moyoni wakati akiokota nguo zake na za Manka.
Kwa kuwa kiu yake ilimuisha, alivaa boksa kisha alijongea kwenye jokofu akachukuwa chupa iliyokuwa na maji ya baridi akayamimina kwenye glasi na kuyanywa.
âKweli kidume nimeanza kazi rasmi, Rhoda nimeshamlamba, Rey nimetia ndani, Manka ndiyo huyu kalala hana ujanja, bado Stella, lazima nijenge heshima mtoto wa kiume,â Beka alijisemea moyoni na kuachia tabasamu.
Baada ya kunywa glasi mbili za maji, alikwenda kukaa pembeni ya kochi na kumshika Manka aliyekuwa mtupu usawa wa nyonga.
Kufuatia kushikwa huko, Manka alijigeuza na kumwangalia Beka kisha aliachia tabasamu na kumuuliza kama alikuwa na msichana aliyekuwa akitokanaye.
âSiwezi kukuficha, Maramba kwa bibi alikuwepo msichana mmoja ambaye nilipogundua hajatulia niliachana naye, naona nafasi yake umechukua wewe!â Beka alimdanganya.
Manka alifurahi sana kusikia hivyo, aliamka wakakumbatiana, wakapigana mababusu ndipo Beka alimuongoza msichana huyo bafuni.
Wakiwa huko, walioga na kufanyiana michezo ya kimalovee kisha walivaa nguo ndipo Manka alimuaga Beka, kabla ya kuondoka aliahidi angerudi jioni kwa ajili ya kupiga stori.
Je, kilifuatia nini? Usikose wiki ijayo. Maoni nicheki kwa namba zilizopo juu.