Kwa kweli.,naona kimsingi serikali imekubali suala la katiba mpya, wanashindwa kutamka straight ili kumlinda Mama Kombani kwa matamshi yake ya kukurupuka! Ni wakati muafaka wa kuwa na katiba mpya.,we need it urgently sio suala la kusubiri muda mrefu
Katiba mpya haihitaji masharti
[]Na Ndimara Tegambwage - Imechapwa 15 October 2010
*
Kwa hiyo zoezi lolote la kwenda kwa mwananchi na kumuuliza iwapo anataka haki yake; siyo tu litalenga kuchelewesha uhuru wa raia, bali ni dhihaka; ni uchokozi.
Chukua mfano wa mwizi aliyeiba shati au blausi yako. Anakuja kwako na kukwambia kuwa aliiba nguo yako. Anakuuliza iwapo unataka akurudishie au asikurudishie! Si atakuwa anachumbia kisirani?
Tena mwizi huyohuyo, anayekuuliza kwa jeuri, anakuwekea muda na taratibu za kurudisha nguo yako ikiwa ni pamoja na wewe kuifuata atakakokuelekeza. Huko si kuleta kisirani?
umesema mengi, wananchi wanajua haki zao? Gazeti lako linawafikia walengwa, wananchi? Au linatufikia sisi tunaojua haya unayoyasema!