Chenge, StarTV na Utaalam wa kisasa

Awali ulisema hivi;


Na sasa unasema hivi;

Hii nayo inahitaji rocket scientist?


Masatu, rejea mtundiko wako hapo juu ukijibu mtundiko wa Enigma.

Bila kuchagua upande, ni vizuri uelewe tu namna jengo la bunge linavyofanya kazi.

Wabunge na wageni wana muda maalum wa kuingia kwenye ukumbi mkuu wa mijadala wa bunge. Wafanyakazi wa bunge (si wote) na waandishi (pia si wote), wanaruhusiwa kuwa maeneo kadhaa ya ukumbi mkuu hata kama huo si muda wa wabunge na wageni kuwepo. Waandishi wengi huwa wanakuwa kwenye media room inayoangalia ukumbi kwa chini, aidha wakimalizia reports zao au wakikamilisha kutuma reports kwenye vituo vyao vya kazi. Ni nadra sana kuwakuta wabunge ndani ya ukumbi baada ya milango mikuu kufungwa, ila ni rahisi sana kuwaona waandishi na wapiga picha katika maeneo ya juu yanayozunguka ukumbi (siyo ndani ya ukumbi wenyewe) hadi usiku sana.

Kinachoshangaza ni kwa nini (kama kweli) Chenge aliachiwa akaingia peke yake? Kawaida wabunge wakisahau vitu ndani, na inatokea mara nyingi sana, aidha ataingia mbunge na ushers au ataingia usher na kumletea mbunge vitu alivyosahau. Nimeona pia mara kadhaa wabunge wakiwatuma madereva kurudi na kuchukua vitu walivyosahau ndani, na ni ushers ambao huingia na kuleta.

Nadhani hiyo ya Chenge (kama ni kweli) itakuwa tu ni 'za mwizi ni arobaini..' kama hata watu wa TV walikuwa hawajamaliza kazi zao na cameras zilikuwa bado ON. Security cameras ziko ON masaa 24, na labda 'mtu' alipitiwa kwa hilo.
 
ina maana hata huko bungeni, hawana wasaidizi ?? hii kitu nashindwa kuielewa, story nzima imekuwa badly staged, hivyo kuamini kwangu itakuwa vigumu ! Maelezo ya mtoa mada yanachanginyi !
 
Vyanzo vya kuaminika vimethibitisha kuwa siku ya Jumanne baada ya kikao cha wabunge wa CCM Bw. Chenge aliomba udhuru wa kurudi ndani ya ukumbi wa Bunge ambao ulikuwa tayari umefungwa. Alifunguliwa na Afisa mmoja wa Bunge ili kwenda kuchukua/kufanya alichotaka kwa dakika chache.

Kiungani,

Bandiko linasema ukumbi ulishafungwa how comes waandishi wa Startv wabaki ndani ya ukumbi uliofungwa? ina maana walifungiwa ndani? Kwani hata Mh Chenge "aliposahau" kitu ilibidi "afunguliwe"
 
Masatu.. miya nadhani nimeelewa "ukumbi kufungwa" kwa maana ya ule wa mkutano siyo Jengo la Bunge kufungwa. Maelezo ya kiungani yanaleta mantiki zaidi hasa ukiangalia jengo lenyewe la Bunge lilivyo. Ukumbi wa mikutano unaweza kufungwa lakini haina maana mtu akiingia hawezi kuonekana. Kiungani amenipa wazo la kuangalia picha za ukumbi huo kuona kama yawezekana mtu kuonekana akiingia bila ya yule anayemuona kuwemo ndani ya huo huo ukumbi.

13New.JPG


Hapa ni kutoka mojawapo ya vyumba vya juu

Na hii ni kutoka kwa upande mwingine:

12New.JPG
 
Kiungani,

Bandiko linasema ukumbi ulishafungwa how comes waandishi wa Startv wabaki ndani ya ukumbi uliofungwa? ina maana walifungiwa ndani? Kwani hata Mh Chenge "aliposahau" kitu ilibidi "afunguliwe"

Masatu, hii inaonyesha kuwa hujui jinsi ukumbi wa bunge ulivyo.

Kuna milango miwili mikubwa inayokupa access kwenye UKUMBI wenyewe, katika ground floor. Pia kuna mlango wa kutokea kwenye Speaker's Chamber ambao pia unakupa access.
Hii milango ikifungwa, ni kweli huwezi kuingia kwenye 'UKUMBI' ila bado unaweza kuingia ndani ya jengo lenye UKUMBI wa bunge. Unaweza kuuona ukumbi hata kama milango imefungwa ikiwa:
1. Umepanda juu na kukaa kwenye mojawapo ya Visitor's Galleries (kulia au kushoto kwa Speaker).
2. Umepanda juu na kukaa kwenye Speaker's Gallery (inatizamana na Speaker).
3. Umepanda juu na kukaa kwenye media rooms (ambazo kama sikosei ziko nne) ambazo zina vioo vikubwa.

Hii yote ni pamoja na kuwa 'UKUMBI' umefungwa, kwa maana kuwa huwezi kuingia sehemu ambayo wabunge wanakaa na kuendesha mijadala, maadamu tu milango mikubwa kabisa ya nje (siyo ya ukumbi) iwe wazi, na huwa inakuwa wazi muda wote.

Wafagizi, waandishi wa habari na wahudumu wa ukumbi huwa pale masaa kadhaa kabla wa wabunge na wageni kuja, na pia masaa kadhaa baada ya wabunge na wageni kuondoka. Watu wa TV stations huacha camera zao ndani na labda wataondoa vitu kama tapes, laptops na vitu vidogo vidogo. Pia ni kawaida sana watu wa TV (siyo StarTV tu) kuendelea kuwepo hadi wakimaliza kurusha programs zao baada ya saa nne usiku.
Milango ya kuingia kwenye 'UKUMBI' hufungwa mara tu kikao kikimalizika (symbolic), na watu wakipungua sana hufunguliwa kwa ajili ya kufanya usafi, kupanga karatasi, kurekebisha viti, n.k.

Hiyo mikubwa ya nje huwa wazi, ila kunakuwa na walinzi watatu/wanne muda wote katika eneo hilo na kwenye chumba kidogo cha security wanaagalia maeneo karibu yote kwa cameras.

Sijawasiliana na waliopo Dom kujua ni nini haswa kimetokea, ila sioni sababu ya watu kuzusha kitu kama hiki which can be dis-approved very easily in the absence of the videotape.
 
Masatu.. miya nadhani nimeelewa "ukumbi kufungwa" kwa maana ya ule wa mkutano siyo Jengo la Bunge kufungwa. Maelezo ya kiungani yanaleta mantiki zaidi hasa ukiangalia jengo lenyewe la Bunge lilivyo. Ukumbi wa mikutano unaweza kufungwa lakini haina maana mtu akiingia hawezi kuonekana. Kiungani amenipa wazo la kuangalia picha za ukumbi huo kuona kama yawezekana mtu kuonekana akiingia bila ya yule anayemuona kuwemo ndani ya huo huo ukumbi.




hii itakuwa misleading, iwapo tapes zipo then hazibandikwi hapa na kilichobaki ni kuanza kuspeculate ! CAMERA siku zote haidhani, bali inatoa Clear, tena right angle ! cha msingi, ni kuonyeshwa hizo tapes, na kama hazitoonyeshwa then tutakuwa tunaumizana vichwa tu humu ! kila mtu atakuja na lake ! - - ni ushauri tu !
 
Masatu, hii inaonyesha kuwa hujui jinsi ukumbi wa bunge ulivyo.

Kuna milango miwili mikubwa inayokupa access kwenye UKUMBI wenyewe, katika ground floor. Pia kuna mlango wa kutokea kwenye Speaker's Chamber ambao pia unakupa access.
Hii milango ikifungwa, ni kweli huwezi kuingia kwenye 'UKUMBI' ila bado unaweza kuingia ndani ya jengo lenye UKUMBI wa bunge. Unaweza kuuona ukumbi hata kama milango imefungwa ikiwa:
1. Umepanda juu na kukaa kwenye mojawapo ya Visitor's Galleries (kulia au kushoto kwa Speaker).
2. Umepanda juu na kukaa kwenye Speaker's Gallery (inatizamana na Speaker).
3. Umepanda juu na kukaa kwenye media rooms (ambazo kama sikosei ziko nne) ambazo zina vioo vikubwa.

Hii yote ni pamoja na kuwa 'UKUMBI' umefungwa, kwa maana kuwa huwezi kuingia sehemu ambayo wabunge wanakaa na kuendesha mijadala, maadamu tu milango mikubwa kabisa ya nje (siyo ya ukumbi) iwe wazi, na huwa inakuwa wazi muda wote.

Wafagizi, waandishi wa habari na wahudumu wa ukumbi huwa pale masaa kadhaa kabla wa wabunge na wageni kuja, na pia masaa kadhaa baada ya wabunge na wageni kuondoka. Watu wa TV stations huacha camera zao ndani na labda wataondoa vitu kama tapes, laptops na vitu vidogo vidogo. Pia ni kawaida sana watu wa TV (siyo StarTV tu) kuendelea kuwepo hadi wakimaliza kurusha programs zao baada ya saa nne usiku.
Milango ya kuingia kwenye 'UKUMBI' hufungwa mara tu kikao kikimalizika (symbolic), na watu wakipungua sana hufunguliwa kwa ajili ya kufanya usafi, kupanga karatasi, kurekebisha viti, n.k.

Hiyo mikubwa ya nje huwa wazi, ila kunakuwa na walinzi watatu/wanne muda wote katika eneo hilo na kwenye chumba kidogo cha security wanaagalia maeneo karibu yote kwa cameras.

Sijawasiliana na waliopo Dom kujua ni nini haswa kimetokea, ila sioni sababu ya watu kuzusha kitu kama hiki which can be dis-approved very easily in the absence of the videotape.

i cant afford to agree with this, cha msingi weka tapes ambazo zinadaiwa kuwepo ! other wise, this will be another ball rolling, huku watu wasidiscuss alichosema zitto ! maelezo yooote haya is nothing compared to a five second movie clio, tuonyesheni hata kidogo na tujudge wenyewe, lakini kujudge kutokana na maneno yanayotungwa, is like playing with our heads !
 
i cant afford to agree with this, cha msingi weka tapes ambazo zinadaiwa kuwepo ! other wise, this will be another ball rolling, huku watu wasidiscuss alichosema zitto ! maelezo yooote haya is nothing compared to a five second movie clio, tuonyesheni hata kidogo na tujudge wenyewe, lakini kujudge kutokana na maneno yanayotungwa, is like playing with our heads !

WENYEWE WANAONA BORA KUMEPOA.....!
DOGO KACHEMKA.......... NA HUU NDO UKWELI...... AKUBALI KUKOSOLEWA BADALA YA KUSIFIWA TU....!
NINYI WASHAURI WAKE MWAMBIENI UKWELI.......!
 
13New.JPG


Yule ni kama Muungwana anaingia pale au? Na mzungu mbele ya Muungwana nani yule ,au ni shemeji yake, Mrs. Sinclair? Jim aangalie!

Halafu hivi kwa nini Wangwana wa Bongo wanatembea na wa-Mura badala ya makachero wa kiraia?

Hamna kibaya sana, isipokuwa ila tu nadhani Vasco anapoenda sehemu sehemu kazungukwa na wa-Mura, anapoteza image of a civilian president.
 
watu wanadai tapes utadhani JF inafanya kazi Bungeni! inachekesha. Hili jambo limetokea siku ya Jumanne, sasa watu waende kuiba tapes..?
 
Masatu, hii inaonyesha kuwa hujui jinsi ukumbi wa bunge ulivyo.

Kuna milango miwili mikubwa inayokupa access kwenye UKUMBI wenyewe, katika ground floor. Pia kuna mlango wa kutokea kwenye Speaker's Chamber ambao pia unakupa access.
Hii milango ikifungwa, ni kweli huwezi kuingia kwenye 'UKUMBI' ila bado unaweza kuingia ndani ya jengo lenye UKUMBI wa bunge. Unaweza kuuona ukumbi hata kama milango imefungwa ikiwa:
1. Umepanda juu na kukaa kwenye mojawapo ya Visitor's Galleries (kulia au kushoto kwa Speaker).
2. Umepanda juu na kukaa kwenye Speaker's Gallery (inatizamana na Speaker).
3. Umepanda juu na kukaa kwenye media rooms (ambazo kama sikosei ziko nne) ambazo zina vioo vikubwa.

Hii yote ni pamoja na kuwa 'UKUMBI' umefungwa, kwa maana kuwa huwezi kuingia sehemu ambayo wabunge wanakaa na kuendesha mijadala, maadamu tu milango mikubwa kabisa ya nje (siyo ya ukumbi) iwe wazi, na huwa inakuwa wazi muda wote.

Wafagizi, waandishi wa habari na wahudumu wa ukumbi huwa pale masaa kadhaa kabla wa wabunge na wageni kuja, na pia masaa kadhaa baada ya wabunge na wageni kuondoka. Watu wa TV stations huacha camera zao ndani na labda wataondoa vitu kama tapes, laptops na vitu vidogo vidogo. Pia ni kawaida sana watu wa TV (siyo StarTV tu) kuendelea kuwepo hadi wakimaliza kurusha programs zao baada ya saa nne usiku.
Milango ya kuingia kwenye 'UKUMBI' hufungwa mara tu kikao kikimalizika (symbolic), na watu wakipungua sana hufunguliwa kwa ajili ya kufanya usafi, kupanga karatasi, kurekebisha viti, n.k.

Hiyo mikubwa ya nje huwa wazi, ila kunakuwa na walinzi watatu/wanne muda wote katika eneo hilo na kwenye chumba kidogo cha security wanaagalia maeneo karibu yote kwa cameras.

Sijawasiliana na waliopo Dom kujua ni nini haswa kimetokea, ila sioni sababu ya watu kuzusha kitu kama hiki which can be dis-approved very easily in the absence of the videotape.

kama mtu haelewi hili basi hawezi kuelewa. Asante mkuu!
 
As long as maelezo ya bandiko yamedai kwamba mhusika alifika mpaka kwenye kiti cha enzi cha Spika, sidhani kama hilo swala linaweza kumalizwa kimya kimya, lazima itafika mahali litawekwa wazi tu kwa kuwa mhusika atatakiwa kujieleza ni sababu ipi ilimfikisha kule kunako enzi ya mwenyewe Six. Ukizingatia kwamba Six ana uchungu na wana siasa wa maji taka basi tutarajie mtu mzima akiumbuliwa na itakuwa nafasi pekee kwa Six kuonyesha makucha yake na kudhihirisha kwamba kuna watu wanamfuatilia kwa nyuma kama ambavyo amekuwa akilalamika.

Kama kuna media house imenasa tukio hilo basi tunawaomba waje watuwekee hapa ili kumaliza ubishi, maana tapes za Bunge sidhani kama zinaweza kupatikana kirahisi.

Kwa uhakika mhusika hawezi kutuhumiwa kwa kosa la ushirikina, maana serikali haina imani na mambo hayo. Na kuonekana kwenye viti vya wabunge wengine sidhani kama ni kosa, maana anaweza kujitetea kwamba alipitia tu ama aliona kitu akataka kuchukua au kuwakabidhi wasalama wa Bunge kwa ajili ya kukitunza. Kosa ninaloliona ni kwenda kule kwenye kiti cha enzi, kama kweli alifika huko basi ana tuhuma ya kujibu.
 
Du! Waungwana sasa mumezidi... yaani... hata huyo utunzi wa riwaya yenyewe haonyeshi kwamba huyo mtunzi ni mtaalamu...

Anyway JF ni ya wenye madhehebu na wale wapagani... endeleeni tu kutunga as much as you can
 
As long as maelezo ya bandiko yamedai kwamba mhusika alifika mpaka kwenye kiti cha enzi cha Spika, sidhani kama hilo swala linaweza kumalizwa kimya kimya, lazima itafika mahali litawekwa wazi tu kwa kuwa mhusika atatakiwa kujieleza ni sababu ipi ilimfikisha kule kunako enzi ya mwenyewe Six. Ukizingatia kwamba Six ana uchungu na wana siasa wa maji taka basi tutarajie mtu mzima akiumbuliwa na itakuwa nafasi pekee kwa Six kuonyesha makucha yake na kudhihirisha kwamba kuna watu wanamfuatilia kwa nyuma kama ambavyo amekuwa akilalamika.

Kama kuna media house imenasa tukio hilo basi tunawaomba waje watuwekee hapa ili kumaliza ubishi, maana tapes za Bunge sidhani kama zinaweza kupatikana kirahisi.

Kwa uhakika mhusika hawezi kutuhumiwa kwa kosa la ushirikina, maana serikali haina imani na mambo hayo. Na kuonekana kwenye viti vya wabunge wengine sidhani kama ni kosa, maana anaweza kujitetea kwamba alipitia tu ama aliona kitu akataka kuchukua au kuwakabidhi wasalama wa Bunge kwa ajili ya kukitunza. Kosa ninaloliona ni kwenda kule kwenye kiti cha enzi, kama kweli alifika huko basi ana tuhuma ya kujibu.


Keil.. kuna mambo ya kichawi ambayo ni makosa katika sheria zetu...
 
Tuwe tunasubiri taarifa angalau INAIVAIVA kidogo. Au ndio katika kukimbilia U-SENIOR na U-EXPERT na CREDIT nyingi?
 
ina maana hata huko bungeni, hawana wasaidizi ?? hii kitu nashindwa kuielewa, story nzima imekuwa badly staged, hivyo kuamini kwangu itakuwa vigumu ! Maelezo ya mtoa mada yanachanginyi !

Kada you need not even understand as long as you already decided your part on the story.Wewe hutaki tu kuelewa kwa sababu HUTAKI,sisi tutasubiri na kufuatilia mpaka tujue mwisho.

After all wewe ni nani bana hadi uwe unataka kuthibitishiwa kila stori kwa viwango vyako bana?Ahh!!
 
Kiungani,

Bandiko linasema ukumbi ulishafungwa how comes waandishi wa Startv wabaki ndani ya ukumbi uliofungwa? ina maana walifungiwa ndani? Kwani hata Mh Chenge "aliposahau" kitu ilibidi "afunguliwe"

Masatu na wewe hutaki tu kuelewa kwa vile hutaki.Ukisoma vizuri bandiko la Kiungani kasema ukumbi MKUU ambapo wabunge ndio huuutumia.Waandishi hukaa juu ya ukumbi mapo wanaruhusiwa kuendelea na shughuli zao.Labda tu aliyepost habari hii mara ya kwanza hakuweka neno ukumbui MKUU kwa kujua kwamba ingeeleweka kabisa.Sasa nyie naona mnajaribu tu kucheza na maneno badala ya kuangalia content ya post hii.Hii inathibisha ni kwa jinsi gani mmeiva kipropanda za CCM.I wonder why you chose those chaps Makamba and Tambwe Hiza into those positions.
 
Serikali yetu haiamini ushirikina lakini si jambo geni kwa baadhi wabunge hao, wanajulikana sana kwa ushirikina, yanasemwa mengi sana kuhusu ushirikina wao
 
Back
Top Bottom