Infinite_Kiumeni
JF-Expert Member
- Jan 23, 2023
- 382
- 661
Hapa naongelea mwanamke ambaye ulikua naye vizuri lakini sasa analeta jeuri. Ila kama mwanamke ana hulka ya ujeuri, huyo hakuna haja ya kupasua kichwa.
.
Mwanaume kuwa dhaifu baada ya muda. Mara chache mwanamke atakuambia umekua dhaifu, hivyo njia rahisi kwao ni kuleta ujeuri wakiwa na matumaini utawaelewa na kufanyia kazi (hapa ndo wengi hupata shida). Hivyo kabla hujaanza kumshutumu mwanamke pitia upya misimamo yako, malengo yako, mipaka yako na hali yako ya ujasiri sababu we ndo kiongozi. Inawezekana wakati unamtongoza mwanamke ulikua mwanaume jasiri lakini sasa mmeshazoeana umebweteka, mnachukuliana poa. Kwa hilo jeuri ya mwanamke maana yake kuna sehemu umelega na anataka uwe kama yule mwanaume kipindi anamtongoza, aliyekua na mipaka, msimamo na ni jasiri haendeshwi na mwanamke hovyo.
.
Majaribu ya mwanamke. Mara nyingine mwanamke humjaribu mwanaume wake ili kuona je upo ngangari, ataongea/ kufanya vitu vya ajabu ili akuchokoze aone kama utamuadhibu au utajichekesha tu na kumuacha. Usipomrudisha katika mstari unaotaka wewe heshima yake itashuka na ataanza kukudharau. Mfano, mwanamke amekununia bila sababu na kila unapojaribu kumfanya afunguke anagoma au kukujibu kimkato au anapiga makelele, apo inabidi kuonesha msimamo na mipaka yako kuwa huwezi vumilia usichotaka na kumuambia kitu kama “baby, unaonekana kuna kitu kinakusumbua lakini hutaki kusema, sasa ukiwa tayari kuongea kiutu uzima uje tuongee vizuri, na usinifate kwa makelele” kisha muache mpaka akiwa tayari atajileta mwenyewe. Pia katika kipindi kama hiki ndo utamjua vizuri mwanamke uliyenaye.
.
Mwanaume kumpa nafasi kubwa mwanamke. Unamuona kama ye ndo mwanamke pekee duniani, au ndo mwanamke mkweli kuliko watu wote na hutaki kukubali anaweza kukusaliti au ndo ile umeongea naye tu leo unaanza kuwaza maisha yatakuaje mkiwa wawili nyie au kumshirikisha mwanamke kwa kila kitu chako kwa mapana. Watakuona huna kitu chochote maishani mwako zaidi ya mwanamke, hivyo atakudharau na kuweka kiburi. Mwanamke ukimsikiliza atakuambia anataka awe namba moja (ndo kila kitu) kwa mumewe lakini hiyo siyo nafasi yao, hivyo usiingie kwenye huo mtego. Ila mfanye ajisikie wa thamani kwako kuliko wanawake wengine.
.
Hapo juu utaona mwanaume ndo anaanza kuruhusu ujeuri uwepo kwa mwanamke ambaye hakua jeuri, hivyo ni muhimu mwanaume kuwa kiongozi wa mahusiano yako na kutambua unapolega/ jeuri inapoanza na kumuongoza mwanamke wako awe mwenye upendo na sio jeuri. Nakazia tena, kama kiburi ni hulka ya mwanamke hauna haja ya kuumiza kichwa.
.
Mwanaume kuwa dhaifu baada ya muda. Mara chache mwanamke atakuambia umekua dhaifu, hivyo njia rahisi kwao ni kuleta ujeuri wakiwa na matumaini utawaelewa na kufanyia kazi (hapa ndo wengi hupata shida). Hivyo kabla hujaanza kumshutumu mwanamke pitia upya misimamo yako, malengo yako, mipaka yako na hali yako ya ujasiri sababu we ndo kiongozi. Inawezekana wakati unamtongoza mwanamke ulikua mwanaume jasiri lakini sasa mmeshazoeana umebweteka, mnachukuliana poa. Kwa hilo jeuri ya mwanamke maana yake kuna sehemu umelega na anataka uwe kama yule mwanaume kipindi anamtongoza, aliyekua na mipaka, msimamo na ni jasiri haendeshwi na mwanamke hovyo.
.
Majaribu ya mwanamke. Mara nyingine mwanamke humjaribu mwanaume wake ili kuona je upo ngangari, ataongea/ kufanya vitu vya ajabu ili akuchokoze aone kama utamuadhibu au utajichekesha tu na kumuacha. Usipomrudisha katika mstari unaotaka wewe heshima yake itashuka na ataanza kukudharau. Mfano, mwanamke amekununia bila sababu na kila unapojaribu kumfanya afunguke anagoma au kukujibu kimkato au anapiga makelele, apo inabidi kuonesha msimamo na mipaka yako kuwa huwezi vumilia usichotaka na kumuambia kitu kama “baby, unaonekana kuna kitu kinakusumbua lakini hutaki kusema, sasa ukiwa tayari kuongea kiutu uzima uje tuongee vizuri, na usinifate kwa makelele” kisha muache mpaka akiwa tayari atajileta mwenyewe. Pia katika kipindi kama hiki ndo utamjua vizuri mwanamke uliyenaye.
.
Mwanaume kumpa nafasi kubwa mwanamke. Unamuona kama ye ndo mwanamke pekee duniani, au ndo mwanamke mkweli kuliko watu wote na hutaki kukubali anaweza kukusaliti au ndo ile umeongea naye tu leo unaanza kuwaza maisha yatakuaje mkiwa wawili nyie au kumshirikisha mwanamke kwa kila kitu chako kwa mapana. Watakuona huna kitu chochote maishani mwako zaidi ya mwanamke, hivyo atakudharau na kuweka kiburi. Mwanamke ukimsikiliza atakuambia anataka awe namba moja (ndo kila kitu) kwa mumewe lakini hiyo siyo nafasi yao, hivyo usiingie kwenye huo mtego. Ila mfanye ajisikie wa thamani kwako kuliko wanawake wengine.
.
Hapo juu utaona mwanaume ndo anaanza kuruhusu ujeuri uwepo kwa mwanamke ambaye hakua jeuri, hivyo ni muhimu mwanaume kuwa kiongozi wa mahusiano yako na kutambua unapolega/ jeuri inapoanza na kumuongoza mwanamke wako awe mwenye upendo na sio jeuri. Nakazia tena, kama kiburi ni hulka ya mwanamke hauna haja ya kuumiza kichwa.