CHADEMA yashindwa vibaya Arusha

CHADEMA yashindwa vibaya Arusha

Wana jf hebu tuone aibu
kidogo na tuwaulize hawa wenzetu hiyo people's power yao iko wapi ikiwa
hata kutoka tu ndani kwenda kituoni kupiga kura wameogopa kati ya
wapiga kura 60,000 wanajitokeza 6,000 tu si kituko hiki sasa hao sisiem
zaidi ya 20,000 wangejitokeza si ingekuwa gharika. Haya mambo ya
people's power za kishabiki hazitapeleka cdm ikulu kama
wanavyojinasibu hebu tuwape ushauri

kwa hiyo unataka kusemaje???
kwamba ccm ndio imeshinda arusha?
hongereni ccm kwa ushindi mnono
hahahaha
daaaah hapa duniani kuna watu wa ajabu sana.!?
 
Wana jf hebu tuone aibu kidogo na tuwaulize hawa wenzetu hiyo people's power yao iko wapi ikiwa hata kutoka tu ndani kwenda kituoni kupiga kura wameogopa kati ya wapiga kura 60,000 wanajitokeza 6,000 tu si kituko hiki sasa hao sisiem zaidi ya 20,000 wangejitokeza si ingekuwa gharika. Haya mambo ya people's power za kishabiki hazitapeleka cdm ikulu kama
wanavyojinasibu hebu tuwape ushauri
Ulitaka tujitokeze kwa maelfu ili mtulipue tena kama mlivyofanya kwa kusaidiwa na mapolisi wenu ile siku ya kuhitimisha zile kampeni?
Kwa taarifa zako wengi waliojitokeza walikuwa wafuasi wa CCM waliochoshwa na jinsi chama chao cha kijangiri na kigaidi hicho kinavyowahujumu wakazi wa mkoa huu.
Hivi hamna hata mshipa wa aibu kuleta tena nyuso zenu huku wauaji na wabakaji wa demokrasia wakubwa nyie?
Down with CCM.
 
Kwa mawazo yako unataka kutuambia kuwa hao watu 60,000 wangejitokeza kupiga kura sisiem ndo wangeshinda? Kwa taarifa yako ingekula kwao fulmazinonda. Sisiem si kitu kwa CDM Arusha. Ila mfa maji haachi kutapatapa.
 
Wana jf hebu tuone aibu kidogo na tuwaulize hawa wenzetu hiyo people's power yao iko wapi ikiwa hata kutoka tu ndani kwenda kituoni kupiga kura wameogopa kati ya wapiga kura 60,000 wanajitokeza 6,000 tu si kituko hiki sasa hao sisiem zaidi ya 20,000 wangejitokeza si ingekuwa gharika. Haya mambo ya people's power za kishabiki hazitapeleka cdm ikulu kama
wanavyojinasibu hebu tuwape ushauri

Ngoja nijaribu kusaidia kukuelewesha. Naishi Arusha. Wananchi wametishwa sana kuhusu huu uchaguzi, na waliokuwa wanatisha watu ni polisi na uongozi wa serikali wa mkoa na wilaya. Jumamosi jioni kuna watu wamepita nyumba kwa nyumba kuwakumbusha kuhusu bomu la Soweto. Watu wametangaziwa wakae majumbani kwa kuwa kuna tishio la mabomu. Wakati huohuo CCM walikuwa wanatuma ujumbe wa simu kukumbusha watu kwenda kuwapigia kura (mimi pia nilitumiwa sms na balozi wa mtaa wetu ambaye nina uhakika hauelewi mrengo wangu maana huwa sijadili hizi siasa mtaani kwangu). Jana jumapili mitaani kulikuwa na polisi tele, wamevaa kivita (bullet proof) na silaha nzitonzito, na katika vituo vya kura walizungushia utepe na kuuzingira. Nimeshuhudia watu wakikamatwa na kusweka kwenye magari yanayodaiwa ni ya polisi (hayakuwa na namba za polisi, lakini tunafahamu silaha zile hakuna raia anazo). Hii yote ilikuwa kutishia CHADEMA wasiende kupiga kura. Na kweli wengi hawakwenda. Hao wachache ambao ilidhaniwa kuwa ni CCM, walipoingia chumba cha kura wakachagua kilicho moyoni: CHADEMA. Ndipo watu wa Arusha walipofikishwa.
 
Sijui ni kwa nini ama ni nini kipo.

Lakini elimu juu ya uhuru na haki ya kura miongoni mwetu ni tatizo. Tutizame uchaguzi mkuu ulipita mwaka 2010 wapliopiga kura walikuwa ni watu wachache sana ikilinganishwa na waliojiandikisha.

kwenye chagauzi ndogo hali inajirudia licha y kuwa na mahudhurio mazuri kwenye kampeni na usajili wa wapiga kura. Binafsi mimi ni miongni mwa watu ambao hawaendagi kupiga kura kabisa licha ya kwamba najua umuhimu na faida yake. swali amballo huwa sina jibu lake ni hivi ni kwann sipendi ama siendi kupiga kura?? na pia uwa najiulaiza kuna watu wangapi wenye tabia kama hii??

maswala mengiine nafikiri siyo ya vyama vya siasa ila ni ya mtu binafsi tu kwamba anapenda ama hapendi na ni uhuru wa mtu kupiga ama kutokupiga kura

Kama unajua umuhimu wa kupiga kura halafu huendi kupiga kura, je wasiojua umuhimu wa kupiga kura na wakauza shahada zao wanafanya makosa? Na je, usipopiga kura (hali ukijua umuhimu wake) na ikatokea waliochaguliwa huwapendi/huwataki utakuwa na haki ya kulalamika?
 
Kilio cha samaki machozi kwenda na maji, mbona hao wanaoimba KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI hawakujitokeza kukidumisha chama chane? Nenda ukamhoji nchimbi akueleze ni kwanini aliamuru kutawanywa mtaani askari wengi kiasi kile ili kuwatisha wananchi?
 
Last edited by a moderator:
Ngoja nijaribu kusaidia kukuelewesha. Naishi Arusha. Wananchi wametishwa sana kuhusu huu uchaguzi, na waliokuwa wanatisha watu ni polisi na uongozi wa serikali wa mkoa na wilaya. Jumamosi jioni kuna watu wamepita nyumba kwa nyumba kuwakumbusha kuhusu bomu la Soweto. Watu wametangaziwa wakae majumbani kwa kuwa kuna tishio la mabomu. Wakati huohuo CCM walikuwa wanatuma ujumbe wa simu kukumbusha watu kwenda kuwapigia kura (mimi pia nilitumiwa sms na balozi wa mtaa wetu ambaye nina uhakika hauelewi mrengo wangu maana huwa sijadili hizi siasa mtaani kwangu). Jana jumapili mitaani kulikuwa na polisi tele, wamevaa kivita (bullet proof) na silaha nzitonzito, na katika vituo vya kura walizungushia utepe na kuuzingira. Nimeshuhudia watu wakikamatwa na kusweka kwenye magari yanayodaiwa ni ya polisi (hayakuwa na namba za polisi, lakini tunafahamu silaha zile hakuna raia anazo). Hii yote ilikuwa kutishia CHADEMA wasiende kupiga kura. Na kweli wengi hawakwenda. Hao wachache ambao ilidhaniwa kuwa ni CCM, walipoingia chumba cha kura wakachagua kilicho moyoni: CHADEMA. Ndipo watu wa Arusha walipofikishwa.
Ndio sasa nasema msitumie kauli mbiu ya people's power kirejareja kwa maana hamuiwezi kinadharia people's power ni kama ile pale Tahrir square Misri na ni kwamba ije mvua, yaje mabomu, zije risasi watu wanatoka tuuu na wala hawastuki mshipa wa fahamu; mpoooo? people'sssssssssss
 
Kama unajua umuhimu wa kupiga kura halafu huendi kupiga kura, je wasiojua umuhimu wa kupiga kura na wakauza shahada zao wanafanya makosa? Na je, usipopiga kura (hali ukijua umuhimu wake) na ikatokea waliochaguliwa huwapendi/huwataki utakuwa na haki ya kulalamika?

na siyo kwamba hayoa yote siyajui.
myself sitegemei mwanasiasa aniletee mabadiliko kamwe........... manake nimekuwa nikakuta hakuna walichokifanya na wala hakuna kinachofanywa nao zaid ya kula na kujineemesha wao.
sasa kuliko nimpe mtu kura ya kwenda kuninyonya heri nisimpe kabisa nijue ananinyonya kwasababu karuhusiwa na wengine ile sio mimi niliyemruhusu.
 
Wana jf hebu tuone aibu kidogo na tuwaulize hawa wenzetu hiyo people's power yao iko wapi ikiwa hata kutoka tu ndani kwenda kituoni kupiga kura wameogopa kati ya wapiga kura 60,000 wanajitokeza 6,000 tu si kituko hiki sasa hao sisiem zaidi ya 20,000 wangejitokeza si ingekuwa gharika. Haya mambo ya people's power za kishabiki hazitapeleka cdm ikulu kama
wanavyojinasibu hebu tuwape ushauri

Mungu ana taabu sana na nyie viumbe wake, alikuumba na ufahamu kamili lakini kwa sababu unazozijua wewe umeamua kujitoa ufahamu. Kazi ipo...!
 
na siyo kwamba hayoa yote siyajui.
myself sitegemei mwanasiasa aniletee mabadiliko kamwe........... manake nimekuwa nikakuta hakuna walichokifanya na wala hakuna kinachofanywa nao zaid ya kula na kujineemesha wao.
sasa kuliko nimpe mtu kura ya kwenda kuninyonya heri nisimpe kabisa nijue ananinyonya kwasababu karuhusiwa na wengine ile sio mimi niliyemruhusu.

Mwanzoni nami nilikuwa nafikiria kama wewe. Baadaye nikagundua kwamba wanasiasa wanapenda watu wanaozira mambo ya siasa (ndiyo maana wakaleta slogan kama siasa ni mchezo mchafu n.k) ili watu weledi wasitamani kuingia huko. Ndiyo maana mwanafalsafa mmoja wa Urusi akasema 'politics is too important to be left to politicians'.

Lakini ukweli unabaki kwamba politics rules the world, and if you dont want to play politics then cast only the vote otherwise some funny people will continue deciding your fate.

Go voting now, not only to your own good, but to the better life of many others.
 
Mungu ana taabu sana na nyie viumbe wake, alikuumba na ufahamu kamili lakini kwa sababu unazozijua wewe umeamua kujitoa ufahamu. Kazi ipo...!

Haya ni maneno ya kwenye khanga sio jibu la hoja sasa sijajua kama ufahamu hapo upo au ndio walewale
 
kwa hiyo unataka kusemaje???
kwamba ccm ndio imeshinda arusha?
hongereni ccm kwa ushindi mnono!
Duniani kuna watu wa ajabu sana!

Kweli mkuu CCM kazi yao ni kusema "this is white" while kila mtu anaona ni nyeusi.
 
Kwa ufahamu wako mdogo tukufahamishe wenye akili walishahama ccm zile kura ulizoziona za ccm ndio wanachama waliobaki.
 
Back
Top Bottom