CHADEMA yaizika CCM Ukonga

CHADEMA yaizika CCM Ukonga

Ninafarijika mongola ndege wamedelete CCM. ..
 
Operesheni ya Chadema ni Msingi na vuguvugu la Movement for Change jimboni Ukonga imeonekana kukisimika vyema chama hicho jimboni humo.

Wanachama wa Chadema jimboni Ukonga hawasiti kuupongeza uongozi wa jimbo hilo chini ya Mwenyekiti Thomas Nyahende maarufu kama Mwita Maranya kwa kazi kubwa waliyofanya tangu waingie madarakani.

Jimbo la Ukonga lenye ubovu mkubwa wa barabara limekuwa ngome kuu ya CCM kwa miaka mingi.

Hata hivyo katika uchaguzi uliofanyika wa Serikali za Mitaa wiki iliyopita Chadema wamejipatia ushindi mkubwa katika mitaa 10 huku washirika wao CUF chini ya mwavuli wa Ukawa wakijipatia mitaa 2.

Kikubwa zaidi ni kwa chama hicho kuweza kujipatia mitaa miwili muhimu.Mitaa hiyo ni ule anaokaa Meya wa Ilala Jerry Silaa wa Guluka Kwalala Gongolamboto na Mtaa wa Kivule unaoaminika kuwa na wakazi wengi zaidi kuliko mtaa wowote DSM.Kwa mfano katika mtaa huo wa Kivule mshindi alikuwa ni Afisa wa Chadema makao makuu Kamanda Mwita Mwikabe Waitara aliyepata ushindi wa kimbunga wa kura 1262 huku CCM wakiambulia kura 663

Kabla ya uchaguzi huu upinzani kwa ujumla walikuwa wanaongoza mitaa 2 tu kwa jimbo zima.

Jumapili wiki hii kutakuwa na marudio ya uchaguzi kwa mitaa 23 ambayo haikufanya uchaguzi wiki iliyopita.

Katika mahojiano na wanachama na baadhi ya viongozi wa misingi wamepongeza uongozi bora wa Mwita Maranya unaoshirikisha viongozi wote wa ngazi za chini na uwajibikaji uliotukuka.

Pia wanachama wameutaka uongozi wa Jimbo kutokubweteka kwa matokeo haya mazuri bali waendelee kukijenga chama bila kuchoka ili mwakani waweze kupata mbunge na madiwani wengi kwa lengo la kuongoza Manispaa ili walau wasimamie fedha za wananchi na hatimaye barabara za Ukonga zijengwe.

Hawa madiwani waliopoteza hii mitaa yote wawajibishwe. ccm ilitangaza kuwa itawafukuza kwenye nafasiz zao za udiwani. hatuwezi kuendelea kuona watu wanaharibu halafu hawawajibishwi.

Hatua za kuwafukuza zianze kutekelezwa. ccm haiwezi kuvumilia kushindwa kizembe namna hii.

Tehe tehe inhi inhi ccm ishakufa.
 
Mkuu kama atagombea Ukonga itakuwa njema maana ataepusha mgongano na Heche kule Tatime! Huo mkakati nimeupenda nchi lazima tuigawane! Kama Kishapu nako hatuna mgombea ni bora Mpendazoe akarudi ili Segerea tuliachie jembe jingine la UKAWA!

Kamanda umenikumbusha mbali sana...Kishapu!!
 
Kamanda tpaul kuhusu hilo atalisemea mwenyewe.Kama ana nia na jimbo la Tarime naamini wakati ukifika atafuata taratibu za kawaida za chama kuomba nafasi ya kuwakilisha chama.

Tarime huko pia kwenye uchaguzi huu CCM imefutwa rasmi.

tuko pamoja mkuu Molemo.
 
Last edited by a moderator:
Bila kusahau wale wanaopisha mradi wa gesi mwaka wa tatu huu awajui malipo yao yatakuwaje. Wengine wasitisha ujenzi wa nyumba ili hali bado azijakamilika wakihofia kupat hasara! Makamanda wa ukonga walifatilie hili linaweza likawa janga lengine laupigaji hela...

Mikidadi Chisala

Umepigilia msumari wa moto.Wananchi wamesitishiwa ujenzi na biashara zao kwa zaidi ya miaka mitatu sasa kwa madai watalipwa wahamie maeneo mengine.

Hakuna chochote kilichofanyika na wananchi wakiwaulize mbunge na madiwani wa CCM wanajibiwa kwa kejeli kubwa.

Wananchi wa maeneo hayo wamekata tamaa.Na wanaamini salama yao ni kumchagua mbunge wa Chadema na madiwani wa Chadema ili kupigania maslahi yao!

Baada ya ushindi huu inabidi viongozi wa Chadema wa Ukonga wakutane na wananchi ili kuangalia namna bora ya kupigania haki yao!

CC Mwita Maranya
 
Last edited by a moderator:
Ninafarijika mongola ndege wamedelete CCM. ..

Ni mwendawazimu pekee anayeweza kupigia kura CCM huku akitumia shilingi 5,000 kufika Banana kutokana na Ubovu wa Barabara!
 
Mkuu Mwita Maranya kumbe ukiona kobe ameinama ujue anatunga sheria; umekaa kimya sana kumbe unajiandalia ushindi. Hongera kwa kupata ushindi huko kivule. Sasa yule ndugu yako Diwani wa Kivule una mpango gani naye, unataka kumuondoa?
 
Last edited by a moderator:
kama anakubalika ukonga si amwachie HECHE tarime na yeye awakongori magamba hapo dar?
Molemo?

Marire

Haya mambo yanazungumzika usihofu.Bahati njema Chadema ina hazina ya viongozi wenye hekima kubwa hususan majemadari wakuu Freeman Mbowe na Dr Wilbroad Slaa.
 
Last edited by a moderator:
Kamanda Mwita Maranya hongera sana kwa ushindi wa Sunami jipange baba 2015 siyo uchukue jimbo.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mwita Maranya kumbe ukiona kobe ameinama ujue anatunga sheria; umekaa kimya sana kumbe unajiandalia ushindi. Hongera kwa kupata ushindi huko kivule. Sasa yule ndugu yako Diwani wa Kivule una mpango gani naye, unataka kumuondoa?

Mkuu Kimbunga upo?

Nilikusoma mahali ukikiomba CCM kimpitishe John Magufuli kugombea Urais vinginevyo Ukawa watachukua nchi!

Nilicheka sana!!
 
Last edited by a moderator:
Popote ulipo Habinder Singh Seth hakikisha unakwamisha maazimio ya Bunge letu TUKUFU ili mziki huu uwe mnene mwaka mzima mpaka uchaguzi MKUU utasaidia sana na watanzania wengi watakuwa wameamka juu ya wizi wa kutisha uliofanywa.JK na wewe kaa kimya ili watu wawe na akili maana uvivu wa kufikiri kwa watanzania ni mkubwa ili wajue kama wameibiwa wanatakiwa hata wakienda hospitali Wafie milangoni maana Dawa hakuna,UMEME upande ikiwezekana watu walipe laki mbili na nusu kwa mwez.maana hili TAIFA ni la Vilaza.kikwete oyeeeeeeee,Harbinder Singh Seth oyeeeeeeeee,maisha magumu kwa kila MTANZANIA safiiiiiiiiiiiiiii.
 
Mbona huyu mama afisa uhusiano wa manispaa ya ilala ameitaja kivule kuwa uchaguzi unarudiwa?
Bora ya wewe umegundua hizi habari za Mleta mada ni kujipiga Chapuo na maPro mengi tu ya CHADEMA
Hivi wameshinda mitaa mingapi mpaka waitane majina ya Kikamanda?
kumbe uchaguzi unarudiwa
kumbe wameshinda mitaa miwili tu?
kweli mahali akikutana Mchagga na Mkurya ni vigumu kutawalika
yetu macho
 
Mkuu Kimbunga upo?

Nilikusoma mahali ukikiomba CCM kimpitishe John Magufuli kugombea Urais vinginevyo Ukawa watachukua nchi!

Nilicheka sana!!

Nipo Imara kama chuma cha pua. Naona tu harakati zenu za kutaka kunyakua dola. Mmeacha uanaharakati sasa mnaingia kwenye siasa za ushindani. Sasa naona siasa zinanoga manake utamu wa siasa ufike mashinani hapo ndipo utaona kwamba siasa imetapaa nchi nzima. Siyo siasa za Arusha tu na Tarime, zifike Kyamyorwa, Umugakorongo, Nyabihanga, Matiri, Lityumbandosi, Mikunya, Lilondo, inyonga, nk.

Mzee siasa za nchi hii nazifamu ndio maana nikasema vile manake ukawa naona mmeingia chini kabisa kwa wakulima, wakwezi na wafugaji. Ili kuleta ushindani inabidi CCM watafute kifaa vinginevyo mnaweza kupita na moto wa tipa.

Mbona kamanda Mwita Maranya yupo kimya sana?


 
Last edited by a moderator:
Popote ulipo Habinder Singh Seth hakikisha unakwamisha maazimio ya Bunge letu TUKUFU ili mziki huu uwe mnene mwaka mzima mpaka uchaguzi MKUU utasaidia sana na watanzania wengi watakuwa wameamka juu ya wizi wa kutisha uliofanywa.JK na wewe kaa kimya ili watu wawe na akili maana uvivu wa kufikiri kwa watanzania ni mkubwa ili wajue kama wameibiwa wanatakiwa hata wakienda hospitali Wafie milangoni maana Dawa hakuna,UMEME upande ikiwezekana watu walipe laki mbili na nusu kwa mwez.maana hili TAIFA ni la Vilaza.kikwete oyeeeeeeee,Harbinder Singh Seth oyeeeeeeeee,maisha magumu kwa kila MTANZANIA safiiiiiiiiiiiiiii.
Mawazo ya kitoto kabisa hayo
  • Huu umeme unaoutumia unaulipia? km ni kweli sasa Habinder na wenzake wasichukue chao
  • hizi 100megawatt zinazozalishwa na IPTL Tegeta zinapoingia Grid ya Taifa hazina umuhimu? kwanini basi walioleta mitambo na kuisimika wasilipwe
  • Mitambo kila siku inahitaji spea vialainishi na check-up ili mpate umeme soda na viberiti vitengenezwe
kuushabikia UJINGA ili tu mbebe kura ni kazi, sana hasa kwa binadamu mwerevu
HILI NI JANGA LA KITAIFA kuwa na watu km hawa
 
Back
Top Bottom