CHADEMA yaijibu JWTZ

CHADEMA yaijibu JWTZ

Unakubaliana nasi kuwa shimbo alifanya siasa.
kwa kuwa tamko lilihusu uchaguzi na vyama vya siasa, mtoa tamko sahihi angekuwa kama si msajili wa vyama vya siasa basi angekuwa mwenyekiti wa tume ya uchaguzi.
Ikiwa kwa kitisho cha mpaka na malawi mkuu wa majeshi yetu hatakiwi kusema kitu sembuse kwa kazi isiyomuhusu kabisa!!!
Hawa wajeshi wajiongeze kidogo, wanaposema wanakitii chama kinachounda serikali wamepaswa kujua kuwa utii wao kwa kipande hiki si utii wa kijeshi, kwani waamrishaji si wanajeshi, ama la sivyo hawa wastaafu wa jeshi wanasomeka kuwa ni wanajeshi.

I think its a blasphemy kusema jeshi is loyal au linatii chama kinacho ongoza serikali. I dont know about the laws za jeshi ila i think he should have said ´Jeshi linatii na kuheshimu kanuni na sheria za jamuhuri ya muungano bila kujali chama au mtu au taasisi´. Hawa viongozi wetu bana, they need more pressure ili wawezekujitambua.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Ndomba alipokuwa Mkuu wa Mkoa alikuwa amestaafu sio? Na Mkuu wa Mkoa ni mjumbe wa kamati ya mkoa ya CCM! Sasa hivi Ndomba ni nani jeshini!? Ndio maana Mboma na Mahita walipostaafu uCDF na uIGP wakaenda kugombea ubunge kupitia CCM, na Tubaigana pia!

CCM ielewe kuwa haifanyi haya kwakujifaidisha bali kujitengenezea kitanzi...Serikali yake imeshindwa kabisa kutenganisha siasa, professionalism na mambo ya ulinzi na usalama wa nchi na raia; matokeo katika kila kitu CCM ndiyo inayoshika hatamu bila kujua hiyo tu pekee ndicho kinachopelekea kila mtu anayetaka kuwa independent na siasa kuichukia CCM kupita maelezo.
 
I think its a blasphemy kusema jeshi is loyal au linatii chama kinacho ongoza serikali. I dont know about the laws za jeshi ila i think he should have said ´Jeshi linatii na kuheshimu kanuni na sheria za jamuhuri ya muungano bila kujali chama au mtu au taasisi´. Hawa viongozi wetu bana, they need more pressure ili wawezekujitambua.

Wote hao ni masalia ya kada wa chama na I guess wote walishapitia kivukoni enzi zao...Sasa baada ya kuondoa kushika hatamu ya chama kwenye karatasi bila kubadilisha mfumo na attitude ndiyo mambo yakaendelea ki hivyo mpaka leo unashangaa kusikia a senior person ndani ya jeshi eti anatoa tamko kama hilo bila woga wala aibu bila kujua madhara yake mbele ya safari katika umoja na mshikamano wa kitaifa ambao ndiyo una determine amani.
 
Ipo siku nchi itakuja kupinduliwa,kama mmomonyoko wa maadili utaendelea kukuwa kwa kiasi hiki!
hadi hapa maadili hakuna hata kidogo, yaliyopo mengine ni uovu uliohalalishwa.Ni rehema za Mungu tuu zinzoshikiliwa na wachache walio ktk wema na wasio hat ajua nini kinaendelea.
 
huyu mnyika angekaa kimya tuu , jeshi na siasa ni vitu viwili tofauti , Amiri jeshi mkuu ni rais wa jamhuri ya muungano kwa hiyo ni sahii kwa msemaji wa jeshi kusema kwamba wanafuata serikali iliyo madarakani ,in this case ya ccm , wizara zote ,vyombo vyote vya usalama kuanzia polisi mpaka TISS ni lazima viheshimu sera za serikali iliyopo madarakani , kama wewe ni mwanajeshi ,polisi, usalama wa taifa unapenda sana sera za chadema au chama cha upinzani hutakiwi kujiingiza kwenye siasa labda utoke kwenye hiyo kazi . Dr slaa angekuwa rais si inamaa angekuwa amiri mkuu wa majeshi na vyombo vyote vya usalama vingefuata sera za chadema ...nini tatizo kufuata sera za ccm si ndo demokrasia ya vyama vingi ambayo tunaitaka
 
NI Kweli kuwa jeshi haliji halijihusishi na siasa lakini tunaona wengi wakistaafu utumishi hupewa nafasi za mkuu wa mkoa ,mkuu wa wilaya hawa ni wanasiasa kwa upande mwingine ,kwa sababu kama huna hata idea kidogo ya siasa hizi posti wengi wangezikataa na wengi wao hukubali bila shingo upande .

Ni aina nyingine ya rushwa kama ile itolewayo kwa wabunge na ma-academecian kwa kulipwa mishahara minono huku majority of population living with less a dollar per day.


Hiyo ndiyo njia pekee ya viongozi wasio na maono kuoongoza taifa ili kunyamazisha wote wanaoweza kuwa wajibisha katika utendaji wao.

Hii haikubaliki hata kidogo, kama nchi ni masikini basi kila mtu anatakiwa a feel huo umasikini siyo wengine wawe peponi na wengine wawe jehanam katika nchi hiyo hiyo na mwisho wa siku eti tunajidai kinafiki naipenda Tanzania, what a hypochricy!
 
Kwa ujumla taifa letu ccm wanalipeleka pabaya,haiwezekani viongozi wa serikali kupitia ccm wanateua wanajeshi kuwa wakuu wa mikoa ili wakaitumikie ccm, halafu mwanajeshi mmoja anahukumiwa kwa sababu eti kapiga picha na mbunge. Hii haingii akilini. Kweli ccm ni zaidi ya uijuavyo!
 
Dah ! Kama kweli Ndomba alikuwa mkuu wa mkoa na sasa amejaza nafasi ya Shimbo basi usishangae siku moja Kinana akirudi tena Jeshini ! Hawa wakuu wa mikoa na wilaya lazima wakataliwe kabisa kabisa ndani ya katiba mpya .
 
Ninaamini hawatakusikiliza haya mpaka yatakapowatokea kama yale ya Misri walipogoma kusikiliza amri zao. Kiburi na jeuri ya madaraka huwa ni mbaya sana.

Hata kama hawatapenda kuelewa ni kuwa huwezi danganya watu kwa muda wote na hasa kama huo uwongo unahusu maisha ya watu...Ebu niambie package formal na informal za hawa watu wanaojiita ma chief execautive na watumishi wengine wa umma una tofauti gani? Kuanzia majeshi, mashirika ya umma, na serikali zote kuu na za mitaa, njoo kwenye wabunge linganisha na wana siasa wengine, uje kwenye vyama vyenyewe vya siasa jinsi viongozi wa vyama hivyo vipatao vyao vinavyotofautiana na fursa..Je hapo nani akubali wengine wajipangie tu ukubwa wa keki wengine watazame kwa macho tu? How long can you fool people?

Matokeo yake ndiyo haya sasa kila mtu kageuka mwizi tapeli ilimradi tu apate nafasi ya ku-fisadi kwa manufaa binafsi what kind of country are we building? Eti wanajitetea ni ubebari upi huo? Hata ubepari una miiko na msingi mkubwa wa ubepari ni kila mtu analipwa kwa jinsi awezavyo kuzalisha na ku accumulate capital sasa hii yetu ambapo mtu anatafuta sehemu ambapo public good zimekusanywa in terms of chash ndiyo anajigawia in the name of ubepari nani atakubali?

As for me I know I am one among the thieves in my country and I hate it more than any thing na ndiyo maana napiga mayowe kwamba sitaki kuwa favoured at all bali niitumikie nchi yangu ili malipo yangu yawe halali. Lakini unaitumikiaje nchi pasipo viongozi kukubali kuongoza inavyotakiwa? Kila ushauri hauzingatiwi bali siasa tu...Tired of this kwakweli!
 
Hujui unachoakiongea!!!
Jifunze tofauti kati ya mwanajeshi na mwanajeshi mstaafu. Pia jifunze kuongea mambo kwa evidence...
Mkuu soma taarifa iliyotolewa wakati Ndomba anapandishwa cheo cha kijeshi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Meja Jenerali Samuel Albert Ndomba kuwa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Aidha, Rais Kikwete amempandisha cheo Meja Jenerali Ndomba kuwa Luteni Jenerali.

Taarifa iliyotolewa leo, Ijumaa, Septemba 21, 2012, mjini Dar Es Salaam na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Y. Sefue kupitia Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais – Ikulu, imesema kuwa uteuzi huo unaanza leo.

Taarifa hiyo ya Balozi Sefue imesema kuwa kabla ya uteuzi wake, Meja Jenerali Ndomba alikuwa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT).

Jenerali Ndomba anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Luteni Jenerali Abdulrahman A. Shimbo ambaye amestaafu Jeshi kwa mujibu wa sheria baada ya kufikisha umri wa miaka 60.

​Taarifa ya Balozi Sefue pia imesema kuwa Rais Kikwete amemteua Brigedia Jenerali Raphael Mugoya Muhuga kuwa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa kuanzia leo, Ijumaa, Septemba 21, 2012.

Aidha, Rais Kikwete amempandisha cheo Brigedia Jenerali Muhuga kuwa Meja Jenerali.

Kabla ya uteuzi wake, Brigedia Jenerali Muhuga alikuwa Mkuu wa Utawala na Mafunzo wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT).


Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
21 Septemba, 2012

So ametumikia jeshini, akawa Mkuu wa Mkoa na Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM, tukadhani amestaafu jeshi, kisha akapandishwa cheo cha kijeshi na kurudi kwenye kazi za jeshi. Kwa hiyo huyu hakuwa askari mstaafu. Na bado alikuwa kiongozi wa CCM.

Arusha kuna barabara imeitwa kwa jina la Ndomba kukumbuka utumishi wake kama RC.
COL. NDOMBA ROAD
It starts near the railway crossing with Njiro road-through the former Maboxini settlement to breweries road. This is another bypass. The vehicles that are going to Esso/Unga ltd. Industrial area or Daraja Mbili instead of going to the city centre they will use this road. It will also reduce traffic congestion between RTD area and Kijenge round about and clock tower. It is named after the former Regional Commissioner for Arusha Col. Ndomba who convinced Arusha business community to contribute towards opening this important by pass. This by pass is 1.4 km.
Source; Arusha Times.

Hii sio shida, ila askari mdogo kupiga picha na chadema ni suala zito sana.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
busara na hekima zinahitajika sana ktk kuamua hili la mwanajeshi.tuache porojo,ngonjera,kejeli na jeuri za ulevi wa madaraka kumbukeni mnatawala watu wenye akili nyingi pengine kuliko viongozi.acheni siasa jamani hii nchi ni watanzania wote hakuna mwenye hati miliki.
 
Hata kama hawatapenda kuelewa ni kuwa huwezi danganya watu kwa muda wote na hasa kama huo uwongo unahusu maisha ya watu...Ebu niambie package formal na informal za hawa watu wanaojiita ma chief execautive na watumishi wengine wa umma una tofauti gani? Kuanzia majeshi, mashirika ya umma, na serikali zote kuu na za mitaa, njoo kwenye wabunge linganisha na wana siasa wengine, uje kwenye vyama vyenyewe vya siasa jinsi viongozi wa vyama hivyo vipatao vyao vinavyotofautiana na fursa..Je hapo nani akubali wengine wajipangie tu ukubwa wa keki wengine watazame kwa macho tu? How long can you fool people? Matokeo yake ndiyo haya sasa kila mtu kageuka mwizi tapeli ilimradi tu apate nafasi ya ku-fisadi kwa manufaa binafsi what kind of country are we building? Eti wanajitetea ni ubebari upi huo? Hata ubepari una miiko na msingi mkubwa wa ubepari ni kila mtu analipwa kwa jinsi awezavyo kuzalisha na ku accumulate capital sasa hii yetu ambapo mtu anatafuta sehemu ambapo public good zimekusanywa in terms of chash ndiyo anajigawia in the name of ubepari nani atakubali?
tatizo linaweza kuwa kipato kama haifikii kiasi cha kumaliza matatizo ya msingi +angalau kuweka akiba.Pia kuwe na tofauti za kifamilia za kijeshi na za raia wanaofanya kazi nyingine kwani wao wanakuwa exposed ktk mazingira ya hatari na kuwa mbali na familia zao bila mpangilio. Mara nyingi mambo ya msingi yakifikiwa kinachomshikiliwa mfanyakazi sehemu ni level ya satisfaction anayopata ktk hiyo ajira, na wengine ni kufanya kazi aipendayo ya ndoto yake.Wanajeshi wengi tuu wanaona raia wanaishi vizuri kuliko wao na kwa uhuru mkubwa.wengi wan amarafiki uraini kuliko kambini na wapo friendly ila bado hawajapata majibu ya maisha yao kam wanahitaji baki katika jeshi.Ni tafiti za jeshi tuu ndio zitakazowafungua hawa wakubwa-wababe akili na kujua hali halisi.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Watu tuna siasa za makengeza sana humu
Sipati picha kama askari huyo angepiga picha na Mwigulu nchemba au Nape
 
Mkuu soma wasifu wa Ndomba wakati anapandishwa cheo cha kijeshi.
So ametumikia jeshini, akawa Mkuu wa Mkoa na Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM, tukadhani amestaafu jeshi, kisha akapandishwa cheo cha kijeshi na kurudi kwenye kazi za jeshi. Kwa hiyo huyu hakuwa askari mstaafu. Na bado alikuwa kiongozi wa CCM.

Arusha kuna barabara imeitwa kwa jina la Ndomba kukumbuka utumishi wake kama RC.

Hii sio shida, ila askari mdogo kupiga picha na chadema ni suala zito sana.

Bora muwaonyeshe hao wanafiki chief executives ambao wamepewa rushwa ya vipato vikubwa ili kutumikia wanasiasa badala ya nchi na raia wake....Unafiki huu hautufikishi popote maana nikujidanganya wenyewe. kama ni amani itatoweka none will be safe, kama ni kutokuendela basi sote tutaishi chini ya relative poverty no matter how much you will be paid. Ndiyo maana ushirikina na uchawi hauishi miongoni mwetu maana wenye ku-envy wengine katika maisha ni chungu mzima. Wewe una kula na kusaza lakini inside your ukoo watu wote hata viatu kuvaa shida..What a stupid mentality!
 
Mda utafika changes itatokea, askari wa chini ndio wapiganaji na ndio wenye hali ngumu.
 
Watu wengi walishahoji hili la Ndomba huko nyuma bila kupata majibu ya kuridhisha.
kuhusu ndomba kwa kweli sijaelewa maana mara anakuwa DC (Ngara) then RC (Arusha) baadae anarudishwa Jeshini hakika sijaelewa formula iliyotumika kumrusha rusha katika maeneo mawili tofauti (Jeshini) then SIASA then Jeshini au ni swahiba wa Mkulu?
Duuh! hapa lipo jambo, ninavyoelewa U DC ni cheo cha makada wale waliokosa nafasi zingine za wizarani na bungeni, hivyo hupewa U DC na RC wasikae kijiweni. na hii ni kwa washikaji wa karibu wa mkulu kwa namna moja ama nyingine.

DC ni mjumbe wa kamati ya siasa ya CCM wilayani, kadahalika na RC mkoani. Sasa huyu jamaa atawezaje kutekelza ile dhana kuwa wanajeshi hawaruhusiwi kuwa wanasiasa, jee? atakuwa ameachana na Ukada!
Wale wale walioshindwa kujibu hili, leo wanakwazwa na mwanajeshi mdogo kupiga picha na Lema.

Tuwe na standard moja ya kuhukumu please!
 
Mda utafika changes itatokea, askari wa chini ndio wapiganaji na ndio wenye hali ngumu.
Na ndio walioandaliwa ku risk zaidi.Wale wakubwa wanafundishwa kuwa hawastahili ku risk , na mara zote inabidi walindwe tena na hawa wadogo na wanaopigika.
 
Unakubaliana nasi kuwa shimbo alifanya siasa.
kwa kuwa tamko lilihusu uchaguzi na vyama vya siasa, mtoa tamko sahihi angekuwa kama si msajili wa vyama vya siasa basi angekuwa mwenyekiti wa tume ya uchaguzi.
Ikiwa kwa kitisho cha mpaka na malawi mkuu wa majeshi yetu hatakiwi kusema kitu sembuse kwa kazi isiyomuhusu kabisa!!!
Hawa wajeshi wajiongeze kidogo, wanaposema wanakitii chama kinachounda serikali wamepaswa kujua kuwa utii wao kwa kipande hiki si utii wa kijeshi, kwani waamrishaji si wanajeshi, ama la sivyo hawa wastaafu wa jeshi wanasomeka kuwa ni wanajeshi.

huyu mnyika angekaa kimya tuu , jeshi na siasa ni vitu viwili tofauti , Amiri jeshi mkuu ni rais wa jamhuri ya muungano kwa hiyo ni sahii kwa msemaji wa jeshi kusema kwamba wanafuata serikali iliyo madarakani ,in this case ya ccm , wizara zote ,vyombo vyote vya usalama kuanzia polisi mpaka TISS ni lazima viheshimu sera za serikali iliyopo madarakani , kama wewe ni mwanajeshi ,polisi, usalama wa taifa unapenda sana sera za chadema au chama cha upinzani hutakiwi kujiingiza kwenye siasa labda utoke kwenye hiyo kazi . Dr slaa angekuwa rais si inamaa angekuwa amiri mkuu wa majeshi na vyombo vyote vya usalama vingefuata sera za chadema ...nini tatizo kufuata sera za ccm si ndo demokrasia ya vyama vingi ambayo tunaitaka

Ben, I think your point is too vague and out of grasp.

First, try to be more specific when you say sera. I hope you dont mean a political party, its leaders or whatever.

Second, i think it will be logical to say that powers anazopewa president is not for his political party, and his being amiri jeshi doesn't make the army loyal to his political party, its members, leaders, or its sera in any way. But, the powers are constitutional.

Third, being loyal to a party is like saying your duty when you wake up in the morning is to protect ccm and all its rubbish. Give me a break!! I think the army should be loyal to the country, its constitution and its people.

I disapprove hii kauli ya huyu msemaji wa jeshi. Its just too embarrassing!
 
huyu mnyika angekaa kimya tuu , jeshi na siasa ni vitu viwili tofauti , Amiri jeshi mkuu ni rais wa jamhuri ya muungano kwa hiyo ni sahii kwa msemaji wa jeshi kusema kwamba wanafuata serikali iliyo madarakani ,in this case ya ccm , wizara zote ,vyombo vyote vya usalama kuanzia polisi mpaka TISS ni lazima viheshimu sera za serikali iliyopo madarakani , kama wewe ni mwanajeshi ,polisi, usalama wa taifa unapenda sana sera za chadema au chama cha upinzani hutakiwi kujiingiza kwenye siasa labda utoke kwenye hiyo kazi . Dr slaa angekuwa rais si inamaa angekuwa amiri mkuu wa majeshi na vyombo vyote vya usalama vingefuata sera za chadema ...nini tatizo kufuata sera za ccm si ndo demokrasia ya vyama vingi ambayo tunaitaka
Ni sawa kuwa vyombo vya ulinzi na usalama hutekeleza majukumu yake chini ya amiri jeshi mkuu, ambaye ni rais wa nchi.

Issue yetu ni kuwa, baadhi ya wanajeshi ambao bado hawajastaafu wanapewa vyeo ambavyo vinaambatana na ukada wa CCM. Mfano ni Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya.

Mfano wa wazi umetolewa kuhusu Ndomba ambaye akiwa Kanali alichaguliwa kuwa DC wa Ngara, kisha akapandishwa cheo kuwa RC wa Arusha. Baadaye alipandishwa vyeo vya kijeshi na sasa ni Meja Jenerali na Mnadhimu wa JWTZ.

Hii inadhihirisha kuwa alikuwa hajastaafu, kwa kuwa mwanajeshi aliyestaafu harudi kwenye utumishi wa jeshi isipokuwa wakati wa mapambano.

Sheria inayokataza wanajeshi kuwa wanasiasa iko kwenye katiba:
ibara ya 147(3) ya Katiba inayosema,
"itakuwa ni marufuku kwa mwanajeshi yeyote kujiunga na chama chochote cha siasa...."

Ibara ya 147(4) inatafsiri ‘mwanajeshi' kuwa
"... ni askari aliyeajiriwa kwa masharti ya muda au ya kudumu katika Jeshi la Ulinzi, Jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza au Jeshi la Kujenga Taifa."

Ukiwa Mkuu wa Mkoa unakuwa mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM (M), ambao ni uongozi wa CCM, na bila shaka inathibitisha uanachama kwa kuwa huanza uanachama ndipo uongozi unafuata.
 
Back
Top Bottom