EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,483
- 15,308
Chadema imeipa polisi saa 24 kuwakamata watuhumiwa wote wanaotuhumiwa kuwashambulia viongozi wa Chadema kwenye kampeni za uchaguzi Arumeru Mashariki. Katibu wa chama hicho Dr. Slaa amesema kwa kushindwa kuwakamata watuhumiwa, yeye binafisi ataongoza maandamano yatakayowajumuisha maelfu ya wakazi wa Arumeru kwenda Ikulu kushinikiza kujiuzulu kwa maafisa wa ngazi za juu wa polisi.
Dr Slaa amedai kuwa viongozi wa Chadema wamekuwa wakishambuliwa na watu fulani kutoka CCM kwa muda wa siku tatu sasa, lakini pamoja na kuwaripoti watu hao polisi, hakuna hatua zozote ambazo zimechukuliwa. Alisema badala yake viongozi wa CCM ndio wanaodai kwenye vyombo vya habari kushambuliwa na Chadema huku wakitoa statements zao chini ya escort ya polisi.
Akiongea na wananchi wa sehemu ya Mgungani iliyoko kata ya Mbuguni, Dr Slaa amesema, maandamano hayo ambayo hayajawahi kufanyika Tanzania, yatawahusisha wananchi wa Meru na Arusha kwa kuandamana mpaka Ikulu, Dar Es Salaam. Wananchi waliokuwa kwenye mkutano walimjibu Dr Slaa kuwa wako tayari kuandamna hadi Ikulu baada tuu ya kumalizika kwa mkutano.
Dr. Slaa aliongeza kuwa wakati wakiandamana kutokea Meru watawasiliana na Watanzania wengine kutoka kona mbalimbali za nchi ili nao waandamane na kukutana jijini Dar Es Salaam.
Nikiripoti kutoka eneo hili la Migungani lililopo kwenye kata ya Mbuguni ni mimi EMT wa JF.
Dr Slaa amedai kuwa viongozi wa Chadema wamekuwa wakishambuliwa na watu fulani kutoka CCM kwa muda wa siku tatu sasa, lakini pamoja na kuwaripoti watu hao polisi, hakuna hatua zozote ambazo zimechukuliwa. Alisema badala yake viongozi wa CCM ndio wanaodai kwenye vyombo vya habari kushambuliwa na Chadema huku wakitoa statements zao chini ya escort ya polisi.
Akiongea na wananchi wa sehemu ya Mgungani iliyoko kata ya Mbuguni, Dr Slaa amesema, maandamano hayo ambayo hayajawahi kufanyika Tanzania, yatawahusisha wananchi wa Meru na Arusha kwa kuandamana mpaka Ikulu, Dar Es Salaam. Wananchi waliokuwa kwenye mkutano walimjibu Dr Slaa kuwa wako tayari kuandamna hadi Ikulu baada tuu ya kumalizika kwa mkutano.
Dr. Slaa aliongeza kuwa wakati wakiandamana kutokea Meru watawasiliana na Watanzania wengine kutoka kona mbalimbali za nchi ili nao waandamane na kukutana jijini Dar Es Salaam.
Nikiripoti kutoka eneo hili la Migungani lililopo kwenye kata ya Mbuguni ni mimi EMT wa JF.