Episode 7.
Tupo ndani,,tumezungukwa na kikundi cha wahindi kikiongozwa n kiongozi wa mataa,,
wakituamrisha tufunguwe mlango,,
Ili wanihoji juu ya uhusiano na binti wa kihindi Sapna.
Tuligoma kwa muda hata wakatishia kuuvunja mlango wetu.
Mwishowe wakaja police ,,tukafunguwa mlango,
Na ktk mahojiano ya hapa na pale,,
Sikukutwa na ushahidi wa moja kwa moja kimahusiano na Sapna,
Kwani hata sapna alipoulizwa alikataa.
Basi nilionywa kuwa karibu na binti yule,,
Hilo likapita..
Baada ya miezi kadhaa kupita mambo yangu yalikuwa powa sn,,
Nilipata connections nyingi sana nikapata pesa kama dola 5000 hivi.
By that time ilikuwa pesa nzr sn,,
naikumbuka change ya dola to shilling ilikuwa 1200 sh..1$.
Nikafikiria kurudi Tanzania,, lakini nitamuambiaje chenai?
Sikutaka ajuwe kama nakwenda Tanzania,
Nikatengeneza story kwamba nipo likizo sasa nakwenda Thailand for Holiday,,
Ilikuwa ni kawaida sana kwa wanafunzi pale India,,
wakati wa likizo kwenda popote duniani,,
Na viza zake haisumbuwi kabisa.
Nakumbuka kipindi kile Thailand ni free kwa Tanzanian passport. Ikawa rahisi kwangu kudanganya.
Week kabla sijasafiri,,chenai aliomba tuonane,,
Nikaitikia wito,,
akaja na house girl wao,, tukakutana Indira market kama ilivyo kawaida.
Basi akanambiya..
Mwandende ,,do you really go?
Yes I do,,but I won't take long my love.
Nilijibu kwa kumtoa hofu,
Ghafla akaanza kulia kwa sauti hata kuwavuta wapitanjia waliopo Jirani na pale.
Nikambembeleza kidogo akatulia lakini akawa bado analia kwa kwikwi,,
kama mtu ambaye bado ana uchungu mwingi moyoni na haujakwisha..
You know why chenai still crying?
Aliniuliza swali yule house girl wa kipindi,simkumbuki jina..
Nikajibu,,
No,,I don't know.
House girl,
She has a feeling that you won't come back mwandende.
That's why,,,, she has been crying since you told her about going to Thailand.
Nilishangaa sana,,nikasema kwenye mapenzi ya kwl mara nyingi mioyo huongea pamoja,
Chenai amejuwaje kama sitorudi India tena?
Nilimbembeleza,,nikawa nazidisha muda mwingi wa kuwa nae pamoja,,ili kumliwaza..
Nilitoka India nikafika daresalam salama,
Nilifanya fujo nyingi sana mtaani ,,
hakuna mwanamke aliyekuwa na uwezo wa kunikataa mwandende.
Nilikuwa natamba mm tu mitaa yote.
Kwa nguo Kali na perfumes za hatari.
Nilikuwa nikipita mtaani kila mtu anajuwa mwandende kapita,
,naikumbuka perfume yangu ya hatari sana,,XS PACCO RABANNE..
hiyo ndy ilikuwa kama salam za mwandende kapita hapa.
Au yupo eneo hilo.
Ninapokuwapo na pacco rabanne yupo.
Ilikiwa ni ngumu kututenganisha,,ilikiwa perfume nzr sana.
Miezi,,miaka ilipita,,nikasahau kuhusu chenai,,
nikasahau kuhusu India,,
sikumtafuta tena chenai,,
habari za India zilifutika kabisa,,
nikasahau kila kitu,,
na maiaha yakaendelea upande mwingine.
Nipo Lusaka ndani ya bus la Taqwa,, nikitokea south kupitia Zimbabwe.
Bado ilikuwa tunasubiri muda ufike tuanze safari tena ya Lusaka --Tunduma.
Nilkuwa nimechoka sana,,maana safari ya south Lusaka ni hatua ndefu sana.
Nipo karibu kupata usingizi,,
nikashtuliwa na kelele za huko nje,
nikazipuuzia maana hapo intercity bus terminal walevi ni wengi.
Kilichonifanya nishtuke ni kusikia wanazungumza kiswahili,,
na kusikia kila kinachoendelea.
Nikasema ngoja nikajaribu kufuatilia shida nn huko chini.
Nikajisogeza karibu ya ule ugomvi,,
nikaona jamaa mmoja kakunjwa shati lake hata kufikia kuacha eneo zima na tumbo na kifua kipo wazi.
Nikaja kugunduwa kwamba hawa jamaa mmoja ni conductor wa basi lile na mwingine alikuwa ni abiria.
Conductor,
Ulisema ukifika Lusaka utatoa pesa za nauli,,
Umefika hapa unasema unatoa pesa Tunduma,,
Hilo hakiwezekani,,toa pesa,,toa pesa..
Hebu nishikie simu yangu.
Duu ,,,!!!!yule konda akiomba msaada ashikiwe simu ili amtie adabu yule abiria.
Nikamuangalia kwa makini yule jamaa,,
Duu, aisee!!!!!,nikashtuka sana,,
Kumbe ni sued,, yule homeboy wangu niliyekuwa naishi nae vasant vihar India 1999.
Yule sued aliyenitolea $100 kwa ajili ya kunisaidia kukomboa passport yangu kwa police wa kihindi..
Miaka 16 sasa imepita ,,naonana na mtu niliyekuwa nae bega bega ktk kutafuta maisha India.,
Pale pale nikaingilia ugomvi ule,,
Kwani huyu jamaa anadaiwa kwacha ngapi?
Konda akasema alipaswa anipe$ 20 kutoka harare hadi Lusaka.
Nimwambiya yule jamaa kwani safari yako ni wapi?
Akanambiya daresalam,,
Pale pale nikatoa 600 rands nikamlipia sued pesa zote hizo..
Ajabu muda wote sued bado hajanikumbuka mwandende.
Nikamuita jina sued,,vasant vihar,
Sued alinikumbuka,,
akanikumbatia,,
alilia sana mbele yangu.
Hata nikajisikia vibaya sn.
Nikaona nimtoe eneo la tukio maana watu walishaanza kujaa tena pale.
Tukiwa tumeshapata msosi wa ugali samaki choma na kachumbari,,
Nje kidogo ya terminal ya usaka intercity.
Huku tukishushia na juice ya mixed fruit,,
ndy nilipopata nafasi ya kumuuliza sued habari za India.
Akanambiya ni long story mwandende..
Itaendelea.