Simiyu Yetu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2013
- 18,949
- 4,645
chadema wanambagua zito au zito anabaguliwa na chadema
nani mchaga kati ya chadema na zito ukipata jibu hilo utajua nani anabaguliwa.
chadema wanambagua zito au zito anabaguliwa na chadema
Ni propaganda tu, na mnalipwa kwa kazi hiyo. Mimi niko Kigoma, nakaa Mwanga mtaa wa Shaurimoyo.unapaswa kusaidiwa na hiyo akili yako kwani hii post unayochangia inakwambia nini.
Chadema sio mchaga na Zitto sio mchaga. Ni majungu tu.nani mchaga kati ya chadema na zito ukipata jibu hilo utajua nani anabaguliwa.
Hujajibu swali langu narudia:
Hivi Zitto ana tofauti gani na Slaa kiitikadi? Je wanampinga Slaa kwa itikadi gani na wanamuunga mkono Zitto kwa itikadi gani tofauti?
Natumaini unaelewa maana ya itikadi.
Hayo ni ya uongo na zitto mwenyewe alishayakanusha hata humu JF. Tamko la Zitto hili hapa:Wenye itikadi kamwe mmoja hawezi kuajiri kikundi cha watu kumdhuru mwingine. Kumshushia credibility, uaminifu wake kwa mambo ya kutunga. Slaa itikadi yake sio iliyokatika makaratasi ya chadema ambayo zito ndio anasimamia itikadi hiyo. Zitto amekuwa mtu wa busara na asiemnafiki. Umesahau kuwa slaa amemuunga mkono kagame dhidi ya nchi?
Umesahau jinsi anavyopinga kila jambo linaloanzishwa au kufanywa na ccm hata ikitokea nila muhimu kiasi gani kwa taifa?
Si kweli kuwa anapinga kila kitu. Slaa anapiga vita rushwa, na ufisadi, na hili ni jambo la kitaifa. Slaa anapigania matumizi mazuri ya rasilimali zetu.Katika gazeti la Mtanzania toleo na. 7269 la Jumatano Machi 27, 2013 kuna habari yenye kichwa chenye maneno ‘SIRI YA KUUWAWA ZITTO YAFICHUKA' na vichwa vidogo ‘yadaiwa ilipangwa anyweshwe sumu hotelini' dk. Slaa atajwa kumtuma Saanane kummaliza'. Habari hii imeniletea usumbufu mkubwa kwani ndugu, jamaa, marafiki na wapiga kura wangu, wamejazwa na wasiwasi mkubwa sana kwamba ninaweza kuuwawa.
Napenda kusema yafuatayo:
Moja, sijawahi katika maisha yangu yote kukutana na mtu anayeitwa Ben Saanane na hivyo hicho kikao ambacho inasemekana nilikuwa naye na akajaribu kunipa sumu hakijawahi kutokea. Imetajwa Hoteli ya Lunch Time ambayo sio tu sijawahi kufika, pia hata siijui ipo wapi. Haijawahi kutokea mimi kufanya kikao cha pamoja na Ben Saanane, Juliana Shonza na Mtela Mwampamba. Hivyo habari iliyoandikwa ni ya kufikirika na hivyo naomba mwandishi ahakikishe kuwa vyanzo vyake vya habari vimempa habari sahihi.
Pili, Siamini kamwe kuwa Katibu Mkuu wa chama changu anaweza kupanga kuniua maana hana sababu ya kufanya hivyo. Napenda kurudia kusema kwamba mimi ninaamini kuwa kila nafsi itaonja mauti. Kila mtu atakufa. Kama nitakufa kwa kuuwawa na mtu mwingine ndio itakuwa nimeandikiwa hivyo na Mungu. Ndio maana hata siku moja silalamiki kuhusu vitisho vya kuuwawa nk. Kama kuna mtu anafikiria kuwa kumuua Zitto ndio furaha ya maisha yake atakuwa anajidanganya tu maana Zitto anaweza kufa kimwili lakini mawazo, fikra na maono ya Zitto yataishi tu. Siogopi kufa maana maisha niliyoyachagua ndio haya ambayo yamejaa vitisho. Muhimu kwangu ni kufanya kazi zangu kwa bidii, uhodari na uaminifu. Siku zote nitasimamia ukweli bila kujali uchungu wa ukweli huo.
Tatu, nawashauri watu ambao wamehama CHADEMA na kuhamia vyama vingine watumie muda wao kujenga vyama vyao badala ya kila siku kuzungumzia masuala ya chama ambacho wao sio wanachama tena. Kama mtu kaamua kuhama CHADEMA anapoteza haki ya kujadili masuala ya CHADEMA maana kama angekuwa anapenda kuyajadili asingehama. Naonya mtu yeyote ambaye anatumia jina langu ili kufanikisha malengo yake ya kisiasa. CHADEMA sio pango la watesaji wala wauaji. Kama kuna mwanachama wa chama kingine cha siasa anayedhani kuna mtu ndani ya CHADEMA anapanga mipango ovu aende kwenye vyombo vya sheria kumshtaki. Matendo ya mtu mmoja yasifanyiwe propaganda kama ni malengo ya taasisi.
Nne, Nawashauri viongozi wenzangu wa CHADEMA na hasa wanachama tutumie muda wetu kujenga mshikamano ndani ya chama. Fitna, majungu, uongo, uzandiki nk kamwe havijengi chama. Chama chetu lazima kiwe mfano bora wa kuheshimu demokrasia na haki za binaadamu. Wananchi hawawezi kutoa dola kwa chama chenye mifarakano. Tusiruhusu kugawanywa kwa matakwa ya watu wachache. Tusimamie misingi ya kuanzishwa chama chetu.
=============Thread inayoongelea kilichoandikwa na Mtanzania hii hapa - https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...ajwa-kumtuma-ben-saanane-kummaliza-zitto.html
:A S 2152::A S 2152:Tehe tehe tehe....! wakati chadema wanatumia nguvu nyingi kuitafuta nafasi ya kuingia Ikulu basi CCM wanacheza na Pychology na kutumia akili kuwa maliza
Source please!
Habari yako tutaendelea kuichukua kama ulivyoeleza kwenye red hapo juu.Kutokana na mvutano unaoendelea ndani ya Chama cha demokrasia na maendeleo na Chadema imesababisha Chama hicho kusambaratika na kupoteza mvuto mkoani kigoma, sababu hasa inaonekana ni kutengwa kwa kijana wao zitto kabwe ndani ya chama hicho, na hata tetesi zinazoongelewa katika vijiwe vya siasa mkoani kigoma, aliye kuwa mgombea wa chama cha chadema Mwaka 2010 Ally mlee akakihama Chama muda wowote kuanzia sasa. Hali ni mbaya mkoani hapa, kila kijiwe kinaongelea ubaguzi ndani ya chama hicho.
Sasa kama mpendwa wako ZITTO ameshindwa kuijenga CHADEMA mkoani kwake tu vipi angekabidhiwa CHADEMA TAIFA? Alipotaka kugombea uenyekiti taifa ilikuwa ni mpango wa kuisambaratisha CHADEMA bahati mbaya kwake na wapambe wake wakashitukiwa mapema!! CHADEMA mkoani Kigoma inasambaratishwa na ZITTO mwenyewe kwa sababu ya UJUAJI NA TAMAA ZAKE!! The guy has got self interests na hakuna aliyemtenga bali amejitenga yeye mwenyewe!! Pamoja na elimu yake lakini anasumbuliwa na USWAHILI!!!
Ni kipi alichofanya kuindeleza CHADEMA mkoani Kigoma na mikoa jirani? Tueleze mafanikio yake kisiasa mkoani humo: Je tangu awe mbunge na hizo sifa mnazompa amefanikiwa kuongeza madiwani na wabunge wangapi? Kama wewe siyo MGANGA NJAA natumaini utakuja na majibu ya maswali yangu!!
Kigoma ninayoijua mimi, ni Kigoma ambayo CCM ndicho chama kisichopendwa.vijiwe mbali mbali vya kigoma .
Ukweli kuondoka baadhi ya wanachama kwa sababu binafsi kama hizo ni afya kwa chama!! UBAGUZI UBAGUZI UBAGUZI ukweli wote wenye matakwa binafsi wanatakiwa waondoke!! ni hasara si faida! wale wote wanaozikubali sera na ujinga wa CCM waondoke wakaangalie kwa nje! labda wataona tofauti!!Kutokana na mvutano unaoendelea ndani ya Chama cha demokrasia na maendeleo na Chadema imesababisha Chama hicho kusambaratika na kupoteza mvuto mkoani kigoma, sababu hasa inaonekana ni kutengwa kwa kijana wao zitto kabwe ndani ya chama hicho, na hata tetesi zinazoongelewa katika vijiwe vya siasa mkoani kigoma, aliye kuwa mgombea wa chama cha chadema Mwaka 2010 Ally mlee akakihama Chama muda wowote kuanzia sasa. Hali ni mbaya mkoani hapa, kila kijiwe kinaongelea ubaguzi ndani ya chama hicho.
Ni propaganda tu, na mnalipwa kwa kazi hiyo. Mimi niko Kigoma, nakaa Mwanga mtaa wa Shaurimoyo.
Mimi akili yangu ni nzuri sana, hainunuliwi kwa propaganda nyepesi kama hizi.
Nathibitisha kuwa hayo yanayosemwa ni uongo mtupu! Anahitaji alete ushahidi hapa nami ntaleta ushahidi dhidi ya ushahidi wake.
Kutokana na mvutano unaoendelea ndani ya Chama cha demokrasia na maendeleo na Chadema imesababisha Chama hicho kusambaratika na kupoteza mvuto mkoani kigoma, sababu hasa inaonekana ni kutengwa kwa kijana wao zitto kabwe ndani ya chama hicho, na hata tetesi zinazoongelewa katika vijiwe vya siasa mkoani kigoma, aliye kuwa mgombea wa chama cha chadema Mwaka 2010 Ally mlee akakihama Chama muda wowote kuanzia sasa. Hali ni mbaya mkoani hapa, kila kijiwe kinaongelea ubaguzi ndani ya chama hicho.