Chama Kipya (CCJ) na Hatima ya CCM - lisemwalo...

Chama Kipya (CCJ) na Hatima ya CCM - lisemwalo...

Tunaanza upya tu... yale yale ya akina Mabere Marando, Makani et al.. mwisho tunaanza nambari wani nambari wani....

Kwa maoni yangu hao wote wako 'kuyumbisha' matokeo ya uchaguzi unaokuja, kama vigogo nao wapo matokeo ni rahisi kutabirika....

Mwito kwa wananchi: Vyama vinavyothibitika kuwa na uwezo wa kuondoa baadhi ya manung'uniko vinaeleweka CCM, CUF, CHADEMA, etc etc na sio kwa mpangilio huu- Kabla wananchi hawajapiga kura, kuna umuhimu wa kuangalia historia ya nchi hii(kuanzia mwanzoni mwa kukubalika kwa vyama vingi) na historia ya hao vigogo(chama kipya) kama kipo/wapo

Hakuna ubaya kukawa na Chama kingine kipya, vilevile hakuna ubaya kama Wananchi watakuwa wamejifanyia mazingaombwe na kuona huo mbadala.

Piga kura kwa uangalifu!

Ahsante.

Haya ndio matatizo ya kutaka kuwa katikati kama Kikwete vile. Uwe na msimamo maana mi naona hapa unazungukazunguka pale pale, ingawa ulianza vizuri tu.... Hivi CCM Kwa jinsi kilivyo kibovu ndiyo ukipange na CUF na CHADEMA, wanafanana kweli?.

CUF na CHADEMA ni vyama vyenye wanachama wa kweli kutoka moyoni. Hawaogopi kufanyiwa UBAREGU....................upo hapo? Ni vyama vya watu majasiri, makini, wenye uzalendo na uchungu wa kweli wa nchi. Wanatetea watu wasiostahili kutetewa maana watanzania ni watu wa kufuata upepo kama bendera na ndio maana tunastahili kuendelea kuibiwa MCHANA KWEUPE. TUMEKUWA KAMA MANDONDOCHA NA U-CCM WETU.

CCM ni chama cha waoga, watu waliojiunga ili kupata ulaji, madili, misheni town, wanabebwabebwa na wajomba, mafisadi, watu wasio na msimamo sikuzote wako katikati. Huwezi kuwa mwanachama mzuri CCM kama Kikwete bila kuwa na Phd ya Unafiki, Kujikombakomba, na uongo wa kizamani wa enzi za Zinjanthropus.

CCJ ni chama cha mafisadi waliokosa hisa kwenye serikali ya Kikwete na hivyo wanajifanya ni wapinga ufisadi kwa sababu za visasi. Saa hizi wanapima upepo, ni ndumilakuwili na ndio maana wanajificha, watu wa hivyo hawatufai hata kidogo, hawawezi kulitetea taifa hili dhidi ya ubabe wa ubeberu mamboleo. Wanataka kutumia mwanya uliopo ili kuhakikisha wanashika hatamu 2010. Hawataki kurudia makosa ya 2005 yaliyowafanya waishie kwenye ubunge tu na kukosa mashavu mengine. Lakini pia kinaungwa mkono na mafisadi walioburuzwa kortini na kudhalilishwa hadharani, na kwenye vyombo vya habari ili kulipa kisasi dhidi ya Kikwete mlea ufisadi.

CCJ ni kama CCM tu kwa kuwa ni watu wanaotaka kuingia madarakani kwa maslahi yao binafsi na familia zao huku wakiudanganya umma kuwa wanataka kuweka mambo sawa, na kujifanya wanataka kuiangalia jamii....bla..bla...bla.

Suala hapa ni kuwa tusikubali kudanganywa na mwanasiasa yeyote kwa vitendo avifanyavyo 2010. Tuwapime wamefanya nini 2005 mpaka 2009. kwa sababu hapa 2010 kila mmoja anakuja na danganya toto ili akubalike kwenye uchaguzi.

Walikuwa wapi kuunda chama sikuzote hizo...MPAKA WANYIMWE MKATE NDO WAJIFANYE WANATUPENDA SANA WATANZANIA? WANAFIKI WAKUBWA!!!!!!!!!!!

CCM- CHAMA CHA MAFISADI

CCJ - CHAMA CHA JANGILI

ENDELEENI KUSEMA KIDUMU UONE NINI KINADUMU NCHINI.....SHAURI YENU!!!!!!!
 
Kisije kikawa ni Chama cha Mafisadi, No. 2, in disguise!

Kabla hatujafanya maamuzi, tutahitaji kuona akina nani wanaunda CHAMA CHA JAMII (CCJ). tukishawajua, na sisi tunajua waliosafi miongoni mwa wanaCCM, basi tutawaunga mkono au kuwakataa.
 
Kisije kikawa ni Chama cha Mafisadi, No. 2, in disguise!

Kabla hatujafanya maamuzi, tutahitaji kuona akina nani wanaunda CHAMA CHA JAMII (CCJ). tukishawajua, na sisi tunajua waliosafi miongoni mwa wanaCCM, basi tutawaunga mkono au kuwakataa.
 
So far mtazamo wa chama kama tulivyoona ni mzuri. Lakini maneno ya kwenye karatasi si hoja tunataka kuona akina nani hasa wameyaandika maneno hayo. Je, ni chui ndani ya ngozi ya kondoo?? Au kazaliwa masia mwokozi wetu?????tuliyekuwa tunamsubiri kwa hamu???? Yote hayo tutayaona. Lakini nasikia na lowasa naye yumo hahahahhahahhahhaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!
 
Wameona chama chao (CCM) kinanuka ufisadi wakaamua kuanzisha chama chengine wapate kuwatia changa la macho wananchi waone mafisadi papa wametoka CCM hili wapate kupigiwa kura.
 
Nasikia hiki chama kipya cha CCJ maana yake ni "SISI JEEE?"!
 
Ni vizuri kujifunza kukubali kuwa upinzani sio vita na kukubali kuwa amani ya nchi hii haipo kwa sababu ya CCM, ipo kwa sababu Watanzania wanapenda amani.
Jinsi CCM inavyomeguka ndivyo upinzani utakavyoimarika. Pale CCM watakapofanya mabadiliko ya katiba yao na kufanya kuwa Mwenyekiti wa Chama si lazima awe rais basi demokrasia itafunguka zaidi na dola itaacha kuikumbatia CCM na dola ikafanya kazi zake bila kuingiliwa na wachezaji rafu wa siasa za utapeli, umimi, ubwanyenye, na wizi.
 
CCJ changa la macho tu. Komredi ogopa sana wanasiasa wanaojitutumua kufanya jambo 2010. It is too late. 2005 yoote mpaka 2009 walikuwa wapi? Hawa ni wanafiki wale wale tu wa siku zote, Ila mkate ni mdogo na kila mmoja anautaka na kifimbo ndo alishalala kwa hiyo hakuna kiranja.....Kumeguka kwao CCM kutaifaa nchi kama wakichukua wapinzani wa kweli...NA SIO HAWA WALIONYIMWA MKATE KWA HIYO WANAONDOKA KWA CHUKI...HUKU WAKIDANGANYA KUWA WANAPIGA VITA UFISADI.

CCJ ni matokeo ya huruma za fisi...fisi huyu amesimama kwa mbali akimwonea huruma swala anayeliwa na simba,...haimaanishi akipata nafasi atamwokoa swala yule.....itakuwa mbaya zaidi maana atakula na kubakiza nyasi zenye damu tu kama ushahidi kuwa kuna mnyama kaliwa....HAKIBAKI KITU.....ffffffuuuu!!!!!!!!!!!!!

KOMREDI AMKA....EBO!!!!!!!!!


Komredi akashube nafikiri wengi wanaoshabikia hili la CCJ si kwamba ndio wamekuwa wanachama wa CCJ au watakipigia kura la ila tunachofurahia ni kule kumeguka kwa CCM tu.

Hatujui ni akina nani wamo humo I dont care CCJ iwe ya walewale Mafisadi au iwe ya wale wanaojidai wapinga Mafisadi it does't matter to me baada ya kujulikana na baada ya CCM kumeguka hapo ndipo tutakapo jua twende wapi CCJ au CCM masalia au tubaki kwenye hivi vyama vyetu vya upinzani tulivyonavyo.
 
Kiwavi nakubali maneno yako kwa asilimia zote.Hiyo ni Janja tu ya kutafuta mkono kwenda kinywani.Hiyo ni Mbinu ya Wachache waliozidiwa ujanja na wenzao katika CCM.
 
Komredi akashube nafikiri wengi wanaoshabikia hili la CCJ si kwamba ndio wamekuwa wanachama wa CCJ au watakipigia kura la ila tunachofurahia ni kule kumeguka kwa CCM tu.

Hatujui ni akina nani wamo humo I dont care CCJ iwe ya walewale Mafisadi au iwe ya wale wanaojidai wapinga Mafisadi it does't matter to me baada ya kujulikana na baada ya CCM kumeguka hapo ndipo tutakapo jua twende wapi CCJ au CCM masalia au tubaki kwenye hivi vyama vyetu vya upinzani tulivyonavyo.

Komredi nimekupata. Kweli CCM imetuchosha mno. Na CCJ ina shombo la CCM, Ila reasoning yako hapo juu ni very true. Inaonekana wewe umechoka kuliko mimi mpaka uko tayari hata zingekuwa CCMA, CCMB, CCMC, CCM Wafanyakazi, CCM Wafanyabiashara, CCM Wakulima, CCM Kanda ya Ziwa, CCM Tarime, CCM Monduli, CCM Longido, CCM Loliondo, CCM Pemba, CCM Unguja, CCM RC, CCM BAKWATA......yaani haya makundi yote yakijimega yakaunda vyama shwari tu...NIMEKUPATA.

Hili sikuliona na ndo mana nakiri umenizidi kidato hapa. Kweli wameguke tu EBO!!!!!!!!!!!
 
Waungwana.

Nadhani yapo mambo hapa yanaendelea chini kwa chini hadi kutufikisha hapo. Wakati chama hiki kikiwasilisha maombi kwa msajili, vile vikao vya juu vya CCM vinatarajiwa kukutana mwisho wa juma hili. Ajenda mojawapo, taarifa ya kamati ya Mwinyi,......

Kwa hiyo, mimi sioni kama haya yote yanatokea kwa bahati mbaya. Nadhani kuna kitu kimetegeshewa hapa!

Lakini, mimi ningedhani kwamba waasisi wa kweli wa chama hiki hawatakiwi kuwa nyuma ya pazia. Ingefaa waachie nyadhifa zote walizonazo kwa sasa; Ubunge, Uwaziri,.......(pamoja na marupurupu yake) wakasimama jukwaani kututangazia nia yao ya dhati kufanya hivyo. Kwa kufanya hivyo wataeleweka na wengi zaidi badala ya kusubiri washindwe kwenye kura za maoni.

Kundi la mwanzo linatakiwa kuwa na waasisi toka vyama mbalimbali, na sio watu fulani toka CCM pekee.
 
Waungwana.

Nadhani yapo mambo hapa yanaendelea chini kwa chini hadi kutufikisha hapo. Wakati chama hiki kikiwasilisha maombi kwa msajili, vile vikao vya juu vya CCM vinatarajiwa kukutana mwisho wa juma hili. Ajenda mojawapo, taarifa ya kamati ya Mwinyi,......

Kwa hiyo, mimi sioni kama haya yote yanatokea kwa bahati mbaya. Nadhani kuna kitu kimetegeshewa hapa!

Lakini, mimi ningedhani kwamba waasisi wa kweli wa chama hiki hawatakiwi kuwa nyuma ya pazia. Ingefaa waachie nyadhifa zote walizonazo kwa sasa; Ubunge, Uwaziri,.......(pamoja na marupurupu yake) wakasimama jukwaani kututangazia nia yao ya dhati kufanya hivyo. Kwa kufanya hivyo wataeleweka na wengi zaidi badala ya kusubiri washindwe kwenye kura za maoni.

Kundi la mwanzo linatakiwa kuwa na waasisi toka vyama mbalimbali, na sio watu fulani toka CCM pekee.


It is true Mpingo, kama kweli wako serious na hawakubaliani na yanayoendelea ndani ya chama chao kwa nini waendelee kujificha ina maana kwa kipindi hiki hadi kura za maoni wakipata wanacho kitafuta ambacho nadhani ni nafasi za kugombea CCJ kitakufa?

Mimi nimeshasema I dont care ni kina nani wanaoanzisha CCJ kwa sababu Im not binded and I will never be binded na chama chochote, watakapoonekana ndipo nitakapojua ni kipi niki-support isije kuwa CCM masalia ndiyo itakuwa bora kuliko CCJ.
 
Kiwavi nakubali maneno yako kwa asilimia zote.Hiyo ni Janja tu ya kutafuta mkono kwenda kinywani.Hiyo ni Mbinu ya Wachache waliozidiwa ujanja na wenzao katika CCM.

Mawazo mgando kama haya ndio yanatufanya tuendelee kukandamizwa daima. Nani kakwambia hao wazalendo lengo lao ni 'mkono kwenda kinywani' tu. Na eti ni wachache waliozidiwa ujanja na wenzao katika CCM?! Ni lazima tuwaunge mkono watu wanaoonyesha uzalendo wa kweli na wenye nia ya kutuonyesha njia ya kutokea. Udhalimu wa CCM umeshawakifu watanzania.
 
Siasa za Tanzania ni taabu kweli kweli. Chama hiki pia kinaweza kujaishia kama safina ya kule Zanzibar ambayo walidhani kuwa ingekuwa tishio kwa kuwa waasisi wake walimeguka kutoka ccm zenj.

Mashinery inayoendesha mfumo mzima wa siasa za Tanzania inahodhiwa na ccm, hivyo ili kuweza kufanikiwa kwa awaye yote lazima afahamu hilo na akatae katakata kufanya majidiliano na ccm au kufuata taratibu za viini macho vilivyowekwa na ccm.

Changamoto kubwa kwa ccj kwa sasa sio wanachama, ila ni usajili ili kiweze kushiriki katika siasa Tanzania.
1. Watapita wapi kupata usajili wakati msajili ni mteule wa mwenyekiti wa ccm?
2. Watapita wapi sasa wakati nec ni ya mteule wa mwenyekiti wa ccm?
3. Nani aliyeko tayari kujidhihirisha kwa umma wa watanzania sasa na kupoteza maslahi yake kwa ajili ya watanzania? isije ikawa wanasubiri kupata viinua mgongo vyao ndani ya ccm ndio waondoke.
4. wamejiandaa vipi kushirikiana na wapinzani wenzao kubadilisha hali halisi ya siasa za ccm Tanzania. Je, ni ule ule mtindo wa kusubiri ccm wapige filimbi nao wacheze? Wataweza je kama hadi sasa wameshindwa kujianisha bayana?

Ili tanzania tufanikiwe kufanya mageuzi ya kweli, ni lazima tufike tukubali kuwa sasa imetosha na tunahitaji kubadilika, lakina bahati mbaya bado tunaishi kwenye chupa na hatujui linalotokea nje ya chupa. Matokeo yake tumeendelea kuamini kuwa bila ccm hakuna maisha, hakuna amani, hakuna mvua wala jua. Badala ya kufahamu kuwa bila sisi wanachi hata hiyo ccm hakuna. Sio serikali kwa ajili ya ccm ila serikali kwa ajili ya watu/watanzania.

Inatia kinyaa watu wengine wenye upeo mfupi wanapodai, eti hao wapinzania watatoa wapi nguvu kazi ya kutawala kama tukiwapa madaraka? wanasahau kuwa leo hii Tanzania ina nguvu kazi kubw akuliko wakati wa uhuru. wanasahau kuwa wewe na mimi tunaoiweka serikali madarakani ndio watumishi wa hiyohiyo serikali!
 
Ili tanzania tufanikiwe kufanya mageuzi ya kweli, ni lazima tufike tukubali kuwa sasa imetosha na tunahitaji kubadilika, lakina bahati mbaya bado tunaishi kwenye chupa na hatujui linalotokea nje ya chupa. Matokeo yake tumeendelea kuamini kuwa bila ccm hakuna maisha, hakuna amani, hakuna mvua wala jua. Badala ya kufahamu kuwa bila sisi wanachi hata hiyo ccm hakuna. Sio serikali kwa ajili ya ccm ila serikali kwa ajili ya watu/watanzania.

Natamani haya maneno wangekuwa wanayasoma hao wa CCJ na CCM na Viongozi wa wote wa upinzani.
 
Wameona chama chao (CCM) kinanuka ufisadi wakaamua kuanzisha chama chengine wapate kuwatia changa la macho wananchi waone mafisadi papa wametoka CCM hili wapate kupigiwa kura.
Mbona watanzania tunakuwa waoga sana?so far CCM imekuwa very strong kuliko vyama vilivyopo na CHADEMA na CUF bado hawana visible plan ya kuchange things todate, na to do nothing is not an option hivyo kama kuna group la watu wa CCM wakajitoa na kushake the balance of power katika nchi hii, ni jambo jema kisha mengineyo tutaendeleza kuanzia hapo.
 
Kiwavi nakubali maneno yako kwa asilimia zote.Hiyo ni Janja tu ya kutafuta mkono kwenda kinywani.Hiyo ni Mbinu ya Wachache waliozidiwa ujanja na wenzao katika CCM.
Haya mawazo ndio yanayoifanya CCM iendelee kuwa madarakani....,hatuisaidii nchi yetu kwa mtindo huu,na mwishowe tunabaki tu kulalamika.
 
Naamini katika kipindi cha mwezi mmoja kuanzia sasa, mambo yatakuwa wazi zaidi kuhusu hiki chama cha jamii (CCJ).

Mh! Jamii kama JF?
 
Back
Top Bottom