Changamoto za kupata wachumba wa mtandaoni

Changamoto za kupata wachumba wa mtandaoni

Muda mrefu umepita niliwahi kutuma post ya kutafuta mchumbawa kuoa hapa Jamii Forum, nashukuru Mungu baadhi ya wasichana wali respondvizuri nikafanya nao mawasiliano then nikaamua kuchagua mmoja.
Ulishawahi kujiuliza nini matokeo ya kuomba uchumba,urafiki nk. Kwenye mitando? Kama jibu ni ndio ulichokiomba ulikipata namazingira ya kuanzisha mahusiano katika mitandao ndio hayo, ikiwa kamaulifikiria mara mbili basi kubaliana nalo. Pili kama ulitamani mahusiano yakoyawe ya kuonana uso kwa uso usingetumia social media kuomba mahusiano. Sasaumempata umtakae.

Tulianza kuishi kama wapenzi kwa mawasiliano lakinichangamoto iliyojitokeza yule binti alianza kuniomba pesa za matumizi nimtumielakini mmi sikumpa nilimwambia sina baada ya hivyo binti akaanza kulalamikakuwa mmi simpendi na mambo mengine mengi!, Hivi wandugu kweli inawezekanakumhudumia mpenzi ambae hujawahi kuonana nae live yani face to face? Ambae piabado hujamsoma tabia yake vizuri zaidi?

Mtu ambaye hujaonana nae na unamuhofia unawezajekuanzisha mahusiano nae ya kimapenzi ? Kama utasimamia matamshi yako binti huyoulimwadaa kama sio kumrubuni nae akakuamini kiasi cha kukuomba umtimiziemahitaji yake ikiwa ni pamoja na noti! Sasa unashangaa ni nini? Toa noti.
Sio siri huyo binti moyo wangu ulimpenda sana

Mtu ambaye moyo wako uradhi dhidi yake bado unamuhofia nakushindwa kusaidia njuluu kiasi za kujikimu!
Hivi huyu binti anastahili kutumiwa pesa kweli?
Anasitahili kutokana na mazingira uliyomjengea tokamwanzo si unampenda why don’t you help her now! Kwani shida alizonazo sasa naatakazo kuwanazo baada ya kuonana nae ni tofauti au ndio zitakuwa genuine kamafungu lipo mpe tu anashida.

 
ebooo hujatuma tu hadi leo hiyo pesaa..jihesabie ushapigwa kibut teh teh..
 
Usitume hela mkuu hadi muonane ma umgegede kwanza!
 
Inategemea na kiwango..at most iwe 50 bas hapo ni normal tu haiumi hata mkipotezeana mbele..ila umnyime kabsaa haijengi kitu,mapenzi mazuri yanakuaga na pesa kidgo haiangalii mmeonana or not..
 
Boss, sidhani kama kuna Mwanamke/Manzi yeyote humu ambaye utatangaza unatafuta mchumba/mke, ajitokeze na awe normal. Lazima ana flaws za kutosha ndio maana kashindwa kupata mtu in the real world. Vizuri havipatikani kirahisi kamwe. So wanaojitokeza kutangaza hizo nafasi, inabidi wawe wamejiandaa kisaikolojia.

Upo sawa kabisa mkuu,tuko pamoja sana!
 
Achana naye huyo sio mpenzi. yeye mwenyewe hajitambui. hana mshipa wa aibu. ether bado mtoto kimawazo au ndio wale wa kuchuna watu tu kuwafanya atm machine. mtu hajawai kukuona. mawasiliano tuu kwa sms au sim. unapata wapi guts za kuanza kuomba hela. achana naye kabla hujaleta uzi/post nyingine hapa ya kulaumu kupotezewa muda au kupigwa mizinga sana.
 
Hivi unaanzaje kuomba hela mtu hujawahi hata kuonana nae duuh. Hatari sana
 
Kuna mwingne kamliza jamaa yangu,ila muda si mrefu no yake itawekwa humu,
 
Maoni yangu unaweza kumpatia pesa za vocha kwa mawasiliano....zaidi ya hapo unamwambia uko broke
 
Tabia za kina Dada zetu was Kibongo ni za ajabu sana, Na hii yote inatokana sijui tuseme ni urithi au ukosefu wa elimu au ni kuwaza kuiba tuu.

Hata ukikosea no ikiwa imemkuta mdada basi kama umejifanya kuonge kwa mahaba kidogo tuu usubiri kuombwa, wamekalia wizi wizi mtupu.

Wenzetu wachumba na wanaishi pamoja wanashea matumizi Leo NTU anakwambia umetumie pesa ni ujinga hata kuonana bado.
 
Achana naye huyo sio mpenzi. yeye mwenyewe hajitambui. hana mshipa wa aibu. ether bado mtoto kimawazo au ndio wale wa kuchuna watu tu kuwafanya atm machine. mtu hajawai kukuona. mawasiliano tuu kwa sms au sim. unapata wapi guts za kuanza kuomba hela. achana naye kabla hujaleta uzi/post nyingine hapa ya kulaumu kupotezewa muda au kupigwa mizinga sana.

Umeongea point sana mkuu!
 
Kwani mnaishi mtwara na kigoma kiasi kwamba ni shida hata wikiend moja kufika anakoishi mwenzio.??

kuna watu wanalalamikaga humu kuwa wadada wa humu wanaanzaga na kuvuna pesa badala ya kujenga trust kwanza.
hii ni changamoto ambayo dada zetu inabidi waifanyie kazi. sio kila mtu ni mpita njia kwamba maji utamuuzia. wengine ni wakaaji

Umenena kk,hiyo ni changamoto kubwa
 
Back
Top Bottom