Niliwahi kumtembelea Ex -wangu baada ya kufiwa na mumewe, kumpa pole na kujua anaendeleaje. Huyu alikuwa mwanamke wa ndoto yangu wakati wa uvulana,Wajanja waliniwahi, Aliwahi sana kuolewa.Nilipofika nyumbani kwake nilimkuta na kijana wake wa kiume yuko chuo mwaka wa 2.
Nakumbuka alimwita yule kijana na kunitambulisha, na hakuficha alimwambia nilikuwa nani kwake, lakini alienda mbali akaongea kitu ambacho sikutarajia kama angeongea, ilikuwa way way back akiwa na kitoto kidogo alinifuata Job, tukakaa mahali akapiga maji mbaya, akiwa na mtoto huyo huyo kijana wa chuo, Shughuli ilikuwa namna ya kuondoka hapo!!Nilimtafutia gari alifika kwa muwewe salama, akakumbusha ilivyokuwa siku ile bila kumuogopa yule kijana, ilinipa wakati mgumu kidogo lakini ilikuwa salama.