CHADEMA wamfungulia kesi Nape

CHADEMA wamfungulia kesi Nape

Mimi sioni umuhimu wa hii kesi, ni kuendekeza uhasama wa kijinga. CDM walipaswa wampuuze Nape baas! Huku ni kupotezeana Muda na raslimali fedha

Nape amezidi kuropoka,hii siyo mara ya kwanza kutoa tuhuma ambazo zinaweza sababisha nchi yetu kuingia ktk ugomvi na nchi marafiki. Na tatizo ni tuhuma za uwongo. Acha apelekwe mahakamani. Wenzake akina Sofia Simba na Membe wamewahi kutoa tuhuma za hovyo dhidi ya CDM lakini baadaye walizikana.
 
Safi sana abanwe na dawa yake asekwe jela miezi 6 na fidia ya bil3 ili iwe fundisho.
 
Babu slaa ameshamsaidia nape kwa kuuweka ushahidi hadharani japokuwa akasema sio mabilioni ni milioni 60> kwa mwaka sasa sijui ni ushahidi gani tena wanaoutaka
 
Babu slaa ameshamsaidia nape kwa kuuweka ushahidi hadharani japokuwa akasema sio mabilioni ni milioni 60> kwa mwaka sasa sijui ni ushahidi gani tena wanaoutaka

Kabla hujaandika rudi napi achoongea na nini kimepelekwa mahakamani?Acha mihemuko.
 
CDM hawana mchezo kabisa, nao wampeleke Marando kwa kusema mtoto wa kigogo kaingiza mtqmbo feki wa message ili ngoma inoge kabisa.

Thubutuuuu! Waende kama ni wana ubavu. Ni kweli ndio maana wamefyata.

Umesahau mwana mfalme alimpaga Dr.Slaa siku 30 amwombe radhi baada ya kumwita fisadi, la sivyo angempeleka mahakamani. Umeshajiuliza hakwenda kwa nini?

Chezea DR wee!
 
Nape kasema Chadema wanapokea pesa kutoka nje au wampokea. Sasa pesa kutoka nje zinaweza kuwa na maana pana.

Hata kama ni USD 500 walipokea kutoka kwa watanzania waishio USA Nape akitoa ushahidi wa kutosha basi kesi kwishnei.

Rudia alichoongea napi tena acha kukurupuka,napi alisema CHADEMA wameingia mkataba na nje ili wakipata madaraka wawauzie nchi hii.
 
Babu slaa ameshamsaidia nape kwa kuuweka ushahidi hadharani japokuwa akasema sio mabilioni ni milioni 60> kwa mwaka sasa sijui ni ushahidi gani tena wanaoutaka

Na aliyekwambia kwamba ni siri kuwa CDM inapokea 60m ni nani?

Kuna post page no.1 nenda usome kabla hujajiaibisha kwa kuwa na akili kama za nape.
 
nape..(1).jpg

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye


Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimemfungulia kesi Mahakama Kuu Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye, kutokaa na madai yake kwamba Chadema wanapewa mabilioni ya fedha na mataifa tajiri.

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk.Willibroad Slaa, alisema hayo jana wakati wa semina ya viongozi wa chama hicho pamoja na wanachama wa Chama cha Christian Demokratic Union (CDU) cha Ujerumani.

Semina hiyo kuhusu Uhuru, Demokrasia na Mshikamano inawashirikisha baadhi ya wabunge na viongozi wa Kamati Kuu ya Chadema ambapo wanajadili masuala ya kukuza uchumi wa soko unaoshirikisha watu wenye kipato cha chini na juu ambao unaleta dhana ya uwajibikaji kwa taifa na serikali.

Dk. Slaa alisema Chadema kimemfungulia kesi namba 186 /2012 Nape ili aweze kuthibitisha madai yake kwamba chama hicho kinapata mabilioni ya fedha toka kwa mataifa tajiri.

Alisema uamuzi huo umechukuliwa kufuatia propaganda ambazo zimekuwa zikielezwa na baadhi ya watu kuwa Chadema wanapata mabilioni ya fedha kutoka nje wakati hakuna ukweli wa suala hilo.

“Ipo propaganda kuwa chadema inapata mabilioni ya fedha toka nje, kimsingi, marafiki zetu kama Konrad Adenauer Stiftung wanatusaidia kwa ajili fedha za kujengea uwezo, lakini siyo kwa ajili ya kuendesha kampeni au shughuli za kiasiasa,” alisema Dk. Slaa.

Chadema hivi karibuni walimtaka Nape kukiomba radhi chama hicho pamoja na kutoa Sh. bilioni tatu, baada ya kudai kuwa Chadema kinapata mabilioni ya fedha toka mataifa ya nje ambapo alikataa kuomba radhi kwa kueleza tuhuma alizitoa dhidi ya chama hicho ni za kweli.

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alisema mifumo ya uchumi katika nchi yeyote inategemea itikadi na sera ya nchi. lakini serikali ya CCM inaegemea ujamaa na kujitegemea ilhali sekta za uchumi zipo chini ya soko huria.

Alisema kwa Chadema inafuata mlengo wa katikati ambapo imechukua yale mazuri ya mfumo wa ujamaa na kujitegemea na kuchanganya na sera ambazo zinalenga kumwinua mwananchi kiuchumi.



CHANZO: NIPASHE


 
hapo poa sasa. VUVUZELA LIMEJAA MIMATE MDOMONI, LITASHINDWA KUTHIBITISHA!
 
Ni kesi za kipoteza muda. Wakati slaa akitangaza hivyo alikuwa na wajerumani eti wamekuja kutoa somo. Mjerumani kakili wao wanafadhili chadema. Hata watoto wa chekekea wanajua kuwa chadema huwa inapewa tafu na wazungu.
 
kwani kupewa msaada ni dhambi?,,,,mbona hadi bajeti inachangiwa na misaada,miradi ya maendeleo na misaada.......kila kitu msaasa....ndo Tanzania yetu hii
 
Ni kesi za kipoteza muda. Wakati slaa akitangaza hivyo alikuwa na wajerumani eti wamekuja kutoa somo. Mjerumani kakili wao wanafadhili chadema. Hata watoto wa chekekea wanajua kuwa chadema huwa inapewa tafu na wazungu.
Kuna chama gani duniani kisichopewa msaada? Je kosa la cdm ni kuwa na marafiki? Je urafiki na misaada ya China kwa ccm ina lengo gani? au ndo maana tuna wachina hadi wanaouza mbilimbi pale kariakoo?
 
Chadema naona nao wameanza kufilisika.

Sasa mimi najua siku zote hamna imani na mahakama na mnasema hao majaji wote vimeo sasa inakuwaje tena mnafungua kesi huko huko?

Nafikiri hujamwelewa Tundu Lissu hapo pekundu alisema ni baadhi ya majaji.
 
Ni kesi za kipoteza muda. Wakati slaa akitangaza hivyo alikuwa na wajerumani eti wamekuja kutoa somo. Mjerumani kakili wao wanafadhili chadema. Hata watoto wa chekekea wanajua kuwa chadema huwa inapewa tafu na wazungu.

Unachekesha, kwani serikali yako ya CCM haipewi tafu na wazungu? CCM ilianzaje? Unafikiri vitega uchumi walivyonavyo CCM katika mikoa yote wao wailitumia msuli kuvipata? Leo hii unafikiri CCM haipati misaada toka kwa Chama Rafiki huko nje ya nchi?
Ngoja nisepe naona unaleta ushabiki!
 
CDM wataumbuka vibaya sana na hiyo kesi yao wameingia chaka bayaaaaa
 
Tumaini na makamanda wa makao makuu wanajamvi tunataka mtuambie imefikia wapi baada ya kuifungua kimya kimetawala mno. Je ipo inaendelea lini?
Au mmeimaliza nje ya mahakama au mmeombwa Radhi cha muhimu kwetu ni taarifa chama ni cha wanachama na kinapochafuliwa kikachukua hatua ni haki kulizia
Karibuni
 
Back
Top Bottom