Chadema walamba Dume, Mzunguko wa Kwanza

ukweli ni kwamba hatutakiwi kuwa na uhakikika kama vili serikali ya ccm haijulikani kwa michezo yao ya hovyo hovyo.Iyo issue haitafanyiwa kazi wala nini,
 
Kweli jambo la muhimu ni elimu kutolewa kwa watu wengi kuhusu umuhimu wa katiba mpya!


Naam, tupige hatua sasa. kwamba tunahitaji mjadala wa katiba mpya tumeshatoka huko. Kwa kauli ya Pinda jana, maana yake ni kwamba mjadala uko wazi na huru
 
ukweli ni kwamba hatutakiwi kuwa na uhakikika kama vili serikali ya ccm haijulikani kwa michezo yao ya hovyo hovyo.Iyo issue haitafanyiwa kazi wala nini,

na ukumbuke sasa baadhi ya vyama vya upinzani na baadhi ya wabunge na viongozi wa upinzani katika hatua hii wanaweza kununuliwa. Siyo kila mwanasiasa anayelilia katiba mpya ana nia ya dhati ya katiba mpya, bali wengine wanajua mchakato utawaletea mafao. umakini ni muhimu kwani siyo kweli kwamba madabiliko tunayoyataka ya katiba ni matamu kwa ccm na serikali. tunaweza kujikuta tunaendelea na mvinyo ule ule kwenye chupa mpya.
 
na ukumbuke sasa baadhi ya vyama vya upinzani na baadhi ya wabunge na viongozi wa upinzani katika hatua hii wanaweza kununuliwa. Siyo kila mwanasiasa anayelilia katiba mpya ana nia ya dhati ya katiba mpya, bali wengine wanajua mchakato utawaletea mafao. umakini ni muhimu kwani siyo kweli kwamba madabiliko tunayoyataka ya katiba ni matamu kwa ccm na serikali. tunaweza kujikuta tunaendelea na mvinyo ule ule kwenye chupa mpya.
kwa maslahi ya nchi watu woote tuungane kutengeneza katiba bila kujali chama na WABUNGE wasiangalie uvyama ni hatali hasa kwa wabunge wa ccm.
 
Michezo kama hiyo walifanikiwa tu kuhusu mgombea binafsi! Sasa hivi mambo yamekaa tenge, maana Katiba yenyewe inamtambua Waziri Kiongozi wa Zenj ambaye hayupo! Sasa kama hawatabadili Katiba hata kwa hilo wanahitaji kutimuliwa Ikulu "kwa njia nyingine!"

Kijana uko makini sana.
 
Haya, mhariri wa gazeti la uhuru la leo asema kuandika katiba mpya ni kazi ya serikali. Kwamba serikali imeshachukua jukumu lake, watu binafsi na vyama wasijipendekeze kutafuta mtaji wa kisiasa

Huyu ni mtu anayetumiwa, halafu yeye ni kama kasuku....kama ujuavyo kasuku yeye kazi yake ni kunakili kila kitu kama kilivyo hana uwezo wa kujua anafanya nini na ni kwa nini....yeye ndiyo alivyoumbwa. Sasa ni sawa na huyu muhariri..........unakuwa kibaraka mpaka unapoteza hata uwezo wako wa kufikiri na kuamua Shame...
 
Nadhani kuelimisha watanzania kuhusu katiba iliyopo na kasoro zake ndiyo iwe kazi ya vyama vya siasa vya upinzani kuwanzia sasa hivi. Tunategemea mengi zaidi kutoka kwa wale wenye ruzuku kubwa. Kwa kuwa chadema wamefanikiwa kulianzisha hili, hatua ilipofikia sasa wanatakiwa wajumuishe vyama vingine. kwenye hili sidhani kama vyama vya upinzani vitakuwa na maslahi yanayokinzana, labda baadhi waamue kuwa vibaraka wa ccm

Hongera.
Ni wazi elimu (kwa ujumla) na hasa ya uraia ni duni sana, hivyo juhudi za dhatii na za makusudi za kuwaelimisha WaTz zifanywe maana bila elimu tunaweza tusifanikiwe katika azma ya ukombozi wa Tz na MTz.

Kazi iliyoko mbele si haba, hatari nazo ni kubwa na vikwazo ni vingi lakini tukiwa na nia na upendo wa dhati wa kuisaidia Tz na raia wake tutafika na kushinda. Muhimu kukumbuka kwa mazingira ya sasa Katiba ndio kitu muhimu sana tunaweza kuwapa watoto wetu; kizazi hiki kitakuwa kimefanya wajibu wake. Historia itasomeka na kuhukumu aidha kama tumeshinda au tumeshindwa.

Wadandiaji na watekaji wa hoja ya Katiba wasipewe nafasi katu, siku na wakati wowote tuwaumbue na kuwapinga. Wale wenye mawazo finyu na hasi ya itikadi ya vyama tupambane nao kama tunavyowapinga wa ukabila, udini, nk. Masalahi ni ya Tz kwa ajili ya WaTz wote.

Ni hayo kwa sasa
 
Huyu ni mtu anayetumiwa, halafu yeye ni kama kasuku....kama ujuavyo kasuku yeye kazi yake ni kunakili kila kitu kama kilivyo hana uwezo wa kujua anafanya nini na ni kwa nini....yeye ndiyo alivyoumbwa. Sasa ni sawa na huyu muhariri..........unakuwa kibaraka mpaka unapoteza hata uwezo wako wa kufikiri na kuamua Shame...

nakuunga mkono mkuu, lakini punguza hasira kidogo kwani wewe kama unavyojiita ni mkwere mtarajiwa!
 
kwa maslahi ya nchi watu woote tuungane kutengeneza katiba bila kujali chama na WABUNGE wasiangalie uvyama ni hatali hasa kwa wabunge wa ccm.

Mkuu, nadhani hii ndiyo nia yetu sote. lakini unawajua tena wale wasaliti na makuwadi wanaofikiri kutokea matumboni mwao badala ya vichwani mwao
 
Kwa kuwa sasa mjadala upo wazi hofu yetu iwe ni kwa viongozi watakaonunuliwa na kutusaliti wananchi.
 
:whoo::whoo::whoo::whoo::whoo::whoo::whoo::whoo::whoo::whoo::whoo::whoo::whoo::whoo::whoo::whoo::whoo:
 
Jamani madai ya katiba mpya hayana chama. Kila mtanzania mwenye kuipendea mema nchi hii anahitaji katiba mpya.
Hata hivyo lazima tukubali kuwa Chadema na cuf ni waanzilishi wa mjadala huu tangu wakati wa kampeni na ilikuwa ahadi yao katika manifesto zao. Hilo halipingiki.
 
Haya, mhariri wa gazeti la uhuru la leo asema kuandika katiba mpya ni kazi ya serikali. Kwamba serikali imeshachukua jukumu lake, watu binafsi na vyama wasijipendekeze kutafuta mtaji wa kisiasa

Huyo Mhalili tena wa gazeti la Majambawazi yeye ni nani katika taifa hili mpaka atake kuzuia kilio cha watanzania kudai sheria mama mpya kwa mustakabari wa taifa lao. Huo ubavu hana na nguvu ya Umma itamfuata huko aliko siku moja.

KATIBA MPYA NI LAZIMA SIYO HIARI.
 
Jamani madai ya katiba mpya hayana chama. Kila mtanzania mwenye kuipendea mema nchi hii anahitaji katiba mpya.
Hata hivyo lazima tukubali kuwa Chadema na cuf ni waanzilishi wa mjadala huu tangu wakati wa kampeni na ilikuwa ahadi yao katika manifesto zao. Hilo halipingiki.


Nimeidondokea post yako mkuu! Ccm Ina wanachama wengi, wabunge wengi, madiwani wengi, majeshi, watendaji wa serikali, kuliko vyama vingine vyote vikiunganishwa. Wanapata kila kitu wakitakacho.

Unamaanisha kwamba na wao wanatamani kuwe na katiba mpya? Kama jibu lako ni ndiyo, ili hiyo katiba mpya iwapatie nini ambacho hii ya sasa haiwapatii?
 
na ukumbuke sasa baadhi ya vyama vya upinzani na baadhi ya wabunge na viongozi wa upinzani katika hatua hii wanaweza kununuliwa. Siyo kila mwanasiasa anayelilia katiba mpya ana nia ya dhati ya katiba mpya, bali wengine wanajua mchakato utawaletea mafao. umakini ni muhimu kwani siyo kweli kwamba madabiliko tunayoyataka ya katiba ni matamu kwa ccm na serikali. tunaweza kujikuta tunaendelea na mvinyo ule ule kwenye chupa mpya.

Kumbe umesituka ee
kama vile viongozi wa chadema walivyotoka nje ya bunge eti ili ccm waone kuna mgogoro wakae meza moja wagawawane madaraka. Si unaona walienza kujirengesha baada ya kutoka nje eti TUNAWEZA KAA MEZA MOJA NA CCM. teh teh teh teh tabu kweli kweli
 
inaonekana vijana wa CDM tumekuwa extied sana na habari kama hii za kufurahisha, lakini kwa mtazamo wangu madai ya katiba mpya yalianza zamani, na ss yamekolezwa na CDM, makosa wanasiasa wa tz tunafanya ni kuona hatua muhimu tuliyofikia ni effort za mtu au chama kimoja, la hasha! it is a collective efforts za watu mbalimbali na na vyama mbalimbali. Utaona kila chama kikidai matokeo haya wao ni kisababaishi! who ever is going to win this batle, must kno that this battle was for all of us TZ, and all of us hev fought it. be it CDM, CUF of APPT-Maendeleo, it was our battle and SO CHAMA CHOCHOTE LAZIMA KITAMBUE MCHANGO WA VYAMA VINGINE. nahuzunika kuona kila chama kinafanya vita hii kivyake, natambua umamluki, Uccm nk tusifanye vita hii ni ya kikundi, chama fulani, katika kudai mambo ya msingi kwa taifa hebu tutambuane.
natambua nguvu ya mapambano hayafananani, kuna wanaochangi akidogo, wanaochangia sana nk. hapa nacema vyama vyote tuungane katika hili...
 
Pinda anasema kuwa eti atamshauri Kikwete aunde timu ya mchakato wa Katiba mpya.
Hizi ni njama za Serikali ya CCM (ninimaanisha viongozi) kutaka kuteka (hijacking) muelekeo wa kuunda Katiba mpya.

Wananchi tunao wajibu wa kujadili nini kijadiliwe, na nini na nini viwemo kwenye katiba mpya, na vipi (vilivyomo kwenye katiba ya sasa) visiwemo.

Ilionekana toka mwanzo kuwa CCM na Serikali hii hawana nia ya dhati ya kubadili katiba ili kutengeneza Katiba mpya ambayo italeta faida na manufaa zaidi kwa raia wa Tanzania (rejea kauli ya waziri wa Sheria).
Baada ya kauli nyingi za kudai katiba mpya, sasa wameona hawawezi kupingana na wakati, na wanataka wao ndio wawe madereva wakati hawana nia ya kutupeleka kwenye Katiba ya haki.

Tupinge Kikwete kuunda timu/kamati ya mchakato wa kuunda katiba mpya. Unaweza kuwa mchezo wa kuigiza.

Hii iundwe na wajumbe kutoka kada/nyanja mbalimbali, mfano vyama vya siasa, vyama visivyo vya kiserikali, chama cha wanasheria tanganyika (TLS), wataalam mbalimbali waliobobea katika fani zao, viongozi wa dini, na mwananchi yoyote aweze kutoa maoni yake kwa sms au baruapepe.

Muhimu zaidi ni kuwa katiba mpya inatakiwa ilete uhuru na haki zaidi kwa mwananchi, na kuondoa utawala wa kiimla kwa kupunguza madaraka makubwa kupita kiasi ya viongozi, hasa Rais.
 
Kama mchezo wa karata vile. Nadra mchezo kukamilika kabla ya mizunguko kadhaa. Safari yao ni katiba mpya na tume huru ya uchaguzi. mkakati wao wa kwanza ukawa kutokukubali ushindi wa JK, halafu kususia hotuba yake huku wakitoa wito wa madai yao. Yakasikika ndani na nje ya nchi, mijadala ikapamba moto.

Wameitwa majina, wamebezwa, wametengwa, na wamefitinishwa. Wakashindwa kuzima moto, na hatimaye ccm wakaona wakichelewa watashindwa kuja kusema wao ndio walioanzisha mjadala na mchakato. Ingawa walishakengeuka kupitia yule mama kilaza aliporopoka kwamba Tz haihitaji katiba mpya, wakaona bora wale matapishi yao mapema kweupe kupitia Waziri Mkuu. Hivyo guu lisijeota tende!

kwanini ni ushindi wa chadema hatua ya kwanza. huoni huo ni mtego? Kwamba rais atateua jopo ambalo litamshauri.

Kwa maoni yangu sioni umuhimu wowote wa jopo hili eti la kushauri kama kuna umuhimu wa kuunda katika mpya au kuendelea kuweka viraka. CCM watajibaraguza ili kubuy time na tukija kushtuka tayari tuko 2013. Tamko lao litakuwa kwa sasa hatuna muda wa kutosha wa kuunda katiba mpya hivyo uchaguzi ujao utafanyika kwa kutumia katiba iliyopo.

Mzee Rukhsa kasema kwamba hakuna haraka ya kuunda katiba mpya maana nchi iko "shwari na tuna amani". Huu wakati wa "ushwari na amani" ndiyo wakati mzuri wa kuunda katiba mpya na siyo kusubiri hadi kutokee machafuko na kukatana mapanga (kama ilivyotokea Kenya) ndiyo tuone umuhimu wa kuunda katiba mpya.
 
Kwa kweli.,naona kimsingi serikali imekubali suala la katiba mpya, wanashindwa kutamka straight ili kumlinda Mama Kombani kwa matamshi yake ya kukurupuka! Ni wakati muafaka wa kuwa na katiba mpya.,we need it urgently sio suala la kusubiri muda mrefu
 
Back
Top Bottom