Episode 6.
Tupo palika bazaar ,,,tupo kwenye utabiri wa rajesh,,
Mdosi kutoka Tamil akitubashiria hatma ya maisha yetu pale India.
Basi baada ya Mimi kutabiriwa mafanikio,,
Ikafika zamu ya sued,,nae akachanga karata kama kawaida,,
Akaziweka chini ,,kasuku akachaguwa moja akampa rajesh mtabiri,
Hapo rajesh akamuangalia sued halafu akashika mkono wake wa kulia akamwambiya na wewe utakwenda nyumbani tena soon.
Utapata mafanikio..
Hamidu nae akachukuwa karata,, akazichanga,,akaziweka chini.
Kasuku akachukuwa moja akampa rajesh mtabiri,,akaiangalia ile karata,,
Akamshika mkono hamidu halafu ghafla akauachia kwa nguvu sana.
Kama ameunguzwa na kitu..
Ni Kama vile afanyavyo mtu aliyeunguzwa na kitu.
Akasema ni kama vile sikuoni,,ila hakuna tatizo..
Ila hutofika nyumbani,, utaishia hapa hapa India.
Basi tukacheka,,kimasihara kama kumdhihaki rajesh mtabiri..
Ikaja zamu ya saidi nae akachanga karata,,halafu akaziweka chini,,tena kasuku akachukuwa moja
Akampa rajesh mtabiri.
Akamshika mkono saidi,, rajesh akasema wewe utapata matatizo makubwa sana hapa India..
Duu!! Ulikuwa ni utabiri fikirishi sana,,
lakini tuliupuuzia kama upuuzi
mwingine,
Tulifikiria pengine ni mambo ya kiongo kama wafanyavyo watabiri wengine matapeli
Mungu mkubwa nilipata passport yangu kutoka kwa police,, na mambo yangu yalirejea kama kawaida kufanya mishenishe za biashara..
Ikawa chenai tunawasiliana kwa usiku tu,,au week end moja moja nakutana nae sehem,,
Maana ni kipindi sasa mama yake amesharejea toka Zimbabwe.yupo hapo new delh.
Kwahyo muda mwingi nilikuwa busy,,
hivyo ilimfanya chenai kuchanganyikiwa zaidi na mwandende boy.
Ikawa simu mfululizo hadi kero,,Kama unavyojuwa simu tulikuwa tunashare na Mwenye nyumba,,
Kwa hyo muda mwingi yeye akipiga simu huwa wanapokea huko,,sisi yunakuwa town.
Phone calling!!!!!
Chenai
Hello,,
.sorry
Can I speak to mwandende plz?
"No no,,baadme mwandende abi neihe "
Abi school jaega"
Akimaanisha now mwandende hayupo amekwenda shule.
Basi simu kila wakati hata sometimes tunaongea habari zetu za mapenzi ktk simu bila kujuwa kumbe yupo Binti mmoja wa Mwenye nyumba anaitwa sapna anafuatilia maongezi yetu.
Ilitokea siku moja natoka ndani napita pale kwa Mwenye nyumba kuna jambo fulani la kumwambiya.
Nikakutana na Binti mmoja kama 20 hivi,,,nilikuja kujuwa baadae jina lake anaitwa sapna.
Ambaye ni mtoto yule mama,,nikamsalimia,,akajibu kwa aibu sana.
Then nikamuuliza yule mama akawa hayupo.
Nikamwambiya nitakuja baadae.
Yule binti akanambiya.
You must be mwandende.
Nikajibu
Yes,,iam the one.
Akanambiya ..
Your voice is so family to me.
Nikashangaa sana,,
I used to hear you on the phone with your girl friend talking.
I wish to see her one day..
She is so luck to have you.
Duu..
Nilitetemeka kwa hofu jinsi huyu binti alivyonitamkia,,
Halafu sikuwahi kumdhania chochote,,
Kumbe huyu Binti anatusikiliza maongezi yetu?
Halafu inaonyesha amependa sana sound yangu through phone.
Hii ni hatari sana hii.
Ghafla akaingiia muhindi mmoja Mzee wa makamo kiasi,, ambaye tunakaa wote flat moja,,
Ni Jirani yetu.
Basi alituangalia Jicho Kali sana hata nikahisi kuna kitu zaidi ya utazamaji wake.
Wahindi ni watu wanafki sana,,pia hawapendi kuona mwanamke yeyote muhindi awe karibu na mwanaume mwafrica.
Kwa jinsi alivyotuangalia yule jamaa nikahisi ni tatizo.
Nikarudi zangu ndani kwangu nikaendelea na shughuli zng,,
Siku ,,week zinakatika huku nikiendelea na ukaribu wa yule mtoto wa kihindi sapna..
Na yeye nilipogunduwa anasikiliza maongezi yetu,,
Basi nizidi kuweka sound za kimahaba zaidi,,
nikazidi kumteka sapna,,hata kwao wakaanza kuhisi jambo mbaya kwangu mm na yeye.
Siku moja yupo ndani usiku hapo home,,
walivamia wahindi pale flat na magongo wakiongozwa na mkuu wa kitongozi,
Wakiwalazimisha homeboys wangu tufunguwe mlango,,wana shida na mm,,
Wale jamaa hawakujuwa kosa na sababu ya mm kutafutwa na wale wahindi zaidi ya 10 na magongo ya ctiket mkononi..
Tukaomba aitwe Mwenye nyumba tujuwe sababu ya kwann mm natakiwa nje na wahindi,,nihojiwe kwann natembea na Binti yao,,
maana yake kinachofatia ni kupigwa magongo ya cricket mwilini.
Yule mama kumbe alishalishwa sumu kwamba natembea na spna Binti yake,
Akiongea kwa uchungu wanitoe mm na tuhame mle flat.
Basi ilitokea purukushani pale tufunguwe mlango na sisi hatutaki,,
Itaendelea.