Huwa najiuliza sana kuhusu nini hasa kimesababisha neno Mapinduzi kutamalaki bara na visiwani.Historia ya bara hakuna tukio lolote la kisiasa lililohusisha Mapinduzi tangu wakati wa TAA,TANU na hata katika kupigania uhuru wetu.Maana kwa wasiojua usahihi wa historia Tanganyika haijawahi kutawaliwa na Mwingereza bali mara baada ya WW I Mjerumani ambaye ndio alikuwa mtawala wetu alinyang'anywa koloni la Tanganyika na League of Nations wakawakabidhi Waingereza ili tuwe chini ya uangalizi chini ya mfumo uliojulikana kama (International Trusteeship System),ndio maana Mwl Nyerere alikuwa anaenda UN kudai uhuru kwa kigezo cha kuonyesha utayari wetu wa kujitawala wenyewe ( Maturity).Pale uwanja wa uhuru lilikuwa ni tukio la makubaliano kati ya UN na Tanganyika ndio maana Gavana wa Kiingereza alikuwepo na jopo lake na kukawepo scenario ya makabidhiano ya madaraka na sio Mapinduzi.
Kule Zanzibar ndio kulifanyika Mapinduzi ambayo yaliiweka madarakani serikali ya ASP lakini Mapinduzi yale yalipaswa yatafsiriwe kiuchumi na kijamii kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.
CCM inapaswa kuitafsiri dhana ya Mapinduzi katika uwanja wa kiuchumi kwa kuzingatia mahitaji ya sasa ya kiteknolojia na kidiplomasia, vinginevyo tunaweza kuyatafsiri Mapinduzi yanamaanisha kupindua matokeo ya uchaguzi na kuwapindua wapinzani wa ndani na nje ya Chama.
Kule Zanzibar ndio kulifanyika Mapinduzi ambayo yaliiweka madarakani serikali ya ASP lakini Mapinduzi yale yalipaswa yatafsiriwe kiuchumi na kijamii kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.
CCM inapaswa kuitafsiri dhana ya Mapinduzi katika uwanja wa kiuchumi kwa kuzingatia mahitaji ya sasa ya kiteknolojia na kidiplomasia, vinginevyo tunaweza kuyatafsiri Mapinduzi yanamaanisha kupindua matokeo ya uchaguzi na kuwapindua wapinzani wa ndani na nje ya Chama.