Cheaters: The Series

Cheaters: The Series

Episode 8.

Ras.

Wapi msuba kwanza? Maana sio kwa kuvurugwa huku. Nimevurugwa sio kitoto mazee. Nahisi nahitaji kutuliza akili ili niweze simulia vizuri yaliyojiri. Katika hii simulizi kuna muda mm ndo nlijiona stelingi, ila mpaka mda huu dah, nahisi nimekua mpira tu, watu wanaenda uwanjani wanasema wanaenda kuangalia mpira ila kumbe wanachoenda kuangalia ni wachezaji. Haina noma lakini, am just a ball, bt without me hakuna game hapa.

Mpaka now nadhani kuna watu wanaona mi kama fala flani hivi. Siwakatazi, mnachofikiria fikirieni. Ila nadhani wote mtakubali kuwa mi ni bonge la loyal. Muaminifu sana. Sijawahi kucheat kwenye maisha yangu. Well sio kwa ujanja wangu na wala siko hapa kuwapondea wanaocheat ila niseme kabisa kuwa so far nimekua muaminifu kwa girls wangu. Hua nikifall in love natoa kila ninachostahili kutoa.

Ila kiukweli kati ya vitu viliniuma katika hii dunia ni kusikia kuwa aliyekua mpenzi wangu yaani Zoya anatoka na Stive. Albert ndo alinipa mchongo mzima. Na akanionesha kabisa na ushahidi wa picha. Niliishiwa kabisa nguvu aisee. Then to make matters worse Zoya akawa anakana vyote nnavyomuuliza. kwanza alinidanganya hata khs ratiba yake ya siku ile. Na cha cha kuumiza na kushangaza zaidi ni tukio alilofanya Zoya kwa Marga. Ikabidi nichukue yale maamuzi. Kilichotokea baada ya pale kila mtu anajua.

Maisha na Marga yalikua ya kuinjoi sana. Nlihakikisha mpenzi wangu anafaidi. Kuanzia trip za mara kwa mara na shopping za kutosha. Uwezo si nlikua nao bana. Marga alifurahia kuwa na mm na pia mi nlifurahi. Ila nitakua muongo nikisema nlimsahau Zoya. Utofauti wake na Marga hasa katika personality zao ulikua ni wazi. Zoya alikua ni msichana mpole asiye na makuu na anayeridhika kwa hali yoyote. Marga was the opposite. She is a wild woman. Na hakua akitosheka na kitu chochote cha kawaida. Kama ni zawadi umemletea kama hajaupenda atakuchana live. Although Zoya was cooler, ila ule ucharuko wa Marga uliyafanya mapenzi yawe ya moto balaa. Kama alivyoimba Mary J Blige,

"...... Bad girls are not good, good girls are not fun....".

Ila kwanini tupoteza mida kuongelea yaliyopita? Pamoja na kuwa yanaumiza ila pia kwa sasa kama mjuavyo ndugu zangu, nimefulia. Na kama wanavyosema wahenga wa kibeberu, "the highest ones fall the hardest". Yaani nilihit the lowest point of my life, sio tu kiuchumi bali hata kiitikadi. Nikikumbuka namna nlivyokua juu sikutarajia ntafulia namna hii, yaani inafika mda hata buku jero ya msosi wa mchana nakosa dah! Ukiona mtu anakuomba msaada ndugu zangu kama unao mpe. Hakuna kitu kinashusha thamani kama umasikini.

Kufulia kwangu kulikuja ghafla sana. Sikua nimejipanga kabisa. Nliamini nilichokijenga ni taasisi ambayo ni ngumu kufutika. Ni taasisi iliyokua na malengo na misingi inayoweza vuta pesa kutoka popote kuanzia serikalini mpaka kwa wadau binafsi. Katika kipindi nlichokua fresh nlifanikiwaga tu kununua kiwanja Bunju, sikua na akiba wala asset nyingine. So unaeza imagine mshtuko na hali yangu after kufulia.

Sikufulia kwa sababu ya kutumia pesa vibaya labda. Hapana. Maana wananzengo hamchelewi sema Marga kanifilisi hahahaa. Haikua hivyo. Ilikua hivi. Siku moja Albert aliyekua mhasibu wa shirika langu ofisini. Kaniambia kuna shida kidogo boss, “shida gani" nikauliza kutaka kujua zaidi. “report ya external auditors sio nzuri, inaonesha shirika limetumia kiasi kikubwa cha pesa kwa matumizi ambayo hayakupangwa kwenye bajeti" Albert akanielezea. Nilipotaka ufafanuzi zaidi maana kiukweli yeye kama mhasibu mara zote alikua ananihakikishia kila tunachofanya kipo according to the plan.

Albert akaanza kutoa mifano ya activities tulizogharamikia na ambazo hazikua kwenye bajeti. “Boss unakumbuka ile ziara ya mikoani, bajeti ilisema tutalala hoteli hizi za kawaida ila tukakaa hotels za kitalii kama Mount Meru”, nikasimama kwa hasira, “Albert si ww ndiye uliyesisitiza kuwa fungu linatosha na kwa hadhi ya watu tunaoandamana nao tunapaswa kukaa huko? Inamaana unataka kusema ulinishauri vibaya sivyo?”,

Albert hakuonesha hata kujutia. Na nliona kama anatabasam kwa mbali. Aliendelea kunipa maeneo mengine yaliyoainishwa na external auditors. Maeneo yalikua mengi, bonus zisizo na mantiki kwa wasanii, manunuzi ya gari mbili za ofisi, jengo la ofisi tunayotumia nk. Kimsingi nikamwambia atoke ofisini. Alivyotoka tu nikamuandika barua ya kumfukuza kazi.

Kimbembe kikaja namna ya kumaliza issue na wafadhili. Maana mpaka wakati huu haikua ubalozi mmoja tu unaotupa sapoti, ilikua ni umoja wa ulaya. Ikabidi niende hadi makao makuu ya umoja wa ulaya. Pale nikakuta wale wanaoshughulika na mahusiano na mashirika kama langu wapo kwenye kikao. Sikuhitaji akili ya ziada kujua kilichokua kinajadiliwa. Nimekaa pale mapokezi zaidi ya 2hrs. Baadae nikaitwa ndani.

Kufika si namkuta Albert ndani. Nikajua tu huyu fala ndo katengeneza mchongo mzima. Na amesuka huu mpango for a long time. Kikao changu na wao kilikua kifupi sana. Kiujumla niliambiwa tu kuwa Umoja wa ulaya umepokea taarifa ya wakaguzi kwa masikitiko makubwa. Na kwa maana hiyo hawatatoa tena ushirikiano kwa shirika langu mpaka pale uongozi utakapobadilika. Maana yake ni kuwa walikua wanataka nijiondoe katika shirika. Shirika ambalo mm kwa msaada na ushauri wa Zoya tulilijenga. Nikaelewa sasa namna Steve Jobs alivyofeel alipotimuliwa kwenye ukurugenzi wa kampuni yake mwenyewe ya apple.

Kwa kuwa niliamini shirika linamalengo mazuri, sikutaka kuwa sababu ya shughuri zake kukwama. Nikajiuzuru. Cha ajabu, umoja wa ulaya ukamteua Albert kuwa msimamizi wao katika shirika. Na haikuchukua muda akatake over umiliki wa shirika. Ikawa ushahidi kuwa amesuka.mpango mzima. Alijidai mtumishi mwaminifu, kumbe anamalengo ya kunipindua.

Albert alinipindua kwenye kazi yangu. Kilichoniuma zaidi hakuishia tu kunifilisi, akaenda mbali zaidi kamchukua na mpenzi wangu. Iliniuma sana aisee. Kila nlivokua natoka asubuhi nikijua kabisa Albert atatia tim na kumla mpenzi wangu ndani ya my own room. Yeah, nlijua kila kinachoendelea. Na ilikua inanichoma kinoma. Ila umasikini bana mbaya sana. Pamoja na kujua manzi yangu anagongwa ila nikajidai kipofu, sioni kinachoendelea. Ningefanyaje ss, maana sikua na uwezo wa kuhudumia familia yangu na kipindi hiki nshakua baba tayari.

Kuna muda Zahra ambaye alikua dada wa kazi pale home alikua kama anatamani aniambie kinachoendelea ila akawa anasita. Nakumbuka kuna siku wakati natoka nikaamua kumuuliza, “kuna issue yote inayoendeleaga hapa nikiwa sipo", binti akaangalia tu chini hajibu kitu. “si nakuuliza?” alipoona nasisitiza ikabidi anidanganye “hapana shemeji" huku machozi yanamtiririka. Nikajua hawa huwa wanatiana hata mbele ya housegirl.

Marga alipoona mipango yangu yote ya kurudi kwenye ramani ya pesa inakwama, ikabidi anichane live. One day nikiwa najiandaa kutoka asubuhi akaniomba tuongee kwanza. Alichoniambia, “Ras, samahani kama ntakuudhi, ila am moving out", yaani simple tu. Sometimes wanawake wanaroho ngum aisee. Ila hii niliitarajia pia, siwezi danganya kuwa niliamini Marga atakua na mm mda mrefu na hali yangu ya sasa.,

Mawazo ya kwanza kuja kichwani ni kuhusu mwanangu. sikuwaza tena abt Marga maana tayari najua anachoependa yeye ni pesa tu. Najua hata yeye alijua kuwa tayari najua khs yy na Albert. Na kumake matters worse akaniambia “usipate shida kuhusu mtoto, sio wako". Dadeki nikakaa chini.

Marga alimove out. Ila namshukuru kuwa kabla hajamove aliacha amelipia kodi pale ya mwaka mzima. Aliniachia pia karibia kila kitu. Alibeba tu nguo zake. Nikaanza rasmi maisha ya ubachelor. Yaani ilikua ni kipindi kigum sana kwangu. Bangi tu ndo ilikua inanipa faraja na moyo wa kutokata tamaa. Mtoto nimepokonywa, mpenzi amechukuliwa dah. Na ile kuambiwa mtoto sio wangu nikapata picha kuwa hawa walianza kulana zamani. Ikaniuma zaidi, ila sikua na la kufanya.

Nikapata wazo la kuwa muuza vitabu. Sio kwamba ndo nliona kuwa ni njia itakayonipa pesa, hapana. Kipindi hicho nlitaka tu mahali niwe naenda na kupitisha siku huku nikipata pesa ya kula walau mlo mmoja kwa siku. Ndo kuanza kwenda kuuza vitabu Posta.

Baada ya kama miezi minne tangu Marga asepe, oneday narudi home namkuta Zahra nje ananisubiri. Baada ya salamu nikawa natamani kujua kumetokea nn kule walikohamia. Nikamkaribisha ndani ambako kwa kweli palikua pako vurugu mechi, sox, viatu, boxer kila mahali. Zahra alivyopata sehem ya kukaa ndo akanieleza, “nimeamua kutoka kule maana yule shemeji ananisumbua sana" kwa nnavomjua Albert hata sikushangaa. “amekufanyia kitu kibaya?” nikamdadisi, “hapana, ila kila akiona dada yuko mbali anaanza kunishika na wakati mwingine atanilazimisha tufanye bt nikawa nakimbia namuacha mwenyewe nyumbani. mpaka dada akirudi ndo namm narudi",.

Nikamuuliza kama Marga anajua, akasema mchana wa siku hiyo Marga ameshuhudia kwa macho yake Albert akilazimisha kumkumbatia wakiwa jikoni. Ila Zahra hakusubiri kutimuliwa, akamwambia tu kuwa kwa tabia za huyu mwanaume iko siku atambaka so akaomba aondoke. Marga hakupinga. Na kwakuwa hana ndugu wala mahali pa kwenda hakua na jinsi zaidi ya kuja hapa.

Sikujua niamue nn. Kwanza mm mwenyewe tu hela ya kujihudumia mwenyewe sina ntawezaje kuhudumia watu wawili? Kama alisoma mawazo yangu vile maana akaniambia, “kuja kwangu hapa haina maana kuwa nataka uniajiri, hapana, naomba hifadhi yako tu maana pamoja na kuwa sina mahala pengine pa kwenda, najua uliishi na mm kama ndugu yako” akaendelea, “wanaume wote ambao nimekaa kwao waliishia either kunibaka au kunitaka, ila ww ulikua wa tofauti kwangu. Ww ni mtu pekee ambaye nakuamini utanichukulia kama mdogo wako. Naomba msaada wako kaka yangu maana sina pengine".

Maneno yake yalinisikitisha. Ikabidi nimwambie hali halisi kuwa sio kuwa sitaki kumsaidia ila uwezo wa kumlisha sina. Yaani sina chochote. Akanambia nisijali tutakula kinachopatikana na pia kuna vihela alikua ametunza so hatuwezi kukaa njaa.

Ndo ikawa nimepata mdogo wa hiari. Tuliishi kama ndugu. Alinisaidia walau kupaweka pale home ktk hali ya kustaarabu. Kuwepo kwake kukanipa pia hamasa ya kutafuta pesa zaidi maana nisingependa kuona tunalala njaa. Miezi ikakatiza. Oneday ktk story na Zahra akaniambia angependa kujiendeleza kimasomo maana huu muda alio idle angeweza kusoma ile wanaita QT.

Nikaona ni wazo jema, nikamsaidia kujiandikisha kufanya huo mtihani, ambao ukiufaulu unapata sifa ya kufanya mtihani wa kidato cha nne. Nikawa nikirudi jioni naanza kazi ya kumfundisha. Hii ikanipa hamu ya mm pia kurudi shule. Nlichofanya nikauza kile kiwanja changu kule bunju. Sikutaka kwenda law school, nikajiandikisha kozi ya uzamili (masters), nikalipa kabisa ada ya mwaka mzima. Ikabidi nimwambie Zahra ajiandikishe kwenye kituo cha mafunzo hayo ya QT ili awe anaenda asbh then akitoka awe anakuja posta kunipokea kijiwe cha vitabu ili mm niende chuo kwa masomo yangu ambayo yalikua yanafanyika jioni. Ikawa hivyo.

Baada ya muda nlishangaa kuona mauzo ya vitabu yanaongezeka. Hasa Zahra akiwa ndo anauza. Yaani mm nlikua nikiuza sana ni vitabu viwili, ila Zahra alikua akija jioni kauza si chini ya vitabu 10. Na kwa kuwa kwenye kila kitabu kulikua na faida ya Tsh 2000/ kwa kweli hali ikawa inaenda poa sana. Kila siku tulikua tunaweza weka akiba kidogo. Then Zahra akaja na idea ya kuongeza vitu vya kuuza pale kijiweni hasa cultural products, tshirts za kiras na kofia pia. Nikaona ni wazo zuri. Tukapaongezea vitu pale kijiweni na vikawa vinaenda kwa kweli. Tukawa kimtaamtaa tuko walau fresh. Yaani hatukosi hela ya pango, nauli wala chakula. Nikaona Zahra kweli kichwa ingawa umri mdogo.

Tumelisongesha life namna hiyo kwa muda mrefu. Then one day nipo zangu kijiweni nimekaa kwenye bench nikasikia yule shoe shiner wa jirani yangu anaongea na mdada. Sikutaka kumuangalia anayeongea nae, ila sauti ikawa kama naifananisha, yule mshkaji akawa anamuongelesha kwa namna ambayo ni kama wanafahamiana, “……… ila leo best yako hayupo yupo Ras mwenyewe" kabla hajajibu nikageuka kumcheki anayekaribishwa….

Ndo macho yakakutana na my beautiful Zoya. Ndo nikagundua nlikuaga nampenda kiasi gani huyu mwanamke.

Nikasimama. Nikabaki namuangalia na yeye ananiangalia. Sikuweza sema kitu ndugu msomaji…. Cha kushangaza hata yeye hakusema kitu ananitazama tu. I felt like I should say something, anything…. No……everything, bt I just couldn’t…..
 
Kama nlivyosema weekend hii nimeandika ndefu. So kuna episode nyingine ya kuendeleza ilipoishia hii. Uamuzi ni wenu, ije leoleo, kesho kumalizia weekend au katikati ya wiki?
 
Kama nlivyosema weekend hii nimeandika ndefu. So kuna episode nyingine ya kuendeleza ilipoishia hii. Uamuzi ni wenu, ije leoleo, kesho kumalizia weekend au katikati ya wiki?
Ije mkuu.. Hakuna kula kiporo..kilichoandaliwa kiliwe tuuu tutajuana baada ya kula..
 
Episode 9.

Zoya

Mlinimiss eeh? Hahahahaha I missed you too. Sometimes najiuliza hii story ni kunihusu mimi au Ras, Hahahaha. Anyways tuachane na hayo, ila story hii bado mbichi ndugu wasomaji. The last time tumeonana nliwahadithia siku namuona Ras anauza vitabu posta, right?

Basi bwana, that day baada ya kuhakikisha ni yeye, na kuwa hali yake inaonekana kuyumba sana, nlirudi kwenye gari nikakaa kama nusu saa. Nikawa nafikiria since first time namtia machoni Ras. Nisiwaongopee ndugu wasomaji, nliinama kwenye usukani nikalia.

I cried for all that was supposed to happen bt didn’t. Nlimhurumia pia, ila nikaona ni adhabu tosha kwa Marga. Ingawa anayeteseka ni Ras, ila nlijua huko aliko Marga anaumia pia. Acha waumie. Nikafanya maazimio ya kutowashobokea na familia yao.

Kumuona Ras ikawa imenipa kama utulivu flani wa moyo na akili. Sikua nawaza sana kuhusu yaliyotokea. Hii ikanipa chance ya kuanza kumlegezea Diop. Akawa akipiga napokea, msg najibu, outing nazikubali, hivo yani. so tukajikuta tuko close sana yani.

Diop ni mtu flani mcheshi kinoma. Alafu he was a business genius. Tangu amefika ameshaestablish kampuni mbili, moja ya security nyingine ya kilimo cha maua. Na kwa jinsi anavyoielezea mipango yake bila shaka atamake pesa ya kutosha. Zaidi ya yote alionesha kunipenda kwa dhati. Yaani kuacha vinono vya ulaya na kuhamia bongo kuja kuanza upya just for me ilikua ni ishara tosha ya upendo wake kwangu.

Kama nlivyosemaga mwanzoni. Ingawa niko na pesa ila sikupenda kujionesha sana. Badala ya kukaa mbezi beach au masaki labda, nikapanga nyumba mitaa ya kijitonyama. Oneday Diop alikua amekuja dsm from Arusha kwenye mashamba yake ya maua. Pamoja na kuspend time mara kadhaa na Diop, ilikua bado sio wapenzi. We were just friends.

That day akashauri tukapate indian food mahala, maana ilikua favorite food yake. Kilichokua kinanishangaza, hakua anagusia kabisa suala la kuwa wapenzi. Alikua anainjoi tu my company mwenyewe anasema. Bas that day baada ya dinner akanirudisha mpaka home. Kufika home tukafunguliwa geti na mlinzi, akapaki na tukashuka kwenye gari, then nashangaa mtu ananifuata mpaka mlangoni. Mi nlitegemea ataniaga asepe.

Wakati nashangaa whats happening, nikaona Diop ananisogelea, kanisogezea lips . Of course sikuzipokea. Bt akawa ananiwekea tu, nikikwepesha kulia anazifuata, kushoto hivohivo. Mpaka ikabidi anishike kichwa nisimove. Ndo kunigandamizia lips zake kwenye zangu sasa. Ule usoft wake ukanilainisha kidogo, nikazitanua lips zangu na kumpa mwanya akaanza kuzimung'unya. Yaani kama mlinzi alikua anaona kinachoendele naamini siku hiyo hakulinda hahaha.

Ingawa nlikua natoa ushirikiano nusunusu, sikuweza mzuia alipofungua mlango na kunikokotea sebuleni. Akiwa bado anainjoi lips zangu, akanikalisha kwenye sofa. Akaanza kupapasa paja zangu. Mikono yake ikaendelea kutalii mpaka juu kule paja zinapoishia. Alipogundua kuwa chupi nliyovaa ni ile ya vimikanda tu na eneo kubwa la tako liko wazi nikaona pumzi yake inabadilika.

Hakunipa nafasi ya kubadili mawazo. Ndani ya dkk chache ashafungua zipu ya gauni nlilovaa na kulishusha mpaka kiunoni. Alivyo mtata akanitoa kabisa na bra. Kifua chote wazi. Nkawa naona ona aibu pale, eti najifunika macho, hi hi hi. Aibu zangu hazikumzuia kucheza na kifua changu. Zile chuchu zilipata shida siku hiyo. Baada ya muda aibu zote kwishnei. Nkawa natamani anifanye saa ileile maana Huku chini nlikua nshaloa sana. Sikutaka kuendelea kuteseka, nikajilaza pale kwenye kochi nikajitenga mlalo wa kuliwa.

Jamaa hakuangaika hata kuvua nguo, alifungua zipu tu. Gauni langu akalipandisha likajikusanya juu ya kiuno. Utam wote wazi, kwa ajili yake, anifanye niridhike. Diop hakuchelewa, akamtoa babu juma, akanilalia kwa juu. nikamsaidia kubenjua chupi kidogo, akapata chance ya kupenya.

Baada ya karibu miaka miwili nikawa nimefanya mapenzi tena. Usiku ule Diop alilala kwangu. Na ndo ukawa mwanzo wa mapenzi yetu mubashara.

Baada ya miezi kadhaa kupita, si nikapita tena pale anapouzia vitabu Ras. Sjui hata kwa nn nliamua kupita. Cha ajabu sikumkuta. Nikawa najiuliza what happened to him maana vitabu vipo ila yy hayupo badala yake kuna binti ndo yupo pale. Nikatamani kufahamu kinachoendelea. Ndo maana Harmonize aliimba, “……. Wa kuku-unfollow nitakua mie…” hahahahah. Ila kiukweli sio kuwa nlikua namtaka Ras, ila nlitamani tu kujua what’s going on in his life. Sikupoteza muda. Nlipopata mahala nikapaki gari nikarudi mpaka pale kwa mguu.

“Karibu dada, kuna vitabu vizuri vya hadithi, biashara, dini na hata elimu, chagua", ilikua ni sauti ya huyu binti ambaye baadae nlikuja jua anaitwa Zahra. Nikawa najidai nachagua chagua pale, nikachukua kimoja nikaulizia bei. “5000/= tu dada yangu, na unajua kweli kuchagua vitu vizuri", nikajikuta natabasam. Zahra alikua mchangamfu balaa, alafu anasmile moja matata. Ni ndugu wa Ras au wa Marga? Nikawa najiuliza.

“nina hitaji pia vitabu kwa ajili ya kituo cha watoto, so nataka niwe nachukua hapa kwako ili kukupa support “ nikamueleza huku naona namna ambavyo anafurahia na kushangaa kwa wakati mmoja. “ni biashara yako?”, nikamuuliza. “hapana ya kaka yangu, hua anakuepo hapa mpaka saa nane alafu mm napokea mpaka jioni", akanipa maelezo ambayo walau yalinipa mwanga wa kuwa Ras bado yupo mjini hapa. “Mbona anakupa jukumu zito wakati bado unatakiwa uwe shule?” nikamuuliza maana kwa umri wake nlijua kabisa anapaswa awe sekondari. “nasoma asubuhi mpaka mchana, nikitoka shule ndo nakuja hapa ili na yeye aende chuo". Jibu hili likanipa ham zaidi ya kupata details. “chuo anasoma?” nikauliza, “yeah anachukua masters ya sheria UD".

Sikutaka kuendelea zaidi, bt nikajikuta nimenunua vitabu vitano pale then nikasepa. Kufika kwenye gati nikavitumia kweye buti, mimi sinaga hobbie kabisa ya kusoma vitabu, yaani labda inilazimu ila kwa hobbie tu sina biyo interest kabisa. Kusikia Ras karudi kusoma nlijikuta nampongeza kimoyomoyo, walau amefikiria la maana. Elimu ni kama ngazi, ukiipanda unapata fursa ya kuona mbali zaidi.

Ingawa Zahra aliniambia Ras ni kaka yake, sikuamini kama ni kweli maana ingawa sijawahi kutana na familia ya kina Ras lakini nawajua ndugu zake wote kupitia picha. Kwa kuwa maswali yalikua mengi, nikaazimia kurudi pale kesho yake. Na ndivyo nlivyojikuta namzoea Zahra. Marq kwa mara jioni nlikua napita pale tunapiga story. Na kupitia yeye nikajua Ras ashakimbiwa na Marga. Marga anaishi na Albert. Na life ya Ras kwa sasa kiujumla. Nikajikuta namhurumia Ras na maisha anayoishi sasa.

Nlijua Ras anastahili msaada, na nisingeweza kumpa hela Zahra ampelekee, msaada wangu ukawa kuhakikisha kila siku vitabu vitano au zaidi vinanunuliwa pale. Hata kama sio kupitia mm, sometimes nlituma watu wanunue ili tu isionekane nina agenda binafsi. Kingine nikamshauri Zahra waongeza varieties za bidhaa nyingine pale walipo, nikamwambia amshauri kaka yake aweke vitu vya kiras pale atapata wateja, na kweli baada ya mwezi nikaona kuna tshirts, kofia, culture, slippers yaani wakafuata ushauri.

Ingawa nikawa napata taarifa za Ras, ila penzi langu lilikua kwa Diop. Nikawa sasa niko radhi hata kuolewa na Diop. Biashara zake zilikua mno, alikua na pesa balaa. Nlikuaga naendesha Nissan Xtrail, ila Diop akaninunulia Prado VXL moja matata kinoma. Sikua na haja ya kuhangaika tena. Diop alionesha kunipenda, kunijali na kuniamini. Hakua mtu wa kunilimit au kunifuatilia sana, na pia alinipa uhuru kwenye maisha yake. Yaani muda wowote naenda ofisini kwake, na yule secretary wake alikua akiniona tu shughuri zote zitasitishwa nipewe macare kama mm ndo mkurugenzi.

One day mida ya saa kumi nikasema nikapige story na Zahra. Nikawa nimejiaminisha atakuepo maana ndo mida yake hivyo sikuwa hata nimehangaika kuangalia mahala kijiwe chao kilipo. Ile nafika ndo namuona Ras. Nikatamani nirudi nlikotoka mbio, ila nikajua ataniona nakimbia then ahisi I still care au namuogopa.

Ras mwenyewe alionekana yupo kwenye lindi la mawazo. Ndo yule shoe shiner akaanza kuniongelesha pale. Mara Ras akawa kama kashtuka kutoka alichokua anakuwaza, ndo kuniangalia sasa, macho yakagongana akasimama. Cha ajabu nikuwa sikuweza hata kumsalimia. Sanasana hasira tu zilinijaa kwa alichonifanyia. Tukabaki tunaangaliana.

Mara ghafla si naona mwenzangu machozi yanamtiririka. Sijawahi muona Ras akilia. Yale machozi yaliusuuza moyo wangu. Hakuwahi niomba mshamaha ila palepale nikajua moyo wangu ushamsamehe Ras. Kwa kuwa mwanaume kulia, tena kulia hadharani ni aibu, akawa anajifunika uso kwa mikono. Ikabidi nimsogelee, nikazungusha mikono begani kwake, akatuliza kichwa chake kwenye bega langu, halii kwa sauti wala hatingishiki anabubujika tu michozi.

Baada ya kuona people zinaanza kujaa pale, nikamwambia twende. Nikamshika mkono nikawa namuongoza nlipokua nimepaki gari. Huku nyuma nikawa nasikia watu wanapiga shangwe, wengine miluzi wengine wanasema eti “mbele ya mwanamke hata magangster wanalia….”. nikamfungulia mlango wa gari akazama. Then nikazunguka upande wa dereva, nikawasha ndinga. Sikujua hata tuende wapi jioni ile.

Break ya kwanza Nyumbani restaurant. Nikamkuta Komando mama Samfood mwenyewe, ananijua mteja wake. Bahati mbaya kumbe siku hiyo walikua wanafanya renovation jikoni so hawakua wanapika. Nikamwambia vinywaji tu vinatosha. Akanikaribisha tukakaa na Ras.

“Mambo Ras", nikamsalimia. Akatabasam, of course hatukua tumesalimiana mpaka muda huo. Hakujibu. “how is Marga?”, nikawa najidai sielewi kitu ili apate uchungu wa kunieleza. “siko nae tena, alichukuliwa na mfanyakazi wangu yule Albert". Wakati anaongea mhudum akafika. Nikashangaa Ras anaagiza Safari. Tangu namfaham hajawahi kunywa pombe. Sikuuliza chochote. Mi nikaagiza zangu wine flani nyepesi sana.

Baada ya vinywaji kuja, Ras akaanza kufunguka A to Z. Nikastaajabu aliposema hata ule mpango wa kutuachanisha na yeye uliosukwa na Marga alikuja kuelezwa na Albert, ila kwa kuwa Marga alikua tayari anamtoto wake hakutaka kuchukua hatua. Kilinachomhuzunisha na kumpain Ras mpaka wakati huu ni yule mtoto, maana alijua kabisa ni wake ila kwa kuwa mama mtu ndo kashaamua kusema vile hana budi kumkubalia.

Amemaliza kutoa story yake usiku ushaingia. Na kwa muonekano wake alikua hajala siku nzima huyu mtu, nikaona sio mbaya nimtafutie msosi. Tukaingia kwenye gari mpaka millennium towers pale. Bahati mbaya na penyewe ile restaurant tukakuta hakuna msosi. Dah. Ras akasema nimuache tu aende akale home, mdogowake atakua ameshapika. Wakati nataka nimpeleke akapokea simu ya huyo mdogo wake. Kuuliza anasema dogo anaomba radhi amechelewa maana wanafanya majaribio ya mitihani ya practical za form four now. Nikawa sina jinsi, nikampeleka home nikampikie.

Kufika home, nikamkaribisha akakaa kwenye sofa. Lilelile tunalotianaga na Diop, kidogo nimkataze asikae hahaha. Mawazo haya ya kijinga ndo yakafanya ni.kumbuke mpenzi wangu Diop. Ikabidi nimpigie simu kumwambia tunawageni. Hakupokea. Nikapiga tena, akapokea tule secretary wake, akaniambia bado wako ofisini ila ametoka kidogo akirudi atanipigia. Kweli after few minutes akapiga. Wala hakua na shida. Ndo uzuri wa kudate na wazungu. Hawana conclusion za kipuuzi. Ila Diop akaniambia hata rudi maana inabidi asafiri kwenda arusha that same night. Ni safari ya ghafla ndo maana hajapata wasaa wa kuja hata kubadilisha. Akaahidi kunipigia akifika Arusha.

Nikaanza kuandaa pale mchemsho wa kuku. Nliona ndo msosi wa fasta. Nikachanganya huko viazi, ndizi, hoho, karoti, vitunguu, pilipili na viungo flani hivi vimechanganywa tangawizi na vitu gani sjui. Haikuchukua muda vikawa tayari, nikatenga tukaanza kula. Akaomba pia nimpe upande wangu wa story tangu tumeachana. Nikampa full picture. Mambo mengine hata Diop sijawahi mwambia bt nlijikuta namhadithia Ras.

Baada ya menu nikasema kabla sijampeleka kwake anisubiri nioge. Nikamuacha kajinyoosha kwenye sofa anacheki TV. Kule bafuni nikashangaa naanza pata mawazo ya namna Ras alivyonifumua siku ile bafuni Arusha. Nikayapotezea fasta. Siwezi kuwa msaliti wa namna hii, tena kwenye the same house….No.

Baada ya kuoga nikaenda room, nikatinga jeans yangu na tshirt ili nimpeleke huyu mvuta bangi kwake. Kufika sebuleni nashangaa mtu keshasinzia longtime. Kijasho tu kinamtoka. Nikajua ni shibe ya ghafla baada ya kushinda na njaa the whole day. Na nnavyomfaham Ras akishasinzia kumuamsha ni shughuli, labda uje na maji. Nlichofanya nikaadjust kiyoyozi ili asiteseke na joto, then nikachukua computer yangu nifanye vijikazi kadhaa vya ofisini kwangu.

Kwani kazi zilifanyika basi…. Kila mara namcheki Ras. Sijui ni kale kaubaridi ka kiyoyozi au alikua anaota, maana mashine yake ilikua imetuna ndani ya suruali yake. Mwanzo nikawa naiangaliaaa then natabasam tu.. ila baada ya muda nikaanza kukumbuka yasiyopaswa kukumbukwa. Ule ukubwa na utam wa lile hogo ukawa unapita kichwani kwangu kwa awamu kama feni yenye panga moja, vuuum, vuuum, vuuum.

Ikabidi niondoke pale maana nikaona siconcentrate na nnachofanya. Nikaenda bedroom nikajilaza kitandani. Sikuchukua muda usingizi ukanipitia. Kuja kustuka nikacheki saa ya kwenye simu ni saa saba na nusu usiku. Missed calls kama zote kutoka kwa Diop. Nikampigia, hakupokea. Baada ya muda simu akazima kabisa. Itakua kamind au?

Ikabidi nibadilishe nguo ili nilale vizuri maana nlikua nmelala na nguo nlizovaa nikitaka kumsindikiza Ras. Nikapiga nightdress yangu ya pink, nikarudi bed. Badae nikakumbuka Ras hana shuka pale alipo, nikasema ngoja walau nikamfunike.

Kufika kwenye kochi alilolala nikaona alijiweka comfortable zaidi. Maana alikua kavua shati ila alirudi usingizini tena. Nikalinyoosha shuka nikaanza kumfunika miguuni, nlipofika kiunoni macho yakagota mashineni. Walahi kidogo nimguse sema nikajizuia. Nikaendelea kumfunika hadi kifuani, pale kifuani ndo pakawa hapafunikiki, maana kila nikipafunika napafunua tena kupaangalia, jamani, nyie acheni tu, Mungu anajua kuumba.

Katika kushangaa kwangu, si Ras akastuka. Akanikuta nimepiga magoti nimeshika shuka, niko karibu kabisa na alipo. Macho yakakutana, akasmile. Sjui hata alichotabasamia. Bt kuna mtu alisema tabasamu huambukiza, nikajikuta nasmile pia. Macho yake yakahamia kifuani kwangu, na mm nae badala niondoke nikabaki tu pale najishangaa kwa nn siondoki.

“Asante kwa shuka Zoya, nlishaanza hisi baridi", maneno yake ndo kama yakanizindua hivi. Nikasimama, najua alitamani walau aniguse maana hiki kinight dress changu kwanza ni kifupi alafu transparent. Sikuatka kujifichaficha wala sikua na aibu, kwanza Ras hakuna kitu changu hajawahi kiona. Wakati naondoka nikamgeukia, nikakuta kanikodolea mimacho. Yani wanaume, matako yaliwafanyaje hahahah.

“Unaeza lala chumba cha wageni utakua comfortable zaidi", nikamwambiankwa sauti yangu ya upole. akafikiria kwa muda akasema poa. Nikamuonesha kwa ishara “ni mlango ule wa mwisho, hakiko organized sana utanisamehe" akaitikia "usjali, u have been very kind". Nikamuacha. Sku hiyo usingizi ulikuja kwa taabu. Yaani kukawa na mgongano wa mawazo kichwani. Maana sielewi what im going through. I love Diop, tena sana, ila mbona mbele ya Ras napoteza netwek.

Asubuhi nimeamka mapema tu,. Najuaga Ras anapenda kahawa, so nikamtengenezea na sausages kadhaa na kumkaangia mayai nikaviacha mezani nikarudi room. Then nikakumbuka ile room ya wageni alikolala Ras ndo nimevitupia vitabu vyote ambavyo nlikua navinunua kule kijiweni kwake. Nikapanik, maana akiviona sijui atareact vipi.

Ghafla mlango wa chumba changu ukafunguliwa, kabla hata sijakasirika, kushangaa au kugomba kwanini anaingia room kwangu bila hodi, nikamuona Ras amesimama mlangoni mkononi kashika vitabu kadhaa nlivyonunua kwake. Nikajaribu kumsoma reaction yake wala hasomeki, ananiangalia tu, na mm namuangalia.

“So its you", ndo maneno yaliyomtoka hatimae. Nikaitikia kwa kichwa tu maana sikujua natakiwa niombe msamaha au nijisifu. Nikawa nimetizama chini. Nikahisi ananisogelea, kuinua kichwa huyu hapa kashafika. Machoni kwake machozi yakawa yanamlengalenga. Kwa huruma nliyonayo, nikashangaa mm ndo nadondosha chozi la kwanza. Akanihug, ile kwa nguvu kama anaogopa nitakimbia. Ndo nikaona nae analia. Ikabidi nimbembeleze, shhhhhh, don’t cry man. Don’t cry

“Thank you", akajikuta anatamka baada ya kumtuliza. Akataka kujichomoa nikamng'ang'ania. Akabaki ananiangalia. Ras nae, hajuagi hata kujiongeza. Ikabidi mimi ndo nimsogezee lips. Akazipokea vizuri tu. That kiss reminded me of so many moments with him. I felt like home in his arms.

Bahati mbaya au sijui niseme nzuri, nlikua nimevaa hivi vibukta vifupi vya cotton, na sikua nimevaa chupi ndani. Huku juu nlikua na tshirt flani pana la kilimanjaro marathon lakini fupi, yaani nikinyanyua mikono kiuno kinakua wazi ila nikiishusha inakifunika. So Ras akawa anaenjoy tu mwili wangu. Anatambaa kutoka kiunoni hadi kifuani. Mguso wake ulinipa raha ya hatari, nikawa najihisi kama yani amenizunguka kila eneo la mwili wangu. Nilivo fala eti nikaingiza mkono kwenye suruali yake nimguse mashine yake, ebana eeh, nlivoishika nikahisi natoka vipele vya msisimko.

Akanibeba akanirushia kitandani. Ile kunibwaga kitandani, miguu ikawa huku na huku, na kwakuwa sikua nimevaa chupi, akawa ameona kila kitu. Alichofanya kabla hajapanda kitandani akavua nguo zake zote. Utafikiri nlikua nimesahau Ras anadude kubwa, nikajikuta nashangaa kabisa kama ndo namuona mara ya kwanza. Akatabasam. Nikaona namm nitoe zangu. Tukabaki watupu kabisa, tayari kwa mechi.

Mara nasikia honi nje ya geti. Nikashtuka, ikabidi nikurupuke nivae fasta. Ras nae akabeba nguo zake mkononi kaenda room kwake…

Tukutane jumamosi Mungu akitupatia uhai.

Wasalaam

Kiga.

8141cd37c456dbcadec68418ebb0f48f.jpg
 
Back
Top Bottom